Pages

Wednesday, July 4, 2012

BONGO FLEVA, BONGO MOVIE WAPIGANA MKWARA TAMASHA LA MATUMAINI

Baadhi ya wachezaji wa Bongo Fleva wakiwa mazoezini.
Kala Pina (katikati), akipasha misuli na wenzake.
 Bongo Fleva wakiwa wakiwa ‘siriaz’ mazoezini.
Mchezaji wa Bongo Fleva, Suma G akijinoa.
Amini Mwinyimkuu na wenzake.
Ni Vicent Kigosi ‘Ray’ wa Bongo Movie.
Ni mshambuliaji wa kulia wa ‘Movie’, Hartman Mbilinyi.
JB ( wa kwanza kushoto) ‘akijikomaza’.
Inspector Haroon wa Bongo Fleva.
Mussa Issa ‘Cloud’ wa Bongo Movie.
TIMU za mpira wa miguu za wasanii wa muziki, Bongo Fleva, na wacheza sinema, Bongo Movie, jana zilizidi kutoleana vitisho kwenye mazoezi yaliyozikutanisha katika Viwanja vya Leaders Club Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Timu ya Bongo Movie, Jacob Steven ‘JB’, alisikika akisema kuwa hakuna mechi itakuwa chungu kwa Bongo Fleva kama ya Tamasha la Matumaini itakayofanyika Jumamosi hii, ambapo wanatarajia kuwapakiza mvua ya magoli.
Nao Bongo Fleva, kupitia mchezaji wao Kala Pina, walisema mazoezi wanayoyapata kutoka kwa kocha wao, Seleman Matola, wanawaomba Bongo Movie wajitoe mapema mechi hiyo kwani moto wake utakuwa mkali isivyo kawaida.
(Habari/Picha: Musa Mateja/GPL)

No comments:

Post a Comment