Pages

Wednesday, September 11, 2013

HII NDIYO SAFARI YA MWISHO YA MSANII WA FILAMU MELISA

Jeneza lililobeba mwili wa marehemu likishushwa kwa ajili ya kuingizwa ndani.

 Siku ya jana ndiyo ilikuwa siku ya mwisho ya kuuaga mwili wa aliyekuwa msanii wa filamu Bongo, Zuhura Maftah ‘Melisa’ aliyefariki dunia Jumapili iliyopita katika hospitali ya Hindu Mandal ambapo majonzi yalitawala nyumbani kwa dada yake Mikocheni ulikokuwa ukiagwa mwili wake na kwenda kuzikwa katika makaburi ya Kinondoni, Dar.
  Mtoto wa marehemu, Sabrina akiuaga mwili wa mama yake.
Ndugu, jamaa na marafiki wakiuaga mwili.

  Umati wa waombolezaji wakiwa na nyuso za huzuni.
  Wasanii wa filamu, Chuchu Hans na Vivian wakilia kwa uchungu baada ya kuaga mwili wa marehemu.
   Msanii wa filamu, Monalisa akilia kwa uchungu.
  Mama wa marehemu (kushoto) na dada wa marehemu, Alice (kulia) wakilia kwa uchungu.
  Hapa mwili ukiingizwa kaburini.
(Habari/Picha: Gladness Mallya, Hamida Hassan na Shakoor Jongo / GPL)

1 comment:

  1. tunaelewa sasa hivi ni karne ya 21 lakini muwe mnawasitiri maiti kwenye kupiga picha,kwa nini mnaziachia picha kama hivi,hii ni kwa vyombo vyote.muwe mnawaziba au kutowapiga picha kama hivi jamani.sio ustaarabu kabisa.

    ReplyDelete