EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Thursday, July 16, 2015

KINGUNGE: MCHAKATO WA KUMPATA MGOMBEA URAIS CCM ULIKUWA BATILI

Mzee Kingunge akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwake jijini Dar es Salaam jana.

KADA mkongwe wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kingunge Ngombale Mwiru, amekosoa mchakato uliotumika kumpata mgombea urais wa chama hicho, akieleza kuwa ulifinyangwa na hivyo ni batili, haukubaliki na hauvumiliki.

Aidha, ameshauri kuwa ili chama hicho kiendelee na kampeni za uchaguzi kikiwa kimoja, ni lazima kasoro zilizotokea Dodoma zijadiliwe kwa kina kumaliza tofauti zinazoonekana kujitokeza na kupata maridhiano.

Jumapili iliyopita CCM ilimteua Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, kuwa mgombea wake wa urais na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano), Samia Suluhu Hassan, kuwa mgombea mwenza.

Akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwake jijini Dar es Salaam jana, Kingunge alisema viongozi waandamizi wa CCM wamekiuka kwa makusudi katiba, kanuni na taratibu za chama kuanzia kwenye vikao vya Kamati ya Maadili, Kamati Kuu (CC) hadi Halmashauri Kuu (Nec).

Hata hivyo, alisema maamuzi ya Mkutano Mkuu uliompitisha Dk. Magufuli anayaheshimu kwa kuwa kasoro zilijitokeza CC na Nec.

Alisema Katiba ya CCM pamoja na mambo mengine, inaeleza kuwa Kamati ya Maadili ambayo ameeleza ni kitengo ndani ya chama ina jukumu la kuandaa taarifa kuhusu wagombea na siyo kukata majina.

Alisema taarifa inayoandaliwa na kitengo hicho hupelekwa CC, ambayo kazi yake ni kumsikiliza mgombea mmoja mmoja na kumuuliza maswali yasiyopungua matatu, kisha wajumbe hukaa na kupendekeza majina matano ambayo yanapelekwa Nec.

“Kwa utaratibu wa kikatiba, sekretarieti kazi yake ni kuhudumia CC na Nec kwa kukusanya majina ya watu walioomba, inayapanga vizuri, ikikamilika inawasilisha taarifa yake kwenye Kamati Kuu…sekretarieti si kikao cha maamuzi wala si kikao cha mapendekezo, kwa hiyo mchakato hasa unatakiwa uanze kwenye Kamati Kuu,” alisema.

Kingunge alisema utaratibu ambao umetumika tangu mwaka 1995, kila mgombea atapaswa kuhojiwa na kamati kuu mmoja mmoja na kuulizwa maswali yasiyopungua matatu na kisha wajumbe huwajadili na kutoa mapendekezo ya majina matano kwenda Nec.
“Inaelekea kazi ya kupata wagombea watano ilifanywa na kitengo kinachoitwa Kamati ya Maadili na Kamati Kuu ikafikishiwa majina matano tu, kitendo hicho cha kuinyang’anya Kamati Kuu kazi yake si cha kawaida, ni uvunjifu wa taratibu na hakuna uadilifu ndani yake. Kamati ya Maadili yenyewe inavunja maadili,” alisema.

Kingunge ambaye aliwahi kushika nyadhifa kadhaa ndani ya CCM na serikalini, alisema maadili ya chama yanaanzia kwenye kuheshimu muundo wa chama, sera na taratibu zake; hivyo ukiukwaji uliofanyika Dodoma ni kukinyonga chama hicho.

Alisema inasikitisha kwamba hata baada ya kupelekewa majina matano, CC ilifanya maamuzi yake bila kuwaona wagombea wote 38 waliorudisha fomu za kuomba kuteuliwa kuwania urais na hata wagombea waliokatwa hawakuitwa kwenye hicho kitengo cha maadili badala yake walihukumiwa bila kusikilizwa.

“Kwa hiyo kuna mahala fulani watu wachache wamekaa wakatengeneza orodha yao na wakataka Kamati Kuu imeze. Kilichofanyika si jambo dogo tu…Mzee Abeid Aman Karume alisema nchi hii ni yetu wote na mimi nasema maana yake tunaowapa madaraka wasifike mahali wakafikiria nchi hii ni yao wao, yale madaraka ni dhamana tu; na kwenye chama ni hivyo hivyo, CCM ni mali ya wanachama wote,” alisema.

Kingunge alisema chama hicho kilitoa fomu kwa wanachama ambao waliingia gharama kuzunguka mikoa mbalimbali kusaka wadhamini lakini katika hali ya kushangaza, kitengo cha maadili kiliwapuuza na kufanya maamuzi batili.

Alisema kwa utaratibu wa chama, CC ilitakiwa kuwasilikiliza wagombea wote 38 waliorudisha fomu, kuwajadili na kutoka na mapendekezo ya majina matano kupeleka Nec; utaratibu ambao ulikiukwa.

Alisema vikao vya vyombo mbalimbali ndani ya chama vimewekwa ili kutenda haki kwa wanachama wote hivyo ni muhimu kuviheshimu kwa nia ya kuleta usawa na kwamba kilichotokea Dodoma ni dharau kwa wagombea waliochukua fomu na wanachama wote wa CCM.

“Bahati mbaya katika nchi yetu wananchi ni wavumilivu mno kiasi kwamba tumefanya wakubwa zetu tunaowapa madaraka wanajua wanaweza kufanya chochote kwa sababu hakutakuwa na chochote. Sasa mimi nasema hakutakuwa na chochote sawa, lakini hata kusema?. Kwa hiyo mimi nasema kwa niaba ya wengi walio kimya,” alisema.

Kingunge aliongeza kuwa: “Na mpaka hapo kwenye CC yaliyofanyika si sahihi na kwa kweli ni batili. Upande mmoja Kamati Kuu kunyang’anywa kazi yake na kitengo lakini upande mwingine haki ya asili ya kusikilizwa, watu hawawezi kuhukumiwa tu bila kusikilizwa. Kamati Kuu inatakiwa iandae orodha fupi ya hao walioomba lakini baada ya kuwasikiliza.”

Hata hivyo, alisema Nec ina mamlaka ya kuhoji mapendekezo ya CC, kuyakubali, kukataa baadhi au yote; lakini katika hali ya kushangaza, haikufanyika hivyo.

Alisema mjadala kwenye Nec ulivyokuwa hata wazee wastaafu ndani ya CCM ambao ni marais wastaafu Mzee Ali Hassan Mwinyi, Benjamin Mkapa na Amani Abeid Karume, walipotoshwa na hivyo michango yao iliminya haki za baadhi ya wagombea.

Hata hivyo, alisema pamoja na upotoshaji uliofanywa na kikundi cha viongozi wachache, msimamo wa Nec ulikuwa dhahiri kwamba wajumbe walimtaka mgombea aliyekuwa na nguvu kuliko wengine, Edward Lowassa.

Bila kuwataja viongozi wakuu wa chama hicho na serikali ambao walifinyanga majina ya wagombea watano na kuyawasilisha CC, Kingunge alisema viongozi hao walifanya jitihada na nguvu kubwa kuvunja kanuni na taratibu ili kuhakikisha wanamnyima haki Lowassa.

“Kama tusipofanya critical analysis (uchambuzi kosoa), kuonyesha mapungufu yaliyojitokeza hatima ya chama chetu haitakuwa nzuri…mkasa uliotokea Dodoma ni uongozi wa chama chetu ambao vile vile ni uongozi wa nchi kutumia nguvu kubwa kabisa ya kupuuza wananchi wanasema nini na kuhakikisha kuwa huyo ambaye wananchi wanasema wanampenda, hawatampata,” alisema.

“Jitihada zote zilizofanywa za kuvunja taratibu zilikuwa zinaelekezwa kumzuia mtu fulani asipate haki na mtu huyo ni Lowassa,” alisema.

Aliongeza kuwa: “Yaliyotokea Dodoma mwaka huu yametia kasoro kubwa katika historia ya chama chetu ambacho kinaheshimika sana.”

“Mkitaka nchi itengamae, lazima chama kinachoongoza kijiendeshe kwa misingi iliyosahihi na safi. Msingi wa kwanza ni demokrasia ndani ya chama. Yaliyotokea Dodoma yametia dosari kabisa kwa sababu huwezi ukabadilisha taratibu za msingi katika kupata viongozi ambazo zilipaswa kulindwa na viongozi wa chama.”

Kingunge alidai mchakato wa kumpata mgombea wa CCM ulivurugwa kwa makusudi, hivyo mkutano mkuu siyo kikao cha kulaumiwa kwa kuwa waliokosea ni CC na Nec.

“Mkutano mkuu huwezi kuulaumu kwa sababu wamepelekewa majina matatu na wametamka yule wanayemtaka…uchambuzi wangu kosoa hapa haumhusu Magufuli kwa sababu si yeye aliyefinyangafinyanga mambo,” alisema.

NINI KIFANYIKE
Alisema kutokana na kasoro hizo, ni lazima CCM ijitathimini namna ya kutoka hapo ilipo ili iweze kushinda kwa kishindo Oktoba 25 kwenye uchaguzi mkuu.

“Sisi wana-CCM tutafute njia ya kushikamana na katika hili Lowassa ana nafasi muhimu na ya kimkakati; ana imani ya mamilioni ya Watanzania. Tukitaka kufanikiwa vizuri kama CCM, tutumie nguvu zote tulizonazo twende kwenye uchaguzi tushinde kwa kishindo. Lazima yaliyotokea yazungumzwe ndani ya chama,” alisema.

Alisema bila kufanya hivyo, CCM haitaweza kuendelea kuwa moja kama ilivyokuwa awali.

“Lazima tutoke katika mazingira haya na hatuwezi kutoka hapa bila watu kutoa dukuduku zao,” alisema.

Alisema ni dhahiri kuwa ndani ya CCM kuna mvutano ambao ukiachwa utasababisha mpasuko mkubwa.

UFISADI WA LOWASSA
Alisema tangu mwaka 2008 baada ya kashfa ya Richmond, Lowassa amekuwa akiandamwa kuwa ni fisadi lakini ni ‘hadithi’ ambayo imekosa mashiko kwa kuwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) ilichunguza na kuthibitisha kuwa hakukuwa na vitendo vyovyote vya rushwa.

Alisema Lowassa alilazimika kuwajibika kisiasa kwa maslahi ya CCM na serikali na kwamba siyo wa kwanza kujiuzulu kwani mwaka 1976 Mzee Mwinyi akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani, alijiuzulu baada ya vyombo vya usalama kuthibitika kuchochea mauaji na kuumiza watu.

UADILIFU WA LOWASSA
Alisema Lowassa ni mwanachama mwaminifu wa CCM, mtendaji hodari kwenye chama na serikalini ambaye amepigiwa mfano katika kila wadhifa alioshika.

Alisema Lowassa ni kada anayependwa na wanachama wa CCM na wananchi kwa ujumla hivyo kumwengua kimizengwe ni udhaifu mkubwa ulioonyeshwa na viongozi wa chama hicho.

KUONDOKA CCM
Hata hivyo, Kingunge alipotakiwa kueleza imani yake ndani ya CCM na kama ataondoka, hakuweka bayana badala yake alisema atakapofikia uamuzi wa kutoka atawataarifu waandishi wa habari.

Kuhusu hatima ya kisiasa ya Lowassa, alisema ana amini ni kiongozi makini hivyo atafanya maamuzi sahihi kwa manufaa yake.

NIPASHE iliwatafuta viongozi wa CCM akiwamo Katibu Mkuu, Abdulrahman Kinana na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, kujibu tuhuma hizo lakini simu zao ziliita bila majibu na nyingine hazikupatikana.
CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate