Pages

Saturday, June 30, 2012

Leo imetimiza miaka sita tangu baba yetu Mpendwa ulipotutoka Mzee Obel Benson Mwamfupe

Mzee Obel Benson Mwamfupe! 
Leo imetimiza miaka sita tangu baba yetu Mpendwa ulipotutoka. Kibinadamu ni ngumu sana lakini tunamshukuru Mungu baba wa mbinguni aliyeweza kututia nguvu na faraja tele mpaka leo hii tuko hivi tulivyo! Tunakukumbuka kwa upendo na hekima zako. 

Baba, ulikuwa kama mti mkubwa na sisi tulikuwa kama ndege tulioweka makazi kwako! ulipoanguka tuliyumba sana, tunazidi kumshukuru Mungu hata kwa hili maana hajatuacha! Akatukusanya tena. Unakumbukwa na familia yako yote wakubwa kwa wadogo. Mungu akupe pumziko la Amani.

No comments:

Post a Comment