Pages

Sunday, January 27, 2013

Ofisi ya serikali yachomwa moto Suez

Taarifa kutoka mji wa Suez, Misri, zinaeleza kuwa ofisi ya usalama ya serikali imechomwa moto.
Mapambano mjini Suez
Hayo yametokea wakati maelfu ya watu wakipita mabara-barani kwenye mhadhara wa mazishi ya wale waliokufa katika mapambano ya Ijumaa - siku ya kuadhimisha miaka miwili ya kuanza ghasia zilizomuangusha Rais Hosni Mubarak.
Wanajeshi wa serikali wanaendelea kupiga doria mjini Suez.
Watu kama 10 walikufa katika ghasia za Ijumaa.
Mjini Cairo, mapambano piya yamezuka kati ya askari polisi na waandamanaji karibu na wizara ya mambo ya ndani ya nchi ya Misri.
Polisi walifyatua moshi wa kutoza machozi kujaribu kuwazuwia waandamanaji wasifike kwenye jengo la wizara.

No comments:

Post a Comment