Pages

Monday, March 25, 2013

KAJALA YUPO HURU, WEMA AMLIPIA FAINI YA MILIONI 13

MSANII Wema Sepetu amemlipia faini ya shilingi milioni 13 msanii mwenzake, Kajala Masanja, na kumfanya awe huru. Mapema leo, 
Kajala alihukumiwa kwenda jela miaka 5 au kulipa faini ya shilingi milioni 5. 
Kajala alikuwa anakabiliwa na kesi ya kuuza nyumba iliyowekwa kizuizini na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) baada ya mumewe, Faraji Agustino kukumbwa na tuhuma za kutakatisha fedha haramu. 
Faraji yeye amehukumiwa kwenda jela miaka mitano au kulipa faini ya shilingi milioni 213. Kwa sasa Kajala yupo nyumbani kwao maeneo ya Oysterbay jijini Dar es Salaam pamoja na ndugu na jamaa.

No comments:

Post a Comment