HATIMAYE SERIKALI YAIFUNGA SHULE YA SEKONDARI YA LUTHERAN JOURNIOR YA MJINI MOROGORO BAADA YA WANAFUNZI KUGOMA KWA SIKU TATU.
Mgomo
wa wanafunzi zaidi ya 600 wa shule ya sekondari ya seminari ya
lutheran journior ya mjini Morogoro wa kutoingia darasani mpaka madai
ya kero zao yatatuliwe umeingia hatua mpya baada ya serikali kuchukua
hatua ya kuwafukuza wanafunzi wote shuleni hapo na kufunga shule hiyo
kwa muda usiofahamika .
Hatua
hiyo ya serikali imekuja kufuatia wanafunzi hao kukataa kuzungumza na
kumzomea katibu mkuu wa kanisa la kinjiri la kirutheri KKKT Brighton
Killewa ambaye alitumwa na askofu wa kanisa hilo nchini Alex Malasusa
kusikiliza madai ya wanafunzi hao ambayo ni pamoja na kutaka mkuu
wa shule hiyo aondolewa shuleni hao kutokana na kuendesha shule huyo
kidikteta pamoja na walimu wanaoajiriwa hapo kutokuwa na sifa hali
inayofanya shule kushuka kitaaluma .
Kasilda Mgeni Mulimila kutoka Morogoro anataarifa zaidi.......
Huyu ni katibu mkuu KKKT akiwa hana la kufanya baada ya wanafunzi
hawa kumzumea hata kabla ya kuanza kusikiliza kero zao, hali hii
inalilazimu jeshi la polisi kutuma askari wake kulinda usalama shuleni
hapo kwa siku ya tatu leo huku uongozi wa shule hiyo ukiendelea
kuwasiliana na serikali juu ya yale yanayoendelea shuleni hapo ,na
hatimaye afisa elimu wa mkoa wariambora Nkya anakuja shuleni hapo na
kisha kutoa uamuzi wa bodi ya shule na serikali.Kinyume na
ilivyotarajiwa wanafunzi hao ambao awali walikuwa wakigoma kuondoka
shuleni hapo ,baada ya amri ya afisa elimu huyo ,walianza kuondoka na
mizigo yao ambapo tayari magari yalishafika shuleni hapo kwa kubeba
wanafunzi lakini wengine walionekana hawana fedha na kulazimika
kutembea kwa miguu kuomba hifadhi kwa wakazi wa morogogo wakati
wakiwasiliana na, wazazi wao wawatumie nauli na hapa wanapasa sauti
zao. Hata hivyo Mkuu wa shule hiyo laison Saming'o hakuonekana
shuleni hapo ili kujibu tuhuma zinazomkabili na huku habari zaidi
toka shuleni hapo zikielezakuwa mkuu huyo wa shule alijifungua ofisini
kwake tangu juzi akihofia wanafunzi hao ambao walikuwa na ghadhabu
kubwa dhidi yake na kutaka aondolewa shuleni hapo.
No comments:
Post a Comment