Pages

Thursday, August 8, 2013

HIKI NDICHO AICHOANDIKA RAY C ,LAWAMA ZOTE AMEZIELEKEZA KWA MPENZI WAKE ZA KUTUMIA MADAWA YA KULEVYA.


 
Ray ameandika haya
"The New Ray C, Am a Strong Lady!!!!kila Nipewapo Mtihani mgumu wa Maisha napigana mpka nakuwa mshindi."

RAY C ASIMULIA KILICHOMFANYA AANZE KUTUMIA MADAWA YA KULEVYA........LAWAMA ZOTE AMEZIELEKEZA KWA MPENZI WAKE

Muimbaji wa ‘Niwe Nawe Milele’ Rehema Chalamila aka Ray C jana alifanya interview ya kwanza ya TV tangu takriban miezi 10 iliyopita baada ya kujichimbia kupata matibabu ya madhara aliyokuwa amepata kutokana na matumizi ya madawa ya kulevya.

Akiwa na muonekano mpya, mchangamfu, aliyenawili, mrembo na mwenye afya njema, Ray C alizungumza kwa undani kwenye The Interview ya Clouds TV kuanzia namna alivyoingia kwenye matumizi ya madawa ya kulevya, jinsi yalivyomwathiri na namna alivyosaidiwa hadi leo amekuwa hivyo.

Ray C alisema aliingia kwenye matumizi ya madawa ya kulevya kutokana na kushawishiwa na aliyekuwa mpenzi wake.
 
“I broke up with my ex , nikasema kwanza nimtoe huyu mtu aliyeniletea balaa hili. Hata mama yangu mwenyewe aliona mabadiliko. I loved him so much with all my heart, but then I had to let him, ilibidi aende cause yeye ndiye aliyeniletea balaa lote. 

No comments:

Post a Comment