Pages

Thursday, September 12, 2013

AFRICAN STARS "Twanga Pepeta" si kweli Maseneta wa bendi yetu hawatembei na Ma - dancers wetu.

Kupitia page yao ya Facebook Utawala wa Bendi ya AFRICAN STARS "Twanga Pepeta"  wamekanusha yafuatayo.

TAARIFA TOKA ASET. Utawala wa Bendi ya AFRICAN STARS "Twanga Pepeta" unapenda kupinga shutuma zilizotolewa na admin wa Group la CHEZA KIDANSI, Bernard James, kwamba Maseneta wa Twanga Pepeta wana tabia ya kutembea na ma-dancers wa bend (Wacheza Shoo)i. 
Habari hizo ni za udhalilishaji na za upotoshaji.
Hivyo basi tunachukua fursa hii kuwaomba radhi Wadau wetu wakubwa MASENETA kwa kuwa tunaheshimu mchango wao na pia ikumbukwe kuwa hawa ni watu wazima wenye Heshima zao na wana familia zao pia.
 Haipendezi tukaandika vitu vya Kuwadhalilisha watu wazima bila kuwa na Ushahidi. 
Tunaomba kuchukua Fursa hii kutamka kuwa Jambo hilo halina Ukweli na TUNAMTAKA Mtoa taarifa hizo Akanushe au athibitishe kwakuwa MASENETA wetu hawajapendezwa na Jambo hilo la upotoshaji usiofundisha.

No comments:

Post a Comment