MMILIKI WA SALUTI 5 ..AWAPA CHANGAMOTO BLOGGER WA TANZANIA COPY NA PASTE SOMA HAPA.
Said Mdoe ni mmiliki wa Screen Masters na Saluti 5 mtandao wa habari za Burudani siku ya jana Amesema "Niliwahi
kusema hapo kabla, hizi copy na paste za blogs zetu ni balaa.Uzushi
mmoja kwenye blog moja basi utatapakaa kwenye kila blog,mfano mzuri ni
huu wa Penny kuugua na kukimbizwa hospitali eti kisa Diamond karudiana
na Wema mbaya zaidi na picha ya ambulance wameweka, zaidi ya blog 20
zimehusika. Mwenyewe Penny kabaki anashangaa ...uzushi mtupu. Nakumbuka
kuna siku ilitoka taarifa ya Obama kukatisha ziara ya mbuga za wanyama
mtu mmoja akalianzisha akasema Obama afuta ziara ya tanzania mbona
ilikuwa balaa, blog kibao zikaingia mkenge ...badilikeni jamani".
No comments:
Post a Comment