IRENE MWAMFUPE JAMII BLOG TUNAKUTAKIA MWAKA MPYA MWEMA.
Pages
▼
Tuesday, December 31, 2013
HABARI 10 ZA GPL ZILIZOTIKISA MWAKA 2013
1. MSIBANI KWA BABA WEMA... LULU ATOA MITUSI MIZITO

MSANII nyota wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amejikuta akiporomosha mitusi mizito ya nguoni kwenye msiba wa baba wa Miss Tanzania 2006/07, Wema Isaac Sepetu, mzee Isaac Abraham Sepetu hali iliyowafanya baadhi ya waombolezaji kumkodolea macho ya mshangao...
ZAIDI, INGIA HAPA: MSIBANI KWA BABA WEMA... LULU ATOA MITUSI MIZITO
2. ANAYEDAI KUBAKWA NA KAPUYA HUYU HAPA

Stori: Waandishi Wetu
MNYONGE mnyongeni haki yake mpeni, skandali ya kumbaka na
kumwambukiza Ukimwi mwanafunzi, inamtafuna na kumuumiza Mbunge wa Urambo
Magharibi (CCM), Juma Athuman Kapuya. Kuhusu ukweli wa skendo hiyo,
vyombo vya sheria vitazungumza lakini gazeti hili limejiridhisha pasipo
shaka yoyote kuwa denti husika ni tapeli na anacheza rafu ili kumharibia
Kapuya kwa maslahi yake...ZAIDI, INGIA HAPA: ANAYEDAI KUBAKWA NA KAPUYA HUYU HAPA
3. EXCLUSIVE: SIRI 5 ZA WOLPER ZAVUJA

MOYO huhifadhi mengi mazito hasa ya kuumiza! Staa mkubwa wa sinema za Kibongo, Jacqueline Wolper Massawe amejikuta akimwaga machozi wakati akianika siri tano nzito kuhusu mapenzi katika mahojiano (exclusive interview) na Amani kwa takriban saa mbili...
ZAIDI, INGIA HAPA: EXCLUSIVE: SIRI 5 ZA WOLPER ZAVUJA
4. MAINDA: NIMETOA MIMBA YA RAY

Stori: Jelard Lucas
HILI ndiyo Risasi bwana! Sikia, kama ulikuwa hujui ni kwamba msanii mkongwe katika filamu za Kibongo, Ruth Suka ‘Mainda’ ameibuka na kueleza mengi ikiwemo kutoa mimba ya mpenzi wake wa siku nyingi, Vincent Kigosi, tulia hapohapo...
ZAIDI, INGIA HAPA: MAINDA: NIMETOA MIMBA YA RAY
5. UKWELI KUHUSU ASALI NA MDALASINI KAMA TIBA

ZAIDI, INGIA HAPA: UKWELI KUHUSU ASALI NA MDALASINI KAMA TIBA
6. RAY YAMEMKUTA

TUKISEMA staa wa filamu za Bongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ yamemkuta ni sawa, kisa ni ile ishu yake ya kutengeneza filamu inayoitwa Sister Marry ambapo mapadri wamemtaka asiipeleke sokoni milele, Risasi Jumamosi lina mkanda wote. Ishu hiyo ilitokea kwenye kikao kizito cha saa 5 kilichofanyika Jumanne iliyopita katika Ofisi za Utamaduni jijini Dar es Salaam...
ZAIDI, INGIA HAPA: RAY YAMEMKUTA
7. RAY AKONGOROKA

MWIGIZAJI Vincent Kigosi ‘Ray’ amezua hofu kwa ndugu, jamaa, marafiki na mashabiki wake baada ya kukongoroka ghafla akihisiwa anaumwa, Ijumaa Wikienda limemfuatilia hatua kwa hatua...
ZAIDI, INGIA HAPA: RAY AKONGOROKA
8. DENTI ALIYEDAI KUZAA NA DIAMOND... AUMBUKA, ATISHIA KUJIUA

ZAIDI, INGIA HAPA: DENTI ALIYEDAI KUZAA NA DIAMOND... AUMBUKA, ATISHIA KUJIUA
9. BONGO MUVI WAMSUSIA WEMA MSIBA

HUKU akiwa na majonzi ya kuondo-kewa na baba yake mzazi, Balozi Isaac Abraham Sepetu aliyefariki dunia Jumapili iliyopita kwa ugonjwa wa kisukari, baadhi ya wasanii wanaounda Klabu ya Bongo Movie (muvi) Unity wanadaiwa kumsusia msiba mwingizaji mwenzao, Wema Isaac Sepetu...
ZAIDI, INGIA HAPA: BONGO MUVI WAMSUSIA WEMA MSIBA
10. ANASWA

MfanyabiAshara ‘alwatani’ Bongo, mkazi wa jijini Dar, Allain Tajiri amekumbwa na skendo nzito baada ya kufumaniwa na mwanafunzi wa sekondari wa kidato cha pili mwenye umri wa miaka 16. Tukio hilo la kusikitisha lilitokea Jumatano ya Aprili 24, mwaka huu katika chumba namba 107 kwenye gesti iitwayo Jamboz iliyopo Kinondoni jijini Dar...
ZAIDI, INGIA HAPA: ANASWA!
Monday, December 30, 2013
RAIS KIKWETE AMTEUA ERNEST MANGU KUWA MKUU WA JESHI LA POLISI NCHINI
Kamishna wa Polisi Ernest Mangu aliyeteuliwa na Rais Kikwete kuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho
Kikwete leo, Jumatatu, Desemba 30, 2013, amemteua Kamishna wa Polisi
Ernest Mangu kuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini.Taarifa iliyotolewa usiku wa leo na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue inasema kuwa Kamishna Mangu anachukua nafasi ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini anayestaafu, Saidi Mwema.
Kabla ya uteuzi wake unaoanza keshokutwa, Januari Mosi, 2014, Kamishna Mangu alikuwa Mkurugenzi wa Inteligensia ya Jinai (Director of Criminal Intelligence)katika Jeshi hilo la Polisi.
Aidha, taarifa hiyo inasema kuwa Rais Kikwete amemteua Kamishna Abdulrahman Kaniki kuwa Naibu Mkuu wa Jeshi la Polisi, ambayo ni nafasi mpya katika muundo wa sasa wa Jeshi la Polisi.
Kabla ya uteuzi wake, Kamishna Kaniki alikuwa Kamishna wa Uchunguzi wa Kijinai (Commissioner for Forensic Investigations).
Mkuu wa Jeshi la Polisi mpya ataapishwa kesho, Jumanne, Desemba 31, 2013 katika Viwanja vya Ikulu, Dar es Salaam.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
JACK PATRICK ALIVYONASWA NA MADAWA YA KULEVYA CHINA

MADAI ya kukamatwa kwa tuhuma za kumeza madawa ya kulevya aina ya Heroin nchini China kwa msanii, Video Queen na mwanamitindo maarufu Bongo, Jacqueline Patrick, kumeibua maswali ya kila aina, mengi yamesemwa, uvumi umeenea, lakini Ijumaa Wikienda linadondosha hatua kwa hatua.
Jack Patrick.
Baada ya kuinyaka taarifa hiyo ya aibu kwa staa huyo na taifa kwa
jumla, kwa uchungu mkubwa timu yetu imara ilijipanga na kuingia mtaa kwa
mtaa, nyumba kwa nyumba, mtu kwa mtu kuchimbua, kudadavua na kufukunyua
kwa undani zaidi juu ya tuhuma hizo. Aya zinazofuata zitakupa mwanga.
ALIVYONASWA HATUA KWA HATUA
Wikienda lilichorewa mchoro kwamba, Jack alikamatwa Desemba 19, mwaka huu katika Uwanja wa Ndege wa Macau nchini humo akitokea jijini Bangkok nchini Thailand kuelekea Guangzhou, Mji Mkuu wa Jimbo la Guangdong Kusini mwa China.
Wikienda lilichorewa mchoro kwamba, Jack alikamatwa Desemba 19, mwaka huu katika Uwanja wa Ndege wa Macau nchini humo akitokea jijini Bangkok nchini Thailand kuelekea Guangzhou, Mji Mkuu wa Jimbo la Guangdong Kusini mwa China.
NINI KILISABABISHA?
Inadaiwa kuwa miongoni mwa mambo yaliyochangia kunaswa kwake ni uso wa uchovu, kuanza kuwa na hali mbaya ya mwili, kushindwa kujibu maswali vizuri na hati yake ya kusafiria (passport) yake kuonesha kugongwa mihuri ya kuingia nchini humo kila mara.
Inadaiwa kuwa miongoni mwa mambo yaliyochangia kunaswa kwake ni uso wa uchovu, kuanza kuwa na hali mbaya ya mwili, kushindwa kujibu maswali vizuri na hati yake ya kusafiria (passport) yake kuonesha kugongwa mihuri ya kuingia nchini humo kila mara.
Habari zinasema ndipo maafisa wa uwanja huo walipomweka pembeni na
baadaye kumpeleka kwenye chombo cha kukagua kwa undani mwili wa
binadamu, walipojiridhisha ana ‘mzigo’ wakampa polisi mwanamke (WP) kwa
ajili ya kwenda kusimamia utoaji wa kete hizo chooni kwa njia ya haja
kubwa.
AVALISHWA MASKI, AWEKWA MBELE YA MAPAPARAZI
Baada ya kutoka chooni, ikafuata hatua nyingine. Jack aliwekwa mbele ya mapaparazi akiwa amevalishwa maski nyeusi usoni ili asionekane sura kisha akapigwa picha za kumwaga.
Sheria za Macau, mtuhumiwa huvalishwa maski usoni ili watu wasiione sura yake. Kete alizozitoa ziliwekwa juu ya meza, pia simu zake mbili, Iphone na Samsung nyeupe zilikuwa pembeni. Baadhi ya watu Bongo walizitambua simu hizo kwamba ni zake.
Baada ya kutoka chooni, ikafuata hatua nyingine. Jack aliwekwa mbele ya mapaparazi akiwa amevalishwa maski nyeusi usoni ili asionekane sura kisha akapigwa picha za kumwaga.
Sheria za Macau, mtuhumiwa huvalishwa maski usoni ili watu wasiione sura yake. Kete alizozitoa ziliwekwa juu ya meza, pia simu zake mbili, Iphone na Samsung nyeupe zilikuwa pembeni. Baadhi ya watu Bongo walizitambua simu hizo kwamba ni zake.
AINA YA MADAWA
Jack ambaye ni Miss Ilala Namba 3, 2005, alikamatwa na madawa aina ya Heroin yenye uzito wa kilo 1.1 yakiwa na thamani ya zaidi ya shilingi milioni 223 kwa kuhifadhiwa ndani ya kete 57.
Jack ambaye ni Miss Ilala Namba 3, 2005, alikamatwa na madawa aina ya Heroin yenye uzito wa kilo 1.1 yakiwa na thamani ya zaidi ya shilingi milioni 223 kwa kuhifadhiwa ndani ya kete 57.
ATANYONGWA?
Kwa sheria za Beijing, China mtu akithibitika kubeba unga hukumu yake ni kunyongwa tu lakini waandishi wetu walipozungumza na wataalam mbalimbali wa sheria za kimataifa ili kujua ni adhabu gani inaweza kutolewa kwa mrembo huyo endapo atakutwa na hatia, walisema Beijing si Macau, ni vigumu kula kitanzi lakini kwenda jela miaka mitatu, minne au nane inaweza ikamhusu. Majimbo mengi ya China yanaongozwa kwa sheria zake badala ya sheria mama moja kwa nchi nzima.
Kwa sheria za Beijing, China mtu akithibitika kubeba unga hukumu yake ni kunyongwa tu lakini waandishi wetu walipozungumza na wataalam mbalimbali wa sheria za kimataifa ili kujua ni adhabu gani inaweza kutolewa kwa mrembo huyo endapo atakutwa na hatia, walisema Beijing si Macau, ni vigumu kula kitanzi lakini kwenda jela miaka mitatu, minne au nane inaweza ikamhusu. Majimbo mengi ya China yanaongozwa kwa sheria zake badala ya sheria mama moja kwa nchi nzima.
Hata hivyo, sheria za eneo alilokamatiwa zinasema kuwa uwezekano wa
ndugu, jamaa na marafiki kumuona kwa sasa haupo mpaka Machi, 2014
uchunguzi utakapokuwa umekamilika.
WATU WA KARIBU WALIVYOPOKEA TAARIFA
Awali, baadhi ya watu wa karibu na modo huyo waligoma kuweka bayana kuhusu yaliyompata Jack huko ughaibuni wakidai si wasemaje wake na kuwataka mapaparazi kwenda kuchimba kwenye Ubalozi wa China nchini Tanzania.
Awali, baadhi ya watu wa karibu na modo huyo waligoma kuweka bayana kuhusu yaliyompata Jack huko ughaibuni wakidai si wasemaje wake na kuwataka mapaparazi kwenda kuchimba kwenye Ubalozi wa China nchini Tanzania.
Kwa sharti la kutotajwa jina mahali popote kwenye ukurasa huu, mmoja
wa marafiki wa karibu wa Jack aliyeko China kwa masomo, alisema
amethibitisha ukweli kupitia balozi ndogo ya Tanzania nchini humo.
MJAMZITO AJIFUNGULIA KWENYE KOKOTO


Stori: Gordon Kalulunga, Mbeya
MASIKINI! Mama mjamzito aliyetambulika kwa jina la Sabina Mwakyusa (28), mkazi wa Kijiji cha Iwala, Kata ya Utengule Usongwe wilayani Mbalizi mkoani hapa anadaiwa kujifungulia nje kwenye kokoto.

INASIKITISHA
Tukio hilo la kufungia mwaka lilijiri nje ya Hospitali Teule ya Ifisi-Mbalizi hivi karibuni na kusababisha masikitiko makubwa kwa mashuhuda waliodai kuwa ishu hiyo ni kali ya kufungia mwaka 2013.
Akizungumzia tukio hilo muda mfupi baada ya kujifungua, Sabina alisema alifika hospitalini hapo Desemba 18, mwaka huu na alipimwa na manesi ambapo walimwambia kuwa hawamuoni mtoto tumboni mwake.
“Baadaye alikuja daktari na kunipima, akaniambia mtoto anaonekana vizuri na ningejifungua mtoto wa kike ndipo nikaendelea kusubiri uchungu zaidi,’’ alisema kwa masikitiko.

UCHUNGU
Alisema ulipofika usiku wa Desemba 19, mwaka huu, alianza kujisikia uchungu, ndipo manesi waliompima mwanzo wakamwambia anatakiwa apimwe tena, jambo ambalo alikataa kwa madai kuwa alikuwa akiumia.
Alidai alipokataa kupimwa ndipo wakamwambia aondoke hospitalini hapo kwa sababu ana kiburi.
KUMBUKUMBU MBAYA
Mama mzazi wa mwanamke huyo, Roda Mwakyusa (50), alisema anaumia akikumbuka yaliyomkuta mwanaye ikiwa ni uzao wake wa kwanza.
Alidai walipotoka wodini huku mwanaye uchungu ukimzidi, walifika getini akazidiwa na kuanza kujifungua ndipo walinzi wa kampuni ya Mult-Lion, wakamsaidia kumpeleka katika upenu wa duka la hospitali hiyo ili kukwepa kokoto zilizopo na mvua iliyokuwa ikinyesha.

Naye wifi wa Sabina, Prisca Nafred, alisema alimpeleka mtoto aliyezaliwa katika hospitali hiyo saa 7:00 mchana wa Desemba 20, kwa ajili ya chanjo, lakini hakupata chanjo kwa madai kuwa alikuwa amechelewa kufika.
Desemba 21, familia hiyo ilimpigia simu mwandishi wetu na kumueleza kuhusu maendeleo mabaya ya mtoto ambapo mwanahabari wetu alitoa taarifa kwa Mratibu wa Afya ya Mama na Mtoto, Mkoa wa Mbeya, Prisca Butuyuyu ambapo makubaliano yalifikiwa kuwa mtoto apelekwe Hospitali ya Rufaa, Kitengo cha Wazazi Meta.
MTOTO ANAENDELEAJE?
Mtoto huyo alipokelewa Meta na kuingizwa kwenye chumba cha joto kisha kuanza kupatiwa matibabu kwa kuwekewa dripu za maji hadi Desemba 23, mwaka huu hali yake ilipotengemaa na sasa anaendelea vizuri.
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Louis Chomboko, alipopata taarifa, alichukua hatua ya kwenda kumuona mtoto huyo Meta na kuahidi kulifuatilia suala hilo.
JAJI WARIOBA KUILIZA AU KUIPA KICHEKO CCM LEO
Ni rasimu ya pili mfumo wa Muungano.
Nape: Tusubiri tuone kitakachotokea.
Nape: Tusubiri tuone kitakachotokea.
Tume ya Mabadiliko ya Katiba leo itakabidhi kwa Rais wa Jamhuri ya
Muungano, Dk. Jakaya Kikwete na Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed
Shein, rasimu ya pili na ya mwisho ya katiba mpya, huku
Watanzania wengi wakisubiri kwa hamu kubwa kuona inapendekeza muundo
gani wa Muungano baada ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kukataa serikali
tatu.
Kwa mujibu wa Katibu wa Tume hiyo, Assaa Rashidi, hafla ya kukabidhi
rasimu ya pili itafanyika katika viwanja vya Karimjee, jijini Dar es
Salaam.
Hatua hiyo inachukuliwa na Tume hiyo inayoongozwa na Waziri Mkuu
mstaafu, Jaji Joseph Warioba, baada ya kupitia na kuchambua maboresho
yaliyofanywa na mabaraza ya katiba ya wilaya ngazi ya kata kwenye rasimu
ya kwanza ya katiba mpya miezi saba iliyopita.
Rasimu ya kwanza ya katiba mpya, ambayo ilijadiliwa na mabaraza ya
katiba, kuanzia Julai 12 mpaka Septemba 2, ilizinduliwa na Makamu wa
Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal, Juni 4, mwaka huu.
Saturday, December 28, 2013
SNURA AWASHUKURU WALIOMTOA
Kupitia ukurasa wake wa mtandao mmoja wa kijamii mwanadada Snura
mushi alimua kufunguka yafuatao kwa mdada Wema Sepetu, Tundaman,
Chekibudi na Marehemu Sharo Milionea kwa jinsi walivumsaidia kufika hapo
alipo leo. Snura alisema yafuatayo…
Kwa Wema Sepetu
Msema kweli mpenzi wa mungu wakati narecod wimbo wangu wa kwanza wema alihusika sana...hela yake ilihusika studio, sauti yake ilihusika kwenye wimbo huo ambao ni shogaake mama ...vazi langu la show kwa mara ya kwanza wema ndio alinibunia namm nimeliandeleza vazi hilo mpaka leo kwenye show zangu sina chakukulipa wema ila nakushukuru sana nakuombea kwa mungu akubariki zaidi na zaidi wema sepetu...
Kwa Tundaman
Sijui nianzie wapi lakini huyu ndio mtu alie tumia nguvu kuniingiza kwenye muziki baada ya kuona kama siwaelewi hivi kila waliponiambia ....wakati anazindua album yake ya starehe gharama pale maisha aliamua kutengeneza tangazo ambalo lilisema snura atatambulisha wimbo wake mpya kwa mara ya kwanza kiukweli alinivuruga kwasababu mm sikua na wimbo wowote sasa kwa kuhofia aibu nishatangazwa ndio nikalazimika kwenda kurecod shogaake mama haraka sana na nikafanya hiyo show watu wakanielewa sana huo ndio ulikua mwanzo ....leo hii nimeona faida yake asante sana kakaangu tunda man mungu akubariki sana umekua mtu muhim sana kwenye maisha yangu tuendelee kushikana hivihivi kwa shida na raha nakupenda sana kakaangu tunda man captain ...msambinungwa..
Kwa Wema Sepetu
Msema kweli mpenzi wa mungu wakati narecod wimbo wangu wa kwanza wema alihusika sana...hela yake ilihusika studio, sauti yake ilihusika kwenye wimbo huo ambao ni shogaake mama ...vazi langu la show kwa mara ya kwanza wema ndio alinibunia namm nimeliandeleza vazi hilo mpaka leo kwenye show zangu sina chakukulipa wema ila nakushukuru sana nakuombea kwa mungu akubariki zaidi na zaidi wema sepetu...
Kwa Tundaman
Sijui nianzie wapi lakini huyu ndio mtu alie tumia nguvu kuniingiza kwenye muziki baada ya kuona kama siwaelewi hivi kila waliponiambia ....wakati anazindua album yake ya starehe gharama pale maisha aliamua kutengeneza tangazo ambalo lilisema snura atatambulisha wimbo wake mpya kwa mara ya kwanza kiukweli alinivuruga kwasababu mm sikua na wimbo wowote sasa kwa kuhofia aibu nishatangazwa ndio nikalazimika kwenda kurecod shogaake mama haraka sana na nikafanya hiyo show watu wakanielewa sana huo ndio ulikua mwanzo ....leo hii nimeona faida yake asante sana kakaangu tunda man mungu akubariki sana umekua mtu muhim sana kwenye maisha yangu tuendelee kushikana hivihivi kwa shida na raha nakupenda sana kakaangu tunda man captain ...msambinungwa..
DIAMOND, WEMA WATANGAZA NDOA
HUKU mchumba’ke, Penniel Mungilwa ‘Penny’
akifungasha virago kurejea kwao, mzee mzima Nasibu Abdul ‘Diamond
Platnumz’ ametangaza kumuoa Miss Tanzania 2006, Wema Isaac Sepetu
‘Madam’.
Ishu hiyo ilijiri ndani ya Viwanja vya
Leaders Club, Kinondoni jijini Dar ambapo mkali huyo wa Bongo Fleva
alikuwa akikamua kwenye sherehe ya Krismasi aliyoiandaa mwenyewe.
Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ baada ya kupanda jukwaani katika viwanja vya leaders.
TANGAZO LA AWALI
Awali kabla ya kufikia eneo la kutangaza kuoana, Diamond aliweka wazi jukwaani kwamba yeye na Wema wamerudiana.
Diamond Platnumz akiongea jambo baada ya Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ kupanda jukwaani.
Awali kabla ya kufikia eneo la kutangaza kuoana, Diamond aliweka wazi jukwaani kwamba yeye na Wema wamerudiana.
MTIRIRIKO ULIVYOKUWA
Diamond, akiwa ameshika kipaza sauti alikatisha kuimba na kuwauliza mashabiki wake, hasa watoto waliohudhuria kwa wingi tamasha hilo, je, wanataka kumuona shemeji yao?
“Itakuwa si vizuri mkaondoka bila kumuona shemeji yenu, nikuleteeni mumuone?” aliuliza Diamond. Swali hilohilo akalirudia tena ambapo lilipokelewa kwa shangwe huku mashabiki wakilitaja jina la Wema.
Diamond, akiwa ameshika kipaza sauti alikatisha kuimba na kuwauliza mashabiki wake, hasa watoto waliohudhuria kwa wingi tamasha hilo, je, wanataka kumuona shemeji yao?
“Itakuwa si vizuri mkaondoka bila kumuona shemeji yenu, nikuleteeni mumuone?” aliuliza Diamond. Swali hilohilo akalirudia tena ambapo lilipokelewa kwa shangwe huku mashabiki wakilitaja jina la Wema.
FOLENI KUENDELEA KUTESA JIJINI DAR
Kero hiyo itapungua kwa kiasi kikubwa ikiwa fedha hizo zitapatikana ili kutekeleza miradi mbalimbali iliyopewa kipaumbele katika kukabili tatizo hilo.
Uchunguzi uliofanywa na NIPASHE hadi kufikia mwisho wa wiki iliyopita, umebaini kuwa ujenzi wa barabara za pembezoni unaendelea kwa kasi ya kinyonga huku ujenzi wa barabara za juu kwenye makutano ya barabara kuu ukiwa ndiyo kwanza uko katika hatua ya usanifu.
Aidha, jumla ya Sh. bilioni 171.2, ambazo ni sawa na asilimia 14 ya bajeti yote ya Wizara ya Ujenzi kwa mwaka huu wa fedha wa 2013/2014, ni sehemu tu ya mikakati iliyopewa kipaumbele katika utekelezaji ili kupunguza foleni jijini Dar es Salaam ikihusisha usanifu wa barabara za juu (Sh. bilioni 100), ujenzi barabara ya Kigogo – Jangwani (Sh. bilioni 7.6), fidia kwa majengo ya kandoni mwa barabara ya Kigogo-Jangwani (Sh. bilioni 15.8) na kipande cha kilomita tatu cha barabara ya Kimara Korogwe- Kilungule kinachogharimu Sh. bilioni 3.5.
Fedha nyingine ni Sh. bilioni 13 kwa ajili ya kilomita saba za Mbezi Mwisho-Goba, Sh. bilioni 16 za Tangi Bovu-Goba, Baruti-Msewe (Sh. bilioni 4.6) na Kigogo- Tabata Dampo (Sh. bilioni 5.7).
HALI ILIVYO
Hakika, katika jiji la Dar es Salaam kunahitaji uvumilivu wa hali ya juu, hasa kuhusiana na usafiri wa kutoka sehemu moja kwenda nyingine nyakati za asubuhi na jioni.
Kiukweli, unaweza kujikuta usingizi wako ukiathiriwa na jinamizi la foleni. Unalala ukiwaza foleni itakavyokutesa asubuhi wakati ukienda au kurejea kutoka katikati ya jiji kusaka mkate wa kila siku.
96% DARASA LA SABA KUJIUNGA SEKONDARI
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Jumanne Sagini akitangaza wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza 2014 ofisini kwake Dar es Salaam jana. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Tamisemi anayeshughulikia Elimu.
ASILIMIA 96.15 ya wanafunzi wa darasa la saba waliofanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka huu na kufaulu, ndio waliochaguliwa kujiunga na sekondari za serikali.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu –TAMISEMI, Jumanne Sagini aliwaambia waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kwamba jumla ya wanafunzi 411,127 kati ya 427,609 waliofaulu mtihani huo ndio watakaoanza kidato cha kwanza mwakani.
Alisema wasichana ni 201,021 na wavulana 210,106 na kwamba waliochaguliwa wameongezeka kwa asilimia 31.37 ikilinganishwa na asilimia 64.78 waliochaguliwa awamu ya kwanza mwaka huu.
Kwa mujibu wa matokeo ya mtihani mwaka huu, alama ya juu kabisa kwa wavulana ilikuwa 244 huku ya wasichana ikiwa ni 241 kati ya alama 250 ambapo mwaka jana alama ya juu ilikuwa 237.
“Matokeo yanaonesha kuwa jumla ya wanafunzi 427,609 (wavulana 218,093 na wasichana 209.516) walifaulu kwa kupata alama A-C kati ya 844,938 waliofanya mtihani ikiwa ni sawa na asilimia 50.61 … takwimu zinaonesha ongezeko la asilimia 19 la ufaulu ikilinganishwa na asilimia 30.6 mwaka jana,” alisema Sagini.
Friday, December 27, 2013
SNURA, MAJANGA HADI MWILINI?
KWA wasiomfahamu msichana huyu,
wanamuona kama chipukizi aliyeukwaa ustaa ghafla, lakini wanaofuatilia
mambo ya sanaa na burudani, wanamfahamu kitambo. Ninamzungumzia Snura
Mushi, ambaye anatamba sana na kibao chake cha Majanga.
Ni
mmoja kati ya wasanii wapambanaji, wakisaka mafanikio kwa kujaribu kila
aina ya njia. Amejaribu kwa muda mrefu katika filamu, lakini hakuweza
kufanikiwa ‘kuchomoka’. Kama angetambua tokea mapema kuwa angeweza
kuibuka mara moja katika muziki, nadhani asingepoteza muda wake mwingi
kwenye filamu.
Wimbo wake wa Majanga umeiteka familia ya muziki wa mduara, huenda
kwa sasa ni mmoja kati ya wasanii wachache wanaopata nafasi ya kutakiwa
sana katika majukwaa na hivyo kumfanya pia awe anapata hela za kutosha.
JACK PATRICK ADAIWA KUNASWA NA PIPI 66 ZA DAWA ZA KULEVYA ZENYE THAMANI YA MIL 215.5 CHINA




Inadaiwa kuwa Jack alikuwa akisafiri kutoka Thailand akielekea Macao Jumanne ya Desemba 19, 2013. Aliwaambia polisi kuwa alikuwa anaelekea Guangzhou ambao ni mji wa jimbo la Guangdong huko China.
Jack alipata jina aliposhika namba tatu kwenye Miss Ilala na kushiriki Miss Tanzania mwaka 2005/06. Pia uliuza nyago kwenye video ya mwanamuziki wa Bongo Fleva, Marehemu Albert Magwea ‘Ngwair’ iliyokwenda kwa jina la She Got A Gwain. Kuanzia hapo jina likawa kubwa na akawa mwanamitindo maarufu Bongo.
Ni katika kipindi hicho cha umaarufu akaolewa na mtoto wa aliyekuwa mwanasiasa mkongwe, Abdallah Fundikira, Abdulatif kabla ya jamaa huyo kutupwa nyuma ya nondo za mahabusu ya Keko, Dar akikabiliwa na msala wa kusafirisha mihadarati.