Pages

Thursday, February 27, 2014

LULU AANIKA MCHECHETO KIZIMBANI

STAA wa sinema za Kibongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amefunguka kuwa siku alipokuwa mahakamani akisomewa kesi inayomkabili ya kumuua bila kukusudia msanii mwenzake, marehemu Steven Kanumba, alipata mchecheto sana.
Elizabeth Michael 'Lulu'.
Akipiga stori na paparazi wetu alisema, siku hiyo wakati kesi ikiendelea, alipata mchecheto kiaina na kujikuta ghafla akiwaza juu ya hatima yake hivyo kuangukia katika lindi la hofu.
“Daah! Nilipata mchecheto ghafla hata sijui kwa nini, nilivuta picha ya mbali sana na kujikuta nikijiuliza maswali mengi yasiyokuwa na majibu,” alisema.
Msanii huyo alisomewa shitaka lake hilo Februari 17, mwaka huu kwenye Mahakama Kuu, jijini Dar, kesi hiyo iliahirishwa hadi itakapotajwa tena baada ya msanii huyo kujibu maswali ya kweli au si kweli.

No comments:

Post a Comment