Pages
▼
Monday, March 31, 2014
ROSE NDAUKA: SIWEZI KUZEEKA
STAA wa filamu Bongo, Rose Ndauka amesema licha ya kujifungua, kamwe hawezi kuzeeka kama wengi wanavyomtafsiri.
Rose alisema, kwa upande wake hata siku moja hawezi kumuunga mkono mtu anayesema kuzaa au kulea kunamfanya mtu azeeke kwani inategemea na jinsi mtu anavyojiweka.
Rose alisema, kwa upande wake hata siku moja hawezi kumuunga mkono mtu anayesema kuzaa au kulea kunamfanya mtu azeeke kwani inategemea na jinsi mtu anavyojiweka.
Staa wa filamu Bongo, Rose Ndauka.
“Nawashangaa hata wasanii wasiotaka kuzaa wakiona kama watakuwa
wamemaliza ujana wao, asikwambie mtu hamna kitu kizuri kama kuitwa mama,
nimejitunza na nimezidi kuwa mrembo hata baada ya kuzaa,” alisema Rose.DIAMOND ATAMANI USHOGA!..BAADA YA KUTAJIRIKA, FEDHA ZAMCHANGANYA SASA

ILIVYOKUWA
Hivi karibuni, Diamond alinaswa akiwa amevaa wigi hilo kichwani kisha kupiga nalo picha huku Wema akilitafuta ili alitinge bila mafanikio.
Habari zilieleza kuwa baada ya Wema kutoka nje akiendelea kulitafuta wigi hilo, alipigwa na butwaa kumkuta Diamond amelivaa, tena akionekana kuwa na amani.
WEMA AMWANIKA
“Jamani nimetafuta wigi langu muda mrefu sijaliona, nashangaa namkuta baby wangu (Diamond) amelivaa, lakini limempendezaje?” aliandika Wema kwenye ukurasa wake wa Instagram uliotembelewa na watu kibao.
MWANAMKE BORA WA MWAKA NI MAMA KAMM

Stori: Mwandishi wetu, Dodoma
Pongezi! Waziri Mkuu wa Tanzania, Mizengo Pinda juzi Jumamosi alikabidhi Tuzo ya Mwanamke Bora wa Mwaka (A Woman of the Year Award- 2013/14) mjini hapa.
Katika kinyang’anyiro hicho, Dk. Maria Kamm, ambaye kitaaluma ni mwalimu, aliibuka kidedea na kunyakua tuzo hiyo, medali pamoja na hundi ya shilingi milioni 5.
Wengine walionyakua tuzo hizo (bila medali) ni pamoja na Waziri wa Sheria na Katiba, Dk. Asha Rose Migiro (aliwakilishwa na Anna Abdalah), Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka na Mbunge wa Same Mashariki, Mheshimiwa Anne Kilango Malecela.Sunday, March 30, 2014
WAZIRI MKUU PINDA AKABIDHI TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14, DK KAMM AIBUKA SHUJAA
(PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS / GPL, DODOMA)
SIKILIZA WAWAKILISHI WA WANANCHI WAKIONGELEA KUHUSIANA NA SAKATA LA UJENZI WA MJI MPYA KIGAMBONI
WANAFUNZI WA UDOM MWAKA WA MWISHO, WAAHIDI KUJIUNGA NA PPF
Meneja
Uhusiano na Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Lulu Mengele, akitoa
mada kuhusiana na huduma mbalimbali zitolewazo na Mfuko huo kwenye
semina iliyoandaliwa na Mfuko huo kwa wanafunzi wa mwaka wa mwisho Chuo
Kikuu cha Dodoma (UDOM), ambapo zaidi ya wanafunzi 500 walihudhuria
semina hiyo Jumamosi Machi 29, 2014.
Baadhi
ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM), wakifuatilia mada kutoka
kwa Meneja Uhusiano na Masoko wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, Lulu Mengele.
Saturday, March 29, 2014
KATIBA MPYA NA WANAWAKE!
"Ikipatikana Katiba yenye usawa wa kijinsia, tatizo la wanawake
wanaojiuza litakwisha!" Hayo ni maneno ya mwanamke mpiganaji Bi Sophia
Jonas alipozungumza na Super Woman Joyce Kiria kupitia kipindi cha
Wanawake Live kinachorushwa na EATV kila Jumanne saa tatu kamili usiku.
WANANCHI WA MJI KOROGWE WAUPOKEA KWA KISHINDO MPANGO WA TIKA, WACHANGIA MIL. 1.3
Mkuu
wa Mkoa wa Tanga, Chiku Galawa akifungua mkutano wa siku ya wadau wa
Mfumo wa Afya ya Jamii Mijini wa Tiba kwa Kadi (TIKA) ambapo Lengo la
mkutano huo ilikuwa ni kuchukua maoni yao na kuwaeleza jinsi TIKA
inavyofanya kazi. Kikao hicho kimefanyika leo Machi 28, 2014 katika
ukumbi wa Halmashauri ya Mji wa Korogwe. Pembeni ni Mkuu wa Wilaya ya
Korogwe, Mheshimiwa Mrisho Gambo (kushoto) na Mwenyekiti wa Hamashauri
ya Mji Korogwe ambaye ni Diwani wa Kata ya Kilole, Mheshimiwa Angello
Bendera (kulia).
Mkuu
wa Wilaya ya Korogwe, Mheshimiwa Mrisho Gambo akitoa ufafanuzi wa jambo
mbele ya mkuu wa Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Galawa (kushoto). Pembeni
ni Diwani wa Kata ya Mgombezi ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu,
Afya, Maji na Uchumi, Mheshimiwa Omari Chafesi na Meneja wa Mfuko wa
Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) – Mkoa wa Tanga, Bw. Ally Mwakababu
(kushoto).
Meneja
wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) – Mkoa wa Tanga, Bw. Ally
Mwakababu akieleza umuhimu wa matumizi ya Tiba kwa Kadi (TIKA) mbele ya
mkuu wa mkoa wa Tanga.
TRENI YA MIZIGO YAPATA AJALI ENEO LA GULWE WILAYA YA MPWAPWA
Friday, March 28, 2014
WAZIRI MKUU AONGOZA MAMIA KUAGA MWILI WA MAREHEMU TUPPA
Viongozi
Dini wakiongoza ibada ya kuuaga mwili wa Marehemu John Gabriel Tupa
aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara na hapo awali aliwahi kuwa Mkuu wa Wilaya
ya Dodoma,aliefariki ghafa siku kadhaa zilizopita.
Waziri
Mkuu,Mh. Mizengo Pinda akitoa heshima za mwisho kwa Mwili wa Marehemu
John Gabriel Tupa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara na hapo awali aliwahi
kuwa Mkuu wa Wilaya ya Dodoma,aliefariki ghafa siku kadhaa zilizopita.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar,Balozi Seif Ali Idd akitoa heshima za mwisho kwa Mwili wa Marehemu John Gabriel Tupa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara.
Waziri Mkuu Mstaafu,Mh. Edward Lowassa akitoa heshima za mwisho kwa Mwili wa Marehemu John Gabriel Tupa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara.
Tambwe atangaza kuondoka Simba
STRAIKA wa
kimataifa wa Simba, Amissi Tambwe huenda akavunja mkataba wake na klabu
hiyo na kuondoka zake mara baada ya kumalizika kwa msimu huu, ikiwa
timu hiyo haitapata nafasi ya kuwakilisha taifa kwenye mashindano ya
kimataifa.

Simba ipo katika nafasi ya nne na haina matumaini ya kushika nafasi ya kwanza wala ya pili kwa kuwa imesaliwa na michezo minne, ambapo imezidiwa pointi 10 na Yanga inayoshika nafasi ya pili.
Akizungumza na Championi Ijumaa, Tambwe, raia wa Burundi alisema hatma yake ya kuendelea kubakia Simba itajulikana baada ya kumalizika kwa ligi ya msimu huu ambayo ipo katika hatua za lala salama.
Alisema anaweza kuondoka au asiondoke Simba lakini alisisitiza kuwa kila kitu kitajulikana baada ya Aprili 19 ambapo ligi itakuwa inafikia tamati.

“Wakati najiunga Simba, matarajio yangu yalikuwa ni kushiriki mashindano ya kimataifa, lakini ndoto hizo zinaonekana kugonga mwamba kutokana kwa kuwa hivi sasa timu yetu ipo kwenye nafasi mbaya ambayo haitupi kabisa matumaini ya kumaliza ligi tukiwa kwenye nafasi mbili za juu ambazo kwa sasa zinashikiliwa na Azam na Yanga.
“Kusema kweli hali hiyo inasikitisha na inaniumiza sana kwani natamani kushiriki mashindano ya kimataifa kama walivyo wachezaji wote wanaotaka mafanikio katika mchezo wa soka.
“Hata hivyo kwa sasa siwezi kuzungumza lolote kama nitaendelea kubakia Simba au la ila hilo litajulikana baadaye baada ya kumalizika kwa ligi kuu, lakini nafikiri juu ya hilo,” alisema Tambwe.
Simba ina pointi 36 nyuma ya Mbeya City yenye pointi 42, Yanga yenye ponti 46 na Azam inayoongoza msimamo ikiwa na pointi 50.
Wakati huohuo, Tambwe amesema kama atapata nafasi ya kucheza kwenye mechi dhidi ya Azam katika ligi kuu keshokutwa kwenye Uwanja wa Taifa, atapambana ili kuhakikisha Azam inafungika.
“Azam ni timu tu kama timu nyingine, naiheshimu kutokana na ubora wake, tutahakikisha tunaivunja rekodi yao ya kutofungwa msimu huu,” alisema Tambwe.
Mshambuliaji wa Simba, Amisi Tambwe (kushoto) wakishangilia moja ya bao katika Ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Tambwe ambaye ndiye kinara wa mabao katika Ligi Kuu Bara akiwa na
mabao 19, amesema kuwa matarajio yake wakati anajiunga na klabu hiyo
yalikuwa ni kuiona ikishiriki mashindano ya kimataifa, hivyo kukosa
kushiriki michuano hiyo kutamtibulia mipango yake na ametamka wazi
anafikiria kuondoka klabuni hapo.Simba ipo katika nafasi ya nne na haina matumaini ya kushika nafasi ya kwanza wala ya pili kwa kuwa imesaliwa na michezo minne, ambapo imezidiwa pointi 10 na Yanga inayoshika nafasi ya pili.
Akizungumza na Championi Ijumaa, Tambwe, raia wa Burundi alisema hatma yake ya kuendelea kubakia Simba itajulikana baada ya kumalizika kwa ligi ya msimu huu ambayo ipo katika hatua za lala salama.
Alisema anaweza kuondoka au asiondoke Simba lakini alisisitiza kuwa kila kitu kitajulikana baada ya Aprili 19 ambapo ligi itakuwa inafikia tamati.
“Wakati najiunga Simba, matarajio yangu yalikuwa ni kushiriki mashindano ya kimataifa, lakini ndoto hizo zinaonekana kugonga mwamba kutokana kwa kuwa hivi sasa timu yetu ipo kwenye nafasi mbaya ambayo haitupi kabisa matumaini ya kumaliza ligi tukiwa kwenye nafasi mbili za juu ambazo kwa sasa zinashikiliwa na Azam na Yanga.
“Kusema kweli hali hiyo inasikitisha na inaniumiza sana kwani natamani kushiriki mashindano ya kimataifa kama walivyo wachezaji wote wanaotaka mafanikio katika mchezo wa soka.
“Hata hivyo kwa sasa siwezi kuzungumza lolote kama nitaendelea kubakia Simba au la ila hilo litajulikana baadaye baada ya kumalizika kwa ligi kuu, lakini nafikiri juu ya hilo,” alisema Tambwe.
Simba ina pointi 36 nyuma ya Mbeya City yenye pointi 42, Yanga yenye ponti 46 na Azam inayoongoza msimamo ikiwa na pointi 50.
Wakati huohuo, Tambwe amesema kama atapata nafasi ya kucheza kwenye mechi dhidi ya Azam katika ligi kuu keshokutwa kwenye Uwanja wa Taifa, atapambana ili kuhakikisha Azam inafungika.
“Azam ni timu tu kama timu nyingine, naiheshimu kutokana na ubora wake, tutahakikisha tunaivunja rekodi yao ya kutofungwa msimu huu,” alisema Tambwe.
CHANZO CHAMPIONI IJUMAA
WENGI WAMPA UBUNGE RIDHIWANI CHALINZE
WANANCHI wa vijiji kadhaa vilivyomo katika Jimbo la Chalinze, ambalo Aprili 6, mwaka huu litafanya uchaguzi mdogo wa Ubunge, wamempa nafasi kubwa ya kuibuka mshindi mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
