Mtu mmoja anayejulikana kwa jina la Hamidu Hussein Matimbuka mkazi wa Kinyerezi jijini Dar es Salaam amekutwa hospitali ya Palestina Sinza akiwa na hali mbaya mno akiwa amelala chini bila matibabu yoyote baada ya kuporwa pikipiki na kukatwakatwa na mapanga na watu wasiojulikana!
Chakushangaza madaktari wa hospitali hiyo walionekana wakilandalanda kila kona bila kumsaidia mgonjwa!
Katika hali ya kushangaza zaidi mgonjwa mwingine aliyefika kutibiwa ndiye alionekana kumsaidia kunfunika kanga mgonjwa ambaye kwa wakati huo alikuwa akitetemeka sana kwa baridi huku damu zimemganda mwilini.
No comments:
Post a Comment