Pages

Monday, May 26, 2014

Yanga SC yambakiza Chuji

UONGOZI wa Yanga umesema haujamuacha kiungo mkabaji, Athumani Idd ‘Chuji’.
Hiyo ni siku chache tangu kuwepo kwa taarifa za kiungo huyo kuachwa.
Akizungumza na Championi Jumatatu, Katibu Mkuu wa Yanga, Beno Njovu, alisema Chuji bado ni mchezaji wao mwenye mkataba wa kuichezea timu hiyo.
Njovu alisema hadi hivi sasa, hakuna mchezaji yeyote watakayemuacha kwa wale wote wenye mikataba mirefu ya kuendelea kuichezea Yanga.
“Hizo zote zinazozungumzwa ni tetesi na siyo habari rasmi kutoka kwa viongozi, Yanga haina mpango wa kumuacha mchezaji yeyote mwenye mkataba na Yanga.
“Yanga hivi sasa ipo kwenye mazungumzo na baadhi ya wachezaji kwa ajili ya kuwasajili kwenye msimu ujao, ninaamini yakiendelea vizuri haraka tutawasajili,” alisema Njovu.                                     

No comments:

Post a Comment