Pages

Monday, October 27, 2014

JULIETH: JAMANI SIJAWAHI KUZAA

AKANUSHA! Baada ya tetesi kuzagaa kuwa aliyekuwa Miss Progress International, Julieth William kuwa ana mtoto mchanga, mwenyewe ameibuka na kufunguka kwamba habari hizo ni za kizushi.
Miss Progress International, Julieth William.
Akipiga stori na paparazi wetu, Julieth alisema anashangazwa na maneno hayo ya watu kwamba ana mtoto wakati hajawahi kuzaa hivyo anaumizwa sana na tetesi hizo.

Miss Progress International, Julieth William wakati wa kutwaa taji.
“Sijawahi kuzaa jamani nawashangaa wanaoeneza habari kwamba nina mtoto, mara nyingi nakuwa na watoto wa ndugu zangu hata hivi karibuni nilikuwa na mtoto mchanga maeneo ya Mlimani City, naumizwa sana na habari hizi za uongo,”alisema Julieth.

No comments:

Post a Comment