Na Shani Ramadhani
IMEVUJA!
Mwimba Injili mwenye kasi ya juu, Madam Ruth anadaiwa kuwa ndiye mshenga
katika lile sakata la mume wa staa wa nyimbo hizo Bongo ambaye
wametengana, Bahati Bukuku, Daniel Basila kutaka kufunga ndoa na mwimba
Injili mwingine, Elizabeth Ngaiza ‘Lizy’.
Kwa mujibu wa chanzo cha ndani, Madam Ruth ambaye anatamba na albamu
za Jana Imepita na Kesho Yako Inakuja, anadaiwa kuwa ndiye kiunganishi
cha uhusiano wa Lizy na Basila.
“Elizabeth na Basila walikutana kwa sababu ya Madam Ruth, yeye ndiye
kama mshenga. Ndiyo maana wawili hao wakakaa na kuamua kufanya
maandalizi ya kufunga ndoa,” kilisema chanzo.
Amani lilimsaka Madam Ruth kwa njia ya simu ili kutaka kujua ukweli
wa madai hayo, alipopatikana alicheka na kumtaka mwandishi wetu
kumuuliza habari za utumishi wake kwa Mungu badala ya uhusiano wa mtu na
mtu.
“Niulize kuhusu kazi zangu za kumtumikia Mungu, si uhusiano wa mtu na mtu,” alisema.
Hivi karibuni, gazeti hili liliwahi kuripoti kwamba, Lizy na Basila
walikuwa mbioni kufunga ndoa baada ya ile ya kwanza na Bahati kufeli
safarini. Basila alikanusha, Elizabeth yeye alitaka kumjua aliyetoa
habari hiyo Global bila kusema kweli au si kweli.
No comments:
Post a Comment