Pages

Thursday, April 23, 2015

MAYA: MIMI SIYO MGUMBA

MSANII mkongwe kwenye gemu la filamu Bongo, Mayasa Mrisho ‘Maya’ amefunguka kwamba siyo mgumba wala hana gundu ila ni muda tu haujafika wa kuzaa au kuolewa.
Maya aliyasema hayo kutokana na maneno ya watu wanaomuandama kwamba hazai na ana gundu ndiyo maana haolewi ambapo alisema siyo kweli ila anasubiri wakati ukifika atazaa kwani ana uzazi na hajawahi kutafuta mtoto na kumkosa.
“Bado sijapata mwanaume wa kunioa na sina gundu, kuzaa bado wakati haujafika ila ukifika naamini Mungu atanipatia maana mayai ya uzazi ninayo ya kutosha,” alisema Maya.

No comments:

Post a Comment