Pages

Monday, June 29, 2015

KONGAMANO LA SDG’s LAFANYIKA KWA MAFANIKIO DODOMA‏

IMG_4628
Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Taasisi Huru ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF), Dk. Tausi Kida, akitoa maelezo ya kongamano kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kulifungua kongamano kubwa la siku mbili la kujadili namna taifa linavyojiandaa kutekeleza malengo mapya ya Maendeleo endelevu (SDGs) limefanyika mwishoni mwa wiki mjini Dodoma ambalo liliandaliwa na taasisi yake.
IMG_4606 IMG_4729
Kamishna wa Fedha za Nje wa Wizara ya Fedha, Ngosha Magonya akisoma hotuba ya ufunguzi wa kongamano hilo kwa niaba ya mgeni rasmi Katibu Mkuu wa wizara hiyo katika hoteli ya St. Gasper mwishoni mwa wiki mjini Dodoma.
IMG_4678
Mtaalamu wa masuala ya uchumi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Dar es salaam, Rogers Dhliwayo akitoa salamu za Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) wakati wa kongamano hilo la siku mbili la kujadili namna taifa linavyojiandaa kutekeleza malengo mapya ya Maendeleo endelevu (SDGs) lililofanyika mwishoni mwa wiki mjini Dodoma.
IMG_4949
Afisa Mwandamizi wa uhamasishaji na uwekezaji kutoka kituo cha uwekezaji nchini (TIC), Lilian Mwamdanga akishiriki kuchangia maoni wakati kongamano kubwa la siku mbili la kujadili namna taifa linavyojiandaa kutekeleza malengo mapya ya Maendeleo endelevu (SDGs) limefanyika mwishoni mwa wiki mjini Dodoma.
IMG_5015
Naibu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP)- Programme, Amon Manyama akichangia maoni wakati wa kongamano kubwa la siku mbili la kujadili namna taifa linavyojiandaa kutekeleza malengo mapya ya Maendeleo endelevu (SDGs) limefanyika mwishoni mwa wiki mjini Dodoma.
IMG_4801
Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Taasisi Huru ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF), Dk. Tausi Kida na Kamishna Mipango wa Tume ya Mipango Zanzibar, Ahmed Makame Haji wakifuatilia kwa umakini maoni mbalimbali ya wadau yaliyokuwa yakitolewa kwenye kongamano hilo.
IMG_4739
Pichani juu na chini ni washiriki kutoka Tanzania bara na visiwani walioshiriki kongamano hilo la siku mbili ambalo liliandaliwa na taasisi ya ESRF.
IMG_4702
IMG_4756

Naibu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP)- Programme, Amon Manyama (kushoto) akizungumza jambo na Kamishna wa Fedha za Nje wa Wizara ya Fedha, Ngosha Magonya ambaye amemwakilisha mgeni rasmi Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha (wa pili kushoto) wakati akiondoka katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Saint Gasper mjini Dodoma mara baada ya kufungua kongamano kubwa la siku mbili la kujadili namna taifa linavyojiandaa kutekeleza malengo mapya ya Maendeleo endelevu (SDG's) lililofanyika mwishoni mwa wiki mjini Dodoma. Wengine katika picha kutoka kulia ni Kamishna Mipango wa Tume ya Mipango Zanzibar, Ahmed Makame Haji, Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Taasisi Huru ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF), Dk. Tausi Kida pamoja na Mtaalamu wa masuala ya uchumi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Dar es salaam, Rogers Dhliwayo.
IMG_4778
Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Taasisi Huru ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF), Dk. Tausi Kida (kushoto) akimsindikiza Kamishna wa Fedha za Nje wa Wizara ya Fedha, Ngosha Magonya ambaye alimwakilisha mgeni rasmi Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha mara baada ya kufungua kongamano kubwa la siku mbili la kujadili namna taifa linavyojiandaa kutekeleza malengo mapya ya Maendeleo endelevu (SDGs) limefanyika mwishoni mwa wiki mjini Dodoma.
IMG_5066
Picha ya pamoja ya washiriki.

No comments:

Post a Comment