Pages

Friday, June 26, 2015

NDOA YANGU NA NUHU ZIMEBAKI SIKU CHACHE TU – SHILOLE

3d99b__hhhklMwanamuziki wa mduara, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ akiwa na mpenzi wake Nuh Mziwanda.
Mpenzi msomaji tunakutana tena katika safu hii ambapo mastaa mbalimbali hujibu maswali kumi kikamilifu, leo tunaye mwanamuziki wa mduara, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ ambaye amefunguka mambo mengi alipokuwa akizungumza na Mwandishi Wetu IMELDA MTEMA. Ili kujua aliyoyasema endelea kusoma.
Ijumaa: Vipi kuhusu sakata lako la nguo kukuvuka ukiwa jukwaani limekuathiri kivipi?
Shilole: Halijaniathiri chochote hiyo ni kama mtu anapata ajali akiwa kazini.
Ijumaa: Wakati zile picha zilipokuwa zikisambazwa katika mitandao ya kijamii, mpenzi wako Nuhu alilizungumziaje hilo?
shiloleNUH 
Shilole: Hakuzungumza chochote kwani tulikuwa pamoja siku ya tukio hivyo anajua nini kilitokea.
Ijumaa: Najua una wakwe, je, walipoziona hizo picha hawakumsumbua Nuhu na kuona kama unawadhalilisha?

Shilole: Hapana, tena walikuwa upande wangu sana na kuniambia nisijali.
Ijumaa: Nini ulichojifunza kupitia tukio hilo?
Shilole: Nimejifunza vitu vingi sana, siwezi kufanya shoo bila kupima nguo yangu vizuri.
Ijumaa: Vipi kuhusu ishu ya kumpiga mwanamke aliyedai ana mimba ya Nuhu?
Shilole: Hiyo ishu siyo ya kweli hata kidogo kwa sababu alikiri kuwa alitumwa ili aharibu mapenzi yetu.
Ijumaa: Vipi kuhusu tamko la Basata kutokana na nguo kukuvuka jukwaani?
Shilole: Hamna shida, kwa sasa nimeshamalizana nao.
Ijumaa: Suala lako la nguo kukuvuka lilizungumziwa mpaka bungeni, vipi ulijisikiaje viongozi wa nchi kukujadili kwa suala kama hilo?
Shilole: Kwanza nilifarijika sana na kuona hata viongozi wanafuatilia kazi zangu na wanatambua mchango wangu ndiyo maana waliweza kuongelea ishu hiyo.
Ijumaa: Mumevalispete ya uchumba kitambo sasa, vipi kuhusu ndoa? Maana uchumba hautakiwi kuwa wa muda mrefu.
Shilole: Ndoa inakuja soon, zimebaki siku chache sana tunaweka mambo sawa utaishuhudia tu.
Ijumaa: Wewe tayari una watoto wawili, vipi Nuhu analichukuliaje hilo?
Shilole: Hana neno kwa kuwa ananijua historia yangu kabla hatujawa wapenzi na anawapenda sana watoto wangu.
Ijumaa: Vipi kuhusu kuzaa na Nuhu?
Shilole: Yaani mimba ikiingia ni sawa kwa sababu hatutumii

No comments:

Post a Comment