Pages

Thursday, July 2, 2015

FARHIA MIDDLE AKIRI KULIZWA NA MAPENZI

Mtangazaji wa ITV / Radio One, Farhia Middle.
Brighton Masalu
MTANGAZAJI wa ITV / Radio One, Farhia Middle amesema tangu aujue ulimwengu wa mapenzi hajawahi kukutana na mwanaume mwaminifu na kwamba kila mara amekuwa akilizwa na mapenzi jambo ambalo husababisha kujiona mwenye mkosi.
Akipiga stori na gazeti hili hivi karibuni, mtangazaji huyo alisema licha ya baadhi ya watu kumsifia kuwa ni mrembo kwa sura na umbo, lakini amekuwa akikutana na balaa la kuumizwa na mapenzi kwa kusalitiwa ama kunyanyaswa na wanaume.

“Yaani huwezi amini, wakati mwingine huwa najiuliza kwa nini mimi? Mbona kila mwanaume ninayempata sidumu naye. Kama siyo msaliti basi ni yule mwenye mfumo dume na hulka za kunyanyasa. Najiona kama nina mkosi,” alisema Farhia.

No comments:

Post a Comment