Pages

Thursday, November 29, 2012

MASELE CHA POMBE NAE ‘AMKACHA’ SHARO MILIONEA …ZE COMEDY, ORIJINO KOMEDI NAO HAWAJAONEKANA MAZISHINI.

MCHEKESHAJI Chrispin Masele “Masele cha pombe”, jana alikuwa ni miongoni mwa sura chache zilizokosekana kwenye mazishi ya Sharo Milionea.
Masele ambaye ni msanii wa Al Riyami Production (mabosi wa zamani wa Sharo), ni mmoja kati ya wasanii waliofanya kazi nyingi na kwa ukaribu sana na Sharo Milionea.
Wasanii wa Al Riyami waliiambia Saluti5 kuwa Masele yuko safarini Dodoma pamoja na Mkurugenzi wao Khalfan Abdallah.
Wasanii wengine wa vichekesho walioshindwa kuhudhuria mazishi ya Sharo, hususan wale ambao vituo vyao vya kazi ni Dar se Salaam ni pamoja na Ze Comedy (EATV) na Orijino Komedi (TBC1).
Ukiondoa wasanii hao, karibu wasanii wote wa sanaa za maigizo sambamba na wale Bongo Fleva, walihudhuria mazishi ya kihistoia ya Sharo Milionea.Via saluti5

No comments:

Post a Comment