Mkoani
Geita Mtoto ambaye jina lake limehifadhiwa mwenye umri wa miaka 9
anaishi na Bibi yake baada ya wazazi kutengana amefanyiwa kitendo cha
kikatili na cha udhalilishaji kwa kubakwa na mjomba wake na akimaliza
kumbaka humwita rafiki yake ambaye nae humbaka wakati huo huo.
Mtoto huyo ambaye ni mwanafunzi wa darasa pili katika shule ya msingi
Geita amesema amekuwa akifanyiwa vitendo hivyo mara kwa mara kabla ya
kwenda shule licha ya kukataa mjomba wake humpiga na hata alipotoa
taarifa kwa bibi,bibi alimwita na kumkanya kuacha lakini kijana huyo
aliendelea kumbaka.
Tatizo la mtoto huyo limejulika
shuleni hasa baada ya kuwa anachelewa shule na maendeleo kuwa mabaya
huku wakati mwingi akitumia kwenda msalani kujisaidia hali iliyowalazimu
waalimu kumuhoji na ndipo kugundua unyama huo.
No comments:
Post a Comment