Pages

Thursday, March 28, 2013

BREAKING NEWS. ALIEKUA MBUNGE WA JIMBO LA CHAMBANI AFARIKI DUNIA LEO

ALIEKUA MBUNGE WA JIMBO LA CHAMBANI AMEFARIKI DUNIA LEO BAADA YA KUZIDIWA ALIPOANGUKA KATIKA VIKAO VYA BUNGGE,HABARI KAMILI ZITAFUATE BADO UONGOZI WA CHOMBO HICHI UNAFATILIA KUJUA ZAIDI KUHUSU KIFO HICHO.

SIKU YA JANA..
MBUNGE wa Chambani, Salim Hemed Khamis (CUF), jana alianguka ghafla katika mkutano wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Salim alianguka saa tano asubuhi wakati akihudhuria mkutano wa kamati hiyo, uliokuwa ukifanyika katika ofisi ndogo za Bunge, jijini Dar es Salaam.

Tukio hilo lilizua hofu kwa wabunge wengine waliokuwamo, ambapo mkutano huo ulisitishwa kwa muda na juhudi za kumshughulikia zilianza, kwani alitolewa nje ya ukumbi na kuanza kupepewa.

Hata hivyo mbunge huyo alikimbizwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili na kuingizwa katika kitengo cha wagonjwa mahututi (ICU) kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

Mwenyekiti wa kamati hiyo, Edward Lowassa, alilazimika kutoka nje ya ukumbi ambapo aliungana na wenzake katika kuchanga mawazo kuhusu namna ya kumpeleka hospitali mbunge huyo.

Wakati majadiliano hayo yakiendelea, hali ya mbunge huyo anayedaiwa kuwa anasumbuliwa na shinikizo la damu iliendelea kubadilika, huku akitokwa na jasho jingi.

Habari kuwajia baadae..

No comments:

Post a Comment