ALIEKUA MBUNGE WA JIMBO LA CHAMBANI AMEFARIKI
DUNIA LEO BAADA YA KUZIDIWA ALIPOANGUKA KATIKA VIKAO VYA BUNGGE,HABARI
KAMILI ZITAFUATE BADO UONGOZI WA CHOMBO HICHI UNAFATILIA KUJUA ZAIDI
KUHUSU KIFO HICHO.
SIKU YA JANA..
MBUNGE wa Chambani, Salim Hemed Khamis (CUF), jana alianguka ghafla
katika mkutano wa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa
Kimataifa. Salim alianguka saa tano asubuhi wakati akihudhuria mkutano
wa kamati hiyo, uliokuwa ukifanyika katika ofisi ndogo za Bunge, jijini
Dar es Salaam.
Tukio hilo lilizua hofu kwa wabunge wengine
waliokuwamo, ambapo mkutano huo ulisitishwa kwa muda na juhudi za
kumshughulikia zilianza, kwani alitolewa nje ya ukumbi na kuanza
kupepewa.
Hata hivyo mbunge huyo alikimbizwa katika Hospitali ya Taifa
Muhimbili na kuingizwa katika kitengo cha wagonjwa mahututi (ICU) kwa
ajili ya uchunguzi zaidi.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, Edward
Lowassa, alilazimika kutoka nje ya ukumbi ambapo aliungana na wenzake
katika kuchanga mawazo kuhusu namna ya kumpeleka hospitali mbunge huyo.
Wakati
majadiliano hayo yakiendelea, hali ya mbunge huyo anayedaiwa kuwa
anasumbuliwa na shinikizo la damu iliendelea kubadilika, huku akitokwa
na jasho jingi.
Habari kuwajia baadae..
No comments:
Post a Comment