Pages

Saturday, March 30, 2013

Evander wa Marekani kuzipiga na Mbongo

IMANI MAKONGORO
BONDIA wa Tanzania, Alphonce Mchumiatumbo ametangaziwa zali la kucheza na Evander Holyfield wa Marekani, lakini mwenyewe anabainisha tangu alipoambiwa anajifua usiku na mchana kumkabili mkali huyo wa dunia.

Mchumiatumbo bondia namba moja kwenye uzani wa juu hapa nchini ameeleza kuwa siku ya bambino hilo ataonyesha uwezo wake wote hadi ule wa ziada kwani hiyo ndiyo nafasi ya yeye kutoka.

"Nimepewa taarifa kuwa Evander anakuja Tanzania Julai mwaka huu kama kutalii lakini pia atacheza pambano moja, na mimi ndiyo nitacheza naye, ni pambano la kuhamasisha ngumi hapa nchini," alisema Mchumiatumbo katika mahojiano na Mwanaspoti.

Mchumiatumbo anabainisha kuwa kuna promota kutoka Marekani aliyemtaja kwa jina la Jorge alimfuata baada ya pambano lake na Joseph Marwa na kumwambia ajiandae atacheza na Evander.

"Kwa maelezo ya promota huyo Evandar ameshuka kiuchumi siyo yule wa enzi hizo wakati anampiga Mike 'Iron' Tyson' na sasa ameamua kuja Tanzania kutalii," alibainisha bondia huyo.


"Unajua ni kama zali tangu promota huyo aliponitaka nijifue ili nicheze na Evander, muda mwingi nafanya mazoezi, najua litakuwa pambano la kihistoria."

Rekodi zinaonyesha kuwa Evander ameshinda mara 44 (29 kwa KO), amepigwa mara 10 (2 kwa KO), ametoka sare mara 2 wakati Mchumiatumbo ameshinda mara 9 (8 kwa KO) hajawahi kupigwa ametoka sare mara moja.

No comments:

Post a Comment