Pages

Wednesday, August 7, 2013

Ngassa: Simba SC wanataka kuniharibia.


 
WINGA mpya wa Yanga, Mrisho Ngassa (pichani), jana amejiunga rasmi na kikosi chake hicho zikiwa ni siku chache baada ya kumaliza majukumu yake Taifa Stars, lakini akaeleza kile anachoamini ndiyo sahihi katika sakata lake la kusajiliwa na timu mbili.

Msimu uliopita, Ngassa aliitumikia Simba kwa mkopo akitokea Azam, lakini Simba imekuwa ikidai iliingia naye mkataba wa mwaka mmoja, uliotarajiwa kuanza baada ya ule wa mkopo kumalizika, suala ambalo winga huyo amekuwa akilipinga.

Winga huyo hivi karibuni alisaini mkataba wa miaka miwili na Yanga.
CREDIT: GLP

No comments:

Post a Comment