CHANZO: JAMIIFORUMS
Pages
▼
Wednesday, April 30, 2014
BASI LA AM COACH LAPATA AJALI IPULI NA KUSABABISHA KIFO CHA MWANAFUNZI MMOJA
POLISI MKOANI MANYARA YAKAMATA MISOKOTO 6,000
TAARIFA YA MABADILIKO YA ANUANI YA OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma inapenda kuwafahamisha
wadau wake kuwa anuani yake imebadilika hivyo kuanzia sasa mawasiliano
yafanyike kwa kutumia anuani ifuatayo;
OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA
UTUMISHI HOUSE
8 BARABARA YA KIVUKONI
11404 DAR ES SALAAM
au
PRESIDENT’S OFFICE, PUBLIC SERVICE MANAGEMENT
UTUMISHI HOUSE
8 KIVUKONI ROAD
11404 DAR ES SALAAM
Anuani hii inachukua nafasi ya Sanduku la Posta 2483, Dar es salaam. Hivyo, mawasiliano yote yazingatie anuani mpya.
Limetolewa na
Katibu Mkuu
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
Barua pepe; permsec@utumishi.go.tz
OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA
UTUMISHI HOUSE
8 BARABARA YA KIVUKONI
11404 DAR ES SALAAM
au
PRESIDENT’S OFFICE, PUBLIC SERVICE MANAGEMENT
UTUMISHI HOUSE
8 KIVUKONI ROAD
11404 DAR ES SALAAM
Anuani hii inachukua nafasi ya Sanduku la Posta 2483, Dar es salaam. Hivyo, mawasiliano yote yazingatie anuani mpya.
Limetolewa na
Katibu Mkuu
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
Barua pepe; permsec@utumishi.go.tz
TBC NA CRI YAZINDUA TAMTHILIYA YA KICHINA ILIYOTAFSIRIWA KWA LUGHA YA KISWAHILI
Mkurugenzi Shirika la Utangazaji
Tanzania (TBC) Clement Mshana akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha mgeni
rasmi kwajili ya kuzindua rasmi Tamthiliya ya Mapenzi na Furaha ya Kijana (Jin
Tai Lang) uliofanyika katika Viwanja vya TBC jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari,
Vijana, Utamaduni na Michezo Elisante Ole Gabriel akitoa hotuba yake mbele ya
viongozi mbalimbali wakati wa Uzinduzi wa Tamthiliya ya Mapenzi na Furaha ya
Kijana (Jin Tai Lang) uliofanyika siku ya jana katika Viwanja vya TBC jijini Dar es
Salaam.
Mtendaji Mkuu Kampuni ya Star Media
(T) Ltd Bw. Jack Czhou akieleza jambo wakati wa Uzinduzi wa Tamthiliya ya
Mapenzi na Furaha ya Kijana (Jin Tai Lang) uliofanyika katika Viwanja vya
TBC jijini Dar es Salaam.
UTUMISHI YAIBUKA KINARA WA MPIRA WA PETE MASHINDANO YA MEI MOSI 2014
Fatuma
Machenga (GS) mfungaji bora katika Mpira wa Pete wa mashindano ya Mei
Mosi 2014 akiwa na kikombe baada ya kutangazwa rasmi katika hafla fupi
iliyofanyika katika Uwanja wa Jamhuru mjini Morogoro.
Baadhi
ya wachezaji wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma (jezi za
kijani) wakishangilia kwa kutawazwa mabingwa wapya wa Mpira wa Pete Mei
Mosi 2014 kwa kuifunga timu ya Uchukuzi. Mashindano hayo yalimalizika
jana jioni katika uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Baadhi
ya wachezaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi Umma, pamoja na
mashabiki wao wakipongezana baada ya kuibuka mabingwa wapya wa Mpira wa
Pete kwa kuifunga Uchukuzi katika mashindano ya Mei Mosi 2014
yaliyomalizika katika Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Tuesday, April 29, 2014
SHEREHE ZA MIAKA 50 YA MUUNGANO ZAFANYIKA PARIS UFARANSA
Watanzania
waishio nchini Ufaransa walikutana Jumamosi mchana tarehe 26 Aprili
nyumbani kwa Balozi wa Tanzania mjini Paris ili kusherehekea miaka 50 ya
muungano kati ya Zanzibar na Tanganyika.
Balozi
wa Tanzania Nchini Ufaranza,Mh. Begum Karim Taj akipokea keki maalum
kwa ajili ya sherehe hizo za Muungano wa Tanzania katika hafla
iliyofanyika nyumbani kwa Balozi,Mjini Paris Ufaransa.
Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa akiwa na watoto mjini Paris.
MAMA SALMA KIKWETE AZINDUA WIKI YA CHANJO DUNIANI MKOANI KILIMANJARO
![]() |
Baadhi ya taasisi a NGO'S mbalimbali zilihudhuria uzinduzi huo. |
![]() |
Wanafunzi kutoka shule mbalimbali za msingi wakisikiliza kwa makini mambo mbalimbali yaliyokuwa yakizungumzwa. |
![]() |
Makundi mbalimbali ya watu yalishiriki uzinduzi wa wiki ya chanjo duniani iliyozinduliwa mjini Moshi. |
![]() |
Wanafunzi kutoka shule mbalimbali za msingi wakisikiliza kwa makini mambo mbalimbali yaliyokuwa yakizungumzwa. |
![]() |
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama akizungumza wakati wa uzinduzi wa wiki ya chanjo duniani. |
![]() |
Mwakilishi mkazi wa shirika la Afya Duniani (WHO) Dk Rufaro Chatora akizungumza wakati wa sherehe za uzinduzi wa wiki ya chanjo duniani uliofanyika katika viwanja vya mandela mjini Moshi. |
![]() |
Baadhi ya washiriki katika uzinduzi huo kutoka Asasi mbalimbali mkoani Kilimanjaro. |
![]() |
Mwakilishi wa UNICEF,Sudha Sharma akizungumza wakati wa sherehe za uzinduzi wa wiki ya chanjo duniani uliofanyika katika viwanja vya mandela mjini Moshi. |
Monday, April 28, 2014
NAY WA MITEGO ASAKWA KWA KUTISHIA KUUA
KIMENUKA! RB namba KT/RB/1178/2014-KUTISHIA KUUA KWA NJIA YA MTANDAO
inamsaka staa wa Ngoma ya Nakula Ujana, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa
Mitego’ kwa tuhuma ya kutishia kumuua mdogo wake aliyetajwa kwa jina la
Amani Shija, Ijumaa Wikienda limeinyaka.
Kwa mujibu wa chanzo makini, Nay alikuwa akiishi na Shija kwa zaidi ya miaka mitano nyumbani kwake, Manzese jijini Dar.
Habari zilitonya kuwa ugomvi wa Nay na Shija ulianza zaidi ya miezi mitatu iliyopita ambapo hivi karibuni walikuwa maeneo ya Kijitonyama, Dar, wakipata chakula cha usiku na marafiki zao wengine ndipo ghafla dogo akajichanganya na kujikuta akiropoka neno lililomuudhi Nay, akapaniki.
Ilisemekana kwamba baada ya kupaniki, Nay alianza kumfokea Shija na kutishia kumuua, ambaye alishindwa kujizuia na kujikuta akimwaga chozi.
Akaendelea
kueleza kuwa hata baada ya siku hiyo, Nay aliendelea kumtumia SMS za
kutishia kumuua ambazo bado anazo kama ushahidi Baada ya kudaka mchongo
huo, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Shija ambaye pia ni msanii wa Bongo
Fleva na kumuuliza juu ya malalamiko hayo, akakiri kugombana na kaka
yake huyo.
Kwa mujibu wa chanzo makini, Nay alikuwa akiishi na Shija kwa zaidi ya miaka mitano nyumbani kwake, Manzese jijini Dar.
Habari zilitonya kuwa ugomvi wa Nay na Shija ulianza zaidi ya miezi mitatu iliyopita ambapo hivi karibuni walikuwa maeneo ya Kijitonyama, Dar, wakipata chakula cha usiku na marafiki zao wengine ndipo ghafla dogo akajichanganya na kujikuta akiropoka neno lililomuudhi Nay, akapaniki.
Ilisemekana kwamba baada ya kupaniki, Nay alianza kumfokea Shija na kutishia kumuua, ambaye alishindwa kujizuia na kujikuta akimwaga chozi.

JOKATE, NATURE WATIFUANA!

PASUA jipu! Mastaa wawili wenye majina makubwa Bongo, mwanamitindo Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ na Mbongo-Fleva Juma Kasim ‘Juma Nature’ wanadaiwa kuacha mshangao kwa wasanii wenzao baada ya kutifuana, Ijumaa Wikienda limeng’atwa sikio.
Pamoja na kwamba Nature amekuwa akizuga kutomaindi lakini habari za kushangaza zilidai kwamba mkali huyo wa Temeke amekuwa akimtuhumu mwanadada huyo kuwa amemuibia wazo lake la biashara ya ndala au kandambili.
Kabla ya madai haya mapya, Nature aliwahi kunukuliwa redioni wakati akitambulisha wimbo wake mpya wa Chuma Ulete kuwa yupo mbioni kuingiza bidhaa hiyo sokoni.
Madai ya sasa yanaeleza kwamba Nature amekuwa akilalamika kuwa Jokate ‘amekopi’ na ‘kupesti’ wazo lake la biashara.
Pia ilisemekana kwamba Nature amekuwa akimtafuta Jokate ili kuweka suala hilo sawa bila mafanikio.
“Nature amekuwa akimpigia simu Jokate lakini haipokelewi,” kilidai chanzo hicho kwa sharti la kutotajwa popote hata kwa mtutu wa bastola.
Kwa mujibu wa Nature bado hajabahatika kuziona kandambili za Jokate lakini amekuwa akiambiwa na watu wake kuwa mrembo huyo kamuibia.
Saturday, April 26, 2014
UUJUMBE WA KUMTISHIA MAISHA MZEE WA UPAKO

Ujumbe huo ambao ulitumwa na mtu aliyejitambulisha kama msamaria mwema, ulisambazwa kwa watu mbalimbali mpaka kuwafikia mapaparazi wetu, unaeleza kwamba mbaya wa Rose Mhando ana mpango wa kumuua Mzee wa Upako.
BABA AHUSISHWA KIFO CHA DENTI MWANZA!
Mwili wa marehemu Anastazia Lackfordukiagwa kabla ya kwenda kuzikwa.
Mwili wa marehemu Anastazia Lackford ambaye alikuwa mwanafunzi wa
Shule ya Sekondari Mwanza, umezikwa juzi katika makaburi ya Lunala,
Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza lakini simulizi ya baba mzazi wa
marehemu, Lackford Magafu kuhusishwa na kifo cha mwanaye inashangaza!
Kabla ya kifo.
Kabla ya kifo.
UOZO MAHOSPITALINI: OFM YAIFUNGIA KAZI PALESTINA!

Baada ya kuanika uozo wa hospitali kadhaa – za serikali na binafsi,
sasa kikosi kazi cha Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ cha Global
Publishers, kilitinga katika Hospitali ya Wilaya ya Kinondoni, Palestina
na kugundua udhaifu mkubwa wa huduma mbovu zitolewazo hospitalini hapo.
ACHOMWA KISU KISA MUME WA MTU!

Tukio hilo lililowaacha watu vinywa wazi, lilijiri Aprili 22, mwaka
huu shambani katika Kijiji cha Kigwa, Kata ya Ukondamoyo wilayani Uyui,
Mkoa wa Tabora.
KISU KILIVYOFANYA KAZI
Habari kutoka kwa baadhi ya mashuhuda zinasema kuwa, Amina alichomwa kisu mara mbili, kwenye paja mguu wa kushoto kisha kwenye mgongo ambapo kilizama na kutoka mpini tu!
Habari kutoka kwa baadhi ya mashuhuda zinasema kuwa, Amina alichomwa kisu mara mbili, kwenye paja mguu wa kushoto kisha kwenye mgongo ambapo kilizama na kutoka mpini tu!
KISA KINASIMULIWA
Kwa mujibu wa taarifa za awali, siku ya tukio, Pima alitoka nyumbani kwake na kumfuatilia mumewe huyo kwenye shamba la tumbaku la kaka wa Amina (jina halikupatikana) ambako alisikia kuwa mwanamke huyo yupo na mumewe.
Kwa mujibu wa taarifa za awali, siku ya tukio, Pima alitoka nyumbani kwake na kumfuatilia mumewe huyo kwenye shamba la tumbaku la kaka wa Amina (jina halikupatikana) ambako alisikia kuwa mwanamke huyo yupo na mumewe.
“Pima alisikia Amina ana uhusiano na mumewe. Siku hiyo akasikia wapo
shambani. Akatoka nyumbani na kufuatilia akijua atawanasa laivu,”
kilisema chanzo hicho.
MWANAMKE ALIYECHOMWA KISU
Akizungumza akiwa amelazwa akiuguza majeraha katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tabora, Kitete, Amina alisema:
Akizungumza akiwa amelazwa akiuguza majeraha katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tabora, Kitete, Amina alisema:
“Mimi sina uhusiano na huyo mwanaume jamani. Kwanza huyo mwanamke
simjui kabisa. Nimemwona kwa mara ya kwanza siku hiyo ya tukio.
“Siku hiyo mimi na mwanangu kichanga (wa miezi mitatu) tulikuwa
shambani, mimi nilikuwa nikimsaidia kaka yangu kuvuna tumbaku, akaja
Adam (mwenye mke) naye akawa anasaidia kuvuna. Kuna wakati nilikwenda
kupumzika mahali ili nimnyonyeshe mwanangu.

“Ilikuwa ni hatua chache tu tokea mahali ambako mume wake alikuwa
akivuna. Nilipiga kelele za kuomba msaada, mume wake akaja mbio kusaidia
kwa kumdhibiti mke wake asiendelee kunichoma kisu zaidi,” alisema
Amina.
Akaendelea: “Nilianguka chini na kuanza kugalagala huku damu nyingi
zikinitoka. Ndipo wasamaria wema nao walifika na kumkamata Pima,
wakamfunga kamba na kumpeleka ofisi ya kata ambako alipelekwa Kituo
Kikuu cha Polisi Tabora.”
BODABODA YAMKIMBIZA HOSPITALI
Habari zaidi zinasema kuwa, Amina akiwa hoi na damu chapachapa, alipandishwa kwenye bodaboda na kukimbizwa kweynye hospitali ya rufaa ya mkoa kwa ajili ya matibabu huku hali yake ikionekana si ya kuridhisha.
Habari zaidi zinasema kuwa, Amina akiwa hoi na damu chapachapa, alipandishwa kwenye bodaboda na kukimbizwa kweynye hospitali ya rufaa ya mkoa kwa ajili ya matibabu huku hali yake ikionekana si ya kuridhisha.
Friday, April 25, 2014
Hii hapa top 20 ya 'Mama Shujaa wa Chakula' watakaoingia kijiji cha Maisha Plus wikiendi hii
Shindano
la Mama Shujaa wa Chakula linaloendeshwa na kusimamiwa na Oxfam
limefikia tamati ya hatua ya awali ya kutafuta washindi kwa kutangaza
wanawake 20 kuingia katika top 20 ya shindano hilo la aina yake.
Wanawake
hao wenye wasifu tofauti tofauti sasa wataingia katika kijiji cha
maisha plus kwa muda wa wiki tatu ikiwa ni katika hatua ya kutafuta
mshindi wa shindano hilo ambalo linalenga kuhamasisha jamii juu ya
kilimo, hifadhi ya chakula na namna ya kukabiliana na mabadiliko ya
tabianchi na njaa. Mbali na wanawake hao 20 pia kuna mshiriki mmoja
ambaye yeye amepatikana kwa shindano la mtandaoni.
Hapa nakuletea orodha ya akina mama hao mmoja baada ya mwingine.
GRACE G.D MAHUMBUKA (46) mkazi wa Karagwe Kagera
nambari yake ya ushiriki ni MS 08, ni mkulima wa shamba la ekari 18 na na mfugaji
wa ng’ombe, kondoo na mbuzi.
ANADHANI YEYE NI MFANO WA KUIGWA: Kwa sababu
anawahamasisha wana kijiji kutumia vyema mvua za kwanza na kupanda miti kwa
ajili ya utunzaji wa vyanzo vya maji na kutunza mazingira."Nina shamba lenye ukubwa wa ekari 18.
Kwa mwaka ninavuna mazao gunia 35"
NEEMA URASSA KIVUGO (48) (Mshindi: Mama Shujaa wa
Chakula Mtandaoni) ni mkazi wa Kiteto Manyara, namba yake ya ushiriki ni MS 12,
na mkulima wa shamba la ukubwa wa ekari 10.
ANADHANI YEYE NI MFANO WA KUIGWA:
Yeye ni mchapakazi na anachukulia kilimo kama njia ya kumkwamua dhidi ya
umasikini. Yeye ni mbunifu na hujifunza kwa haraka. Anavuna mazao gunia
78 kwa mwaka.
MARY JOHN MWANGA (52) ni mkazi wa Mkalama Singida,
ni mkulima na mfugaji anashamba la ekari 5 na analima mahindi na anafuga ng’ombe
watano
ANADHANI YEYE NI MFANO WA KUIGWA: Kwa sababu
anashiriki katika shughuli za maaendeleo ya kijiji, michango na mikutano. "Kwa mwaka ninavuna mazao gunia 22" anasema.