Pages

Saturday, June 7, 2014

Azam kuweka kambi Hispania

Wachezaji wa timu ya Azam FC wakishangilia bao katika moja ya mechi ya Ligi kuu ya Vodacom.
KATIKA kuhakikisha wanafanya vyema kwenye msimu ujao wa Ligi Kuu Bara pamoja na michuano ya kimataifa, Klabu ya Azam inatarajia kuweka kambi nchini Hispania ikiwa ni sehemu ya maandalizi.
Azam ambao ni mabingwa watetezi wa ligi kuu, wanatarajia kushiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika mwakani.

Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya klabu hiyo kilisema kuwa, klabu hiyo imepanga kuweka kambi yake nchini humo kwa lengo la kulinda heshima mara baada ya kutwaa ubingwa wa ligi.
Aidha, kilisema kocha wa timu hiyo, Mcameroon, Joseph Omog, anatarajia kurejea kati ya Juni 13, mwaka huu huku kambi ikianza Juni 16.
“Kambi imepangwa kuwa Hispania, lengo likiwa ni kuwapa nafasi wachezaji kujifunza vitu vingi kama ambavyo inajulikana nchi hiyo kwa soka la uhakika, pia mwalimu anaweza kutua Dar kati ya Juni 13,” kilisema chanzo hicho.
Championi lilimtafuta katibu wa timu hiyo, Idrissa Nassor na kuhoji kuhusiana na ishu hiyo ambapo alisema: “Klabu imempa jukumu kocha Omog aamue yeye kambi anataka iwekwe wapi kwa kuwa anajua wapi patamfaa.”

No comments:

Post a Comment