EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, May 5, 2013

Akiuka amri ya Manispaa Kinondoni.

Dar es Salaam
MMILIKI wa jengo la hoteli iliyopo katika kiwanja namba 401 block ‘C’ Sinza jijini Dar es Salaam, Joanes Sanga, amekiuka agizo la Manispaa ya Kinondoni kwa kujenga jengo la ghorofa tisa badala ya tano kama alivyoomba.

Kutokana na kukiuka ujenzi huo uliopewa kibali namba 06809 kwenye mpango namba K133/2009, tayari Manispaa ya Kinondoni imemwandikia barua ya kumuelekeza taratibu za kufuata ili jengo hilo lipate baraka ya kuendelea kujengwa.

Katika barua hiyo ya manispaa ya Aprili 17 mwaka huu, kwenda kwa Sanga ikiwa imesainiwa na Mhandisi wa manispaa hiyo, Gerald Urio, kwa niaba ya mkurugenzi wake, mmiliki huyo analezwa kuwa kwa taratibu za viwango vya ujenzi mjini ukubwa wa kiwango kilichojengwa katika kiwanja hicho hakitoshi kubeba uzito wa jengo unaoendelea.

“Wewe tayari umejenga kwa kibali hicho na kuongeza ghorofa nne, hivyo jengo kuwa la ghorofa tisa (10 storey),” ilisomeka sehemu ya barua hiyo.
Pia barua hiyo inaelezea kuwa hakukuwa na aina yoyote ya ukaguzi uliofanywa katika hatua zote za ujenzi ikiwamo kukagua vifaa vilivyotumika.
Badala ya kuchukua hatua kwa ukiukwaji huo wa taratibu za ujenzi, barua hiyo imemtaka mmiliki ahakikishe jengo hilo linafanyiwa vipimo (structure assessment) kujua ubovu wake ambapo ametakiwa aende katika taasisi ya serikali (BICO na DIT) na kisha majibu yarudishwe manispaa.

Alipotafutwa mmiliki wa jengo hilo kueleza sababu za kujenga bila kufuata taratibu, alisema suala hilo waulizwe Manispaa ya Kinondoni.
Sanga alisema anachofanya ni suala la maendeleo na hajui kama amevunja taratibu.
Alipotakiwa kuelezea sababu ya kushindwa kukagua ujenzi huo, Mhandisi wa Manispaa ya Kinondoni, Gerald Urio, alisema wao kama manispaa hawawezi kukagua kila jengo katika wilaya hiyo.

Alisema sababu nyingine iliyowafanya wasiwe na wasiwasi na ujenzi huo ni kutokana na vibao vinavyowaonesha wajenzi wa jengo hilo kuwa ni wasomi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,
Kuhusu athari inayoweza kujitokeza kutokana na ongezeko hilo, Urio alisema hilo si jambo la ajabu kwa kile alichoeleza kuwa kuna majengo mengi yanaongezwa baada ya ujenzi wa awali kukamilika.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate