Ni
kweli kuachwa kunaumiza sana moyo. Kimsingi usiombe kukumbwa na maumivu
ya kuachwa. Lakini kama hilo limekwishatokea, kwa nini uendelee kuumia
na kumchukia aliyekuwa mpenzi wako?Kitendo cha kukuacha wewe, kinaweza kumtokea hata yeye na kujikuta akilia na kuhuzunika kama wewe. Kama ndivyo basi mapenzi ndivyo yalivyo. Leo kwako, kesho kwake.
Hakuna sababu ya kuchukiana na kuwekeana visasi kwa sababu kama tutafanya hivyo, kwa dunia ya sasa iliyojaa uchepukaji, itakuwa dunia ya visasi kila kukicha.





























