EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, May 5, 2013

Mbatia aibana Serikali • Amshangaa Waziri Kawambwa kutojiuzulu.

SIKU moja baada ya serikali kufuta matokeo ya mtihani wa kidato cha nne na kuamuru yaandaliwe upya, Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia, ametaka wazazi wa wanafunzi waliojinyonga kwa matokeo hayo walipwe fidia.

Wakati akitaka wanafunzi hao walipwe fidia, pia Mbatia alimshangaa Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa, akihoji anasubiri nini kung’atuka wakati kuna wanafunzi wamepoteza maisha kwa uzembe wao.

Alisema Kawambwa anapaswa kujiuzulu kwani Katibu Mkuu wa Baraza la Mitihani nchini, Joyce Ndalichako, hawezi kufanya mabadiliko makubwa ya aina hiyo bila kuishirikisha wizara.
Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini hapa, Mbatia ambaye pia ni Mbunge wa kuteuliwa alisema serikali imekuja na majibu rahisi kwenye jambo gumu, kwani uamuzi wa kufuta na kuandaa upya matokeo hayo kwa utaratibu wa mwaka 2011, hauleti ufumbuzi wa mfumo wa elimu.

“Tume imekuja na majibu mepesi sana kwenye tatizo kubwa. Wanafunzi wamejiua kwa msongo wa mawazo, wengine wamekata tamaa na kuamua kuolewa, wengine kupata ujauzito, leo kwa uzembe wao wanataka kuwafaulisha wanafunzi ili kupata sifa kisiasa, haiwezekani,” alisema.
Akichambua maoni ya tume hiyo, alisema imeibua hoja ambazo yeye aliziwasilisha bungeni kupitia hoja yake binafsi ambayo ilizimwa na wabunge wa CCM kwa sababu za kulinda masilahi ya chama chao.
 Bofya chini kuendelea kusoma..

Alilishambulia Bunge kuwa limekuwa chanzo cha matatizo mengi kutokana na ubinafsi wa vyama bila kujali masilahi ya taifa.
“Bunge linaangamiza taifa kwa sababu ya itikadi. Hizi itikadi za vyama zinaliangamiza taifa. Kuna umimi, ubinafsi kwenye mambo ya masilahi ya taifa. Nawataka wabunge watoke usingizini,” alisema Mbatia.

Juzi serikali ilitangaza kufuta matokeo ya kidato cha nne ya mwaka 2012 na kuagiza yaandaliwe upya.
Uamuzi huo mgumu ulitangazwa bungeni na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi.

Akisoma tamko hilo kwa niaba ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Lukuvi alisema uamuzi huo wa serikali umetokana na mapendekezo ya tume ya waziri mkuu iliyoundwa kuchunguza chanzo cha matokeo ya kidato cha nne mwaka jana kuporomoka kwa kiwango cha kutisha.

Matokeo ya mitihani ya kidato cha nne mwaka 2012 yalionesha kuwa kiwango cha ufaulu kimeshuka kwa kiwango kikubwa ikilinganishwa na miaka ya hivi karibuni.
Matokeo yaliyotangazwa hivi karibuni, yalionesha kwamba kati ya wanafunzi 367,756 waliofanya mtihani huo, watahiniwa 126,847 ndio waliofaulu.

Katika idadi hii, wanafunzi waliofaulu katika daraja la kwanza hadi la tatu ni 23,520, sawa na asilimia 6.4 na daraja la nne ni 103,327, sawa na asilimia 28.1.
Watahiniwa 240,909, sawa na asilimia 65.5 ya wanafunzi wote, waliofanya mtihani wa kidato cha nne mwaka 2012, walipata daraja sifuri.

BAVICHA nao wanena
Lucy Ngowi anaripoti kuwa, Baraza la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA), limemtaka Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa na wasaidizi wake kujiuzulu mara moja ili kupisha wenye uwezo wa kusimamia sekta hiyo.
Katibu Mkuu wa BAVICHA, Deogratias Munishi, alisema hayo katika tamko alilolitoa jana baada ya Tume ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kutoa ripoti ya awali kuhusu sakata la kufeli vibaya kwa wanafunzi waliofanya mtihani wa kidato cha nne mwaka jana.
Akinukuu moja ya sababu za kushindwa kwa wanafunzi hao, Munishi alisema ni kutumika kwa alama mpya tofauti na miaka ya nyuma bila taarifa kwa walengwa.
Alisema kuwa huo ni muendelezo wa siasa na mzaha kwa Watanzania kunakofanywa na serikali ya CCM kwenye masuala nyeti.

“BAVICHA inasisitiza Waziri Kawambwa na wasaidizi wake wajiuzulu nyadhifa zao ili kupisha watu wenye uwezo wa kusimamia sekta hii na taasisi zilizo chini yake,” alisema Munishi.
Aliongeza kuwa viwango hivyo vipya vilivyowekwa na Baraza la Mitihani bila kushirikisha wadau ni kiashiria cha uzembe uliokithiri.

“Kama Baraza lilifanya maamuzi hayo bila waziri kujua nako kunaashiria uzembe uliobobea wa waziri huyu wa kushindwa kujua kinachofanyika na taasisi zilizo chini yake na kwa maana hiyo ni mzigo kwa taifa,” alisema.
Kwa mujibu wa Munishi, suala hilo limeleta athari kwa wanafunzi, kwani baadhi yao wamepoteza maisha kwa kujinyonga.

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate