Akizungumza na mtandao huu muda mfupi uliopita, Badra alisema hadi muda huu polisi hawajanikiwa kuwakamata wahusika waliogonga nguzo moja na kusababisha nyingine kuanguka usiku wa kuamkia leo.
"Tatizo ni kubwa lakini mafundi wetu wapo kazini. tunatarajia hadi ifikapo saa moja usiku umeme utawaka maeneo yote yaliyoathirika hasa Kijitonyama," alisema Badra akiliomba jeshi la polisi kuwakamata haraka wahusika wa tatizo hilo.
Usiku wa kuamkia leo dereva asiyejulikana aligonga nguzo moja ya umeme jirani na Chuo Cha Posta Kijitonyama iliyoangusha nguzo zingine tano na kusababisha mlpuko mkubwa wa moto katika Barabara ya Ali Hassa Mwinyi maeneo ya Bamaga.
No comments:
Post a Comment