EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, June 30, 2012

Mali za Tanzania Heart Institute (THI) za Dkt. Masau kupigwa mnada kesho (?)

Kuna taarifa kuwa siku ya kesho, Jumapili, Julai Mosi, 2012, kila kitu kilichokuwa katika hospitali ya Taasisi ya Moyo (Tanzania Heart Institute - THI) kitapigwa mnada.

Wapo watu waliopelekwa huko kuthaminisha vitu vyote inasemekekana vitu vyote lazima vipigwe mnada.
Picture: Tanzania Heart Institute (THI) ya Dkt. Masau
Mwezi Aprili 2012, Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF), kupitia amri ya mahakama, iliifunga taasisi hiyo na kuwahamishia wagonjwa wote kwenye hospitali nyingine kwa kile kilichoripotiwa ni Taasisi hiyo kushindwa kulipa Shilingi bilioni 7 za pango.

Matangazo yaliyokuwepo kwenye majengo ya hospitali hiyo yalitoa taarifa ya kufungwa kwa hospitali hiyo na kudai kwamba tayari amepatikana mwekezaji mwingine anayetaka kutumia majengo hayo yaliyo barabara ya Tunisia karibu na klabu maarufu ya viongozi ‘Leaders Club’ wilayani Kinondoni.

Tangazo hilo lililokuwa na kichwa cha habari "taarifa kwa umma" lilisema NSSF inatoa taarifa kwa wananchi wote kuwa, kwa mujibu wa amri ya Mahakama Kuu (kitengo cha Ardhi) iliyotolewa Septemba 11 mwaka jana katika shauri na 158/2007 kati ya NSSF na Taasisi ya moyo Tanzania, “Hospitali hii imefungwa kwa amri ya Mahakama. Jengo ni mali ya NSSF na limepata mwekezaji mwingine” “NSSF itatwaa jengo lake lililojulikana kama "Hosteli ya Tazara" ambapo kwa sasa limepangishwa na THI Julai 25 mwaka huu hivyo wagonjwa wote na familia zao wanashauriwa kufanya mpango mbadala ya hospitali ya kuhama au kuhamisha wagonjwa wao kabla ya tarehe hiyo kufika.” ilinukuliwa sehemu ya taarifa hiyo.

Akizungumza na gazeti la HABARILEO Jumapili kuhusu suala hilo, Meneja Uhusiano wa NSSF, Eunice Chiume, alisema ni kweli taasisi hiyo imefungwa na vifaa vyake kushikiliwa na madalali wa Mahakama kwa sababu mmiliki wake alishindwa kulipa kodi ya pango ya zaidi ya Sh. bilioni 7.

Akizungumzia hatua walizopata kuchukua kabla ya kuamua kuifunga ili walipwe, Chiume alisema walikuwa wakimkumbusha mpangaji kuhusu kulipa au kupisha jengo hilo bila mafanikio na badala yake, miaka mitatu baada ya kukabidhiwa jengo hilo na kushindwa kulipa, alikimbilia mahakamani kuzuia kuondolewa.

Taarifa za NSSF zinasema Dk. Massau alikabidhiwa jengo hilo mwaka 2004 na kuachiwa mwaka mmoja wa kuendesha shughuli zake bure, ili ajipange sawa sawa lakini aliendelea kulitumia bila kulipa hadi alipofungiwa.

Chiume alisema zimejitokeza hospitali kadhaa zinazotaka kupanga, ikiwamo ya Apollo ya India na kwamba wako katika mchakato wa kuangalia kwa undani wampangishe nani ili kuepuka yaliyotokea yasijirudie.

Dkt. Massau alikiri kudaiwa kiasi hicho cha pango na kusema sababu za kutolipa zilikuwa wazi kwa shirika hilo.

“Ni kweli wananidai, lakini wanajua kesi ilikuwa mahakamani na tulipaswa kurudi huko Aprili 24, ili kujua kinachoendelea, lakini wamekuja kuvamia usiku wa Aprili 10, na kupiga watu na kubeba wagonjwa kuwapeleka kusikojulikana, tumelalamika mpaka kwa Jaji Mkuu na tutafika mahakamani siku hiyo ya kesi, tukiwa na malalamiko yetu juu ya kukiukwa kwa sheria,” alisema Dkt. Masau.

Alikanusha kupangishwa mwaka 2004 na kudai kuwa alikabidhiwa jengo hilo la ghorofa mbili Mei 2005 likiwa na kasoro nyingi zilizofanya washindwe kuendesha shughuli za upasuaji wa moyo na hivyo kuendesha huduma za matibabu mengine ya moyo tofauti na makubaliano na wafadhili. 
Picture
Dkt. Masau
Mwaka 2008, Dkt. Masau aligoma kuhama katika jengo.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa mkutano wa VC uliopo ndani ya Jengo la Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) muda mfupi baada ya kumalizika kwa semina ya madaktari wa moyo mwaka huo, alisema yeye hawezi kuhama katika jengo hilo kwa sababu NSSF imeshindwa kutimiza makubaliano yao wakati walipompangisha na kuongeza, “Kwanza siwezi kuhama katika jengo hilo kwasababu kuna wagonjwa 15 wamelazwa ambapo kati yao wagonjwa 5 wanategemea kufanyiwa upasuaji wa moyo wakati wowote, pili vitu ambavyo viko ndani ya jengo hilo ni zaidi ya bilioni, makubaliano yetu ilikuwa ni kutengeneza jengo hilo ili liwe na hadhi ya hospitali ya moyo kitu ambacho walishindwa kuyatimiza,” alisema Dkt. Masau.

Alisema moja ya makubaliano yao ni kwamba NSSF wamtengenezee jengo liwe na hadhi ya Hospitali ya Moyo.

Alisema baada ya makubaliano hayo NSSF walimpelekea taarifa kuwa kazi hiyo imeshamalizika hivyo anachotakiwa kufanya ni kukubali kusaini mkataba wa kulipangisha jengo hilo.

“Nilikubali kusaini mkataba wa kama mpangaji baada ya NSSF kunihakikishia kuwa wamenitengenezea jengo hilo kama nilivyowaeleza, lakini baada ya kusaini mkataba na kuingia ndani ya jengo nikagundua kuwa kuna baadhi ya maeneo hayajatengenezwa kama nilivyoyahitaji,”alisema Masau na kuongeza:

“Baada ya kubaini mapungufu hayo tulikubaliana niendelee kulitumia jengo hilo wakati marekebisho hayo yanafanyika, lakini hayo hayakufanyika badala yake nilishangaa kuona taarifa ya kuitwa mahakamani kwa kesi ya madai miezi miwili baada ya mkataba huyo,”alisema.

Alifafanua kuwa baada ya kesi hiyo kuanza kusikilizwa mahakamani miezi miwili baadaye hukumu ilitolewa na mahakama ikaamuru aondolewe katika jengo hilo na kwama baada ya amri hiyo alimfuata Waziri Mkuu Mizengo Pinda ambapo Waziri aliwataka wayamalize nje ya mahakama chini ya Wizara ya Kazi Ajira na Maendeleo ya Vijana.

Hata hivyo, kufuatia taarifa za ndani ya NSSF zilizonaswa na gezeti MWANANCHI, Serikali ilishawahi kutoa tamko kuwa haiwezi kingilia zaidi mgogoro huo na kuwataka wamalize mgogoro huo kwa mujibu wa maamuzi ya mahakama.

Kwa mujibu wa nyaraka hizo za siri pia ilibaini kuwa Julai 5, Waziri wa Kazi Ajiri na Maendeleo ya Vijana wa wakati huo, Profesa Juma Kapuya alimuandikia Dkt. Masau barua iliyosema kuwa endapo atashindwa kulipa sehemu ya deni hilo kama walivyokubaliana katika kikao cha Julai Mosi mwaka huu NSSF itaendelea na uamuzi wake wa kumtoa ndani ya jengo hilo.

“Tulikubaliana kuwa endapo taasisi yako itashindwa kulipa sehemu ya deni hilo kama inavyopendekezwa basi NSSF itaendelea na uamuzi wake wa kuitoa hiyo THI kwenye jengo hilo kama iliyoamuriwa na mahakama bila kutoa notisi nyingine,”ilisema sehemu ya barua hiyo ya Waziri Kapuya.

Hata hivyo, nakala ya barua ilipelekwa kwa Waziri Mkuu,Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii na NSSF. 
picha via Charaz.blogspot.com

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate