EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, October 31, 2012

MCHUMBA WA VENGU AFUNGUKA KUUGUA NI SEHEMU YA MAISHA KWA MPENZI WAKE.

MISS Kinondoni 2009, Stella Mbuge amefunguka kuwa ugonjwa wa mpenzi wake Joseph Shamba ‘Vengu’, memba wa Orijino Komedi si sababu ya kumuacha na kuhangaika na wanaume wengine.

Akipiga stori na mwaandishi wa habari hii , Stella alisema, anatambua kuugua ni sehemu ya maisha na jambo kubwa kwa sasa ni kumuombea mpenzi wake huyo apone haraka na kuendelea na maisha yao kama kawaida.“Vengu ana thamani kubwa kwangu, siwezi kumuacha wala kumsaliti. Ndugu zake wananipenda na kunipa ushirikiano mzuri. Nashukuru anaendelea vizuri na ninaamini siku si nyingi atarudi kazini,” alisema Stella.

MKURUGENZI MTENDAJI TANESCO AFUKUZWA KAZI....KISA?PITIA HAPA.

 Jionee kwa picha hapa chini.

BASI LA ABOOD NAMBA T 545 AZE LA KUTOKEA DAR KWENDA TUNDUMA LAPATA AJALI MAENEO YA SAE(MBILINYI).

BASI LA ABOOD NAMBA T 545 AZE LA KUTOKEA DAR KWENDA TUNDUMA LAPATA AJALI MAENEO YA SAE(MBILINYI) BAADA YA KUGONGANA NA KENTA LILILO SABABISHA AJALI HIYO, MMOJA AFARIKI HAPO HAPO!
 Hivi ndivyo basi La Abood lilivyo pata ajali baada ya kugongana na Kenta
 Basi la Abood 
 Hivi ndivyo Basi Lilivyo Haribika 
 Haya ni mambaki ya Vioo vilivyo vunjika


 Baadhi ya vitu vikiwa vimemwagika chini

 Hili ni Scania ambalo lilikuwa likitokea Zambia 


 Dirisha likiwa limevunjika 

Baadhi ya Abiria wakiwa wanapata maelekezo kutoka kwa polisi 
Hapa ndipo basi la Abbod lilipo gonga 

*********************
BASI LA ABOOD LENYE USAJILI WA NAMBA T 545 AZE LIMEPATA AJALI MAENEO YA SAE SEHEMU MAARUFU  KWA JINA LA KWA MBILINYI LIKITOKEA DAR ES SALAAM KUELEKEA TUNDUMA. AJALI HIYO IMETOKEA BAADA YA LORI LA MIZIGO AINA YA SCANIA LIKIWA LIMETOKEA ZAMBIA KUELEKEA DAR WAKATI WA KUTAKA KUPISHANA NA BASI HILO, NA NDIPO GARI AINA YA KENTA IKAJITOKEZA NA KUJICHOMEKA BARABARANI NA KUSABABISHA AJALI HIYO.

KATIKA AJALI HIYO MTU MMOJA AMBAYE  ANAITWA CHALE KITELEKE AMBAYE PIA ALIKUWA NDIYE KONDA WA BASI HILO AMEFARIKI PAPO HAPO, PAMOJA NA MAJERUHI NANE AMBAO WAMEKIMBIZWA HOSPITALINI .

MPAKA TONE MEDIA LIVE GROUP AMBAO NI WAMILIKI WA MTANDAO HUU TUNATOKA ENEO LATUKIO HIZO NDIZO TAARIFA TUMEFANIKIWA KUZIPATA.

HABARI KAMILI ITAWAJIA KESHO BAADA YA KUPATA TAARIFA KUTOKA POLISI.

PICHA ZOTE NA: MBEYA YETU BLOG

WANAFUNZI WANUSURIKA NA BOMU LA MACHOZI JIJINI ARUSHA .


Kamanda wa Operesheni Maalumwa Jeshi la Polisi, Peter Mvulla akiwa
ameshika bomu la kutoa machozi aloilolichukua kutoka kwa mmoja wa
wanafuzi wa Shule ya Sekondari Kimnyaki iliyopo wilayani Arumeru Mkoa wa
Arusha. Bomu hilo lilirushwa kwa wanafunzi hao askari wa Kikosi cha
Kutuliza Ghasia (FFU) bila ya kulipuka na kuwaepusha na madhara ambayo
yangeweza kutokea. (Picha na Grace Macha)

Kova kuanza kusaka mtandao wa vipeperushi.

Waandishi Wetu
POLISI nchini wamepanga kusambaratisha mtandao unaodhamini na kuchapisha vipeperushi vinavyohamasisha kufanyika kwa maandamano, kutaka kutolewa kwa Katibu wa Taasisi za Kiislamu, Sheikh Ponda  Issa Ponda na wenzake.Hatua hiyo imekuja baada ya waumini hao kupanga kufanya maandamano  Novemba Mosi, ambayo yatahamasisha mahakama hiyo kutoa dhamana kwa kiongozi wa taasisi hiyo na wenzake.
 
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu, Suleiman Kova alisema wataanza kufanya msako wa wote wanaohamasisha, wanaochapisha na wanaotoa vipeperushi ili kuwakamata.
“Tunafuatilia wadhamini na wachapishaji wa vipeperushi kwani ni chanzo cha uchochezi na upotevu wa amani nchini,” alisema Kova.Kova alisema maandamano hayo ambayo yamepangwa na waumini hao yanatishia amani , wananchi watashindwa kwenda kazini na kurudisha nyuma maendeleo ya nchi.
“Hatuna mazungumzo tena kwa suala lolote litakalotishia uvunjifu wa amani hasa kwa yeyote atakayefanya maandamano bila kibali, hatutangalia anatoka dini gani au chama gani hivyo polisi itafanya kazi yake na kuwachukulia hatua kali,” alisema Kova na kuongeza:“Kisheria kumtishia mtu siyo lazima utumie bomu, bali unaweza ukatumia kauli au vipeperushi kama hivyo vya maandamano.”Alisema wazazi watakaoruhusu watoto wa shule kufanya maandamano watachukuliwa hatua za kisheria na kufikishwa mahakamani, ikiwezekana  kufungwa mwaka mmoja jela.“Nimesikia wanataka kuwahusisha watoto wasiende shule, ili wafanye maandamano ambayo yanazuiwa na sheria ya mtoto kutofanya maandamano,” alisema Kova na kuongeza:
 
“Sisi tutahakikisha sheria inachukua mkondo wake, kama kuna mtu amefikishwa mahakamani kuna taratibu zake za kupata dhamana, siyo kufanya maandamano haramu.”
Pia, aliwaomba wananchi wasishiriki maandamano hayo kwani yataleta madhara makubwa kwa familia zao kwa wale watakaokamatwa.“Hii inajidhihirisha pale utakapotembelea familia za wale waliokamatwa katika maandamano yaliyopita, watoto wanashindwa hata kwenda shule kutokana na kukamatwa kwa wazazi wao na wanakosa nauli na chakula,” alisema Kamanda Kova.

Vigogo 10 wahusishwa mabilioni ya Uswisi.

VIGOGO 10 wametajwa kuhusika katika kashfa ya kuficha Sh303.7 bilioni katika benki mbalimbali nchini Uswisi.Katika orodha hiyo inadaiwa kuwa yupo kiongozi mmoja mwandamizi mstaafu, maofisa watatu wastaafu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), mawaziri wastaafu ambao baadhi yao bado ni wabunge na aliyewahi kuwa kiongozi mwandamizi wa Benki Kuu Tanzania (BoT).
Majina hayo ambayo mwandishi wetu amefanikiwa kuyaona, yamo katika orodha ya mchunguzi mmoja wa kimataifa wa masuala ya ufisadi (jina tunalo).
 
Juzi, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe alimshukia Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Dk Edward Hoseah akimtuhumu kuandika barua Uswisi akisema Tanzania haina masilahi na mabilioni ya fedha yaliyofichwa katika benki zilizopo nchini humo. Hata hivyo, Dk Hoseah alikanusha madai hayo akisema hajawahi kufanya hivyo.
Akizungumza jana Zitto alisisitiza kauli yake akisema: “Sijawahi kumsema Dk Hoseah kwa lolote, kwa nini leo nimsingizie? Yeye mwenyewe anajua ushirikiano niliompa wakati wabunge wanapinga yeye asichunguze malipo ya posho mara mbili kwa wabunge.”
“Nilisimama kidete kusema Takukuru wapo sahihi na mimi nilikwenda mwenyewe kwao kuhojiwa na kuagiza wajumbe wa kamati yangu (Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma), waende kuhojiwa. Spika aliyestaafu (Samuel Sitta) akaizima kashfa ya wabunge kupokea posho mara mbilimbili. Mwulizeni amesahau? Sasa leo nimzushie ili iwe nini?.”

Alisema orodha ya Watanzania wenye fedha huko Uswisi, ipo na ameiona na nyaraka zinaweza kutolewa kwa taasisi za Serikali tu.
“Dk Hoseah kazuia nyaraka hizo. Akitaka nimwonyeshe mtu anayeweza kutoa nyaraka hizo, nipo tayari isipokuwa aahidi kuiweka wazi,” alisema Zitto.
Alisema katika orodha ambayo Waziri wa Fedha wa Ufaransa anayo, kuna Watanzania lakini akaituhumu Serikali akisema haitaki kufuata njia halali za kupata orodha hiyo kwa kuwa viongozi wengi na wafanyabiashara wakubwa wana akaunti katika benki za Uswisi.
Juni 26, mwaka huu gazeti hili lilichapisha habari kuhusu utoroshwaji wa fedha hizo na kueleza kuwa Polisi wa Kimataifa (Interpol) nchini kwa kushirikiana na Takukuru inachunguza suala hilo.
Kiasi hicho cha fedha kimedaiwa kuingizwa katika akaunti za Watanzania na kampuni moja ya uchimbaji mafuta na kampuni kadhaa za uchimbaji madini ambazo zinafanya kazi Tanzania.
Chanzo hicho kiliongeza kwamba kiasi hicho cha fedha kipo katika akaunti sita tofauti zinazomilikiwa na Watanzania wakiwamo wanasiasa wakubwa.

Hata hivyo, chanzo hicho kilieleza kuwa tangu akaunti hizo zifunguliwe, wamiliki wake halali hawajawahi kuingiza hata shilingi.
“Uchunguzi wetu unaonyesha kuwa fedha hizo zipo katika akaunti sita tofauti ambazo zinamilikiwa na wanasiasa wakubwa nchini na wenzetu wa Uswisi wameeleza fedha hizo zimeingizwa na kampuni kadhaa ambazo zinahusika na mafuta pamoja na madini hapa nchini,” kilidokeza  chanzo hicho.
Kugundulika kwa kiasi hicho cha fedha katika benki za Uswisi ni kutokana na ripoti ya Benki ya Taifa ya Uswisi (SNB) iliyotolewa mwaka huu.Via Mwananchi.

Udiwani: CCM chapoteza viti vinne.

Waandishi Wetu
LICHA ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kunyakua viti 22 kati ya 29 vya udiwani katika uchaguzi uliofanyika juzi, chama hicho tawala kimepoteza kata nne kilichokuwa kinazishikilia kabla ya uchaguzi huo.
Uchaguzi huo ulifanyika kuziba nafasi zilizoachwa wazi na madiwani walioondoka kutokana na sababu mbalimbali zikiwamo vifo.
Matokeo ya uchaguzi huo yanaonyesha kwamba katika Kata 29, Chadema wameshinda katika kata tano na kukifanya kuongeza madiwani watatu. TLP na CUF kila kimoja kimepata kata moja.
Kabla ya uchaguzi huo, Chadema kilikuwa na Kata mbili za Rombo na Mvomero ambazo kimefanikiwa kuzitetea na kuongeza nyingine tatu, ambazo ni Mlangila (Ludewa), Ipole (Tabora) na Daraja Mbili (Arusha) ambazo awali, zilikuwa zikishikiliwa na CCM.
TLP kilitetea kiti chake katika Kata ya Vunjo (Kilimanjaro) wakati CUF kilitwaa Kata ya Newala ambayo awali ilikuwa ikishikiliwa na CCM.
CCM kimetetea viti vyake vingine vilivyobaki ambavyo ni Msalato (Dodoma), Bang’ata (Arumeru Magharibi), Mletele (Songea), Mwawaza (Mjini Shinyanga), Lwezera (Geita), Bugarama (Kahama) na Bagamoyo mkoani  Pwani.
Viti vingine ni Mnero na Miembeni (Nachingwea), Myovizi (Mbozi), Mpapa (Momba), Mahenge (Ulanga), Vugiri (Korogwe), Tamota (Lushoto), Makata (Liwale), Mpepai (Mbinga), Kiloleli (Sikonge), Miyenze (Tabora), Karitu (Nzega), Lubili (Misungwi), Kilema Kusini (Moshi), Nanjara/Neha (Rombo), Lokokona (Nanyumbu) na Kitangiri (Newala).
Katika Kata ya Rwezera, Misango Jeremiah alishinda baada ya kupata kura 1,309 dhidi ya wapinzani wake, Ibuga Mussa (Chadema) aliyepata kura 933 na Mussa Mtagala (CUC) aliyepata kura 317.  Uchaguzi huo ulifanyika kujaza nafasi hiyo iliyokuwa wazi baada ya aliyekuwa Diwani wa Kata hiyo, Anatory Mkufu kufariki dunia kwa ajali ya gari Februari 23, mwaka huu.

Kilimanjaro
Katika Kata ya Kilema Kusini, Joseph Rubega wa TLP alishinda kwa kura 1,044 wakati Peter Temu (CCM) alipata kura 797 akifuatiwa na Serafine Mbuya (Chadema) kura 736 na Paul Shirima wa DP kura 13.
Katika Kata ya Nanjara Reheha, Rombo, Frank Salakana (Chadema) alishinda kwa kura 2,370 na kumshinda mpinzani  wake pekee kutoka CCM, Dismas Silayo aliyepata kura 1,128.

Lindi
Katika Kata ya Mnero Miembeni, Gervas
Ungele (CCM) alipata kura 818 wakati Jumanne Ali (CUF) alikuwa wa pili kwa kura 611 na Sinji Ali (Chadema) alipata kura 138.

Mbozi na Momba
Katika Kata ya Myovizi, Mbozi Cosmas Nzowa (CCM) alipata kura 1,726 huku Musa Mtakati  (Chadema) akipata kura 1,498.
Katika Kata ya Mpapa, Momba, Nolatico Simbeye (CCM) alishinda kwa kura 903 na mpinzani wake, Ladius Kasonso (Chadema) alipata kura 310.

Morogoro
CCM kilishinda katika Kata ya Mahenge kwa Mark Asenga, kupata kura 710 , dhidi ya Baltazar Kizee (Chadema) aliyepata kura 444.
Katika Kata ya Mtibwa, Mwakambaya  Edward (Chadema), alishinda kwa kura 3,096 na Musa Kingu (CCM) alipata kura 1,372.


Arusha
Kata ya Daraja Mbili, iliyokuwa ikishikiliwa na CCM kabla ya diwani wake, Bashiri Msangi kufariki dunia ghafla mapema mwaka huu, Chadema kiliibuka na ushindi baada ya mgombea wake, Prosper Msofe kupata kura 2,193 dhidi ya Philip Mushi wa CCM aliyepata kura 1,324. Mgombea wa CUF, Zani Hassan Zakaria alipata kura 162, William Msuyakura (TLP) alipata 42, Mohamed Msuya wa NCCR Mageuzi alipata kura 22.
Uchaguzi huo, unafanyika wakati bado kuna viti sita vya
udiwani katika Manispaa ya Arusha, vikiwa wazi. Madiwani watano kati yao walitimuliwa na Chadema na diwani mwingine wa Kata ya Sombetini, Alphonce Mawazo alijiondoa CCM na kujiunga na Chadema.

Nape alonga
Akizungumzia matokeo hayo jana, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema chama chake kinajivunia mafanikio yaliyopatikana katika uchaguzi huo mdogo akisema umeonyesha dalili kwamba wananchi bado wana matumaini nacho.
Alisema uchaguzi huo unaonyesha kuwa kinakubalika na wengi tofauti na inavyofikiriwa... “Tunajivunia ushindi katika Kata 22. Naweza kusema ni sawa na asilimia 75. TLP, ilipata kata moja na CUF kilipata kata moja na Chadema ilipata kata tano.”
Kutokana na ushindi huo, Nnauye aliendeleza malumbano yake na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa akimtaka achane na siasa badala yake awaachie vijana kukiendesha.
“Huu ni ushindi wa kimbunga, huo ni udiwani tu, pamoja na kwamba tumepoteza baadhi ya kata, lakini haisumbui sana kwani ushindi tuliopata ni wazi unaonyesha Chadema imepoteza mvuto kwa wananchi.
“Nawashukuru wananchi waliokiamini chama chetu na kukipa ridhaa ya kuongoza kata zao maana baadhi ya watu wamekuwa wakitoa taarifa za uongo kwamba kinaelekea kaburini lakini uchaguzi mdogo umewaonyesha walivyo waongo,” alisema Nnauye.
Alisema kinachomfanya amtake Dk Slaa kuachana na siasa ni kutokana na jitihada ambazo zimefanywa na chama hicho kuzunguka mikoa yote kikifanya kampeni za Vuguvugu la Mabadiliko (M4C) lakini akasema wameambulia patupu.

Vurugu CCM
Kuhusu vurugu za wanachama wa UVCCM kutwangana hadharani na suala la rushwa katika uchaguzi, Nnauye alisema CCM kinasubiri ripoti kuhusiana na vurugu pamoja na madai ya kukithiri kwa rushwa wakati wa chaguzi za chama hicho.
Katika uchaguzi wa ngazi mbalimbali ikiwamo uwakilishi wa Nec wilaya, mikoa, Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) na ule wa Vijana (UVCCM) suala la rushwa lilichukua nafasi kubwa.
Nnauye alisema mpaka sasa ofisi yake haijapokea malalamiko kuhusiana na chaguzi hizo... “Ingawa malalamiko yote hupelekwa sekretarieti ya maadili  ya uchaguzi ya chama, lakini pia huwa ninapata taarifa isipokuwa kwa sasa hakuna malalamiko yoyote.”
Juu ya kuzuka kwa vurugu baada ya uchaguzi wa UVCCM alisema suala hilo linasubiri ripoti ya matukio ambayo yamejitokeza katika uchaguzi na baadaye tathmini itafanywa.
Aliwataka makada wanaolalamikia kukithiri kwa rushwa katika chaguzi za chama hicho kufuata utaratibu wa chama badala ya kukimbilia majukwaani.
Habari hii imeandikwa na Salum Maige (Geita), Venance George (Morogoro), Mussa Juma na Moses Mashalla (Arusha), Stephano Simbeye (Mbozi), Christopher Lilai (Nachingwea), Daniel Mjema (Moshi) na Gadius Rwiza (Dar).

Tuesday, October 30, 2012

WOLPER ATEMWA RASMI NA MPENZI WAKE DALLAS.

WAKATI hali ya kimaisha ikiwa tete kwa msanii anayefunika kwa urembo bongo movie Jackline Wolper, ambaye alikuwa akitembelea magari ya kifahari kila kukicha, sasa anachoambulia ni pole kwani shosti yake wa karibu Sintah, amedai kuwa kuachana kwao na ‘Dallas’ kutamfanya Wolper ayakumbuke magari yake ya zamani kama vile Noah.

Wolper ni msanii wa kwanza bongo kutembelea magari ya kifahari tena baada ya kumpata jamaa huyo lakini awali kabisa alikuwa akitembelea Noah, na inadaiwa kuwa sasa atakuwa akiyaona kwa macho watu wakiendesha kwani Dallas amechukua funguo zote za magari yake.Ishu hii ikiwa inashika kasi mjini huku watu wakiwa macho juu kutaka kuona nini kinachoendelea kwa WolperSintah hakusita kudai kuwa mara nyingi mapenzi ya kwenye magazeti huwa hayadumu kwani awali kabisa Wolper alijitangazia kuwa hawawezi kuachana na Dallas huku akisahau kuwa kuna wabaya wake wanaomtazama.



Akiongea na mwandishi wa habari  hii, Sintah alidai kuwa kwa jinsi anavyo mfahamu Wolper haoni kama yeye atakuwa ndiye chanzo cha kuachana kwao kwani kuna wabaya wake ambao wamejaa fitna, lakini kwa upande wake anampa pole ili sasa ajipange na kuacha tabia ya kuishi mjini kwa kuwatengemea wanaume, hasa wale anaokutana nao mjini.“Kuachana ni kawaida miaka ya sasa kwanza kama huna hela huwezi kutembea na staa bongo na Dallas alimpenda Wolper kwa sababu ni staa, lakini sioni kama kuna tatizo wao kuachana kwani wamekutana mjini na wanaachana kimjini,” alidai Sintah.

MWANAFUNZI WA DARASA LA TATU SHULE YA MSINGI IWAMBI MKOANI MBEYA AJINYONGA'

Mama mzazi wa marehemu Kervin Patrick (8)Bi Subira Patrick(38) akiwa katika hali ya majonzi kufuatika kifo cha mwanae aliyejinyonga.Mwili wa Mwanafunzi wa darasa la tatu, Shule ya Msingi Iwambi, Jijini Mbeya Kervin Patrick (8) jinsia ya kiume ukiwa umefunikwa baada ya kufariki dunia kutokana na kujinyonga kwa kutumia kamba ya viatu katika bomba ya maji nje ya nyumba yao.

Baadhi ya majirani waliojitokeza kushuhudia mwili Mwili wa Mwanafunzi wa darasa la tatu, Shule ya Msingi Iwambi, Jijini Mbeya Kervin Patrick (8). 
Baadhi ya mashuhuda wakiwa wamekusanyika kushuhudia Mwili wa Mkazi wa Kitongoji cha Gezaulole, Kijiji cha Haporoto Kata ya Ihango Wilaya ya Mbeya Vijijini Mkoani Mbeya Mbwiga Mwandele(50 -55)  amejinyonga kwa kutumia mkanda wa Suruali yake katika Ofisi ya kijiji hicho.

Baada ya kuyaaga mashindano, Norman Severino anawaambia hivi mashabiki wake.

NITAITUMIA VIZURI ELIMU YA MUZIKI NILIYOIPATA EBSS ACADEMY NA NAWAAHIDI MASHABIKI WANGU KUTOA NYIMBO NZURI HIVI KARIBUNI. TUKO PAMOJA NAHITAJI SANA SUPPORT YENU.

POMBE NA MITUNGI YAWAPONZA NISHA NA BABY MADAHA.

MASTAA wa filamu Bongo, Salma Jabu ‘Nisha’ na Baby Joseph ‘Baby Madaha’ juzikati walijikuta wakiingia kujisaidia choo cha kiume bila kujielewa.

Ishu hiyo iliyopigwa chabo na mpekuzi wetu, ilijiri hivi karibuni katika hoteli moja jijini Dar wakati mastaa hao walipokuwa wakimpongeza Flora Mvungi kutokana na kufanyiwa sherehe ya kumtolea mahari.Pasipo kujielewa baada ya kilevi kufika mahali pake, wauza nyago hao waliovamia gemu la muziki, walijikuta wanazama katika choo cha kiume kwenda kujisaidia haja ndogo.

Treni yaanza kwa hujuma.

UZINDUZI wa safari za treni ya abiria jijini la Dar es Salaam, nusura uingie dosari jana wakati kibaka aliyetambuliwa kwa jina la Vincent Michael alipoamua kuiba vyuma vya breki katika moja ya mabehewa yaliyoegeshwa katika kituo cha Yombo.
Tukio hilo lilifanyika muda mfupi kabla ya treni iliyombeba Waziri wa Uchukuzi Dk. Harrison Mwakyembe haijafika katika kituo hicho.
Msafara wa Dk. Mwakyembe aliyeambatana na waandishi wa habari pamoja na maofisa wa Sumatra na wale wa Shirika la usafirishaji la Tanzania na Zambia (TAZARA), ulikuwa unarejea stesheni ya Dar es Salaam, ukitokea katika kituo cha Mwakanga nje ya jiji.
Safari hiyo ilikuwa ni baada ya Waziri Mwakyembe kuzindua usafiri wa aina hiyo kwa treni ya Shirikla la Reli nchini (TRL), uliofanyika eneo la Ubungo Maziwa.

Mmoja wa maofisa wanaolinda katika eneo hilo la Yombo, aliyeomba jina lake lihifadhiwe kwa kuwa si msemaji, alisema kuwa walimkamata kibaka huyo wakati akitekeleza uhalifu wake pasipo kuhofia athari zitakazojitokeza endapo behewa hilo lingeanza kufanya safari zake.
Kufuatia tukio hilo kibaka huyo alibebwa katika moja ya mabehewa yaliyombeba Waziri Mwakyembe na kisha kufikishwa katika Kituo cha Polisi Tazara kwa hatua zaidi.
Awali, Waziri Mwakyembe akizindua treni hizo za Tazara na TRL kwa ajili ya usafiri wa ndani ya Jiji la Dar es Salaam, akisema amefurahishwa kuona ndoto yake imetimia na kutoa pongezi kwa mafundi wa mashirika hayo kusiamama kidete kuhakikisha usafiri huo unaanza kama walivyopanga.

Dk. Mwakyembe alisema usafiri huo ulikuwa ukisubiriwa kwa muda mrefu na wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, hivyo kuwataka kuhakikisha kuwa wanatunza miundombinu iliyopo kwa ajili ya kuokoa fedha za Watanzania zilizotumika kuboresha hali hiyo.
“Kumbukeni kulikuwa na changamoto nyingi juu ya huu mradi, kipekee niwashukuru mafundi wa mashirika yote mawili waliowezesha kufanyika kwa haya mnayoyaona leo, kwa maana waliponiambia inawezekana, mwanzo niliitikia nikiwa siamini kama muda huu watakuwa wamekamilisha kazi, kwa namna mabehewa yalivyokuwa yamechakaa,” alisema.

Aliongeza kuwa kama serikali itaamua kuwekeza kwa dhati kwa Watanzania basi wanaweza kufanya mambo makubwa kwa muda mfupi kama ambavyo imedhihirishwa katika harakati za kuwapatia usafiri wa treni katika Jiji la Dar es Salaam.
Naye Naibu Mkurugenzi wa Tazara, Damas Ndumbaro, alisema wamejipanga kutoa huduma bora ya usafiri ikiwa ni pamoja na kudhibiti mapato yatokanayo na uuzwaji wa tiketi za kila siku.
Habari na Abdallah Khamis.

CHADEMA: Tumeshinda.

WASEMA NAPE ANAPIGA VUVUZELA BILA TATHMINI.Habari na Shehe Semtawa
WAKATI Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC) Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, akitambia ushindi mkubwa walioupata katika kata 22 kwenye uchaguzi mdogo uliofanyika Jumapili, CHADEMA wamemtaka aache kuwa kama vuvuzela, wakidai wao ndio washindi.
Chama hicho kimesema kutokana na idadi kubwa ya kura walizopata katika kata zote hata zile ambazo hawakushinda ni dhahiri kuwa ngome yao inazidi kuimarika maeneo mengi nchini kiasi cha kuweza kuwanyang’anya CCM kata.
Kauli ya CHADEMA ilitolewa na Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Taifa (Bavicha), John Heche, wakati akijibu tambo za Nape na kudai kuwa kada huyo ni sawa na vuvuzela, kwani kama angekuwa anafanya tathmini angeweza kubaini ni kwanini wananchi wanazidi kuikataa CCM.

Akizungumza na waandishi wa habari jana katika ofisi ndogo za chama hicho zilizopo Mtaa wa Lumumba, Nape alisema kuwa idadi kubwa hiyo ya madiwani waliyopata ni ishara kwamba CCM bado kinakubalika kwa wananchi na kitaendelea kushinda katika chaguzi zijazo.
Kauli ya Nape inakuja ikiwa ni siku moja tangu kumalizika kwa uchaguzi huo mdogo kwenye kata 29, ambapo CCM iliweza kurejesha kata zake 22 na kupoteza tatu zilizochukuliwa na CHADEMA iliyoshinda kata tano na CUF ikipata kata moja.
Nape alisema ushindi huo umetokana na chama hicho kuhubiri amani mara kwa mara katika mikutano yake, tofauti na vyama vingine ambavyo sera zao ni za kumwaga damu, kitendo ambacho wananchi hawakikubali.
“Ushindi huu unadhihirisha kuwa hata katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 chama chetu kitawashinda wapinzani,” alijigamba.

Nape aliponda opereshini ya Vuguvugu la Mabadiliko (M4C) inayoendeshwa na CHADEMA nchi mzima, akidai inaandamana na vurugu na kwamba haitakisaidia chama hicho.
Alisema operesheni hizo zimekuwa zikisababisha vurugu na vifo katika maeneo mbambali kilipopita chama hicho.
“Juhudi zote walizofanya Katibu Mkuu, Dk. Slaa na Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe, hazikuzaa matunda, hiyo inatokana na siasa chafu za vurugu, hivyo wananchi wameamua kukinyima ushindi,” alisema.
Nape pia alisema kuwa CCM inalaani vurugu zilizotokea katika baadhi ya maeneo kulikofanyika uchaguzi huo kwamba huo si utamaduni wa Watanzania.

Alisema kuwa uchaguzi ulifanyika katika kata 29 na kati ya hizo 27 zilikuwa za CCM na mbili za CHADEMA, hivyo wao waliweza kuzirejesha kata zao na kutwaa nyingine tatu.
“Nape aache kupiga kelele kama vuvuzela bali wakae chini na kujifanyia tathmini, wajiulize ni kwanini watu wanazidi kuwakataa. Sisi kwanza tumeweka historia tangu mfumo wa vyama vingi uanze kwa kusimamisha wagombea kwenye kata zote, tumeweza kutetea kata zetu mbili na kuchukua za CCM tatu,” alisema.
Katika kujibu hoja hizo, Heche alisema kuwa wanachokifanya CCM sasa ni sawa na kufiwa na watoto halafu ukajipongeza kwa wale waliobaki, huku akibainisha kuwa uchaguzi huo umewawezesha CHADEMA kufika katika vijiji 116 na kusimika matawi.

Kuhusu madai ya Nape kwamba Operesheni ya M4C haikufua dafu katika uchaguzi huo kwa vile inachochea vurugu, alisema kuwa taarifa za magazeti mengi ya jana zilieleza bayana kuwa vitendo vya vurugu kwenye uchaguzi vilisababishwa na CCM kwa kuwashambulia wafuasi wa CHADEMA.
“CCM ni chama cha rushwa na wamechaguana kwa rushwa hata Mwenyekiti wao Jakaya Kikwete amekemea hilo kwenye mikutano ya UVCCM na UWT, sasa kwa mantiki hiyo Nape apime mwenyewe nani kapoteza na kama anafikiri tunafanya mzaha, basi angoje mwaka 2015,” alisema.

TFDA matatani ARV’s bandia.

MAMLAKA ya Chakula na Dawa (TFDA) imewekwa matatani ikielezwa kuwa nayo inastahiki kuchukuliwa hatua kutokana na kuzembea katika ukaguzi wa dawa na hivyo kusababisha dawa bandia za kupunguza makali ya ukimwi (ARV’s) kusambazwa.
Sakata hilo linakuja wiki chache tangu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Hussein Mwinyi, kumsimamisha kazi Mkurugenzi wa Bohari ya Dawa (MSD), Joseph Mgaya, na viongozi wengine kupisha uchunguzi wa tuhuma za kusambaza dawa hizo.
Wengine waliosimamishwa kazi ni mkuu wa kitengo cha udhibiti ubora na ofisa uthibiti ubora huku kiwanda cha dawa cha Tanzania Pharmaceutical Industries Ltd (TPI) kikisitishiwa uzalishaji na usambazaji wa dawa zilizokwishatengenezwa.
Taarifa za ndani ya TFDA ambazo Tanzania Daima imedokezwa na mmoja wa maofisa wake ambaye aliomba kuhifadhiwa jina kwa vile si msemaji, zilisema kuwa mamlaka hiyo nayo ilizembea katika sakata zima la dawa bandia za ARV’s kusambazwa.
Kiwanda chochote kabla ya kuzalisha dawa au chakula nai lazima kipate kibali cha TFDA baada ya kukaguliwa na kukidhi viwango husika.

“Hata dawa ingekuwa inaingizwa kutoka nje ya nchi, vilevile TFDA inapaswa kukikagua kiwanda husika kuona kama kina ubora wa kutengeneza dawa na kukidhi viwango,” kilisema chanzo chetu.
Gazeti hili pia limefanikiwa kupata nakala ya waraka wa TFDA kuhusu hali ya viwanda vya dawa nchini, ambayo inabainisha kuwa Tanzania ina viwanda saba vya dawa vilivyosajiliwa katika mwaka 2011/2012.
Viwanda hivyo ni Shelys Pharmaceuticals Ltd, Zenufa Laboratories Ltd, Mansoor Daya Chemicals Ltd, Keko Pharmaceuticals (1997) Ltd, Tanzania Pharmaceutical Industries Ltd, A.A. Pharmaceuticals Ltd na Tanzansino United Pharmaceuticals (T) Ltd.

Waraka huo unabainisha kuwa kiwanda cha Tanzansino United Pharmaceuticals (T) Ltd, ambacho serikali kupitia Jeshi la Kujenga Taifa ni mmbia mmojawapo kimesimamisha utengenezaji dawa tangu Agosti 2010 kutokana na mwekezaji wa nje kujiondoa.
“Ukaguzi uliofanywa na TFDA katika miaka ya fedha ya 2010/11 na 2011/12 umeonyesha kuwa hakuna kiwanda kilichokidhi viwango vya utengenezaji wa dawa,” alisema ripoti yao.
TFDA katika taarifa yake hiyo inakiri kuwa viwanda vya dawa hapa nchini katika kipindi cha miaka miwili iliyopita vimeshindwa kukidhi vigezo vya usajili wa dawa.
Kutokana na hali hiyo dawa za viwanda hivyo zimekuwa zikiruhusiwa na mamlaka hiyo kuwepo sokoni kwa kuzingatia utaratibu maalumu ambao hauzingatii vigezo vyote vya usajili wa dawa.
“Utaratibu huu ulikuwa wa muda mfupi uliokuwa na nia ya kutoa muda kwa kiwanda husika kurekebisha mapungufu ili dawa zao zisajiliwe. Baadhi ya dawa zinazotengenezwa na viwanda vya ndani ni za tiba za ugonjwa wa malaria na vijiua sumu,” iliongeza taarifa.Via Tanzania Daima.

Pia inafafanua kuwa katika siku za karibuni, sampuli za matoleo (batches) kadhaa za dawa za viwanda hivyo zilizochukuliwa katika soko na kuchunguzwa zimeonekana kuwa na ubora duni na hivyo kuondolewa.
Ni katika mtiririko huo, mtoa habari wetu anasema TFDA haijawahi kutoa kibali kwa kiwanda cha TPI kuzalisha dawa za ARV’s kinachoonyesha kuwa kiwanda hicho kimekidhi vigezo tajwa.
Lakini katika hali inayoonyesha kutokuwepo umakini, TFDA ilizisajili dawa hizo za ARV’s kutoka TPI wakati katika ripoti yake wanakiri kuwa kiwanda hicho hakina sifa za kuzizalisha.

“Dawa inaweza kuwa moja lakini ikawa na matoleo tofauti, hivyo hata toleo hilo la dawa bandia zinazolalamikiwa halikuletwa TFDA kwa ukaguzi maana ingebainika haraka kabla ya kuingia sokoni,” kiliongeza chanzo hicho.
Ofisa huyo anashauri kuwa TFDA ilipaswa kuwa na mkaguzi wake ndani ya MSD ambaye angekuwa anasaidia kukagua na kuhakikisha dawa hizo hazizalishwi na kusambazwa.“Hapa utaona kuwa haikuwa sahihi kumwajibisha mkurugenzi wa MSD pekee na kutuacha TFDA ambao hatukutimiza wajibu wetu. MSD hawana utaalamu wa kuchunguza dawa bandia hiyo ni kazi ya TFDA,” alisisitiza ofisa huyo.
Dawa hiyo bandia aina ya TT-VIR 30 toleo namba OC.01.85 iliyotengenezwa Machi 2011 na kuisha matumizi Februari 2013, nyaraka zake zilionyesha kiwanda cha TPI kiliwauzia MSD.
Waziri Mwinyi alieleza kuwa vidonge vilivyokutwa kwenye vifungashio vya dawa husika vilikuwa vimesajiliwa na TFDA.
Mkurugenzi Mkuu wa TFDA jana alipotafutwa kwa njia ya simu, alisema atatoa ufafanuzi wake leo akiwa ofisini.

Monday, October 29, 2012

Wimbo mpya wa Diamond ni Sample ya wimbo wa Pasha-Amekuwa.


SIKILIZA KISHA TOA MAONI YAKO

 Artist: Diamond Platnumz Song: Nataka Kulewa Studio: A.M Records

Artist: Pasha ft. Tunda man Song: Amekua Studio: Burn Records

NIMEMSAMEHE LORD EYEZ NA WENZAKE"OMMY DIMPOZ

Nyota wa muziki wa  kizazi kipya nchini Ommy Dimpoz amesema kuwa licha ya kutumia kiasi cha  shilingi milioni 5 kurudisha gari yake kwenye hali ya kawaida hawezi kumchukia msanii mwenzake Lord Eyez anayeshikiliwa korokoroni hivi sasa kwa tuhuma za kuiba vifaa kutoka kwenye gari yake.

Akizungumza na mtandao huu  mapema leo Ommy Dimpoz amefunguka kuwa ingawa kwa sasa haruhusiwi kusema lolote  kuhusu jambo hilo lakini anayo haki ya kusema kuwa binafsi amesamehe na anamuachia Mungu.

“Nafahamu kuwa kuwa siruhusiwi kuzungumza lolote kwa kuwa suala liko Polisi,ninachoweza kukwambia  ni kuwa binafsi nimemsamehe Lord na wenzake, sababu huwezi kujua kuhusu kesho, nimepanga  kukutana naye na kumwambia hili jambo, najisikia vibaya lakini nashukuru kuwa gari yangu nimeshairekebisha na sasa ndiyo ninayoitumia tena licha ya kuwa nimetumiagharama kubwa” alisema Dimpoz.

Katika hatua nyingine nyota huyo wa songi la ‘Badae’ ameanika kuwa wimbo huo umemuingizia kiasi kikubwa cha pesa tofauti na yalivyokuwa matarajio yake  huku pia akijikusanyia wingi wa marafiki ndani na nje ya nchi kupitia wimbo huo.

P -SQUARE WAKANUSHA KUMTOA KAFARA MAMA YAO

Mapacha wa kundi la P-Square la nchini Nigeria hatimaye wamefunguka kuzikanusha tetesi kuwa walimtoa kafara mama yao mzazi ili watajirike na kufanikiwa zaidi kimuziki.Katika mahojiano exclusive na gazeti la Vanguard la nchini Nigeria, Peter na Paul wamesema.


“Basi, ni mbaya sana kusikia kuwa watu wanatushutumu kwa kuhusika na kifo cha mama yetu. Hatumlamu mtu yeyote. Watu wako huru kusema chochote wanachotaka kusema. Tunashangaa kama kuna kitu chochote kitakachotufanya tuchukue maisha ya mama yetu mpendwa.

Maisha yake hayawezi kupimwa kwa fedha na umaarufu. Hivyo jibu letu kwa swali hili ni kwamba hatuhusiki na kifo cha mama yetu. Tunakilaumu tu kifo kilichomchukua mbali nasi ambacho kama si chenyewe watu wasingekuwa wanatunyooshea vidole. Alifariki baada ya ugonjwa wa muda mfupi.”

BREAKING NEWS - AZAM FC YAMTIMUA KOCHA WAKE BORIS BUNJAK

Hatua hii imekuja siku mbili baada ya Azam FC kufungwa 3-1 na Simba katika mechi ya ligi kuu.    Sababu kwanini ametimuliwa endelea kutembelea mtandao huu.

Kocha wa Azam FC mserbia Boris Bunjak ametimuliwa rasmi kuifundisha timu hiyo.Taarifa rasmi nilizozipata kutoka ndani ya klabu hiyo inayoshiriki ligi kuu ya VPL zinasema kwamba kocha huyo aliyesaini mkataba wa miaka miwili wa kuifundisha Azam mwezi nane mwaka huu ametimuliwa na sasa viongozi wa klabu hiyo wapo katika harakati za kutaka kumrudisha kocha wao wa zamani Muingereza Stewart Hall.    

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate