Friday, May 24, 2013

Asilimia 31 ya Watanzania ni walevi.

Dodoma. 
Asilimia 26.8 hadi asilimia 31.9 ya Watanzania wanatumia pombe na asilimia 27.4 kati ya hao ambao ni wanaume na wengine asilimia 13.4 ambao ni wanawake, ni walevi wa kupindukia. Bunge lilielezwa jana.


Takwimu hizo zilitolewa na Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Seif Rashid, ambaye alisema kuwa viwango hivyo vimetokana na utafiti uliofanywa kati ya Februari hadi Oktoba mwaka jana 2012.

Kwa mujibu wa naibu waziri, utafiti huo ulifanywa na Shirika la Afya Duniani (WHO).
Alikuwa akijibu swali la Abdallah Haji Ali (Kiwani–CUF) aliyetaka kujua kauli ya Serikali kuhusu utumiaji wa pombe ambao umethibitika kuwa ni hatari kwa afya za binadamu.
Pia alipendekeza pombe ipigwe marufuku kabisa hapa nchini kwa kuzingatia madhara yake.

Naibu waziri alisema tafiti zimeonyesha kuwa watu milioni mbili wanafariki dunia kila mwaka duniani kutokana na madhara ya matumizi ya pombe na asilimia nne ya matatizo ya kiafya yanatokana na matumizi ya pombe.

Hoyce Temu kuwafunda Redds Miss Kigamboni Dar es Salaam,Juni 7.

MREMBO wa Tanzania mwaka 1999, Hoyce Temu, leo anatarajiwa kukutana na washiriki wanaowania taji la kitongoji cha Kigamboni, ‘Redd’s Miss Kigamboni 2013’ ili kuwapa nasaha mbalimbali kuhusiana na sanaa hiyo.

Shindano la Redd’s Miss Kigamboni, linatarajiwa kufanyika kwenye Ukumbi wa Navy Beach kuanzia saa 2:00 usiku hapa jijini Dar es Salaam, Juni 7.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, mratibu wa shindano hilo, Somoe Ng’itu, alisema kuwa maandalizi yako katika hatua za mwisho na lengo la kumualika Hoyce ni kuwapa nafasi warembo kujifunza mambo mbalimbali yanayohusu sanaa hiyo.
Mratibu huyo alisema kuwa washiriki hao watajifunza mambo ya msingi kupitia mrembo huyo ambaye pia atawapa uelewa wa mbinu watakazokutana nazo kwenye mashindano ya kanda, taifa na baadaye fainali za dunia.

“Ni fursa ambayo tunatarajia warembo wetu wapate, nia ya kufanya hivi ni kuwaandaa kufanya vizuri, tumejipanga kupata mafanikio zaidi ya tuliyovuna mwaka jana,” alisema Somoe.
Aliongeza kuwa hadi sasa warembo 12 wanaendelea na mazoezi chini ya mkufunzi Blessing Ngowi.

Aliwataja washiriki hao kuwa ni pamoja na Rogathe Michael, Irene Rajab, Magdalena Olotu, Latifa Mohammed, Axsaritha Vedastus, Angella Lutataza, Sara Makembo, Amina Mussa, Ellen Sulle, Julieth Mwanri na Rachel Reuben.

Alitoa wito kwa kampuni na taasisi mbalimbali, kudhamini shindano hilo ambalo mwaka jana lilitoa mshindi katika kinyang’anyiro cha kanda ya Temeke, ambaye ni Edda Sylivester.
Warembo watano watakaoshika nafasi za juu kwenye shindano hilo, watapata nafasi ya kushiriki kinyang’anyiro cha Redd’s Miss Temeke baadaye mwaka huu.
Wadhamini ambao wamethibitisha kusaidia shindano hilo ni pamoja na Kampuni ya Bia Tanzania kupitia kinywaji cha Redd’s Premium Original, Montage Limited, Clouds Media Group, Papa Z na Break Point.
Taji la Redd’s Miss Tanzania linashikiliwa na Brigitte Alfred wakati Edda alifanikiwa kushika nafasi ya tatu kwenye fainali hizo za taifa mwaka jana.

TUNAPENDA KUWAJUZA KUWA SASA MZIGO MUPYA MLIOKUWA MKIUSUBIRI KWA HAMU UMEINGIA - AK CLASSIC COSMETICS.

STOCK TAKING IKIENDELEA...
Maduka yapo Dar es salaam Sinza kumekucha na  Kinondoni Manyanya tupigie - 0713 468 393 au 0753 482 909. Tutembelee hapa www.akclassic.blogspot.com
WALE WAKUNUKIA KIDESIGNER DESIGNER HATUWEZI KUWAACHA!!MAMBO YENU YAPO..

WALE WA KUPIGA MSASA NGOZI ZAO ILI ZISIFUBAE VITU VILIVYOTHIBITISHWA HIVI HAPA!!INAITWA ETREME GLOW MAMBO YAKE YANAKUBALIKA SAAANA TENA SAAANA!!!

WAZAZI KUKWEPA MAJUKUMU YAO SABABU ZA WATOTO KUJIAJIRI JIJINI MBEYA.

Kutoka kushoto ni Fredrick Simon (12), Lushindiho Simkonda (10) na Colyns John (8) wakiwa na mzigo wa tofali.
Mtoto Colyns John mwenye umri wa miaka 8 ambaye ni mwanafunzi wa darasa la pili Shule ya Msingi Ikuti jijini Mbeya (kushoto), akiwa na mwenzake Lushindiho Simkonda (10) ambaye hasomi shule wakiwa wamebeba matofali kuyapeleka walipoajiriwa ambapo kwa kila tofali moja hulipwa shilingi 30.

TENGENEZA WEBSITE NA BLOG ZENYE MVUTO.

Tupigie simu upate Website na blog yenye muonekano wa kuvutia.Na tunafanya Blog na Website Modification kwa bei nafuu sana.

KOCHA wa Yanga,Ernie Brandts kurejea Rwanda kuinoa timu ya taifa ya Rwanda ‘Amavubi.

KOCHA mkuu wa klabu ya Yanga, Ernie Brandts, anatarajiwa kurejea nchini Rwanda kuinoa timu ya taifa ya Rwanda ‘Amavubi’.

Brandts kabla ya kujiunga na Yanga na kuiwezesha kutwaa ubingwa wa Ligi kuu ya Vodacom msimu huu, alitokea Rwanda alikokuwa akiinoa klabu ya APR.

Rafiki wa karibu wa kocha huyo ambaye hakutaka kutajwa hadharani, aliipasha Tanzania Daima jana kuwa Brandts ameitwa nchini Rwanda kwa ajili ya kukinoa kikosi hicho kilichokuwa kinanolewa na Milutin Sredojevic ‘Micho’ ambaye alitupiwa virago hivi karibuni kutokana na timu hiyo kuvuna matokeo mabovu katika mechi zake kadhaa. Micho hivi sasa kaula timu ya taifa ya Uganda ‘The Cranes’.

Rafiki huyo alisema Brandts alimwambia kuwa anakwenda kufanya nao mazungumzo kwa kuwa tayari ameishapata ofa hiyo na kudai kuwa itakuwa ngumu kurejea Yanga kama mambo ‘yatatiki’ nchini Rwanda.

“Brandts kurudi Yanga ni mpaka mambo yakikataa Rwanda, ila ni asilimia ndogo sana ya kurudi Yanga, kama ambavyo aliniambia mimi,” alisema rafiki huyo.
Shirikisho la soka nchini Rwanda, Ferwafa, lilimtupia virago Micho, April 17, mwaka huu, katika taarifa iliyotumwa na Katibu Mkuu wa Ferwafa, Michel Gasingwa, kupitia mtandao, ambayo ilidai kuwa kamati ya utendaji ilifikia uamuzi huo ili kuinusuru timu isiendelee kuboronga katika mechi zake.

STARS YAJAZWA MANOTI KUSAIDIA KUIUWA MOROCCO.

Wajumbe wa Kamati ya Saidia Taifa Stars Ishinde, wakiwakabidhi nahodha wa Stars, Juma Kaseja na Meneja Leopold Taso Mukebezi, (kushoto), kitita cha sh milioni 30 kama moja ya hamasa kwa timu hiyo kufanya vema katika kinyang’anyiro cha kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia mwakani nchini Brazil. Kutoka kulia ni Dk. Ramadhani Dau, Zitto Kabwe, Mohamed Dewji ‘Mo’ ambaye ndiye Mwenyekiti, Leodegar Tenga na Teddy Mapunda. 

WACHEZAJI wa timu ya Taifa,  Taifa Stars jana walikabidhiwa Milioni 30, ikiwa ni pongezi ya kufanya vizuri dhidi ya Zambia na Morocco, huku wakiwatakiwa kuhakikisha wanashinda mechi ya marudiano dhidi ya Morocco.

Majambazi yatikisa Dar •Yapora milioni 46/- bila upinzani

WATU wanaoaminika kuwa ni majambazi ambao idadi yao haijafahamika, wamepora sh milioni 46, huku polisi wakishuhudia bila kutoa upinzani kukabiliana nao.

Fedha zilizoporwa ni mali ya mfanyabiashara wa bia za jumla jijini Dar es Salaam, Ivon Urio, wa wilayani Temeke.

Wakati majambazi wa Temeke wakipora kiasi hicho bila upinzani, tukio lingine la ujambazi limetokea jana asubuhi katika mtaa wa Sayansi na Kijitonyama wilayani Kinondoni ambapo walipora sh milioni 40, majira ya saa nne asubuhi.
Katika tukio la ujambazi la Temeke ambalo linadaiwa kuwa la nane kwa mwezi huu, lilitokea juzi kati ya saa nne na tano asubuhi katika eneo la Mbagala Rangi Tatu, wakati mfanyabiashara huyo akijiandaa kupeleka fedha hizo benki.

Laana ya gesi • Polisi wampiga risasi mjamzito, waiba vitu

UGUNDUZI wa gesi asilia mkoani Mtwara umegeuka laana kwa wakazi wake wanaoishi maisha ya wasiwasi hivi sasa.
Sauti za milio ya mabomu, risasi, na vipigo ndivyo vinavyonekana kushamiri zaidi kwenye mji huo uliosifika kwa amani na utulivu kwa muda mrefu.

Idadi kubwa ya askari polisi na wanajeshi wakiwa kwenye pikipiki na magari wakizunguka maeneo mbalimbali kwa lengo la kudhibiti vurugu.
Wakati hali ikizidi kuwa tete mkoani humo, jana polisi wanadaiwa kumuua kwa kumpiga risasi mjamzito aliyekuwa nyumbani kwake eneo la Magomeni.

Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Ligula, Mohamedi Kodi amethibitisha kupokea mwili wa mjamzito huyo ukiwa na tundu tumboni, na hivyo kufanya idadi ya maiti zilizopokelewa hospitalini hapo kufikia mbili na majeruhi 18.
“Ni kweli kwa leo tumepokea maiti moja ya mwanamke ambaye ni mjamzito wa miezi saba, amepigwa risasi tumboni.

“Pia tumepokea mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Chuno, amevunjwa miguu yote kwa risasi,” alisema Dk. Ligula.
Habari ambazo Tanzania Daima ilizipata kutoka Mtwara jana, zilidai polisi walishiriki kuchoma moto nyumba tatu za wananchi katika eneo hilo na vibanda vya maduka kadhaa na kupora vitu vilivyomo ndani.

Chanzo kimoja kimedokeza kuwa maeneo ya Magomeni, Chikongola, Nkanaledi na Mikindani, askari walikuwa wakiingia kwenye nyumba za watu na kumkamata mtu yeyote hususan wanaume.
Taarifa zaidi zilieleza kuwa uhalifu uliofanywa na askari hao uliamsha hasira za wananchi jambo lililosababisha kutokea mapambano kati yao.
Baadhi ya vitu vinavyodaiwa kuibwa na askari hao kutoka kwenye maduka ni mchele, sukari, unga wa ngano na nguo.

Wakati polisi wakidaiwa kushiriki kwenye vitendo hivyo, huduma za kijamii zimesimama hali inayochangia mambo kuzidi kuwa tete ndani ya mkoa huo.

TAIFA STARS MCHANA WAITWA IKULU KUTETA NA RAIS.

TIMU ya Taifa 'Taifa stars" ambayo ipo kambini kujiandaa na mchezo wa marudiano na Morocco wa kutafuta kufuzu fainali za dunia 2014 nchini Brazil imealikwa Ikulu kula chakula cha mchana leo.

Taarifa ambazo Lenzi ya Michezo imezipata zinasema Taifa stars imeitwa na Rais leo mchana kula chakula cha mchana paamoja na mambo mengine ambayo yatafahamika baadae.

Stars asubuhi imefanya mazoezi kwenye uwanja wa Karume ikiwa na wachezaji 21 kwani Mwinyi Kazimoto aliumia mguu na Salum Abubakar amefiwa na baba yake mlezi hivyo amekwenda kuhudhuria msiba huo

CHEKI MCHUMBA WA NEY WA MITEGO A.K.A MAMA KIJACHO ALIVYO MREMBO AKIWA PENY WA DIAMOND PLATNUM DAR LIVE

clip_image001[16]
clip_image001
Bila shaka unafahamu kuwa Nay wa Mitego ni baba mtarajiwa. Mara nyingi Nay amekuwa akiweka picha ya mpenzi wake anayetarajia kumzalia mtoto hivi karibuni lakini hujawahi kuona picha yake inayoonekana vizuri zaidi. Tazama picha hizi za shemeji/wifi yetu zilizochukuliwa kwenye show ya Nay na Diamond, Dar Live weekend iliyopita.
clip_image001[6]
Diamond akisukuma kichwa cha Ney na mchumba wake ili wabusiane

JOSE MOURINHO AGREES FOUR-YEAR CHELSEA DEAL.

JOSE MOURINHO will fly to London on June 2 – and sign a four-year contract at Chelsea worth £250,000 a week. 
Mourinho will jet in the day after his final game in charge of Real Madrid to seal his mega deal. 
That is a commitment of around £50m from owner Roman Abramovich for the second coming of The Special One. 
Mourinho is so keen to get started in his new job he will not waste any time after Real’s final game against Osasuna at the Bernabeu. He will be accompanied on the trip by his fitness coach Rui Faria and goalkeeping coach Silvino Louro. 

Thursday, May 23, 2013

Wanafunzi nusura wachome kituo cha polisi wilayani Kalambo, Rukwa.

KITUO cha Polisi Mwimbi, wilayani Kalambo, Rukwa, kimenusurika kutekwa na kuchomwa moto baada ya kundi la wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mwimbi kuandamana kwa lengo la kukiteketeza kituo hicho.

Tukio hilo limetokea juzi, majira ya saa 8:30 usiku baada ya wanafunzi hao kuiteketeza kwa moto nyumba ya mkuu wao wa shule na kisha kuelekea kituo cha polisi kwa madai kuwa wanapinga kitendo cha polisi kuwadhibiti kuiteketeza nyumba ya mkuu wa shule hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Rukwa, Moshi Chang’a, alisema chanzo cha vurugu hizo ni wanafunzi kupinga adhabu ya kufyatua matofali kutokana na kitendo cha kutoroka shuleni mara kwa mara.
Chang’a ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kalambo, alisema baada ya wanafunzi hao kupewa adhabu hiyo waliandaa mkakati kwa siri na kisha majira ya saa 6 usiku wakiongozwa na mwenzao, Aidan Lunguje, mwanafunzi wa kidato cha nne walivamia nyumba ya mkuu wa shule, Willbrod Lucas na kisha kuichoma moto.

Wanaume wahimizwa kuwasindikiza wake zao kliniki.

MKUU wa Wilaya ya Iramba, Yahaya Nawanda, amewahimiza wanaume kuwasindikiza wake zao wanapokwenda kwenye vituo vya kutolea huduma za mama na mtoto ili nao wakasikilize ushauri nasaha ili iwe rahisi kwao kutekeleza.

Mkuu huyo wa wilaya alitoa changamoto hiyo kwenye hafla fupi ya kuzindua huduma ya kliniki tembezi iliyofanyika kwenye kituo cha afya cha Ndago, wilayani hapa.

Alisema halitakuwa jambo la busara kwa wanaume wanapowaona wake zao wakienda kliniki na wao wakabaki nyumbani ama kwenda kwenye shughuli nyingine.

“Naomba niwaase wanaume twende kliniki na wake zetu, haitakuwa na maana yeyote ile iwapo mwanamume atamuacha mkewe anakwenda kliniki peke yake,” alisema.

Translate