Dodoma.
Asilimia 26.8 hadi asilimia 31.9 ya Watanzania wanatumia
pombe na asilimia 27.4 kati ya hao ambao ni wanaume na wengine asilimia
13.4 ambao ni wanawake, ni walevi wa kupindukia. Bunge lilielezwa jana.
Takwimu hizo zilitolewa na Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Seif Rashid, ambaye alisema kuwa viwango hivyo vimetokana na utafiti uliofanywa kati ya Februari hadi Oktoba mwaka jana 2012.
Kwa mujibu wa naibu waziri, utafiti huo ulifanywa na Shirika la Afya Duniani (WHO).
Alikuwa akijibu swali la Abdallah Haji Ali
(Kiwani–CUF) aliyetaka kujua kauli ya Serikali kuhusu utumiaji wa pombe
ambao umethibitika kuwa ni hatari kwa afya za binadamu.
Pia alipendekeza pombe ipigwe marufuku kabisa hapa nchini kwa kuzingatia madhara yake.
Naibu waziri alisema tafiti zimeonyesha kuwa watu milioni mbili wanafariki dunia kila mwaka duniani kutokana na madhara ya matumizi ya pombe na asilimia nne ya matatizo ya kiafya yanatokana na matumizi ya pombe.






