EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, June 30, 2015

WIZKID, YEMI WASHINDWA TUZO ZA BET NA ‘STONEBWOY’


Mwanamuziki maarufu wa Nigeria, Wizkid.
Lagos Nigeria
WANAMUZIKI maarufu wa Nigeria, Wizkid na Yemi Alade, walishindwa kunyakua tuzo za Watumbuizaji Bora za Kimataifa baada ya mwanamuziki wa Ghana, Livingstone Etse Satekla a.k.a Stonebwoy kuwapiga kikumbo.
Yemi Alade.
Washindani wengine katika kundi hilo walikuwa ni Sarkodie (wa Ghana), Fally Ipupa (Congo), The Sauti Sol na AKA wote a Afrika Kusini..

DENTI KIDATO CHA KWANZA AFIA BWAWANI!

Na Kulwa Mwaibale
MSIBA! Mohamed Juma (14) ambaye alikuwa mwanafunzi wa kidato cha kwanza, Shule ya Sekondari ya Toangoma wilayani Temeke, Dar amefia bwawani wakati akiogelea.
Tukio hilo lililoacha majonzi kwa ndugu, jamaa, marafiki na wanafunzi wenzake, lilijiri Juni 26, mwaka huu, majira ya alasiri.
Mwanafunzi wa kidato cha kwanza, Shule ya Sekondari ya Toangoma wilayani Temeke, Dar, Mohamed Juma (14) amefia bwawani wakati akiogelea.
Akizungumza na Uwazi kwa masikitiko makubwa ya kumpoteza mwanaye, baba mzazi, Juma Shaha alisema familia yake imepata pigo kubwa kwa kuondokewa na mtoto wao wa kiume.
“Nashindwa nianzie wapi kuzungumza maana tumepata pigo kubwa sana kuondokewa na mwanangu wa kwanza katika uzao wetu wa watoto watatu wa kiume, inauma sana kwa kweli,” alisema Juma.
Juma alisema, majira ya saa 4 asubuhi ya siku ya tukio, Mohamed aliaga  kwenda twisheni na baadaye saa 8 kuelekea 9 alasiri alikwenda kwa rafiki zake Kilakala, Kongowe.
“Jambo la kushangaza, hadi inafika saa 2 usiku, Mohamed hakuonekana nyumbani ndipo tulianza kumtafuta,” alisema mzazi huyo.

SHOGA: SI LAZIMA MUMEO AKUANZE KILA MARA MNAPOKUWA FARAGHA!

KUJULIANA hali ni jambo la muhimu kwa binadamu, niwafahamishe mashoga zangu kuwa hali yangu na familia ni njema hakuna mushikeri wowote juu ya afya zetu, mategemeo yangu kuwa nyie pia ni wazima na mambo yenu yanasonga kama kawaida.
Kabla sijaianza mada ya leo inayosomeka “Si lazima mumeo akuanze mnapokuwa faragha” niwape pole ndugu zangu ambao mko kwenye mfungo wa Ramadhani, leo ni siku ya kumi na tatu mkiwa kwenye swaum Mungu awatie wepesi mmalize salama.
Nikiuliza mjitokeze mashoga ambao mna uwezo wa kuwaanza waume zenu muwapo faragha ni hakika yangu kuwa wengi wenu mtainamisha vichwa chini au kuangalia pembeni mkimaanisha ni vigumu sana kuonesha uhitaji kwa waume wenu.

HUYU NDIYE ANAYEDAIWA KUUAWA MA MTOTO WA WAZIRI

Deogratius Mongela na Chande Abdallah
INASIKITISHA! Mmiliki wa Shule ya Msingi na Awali (International) ya Mount Zion iliyopo Bahari Beach, Dar, Annah Mizighi Mwambili, 47, (pichani) ameuawa na mwili wake kutupwa ndani ya shule yake baada ya kupotea kwa zaidi ya miezi sita huku mtoto wa aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Tatu Ntimizi, Said Ntimizi akidaiwa kuwa mmoja kati ya watuhumiwa wa mauaji hayo.
Mmiliki wa Shule ya Msingi na Awali (International) ya Mount Zion iliyopo Bahari Beach, Dar, Annah Mizighi Mwambili enzi wa uhai wake.
Duru za awali za upelelezi wa polisi, zinamtaja Said kuwa alikuwa na uhusiano wa karibu na marehemu bila kufafanua alihusikaje na mauaji hayo ya kinyama yaliyofanyika mwishoni mwa mwaka jana, siku na tarehe isiyojulikana na mwili wake kutupwa kwenye shimo la maji taka ndani ya eneo la shule aliyokuwa akiimiliki.
Aidha, nyuma ya taarifa hiyo ya mauaji, deni la shilingi milioni mia tisa (900,000,000) ambalo mwanamke huyo alikuwa akimdai mmoja kati ya watuhumiwa hao ambao majina yao yote bado hayajafahamika likitajwa kuwa ndiyo chanzo cha Annah kutolewa uhai.

ALIANZA KWA KUTOWEKA
Wakisimulia kwa uchungu namna Annah alivyotoweka nyumbani kwake, ndugu wa marehemu walisema, awali Desemba 26, mwaka jana kwenye Sikukuu ya Boxing Day, kuna wageni walifika nyumbani kwake, Boko, Dar, wakazungumza na baadaye wakaondoka naye na hakurudi tena.
 
Mtoto wa aliyekuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Tatu Ntimizi, Said Ntimizi anayedaiwa kuwa mmoja kati ya watuhumiwa wa mauaji hayo.
NDUGU WAPATA WASIWASI, WATOA TAARIFA POLISI
Ndugu hao walisema kuwa siku za kwanza hawakupata wasiwasi kwa vile ilikuwa kawaida ya marehemu kuwa mtu wa safari kutokana na biashara zake na kuongeza kuwa walianza kupata wasiwasi baada ya siku nne kupita huku kukiwa hakuna mawasiliano kati yao na marehemu, jambo lililowalazimu kuripoti Kituo cha Polisi cha Wazo Hill ambao walianza uchunguzi.

Monday, June 29, 2015

WAJUE MASTAA WANANE WA NIGERIA WENYE MAJUMBA YA KIFAHARI


Genevieve Nnaji
Hili ni jumba la mwigizaji Genevieve Nnaji ambalo alilinunua jijini Accra, Ghana. Jengo hilo lina thamani ya dola milioni nne (Sh. Bilioni 8.6) likiwa eneo la Achimota.

Daniella Okeke
Huu ni mjengo unaotisha wa Daniella Okeke ambao una thamani ya mamilioni.

Ini Edo
Haya ni makazi ya Ini Edo, mmoja wa nyota maarufu wa filamu nchini Nigeria ambako anaishi baada ya kuachana na mfanyabiashara Philip Ehiagwina. Mjengo huo una thamani ya Naira milioni 70 za Nigeria. Mrembo huyo anaishi humo na wadogo zake.
Wasiu Ayinde
Haya ni makazi ya mwigizaji Wasiu Ayinde ambaye anamiliki majumba kadhaa jijini Lagos na mji wa nyumbani kwao huko Ijebu.
Mjengo huu unaoitwa ‘Omoojusagbola House’ ulimalizika kujengwa Machi 2012 wakati akiadhimisha mwaka wa 55 tangu kuzaliwa kwake. Ayinde ambaye anajulikana kama K1 pia ana nyumba jijini Ontario, Canada, ambako mke na watoto wake wanaishi.

Dencia
Haya ni makazi ya kuvutia ya mwigizaji Reprudencia N. Sonkey almaarufu kama Dencia. Mrembo huyo mwenye asili ya Cameroon na Nigeria, ambaye ni mwimbaji, modo, mjasiriamali na mtoa misaada kwa maskini, alilionyesha jengo hilo lililoko Los Angeles, Marekani, ambako anaishi, katika akaunti yake ya Instagram.
Inasemekana utajiri wake unakadiriwa kuwa dola milioni 3.1 au Naira milioni 617 za Nigeria.

Don Jazzy 
Haya ni makazi ya Don Jazzy- Mkurugenzi Mkuu na mmiliki wa Mavin Records ambaye pia ni mwimbaji, mtunzi wa nyimbo na prodyuza.
Don ni prodyuza tajiri zaidi wa muziki nchini Nigeria na mwanamuziki anayeshika nafasi ya pili kwa utajiri barani Afrika. Mjengo huu uko eneo linaloitwa Lekki, ukiwa na thamani ya Naira milioni 160 za Nigeria ambapo aliununua mwishoni mwa mwaka 2012.

Chika Ike
Hapa anaishi mwigizaji mrembo Chika Ike eneo la Lekki tangu mwaka 2013 ambapo alinunua jengo hilo kwa mamilioni ya Naira za Nigeria. Katika eneo la jumba hilo kuna bustani, eneo la michezo, ofisi, maegesho ya magari, bwawa la kuogelea na kila aina ya anasa.
Chika Ike ni mmoja wa wanawake matajiri zaidi katika tasnia ya filamu nchini Nigeria. Mbali na mjengo huo pia ana duka linaloitwa Fancy Nancy jijini Abuja.

JOH MAKINI: TUKUBALI KUKOSELEWA KATIKA MUZIKI


Ofisa wa sanaa kutoka Balaza la sanaa (BASATA)Augustino Kihiyo(kushoto) John Saimon 'Joh Makin'(katikati) pamoja na G-Nako.
Baadhi ya wasanii na wanafunzi wa Chuo Cha Habari cha DSJ wakifuatilia mkutano huo.
...Wakifuatilia mkutano huo.
STAA wa muziki wa Hip Hop Bongo, ambaye pia ni memba wa Kundi la Weusi kutoka Arusha, John Simon ‘Joh Makini leo amefungukia wasanii wenzake kukubali kukosolewa.
Akizungumza na waandishi wa habari leo katika Jukwaa la Sanaa linalofanyika kila baada ya wiki mbili katika Ukumbi wa Basata-Sharif Shamba, Ilala jijini Dar es Salaam, Joh amesema  kuwa ili kuweza kupambana changamoto za muziki katika jamii ni lazima kukubali kukosolewa.
“Tunatakiwaa kutengeneza muziki unaokubalika katika soko kwani msanii anayetaka kutoka kimuziki lazima ajitambue katika jamii yake,” alisema Joh Makini anayetamba kwa sasa na Wimbo wa Nusunusu.
(PICHA/HABARI: DENIS MTIM/GPL)

KONGAMANO LA SDG’s LAFANYIKA KWA MAFANIKIO DODOMA‏

IMG_4628
Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Taasisi Huru ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF), Dk. Tausi Kida, akitoa maelezo ya kongamano kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kulifungua kongamano kubwa la siku mbili la kujadili namna taifa linavyojiandaa kutekeleza malengo mapya ya Maendeleo endelevu (SDGs) limefanyika mwishoni mwa wiki mjini Dodoma ambalo liliandaliwa na taasisi yake.
IMG_4606 IMG_4729
Kamishna wa Fedha za Nje wa Wizara ya Fedha, Ngosha Magonya akisoma hotuba ya ufunguzi wa kongamano hilo kwa niaba ya mgeni rasmi Katibu Mkuu wa wizara hiyo katika hoteli ya St. Gasper mwishoni mwa wiki mjini Dodoma.
IMG_4678
Mtaalamu wa masuala ya uchumi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Dar es salaam, Rogers Dhliwayo akitoa salamu za Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) wakati wa kongamano hilo la siku mbili la kujadili namna taifa linavyojiandaa kutekeleza malengo mapya ya Maendeleo endelevu (SDGs) lililofanyika mwishoni mwa wiki mjini Dodoma.
IMG_4949
Afisa Mwandamizi wa uhamasishaji na uwekezaji kutoka kituo cha uwekezaji nchini (TIC), Lilian Mwamdanga akishiriki kuchangia maoni wakati kongamano kubwa la siku mbili la kujadili namna taifa linavyojiandaa kutekeleza malengo mapya ya Maendeleo endelevu (SDGs) limefanyika mwishoni mwa wiki mjini Dodoma.
IMG_5015
Naibu Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP)- Programme, Amon Manyama akichangia maoni wakati wa kongamano kubwa la siku mbili la kujadili namna taifa linavyojiandaa kutekeleza malengo mapya ya Maendeleo endelevu (SDGs) limefanyika mwishoni mwa wiki mjini Dodoma.
IMG_4801
Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Taasisi Huru ya Utafiti wa Uchumi na Jamii (ESRF), Dk. Tausi Kida na Kamishna Mipango wa Tume ya Mipango Zanzibar, Ahmed Makame Haji wakifuatilia kwa umakini maoni mbalimbali ya wadau yaliyokuwa yakitolewa kwenye kongamano hilo.
IMG_4739
Pichani juu na chini ni washiriki kutoka Tanzania bara na visiwani walioshiriki kongamano hilo la siku mbili ambalo liliandaliwa na taasisi ya ESRF.
IMG_4702
IMG_4756

NJOO SABASABA UJUE UMOJA WA MATAIFA, MIAKA 70 YA KUTETEA USTAWI WA DUNIA‏

DSC_0598
Muonekano wa nje wa Banda la Shirika la Umoja wa Mataifa (UN), Tanzania lililopo ndani ya Karume Hall wanaoshiriki katika Maonesho ya 39 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam ya sabasaba yaliyoanza kurindima jana kwenye katika viwanja vya Mwalimu J.K. Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar.(Picha zote na Zainul Mzige wa modewjiblog).
Modewji blog team, Sabasaba
Shirika la Umoja wa Mataifa (UN), Tanzania wapo katika maonyesho ya 39 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar-es-salaam yaliyoanza kurindima mapema jana.
UN Tanzania ambao wapo katika banda la Karume ndani ya mabanda hayo ya Sabasaba, kutoa elimu inayolenga kuionyesha jamii mafanikio, changamoto na fursa zilizopo katika Umoja wa Mataifa ambapo mwaka huu unafikisha miaka 70 tangu shirika hilo lianzishwe.
“Huu ni mwaka muhimu sana kwani safari ya Umoja wa Mataifa ilianza mwaka 1945, hadi kufikia sasa kuwa umefikia wapi, tupo wapi na tunaelekea wapi katika kushughulikia changamoto za kidunia ikiwemo Amani na usalama, changamoto za maendeleo, changamoto za mabadiliko ya tabia nchi, na changamoto zingine”, alieleza Afisa Habari wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Usia Nkhoma Ledama.
Aidha, alibainisha kuwa, UN ambayo imeweza kufikisha miaka 15 ya malengo ya Milenia yaliyokubaliwa na nchi wanachama wa Umoja huo mwaka 2000, yanafikia kilele hapo Desemba 30, mwaka huu hivyo wakuu hao wanchi watakutana tena mwezi Septemba mwaka huu, kupanga malengo mapya ya Maendeleo endelevu (SDGs) ambayo yatakapokubalika yataanza kutumika mwakani.
“Huu ni mwaka muhimu sana. wa kuonyesha hayo mabadiliko, tumekuwa na miaka 15 ya milenia kuna vitu tumefanikiwa na tumekuwa na changamoto. Kwa hiyo malengo hayo yalikuwa ni shirikishi kutoka kwa kada zote”alieleza.
Pia alieleza kuwa katika mkutano mkubwa wa mabadiliko ya tabianchi ambao utakuwa mkutano mkubwa wa 21, utakaofanyika Paris-Ufaransa Disemba mwaka huu. Wakuu wa nchi watakuja na makubaliano ya kuona watafanya nini hivyo makubaliano hayo ni muhimu sana.
Nchi zote duniani zimeona suala la mabadiliko ya tabianchi si la nadharia tena bali ni la wote kuungana kupambana nalo kwani wote tunaathirika.
Hivyo tunawakaribisha sana watanzania kutembelea katika banda letu kujionea na kufahamu na kujifunza na kwa Tanzania mwaka huu tunamalizia program yetu ya kwanza ambayo tunashirikiana mashirika yote kufanya kazi kwa pamoja (Delivering as one) katika kutatua changamoto zinazotukabili hapa Tanzania kwa kushirikiana na serikali.
DSC_0611  
Afisa habari wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Usia Nkhoma Ledama akitoa maelezo ya taarifa mbalimbali zilizoorodheshwa kwenye jarida la vijana lililoandaliwa na Shirika linaloshughulikia idadi ya watu Duniani (UNFPA) kwa mmoja wa wakinamama aliyetembelea banda kwa ajili ya kufahamu shughuli mbalimbali na mchango wa shirika la Umoja wa Mataifa kwa serikali Tanzania.
IMG_5248
Afisa habari wa kituo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC), Usia Nkhoma Ledama akisikiliza swali kutoka kwa raia wa kigeni mwenye asili ya asia aliyetembelea banda la Umoja wa Mataifa katika maonyesho ya sabasaba yaliyoanza kurindima jana katika viwanja vya Mwalimu J.K. Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar.
IMG_5271

Friday, June 26, 2015

VIFO MASTAA KUTIKISA UPYA!

Gladness Mallya na Mayasa Mariwata
MSHTUKO! Wakati wimbi la wasanii Bongo likizidi kuwa kubwa katika kutangaza nia ya kuwania nafasi mbalimbali za uongozi kwenye siasa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka huu, mtabiri maarufu nchini, Maalim Hassan Yahya Hussein amefunguka mazito juu ya vifo vya mastaa hao kutikisa upya huku wale watakaosalia wakipata nafasi za uongozi.
steveveeStaa wa bongo movie Steven Mangele ‘Steve Nyerere’.
TUJIUNGE MAGOMENI-MWEMBECHAI
Akizungumza na gazeti hili ofisini kwake, Magomeni-Mwembechai jijini Dar, mapema wiki hii, mtabiri huyo alisema kuwa, mwaka huu kinyota ni wa mafanikio makubwa kwa wasanii lakini pia vifo navyo vitakuwa vingi kwao.
Wema-SepetuMiss tanzania 2006 na muigizaji wa Bongo movie Wema Sepetu.
NI MWAKA WAO KINYOTA
Alisema kwamba, kwa wale watakaosalimika huku wakiwa wamejiingiza kwenye kinyang’anyiro cha kugombea uongozi wa kisiasa, wote watafanikiwa kwa kuwa mwaka huu ni wao.
Maalim alisema kuwa, mwaka huu kinyota ni wao ndiyo maana wamejitokeza wengi kwenye kuwania nafasi hizo tofauti na vipindi vingine vya uchaguzi vilivyopita.

Real Madrid wametoa uamuzi kuhusu kumuuza Sergio Ramos Man United

 
Saa zisizopungua 48 baada ya klabu ya Manchester United kuripotiwa kutuma ofa ya kumsajili beki wa kimataifa wa Spain, Sergio Ramos, klabu yake ya Real Madrid imepokea ofa hiyo na imetoa uamuzi.
  Manchester United, juzi walituma ofa ya £35million kwa ajili ya kupata saini ya Ramos na klabu ya Madrid wameipiga chini ofa hiyo.

BANZA: MNANIUA SANA JAMANI

banza Mwanamuziki nguli wa dansi, Ramadhan Masanja ‘Banza Stone’.
Gladness Mallya
BAADA ya uvumi kuzagaa mtaani kwamba mwanamuziki wa dansi, Ramadhan Masanja ‘Banza Stone’ amefariki dunia, Banza amesema amechoshwa na watu kumuua sana.
Baada ya uvumi huo, ndugu zake wamesema watu waache kumuua kwa maneno kwani bado yupo hai.
BANZA2‘Banza Stone’ akiwa katika ofisi za Global Publishers (Picha na Maktaba).
Ndungu mmoja aliyejulikana kwa jina moja la Hamis, alisema uzushi wa kifo cha Banza umewasumbua sana kwani watu mbalimbali walikuwa wakipiga simu na wengine kufika nyumbani jambo ambalo lilimuumiza sana Banza japokuwa anaumwa lakini akawa analalamika kwa nini watu wanamuua kwa maneno na si mara moja kutokea.
“Jamani yupo hai japokuwa anaumwa lakini anaongea tatizo lipo kwenye kusimama na kula, watu waache uzushi kwani wanamuumiza zaidi kwa uzushi wao huo,” alisema Hamis.

NDOA YANGU NA NUHU ZIMEBAKI SIKU CHACHE TU – SHILOLE

3d99b__hhhklMwanamuziki wa mduara, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ akiwa na mpenzi wake Nuh Mziwanda.
Mpenzi msomaji tunakutana tena katika safu hii ambapo mastaa mbalimbali hujibu maswali kumi kikamilifu, leo tunaye mwanamuziki wa mduara, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ ambaye amefunguka mambo mengi alipokuwa akizungumza na Mwandishi Wetu IMELDA MTEMA. Ili kujua aliyoyasema endelea kusoma.
Ijumaa: Vipi kuhusu sakata lako la nguo kukuvuka ukiwa jukwaani limekuathiri kivipi?
Shilole: Halijaniathiri chochote hiyo ni kama mtu anapata ajali akiwa kazini.
Ijumaa: Wakati zile picha zilipokuwa zikisambazwa katika mitandao ya kijamii, mpenzi wako Nuhu alilizungumziaje hilo?
shiloleNUH 
Shilole: Hakuzungumza chochote kwani tulikuwa pamoja siku ya tukio hivyo anajua nini kilitokea.
Ijumaa: Najua una wakwe, je, walipoziona hizo picha hawakumsumbua Nuhu na kuona kama unawadhalilisha?

Thursday, June 25, 2015

PAM D ANASWA AKIFAKAMIA UGALI MKUBWA!


IMG_0726 STAA wa Bongo Fleva anayetamba na Wimbo wa Nimempata, Pamela Daffa ‘Pam D’ akifakamia ugali.
STAA wa Bongo Fleva anayetamba na Wimbo wa Nimempata, Pamela Daffa ‘Pam D’ hivi karibuni aliwaacha watu hoi baada ya kunaswa akifakamia ugali mkubwa.
Tukio hilo lilitokea katika Pub moja iliyopo Uwanja wa Sanaa, Legho-Ubungo jijini Dar ambapo ‘wadaku’ waliokuwepo hapo walishangaa staa huyo kufika eneo hilo na kuagiza ugali mkubwa na nyama kisha kuanza kuufakamia wote bila kubakiza kitu.

VICKY KAMATA AMPONGEZA KINANA KWA KAZI NZURI ANAYOFANYA KUJENGA NA KUKIIMARISHA CHAMA

MASHINDANO YA MISS KILIMANJARO YAZINDULIWA DAR


Baadhi ya washiriki wa shindano hilo wakiwa kwenye pozi la pamoja ndani ya Hoteli ya Colloseum maeneo ya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa mashindano hayo Jacqueline Chuwa (katikati) akizungumza jambo mbele ya wanahabari waliokuwa  Hoteli ya Colloseum Mnazi Mmoja jijini Dar. Kushoto ni Mkuu wa Itifaki wa mashindano hayo Angerls Faber na Mratibu wa Shindano hilo Sebu Panya.
Angerls Faber akielezea namna mashindano hayo yatakavyo kuwa.

Wednesday, June 24, 2015

Dkt. Nchimbi atangaza rasmi kutogombea Songea

Mbunge wa Songea mjini Dkt Emmanuel Nchimbi ametangaza rasmi kutogombea tena ubunge katika jimbo, katika mkutano wa hadhara ambapo baadhi ya wanachama wa CCM wameonesha kutokubaliana na uamuzi huo.
Dkt. Emmanuel Nchimbi akihutubia mkutano wa hadhara
Katika hali isiyokuwa ya kawaida baadhi ya wananchi wakiwemo wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) jimbo la Songea mjini mkoani Ruvuma, wamejikuta katika hali ya sintofahamu huku wengine wakimwaga machozi baada ya mbunge wa jimbo hilo, mh. Dkt. Emmanuel Nchimbi kutangaza rasmi kutogombea tena ubunge katika jimbo hilo.

HII NDIO HATMA YA SAMATTA KUCHEZA SOKA ULAYA….

samatta_cska_2Wakala wa mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania Mbwana Samatta, Jamal Kisongo amesema hatma ya mshambuliaji huyo kucheza soka la kulipwa Ulaya sasa itasubiri mwakani kutokana na rais na mmiliki wa klabu yake yake TP Mazembe Moise Katumbi kuonesha bado anahitaji huduma yamchezaji huyo hususan katika michuano ya vilabu bingwa barani Afrika.
“Katumbi ameonesha bado anahitaji kumtumia katika kikosi chake kwenye michuano ya champions league kwa maana hiyo makusudio yetu na matarajio yetu, kunatimu moja kubwa ilitaka kumsaini kwa ‘Euro’ milioni moja lakini bahati mbaya Katumbi alitaka amuache baada ya champions league kuisha”, amesema wakala huyo wa Samatta.

MTITU AKUBALI KUSAMEHEANA NA STEVE


MTITU42 
Staa wa filamu Bongo, William Mtitu.
Brighton Masalu
KUJISHUSHA! Staa wa filamu Bongo, William Mtitu amesema yupo tayari kumaliza ugomvi na Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ kutokana na shinikizo kutoka kwa wasanii wenzake, wadau na mkewe.
Kwa mujibu wa chanzo makini, kikao kizito kikimhusisha Mtitu na wasanii nguli kiliitishwa na kumuonya juu ya suala hilo kabla ya kukubali kuwa yuko tayari kumalizana na Steve.
steve 
Mwigizaji maarufu wa Bongo Movie, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’.
“Kilikuwa ni kikao kizito kaka, Mtitu ‘alipewa vipande’ vyake huku wasanii wakimpa hasara za mabifu yasiyokuwa na faida na yeye alielewa, na sasa yuko tayari kwa suluhu,” alisema mmoja wa wasanii mwenye jina kubwa.
Mwandishi wetu alimtafuta Mtitu ili kusikia chochote kutoka kwake ambapo alisema;
“Duh! Umeipata na hiyo! Ni kweli kabisa, hakuna haja ya kuwa na mabifu katika zama hizi za maisha mafupi, wakiandaa mpango wa kutukutanisha, niko tayari.”
Kwa upande wake, Steve Nyerere alisema asingeweza kulizungumzia suala hilo kwa wakati huo kwani alikuwa na kazi anaifanya. Aliahidi kumtafuta mwandishi baadaye, lakini hadi Risasi Mchanganyiko linakwenda mitamboni, alikuwa hajawasiliana naye.

CCM YABARIKI UBUNGE WA WEMA


WemasMiss Tanzania 2006 na Staa wa Bongo Movie, Wema Sepetu akipokea maelekezo kutoka kwa katibu wa CCM wilaya ya Ikungi, Bw. Alluu Ismaili Segamba kwenye Mkutano uliofanyika Mkoani Singida wiki iliyopita.
Gladness Mallya
BARAKA! Siku chache baada ya mwanadada anayefanya vizuri kwenye filamu Bongo, Wema Sepetu ‘Madam’ kutangaza nia ya kugombea ubunge kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), chama hicho kimempa baraka mrembo huyo kwa uamuzi wake huo.
wemass…Wema akipokelewa na Makada wa Chama cha Mapinduzi, CCM mkoani  Singida.
Akistorisha na gazeti hili, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema kila mwanachama ana haki ya kugombea uongozi wowote ule ilimradi awe mwanachama hai, hivyo kwa Wema kugombea ubunge wa viti maalum ni haki yake na amefanya uamuzi sahihi.
“Kugombea uongozi ni haki ya kila mwanachama, Wema ana haki, kwanza ni mwanachama hai na baba yake alikuwa mwanachama mzuri sana wa CCM mpaka anafariki dunia, hivyo chama chetu huwa hakikutani na watu barabarani tu, bali wanakuwa ni halali kabisa mpaka wanatangaza kugombea,” alisema Nape.
Hata hivyo, alisema wasanii wote waliotangaza kugombea kupitia chama hicho hawajakurupuka bali ni wanachama hai na wamekuwa wakishiriki kwenye shughuli mbalimbali za kichama, tangu kwenye kampeni za mwaka 2010.
Wasanii wengine waliotangaza nia ya kugombea ubunge kupitia CCM licha ya Wema ni Ndumbagwe Misayo ëTheaí (Viti Maalum, Kinondoni) na Wastara Juma (Viti Maalum Morogoro Vijijini).

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate