EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Tuesday, December 31, 2013

HAPPY NEW YEAR 2014

IRENE MWAMFUPE JAMII BLOG TUNAKUTAKIA MWAKA MPYA MWEMA.

HABARI 10 ZA GPL ZILIZOTIKISA MWAKA 2013

1. MSIBANI KWA BABA WEMA... LULU ATOA MITUSI MIZITO
Stori: Waandishi Wetu
MSANII nyota wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amejikuta akiporomosha mitusi mizito ya nguoni kwenye msiba wa baba wa Miss Tanzania 2006/07, Wema Isaac Sepetu, mzee Isaac Abraham Sepetu hali iliyowafanya baadhi ya waombolezaji kumkodolea macho ya mshangao...
2. ANAYEDAI KUBAKWA NA KAPUYA HUYU HAPA

Stori: Waandishi Wetu
MNYONGE mnyongeni haki yake mpeni, skandali ya kumbaka na kumwambukiza Ukimwi mwanafunzi, inamtafuna na kumuumiza Mbunge wa Urambo Magharibi (CCM), Juma Athuman Kapuya. Kuhusu ukweli wa skendo hiyo, vyombo vya sheria vitazungumza lakini gazeti hili limejiridhisha pasipo shaka yoyote kuwa denti husika ni tapeli na anacheza rafu ili kumharibia Kapuya kwa maslahi yake...
ZAIDI, INGIA HAPA: ANAYEDAI KUBAKWA NA KAPUYA HUYU HAPA
3.  EXCLUSIVE: SIRI 5 ZA WOLPER ZAVUJA
Na Sifael Paul
MOYO huhifadhi mengi mazito hasa ya kuumiza! Staa mkubwa wa sinema za Kibongo, Jacqueline Wolper Massawe amejikuta akimwaga machozi wakati akianika siri tano nzito kuhusu mapenzi katika mahojiano (exclusive interview) na Amani kwa takriban saa mbili...
ZAIDI, INGIA HAPA: EXCLUSIVE: SIRI 5 ZA WOLPER ZAVUJA

4. MAINDA: NIMETOA MIMBA YA RAY


Stori:  Jelard Lucas
HILI ndiyo Risasi bwana! Sikia, kama ulikuwa hujui ni kwamba msanii mkongwe katika filamu za Kibongo, Ruth Suka ‘Mainda’ ameibuka na kueleza mengi ikiwemo kutoa mimba ya mpenzi wake wa siku nyingi, Vincent Kigosi, tulia hapohapo...
ZAIDI, INGIA HAPA: MAINDA: NIMETOA MIMBA YA RAY
5. UKWELI KUHUSU ASALI NA MDALASINI KAMA TIBA
WASIOJUA kuhusu uwezo wa asali na mdalasini wanaweza wasiamini wakiambiwa kuwa vina uwezo wa kuzuia na kutibu magonjwa hatari yaliyoshindakana hata hospitalini. Asali na mdalasini zimekuwa zikitumika kama tiba tangu enzi na enzi...
ZAIDI, INGIA HAPA: UKWELI KUHUSU ASALI NA MDALASINI KAMA TIBA
6. RAY YAMEMKUTA  
Stori:Haruni Sanchawa
TUKISEMA staa wa filamu za Bongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ yamemkuta ni sawa, kisa ni ile ishu yake ya kutengeneza filamu inayoitwa Sister Marry ambapo mapadri wamemtaka asiipeleke sokoni milele, Risasi Jumamosi lina mkanda wote. Ishu hiyo ilitokea kwenye kikao kizito cha saa 5 kilichofanyika Jumanne iliyopita katika Ofisi za Utamaduni jijini Dar es Salaam...
ZAIDI, INGIA HAPA: RAY YAMEMKUTA
  7. RAY AKONGOROKA 
Stori: Musa Mateja na Imelda Mtema
MWIGIZAJI Vincent Kigosi ‘Ray’ amezua hofu kwa ndugu, jamaa, marafiki na mashabiki wake baada ya kukongoroka ghafla akihisiwa anaumwa, Ijumaa Wikienda limemfuatilia hatua kwa hatua...
ZAIDI, INGIA HAPA: RAY AKONGOROKA
8. DENTI ALIYEDAI KUZAA NA DIAMOND... AUMBUKA, ATISHIA KUJIUA
MREMBO Sasha Juma, 20, kwa sasa anapitia kipindi cha majuto, analipia gharama ya kujivalisha ubandidu na kujisingizia kupewa mimba na supastaa, Nasibu Abdul Juma ‘Diamond’. Sasha, akiwa na macho makavu, alitamka mbele ya waandishi wetu kuwa mimba hiyo aliyopewa na Diamond, ilimgharimu kufukuzwa shule akiwa kidato cha nne mwaka jana. Unadhani Sasha analo tena? Ameshaumbuka na baada ya simulizi yake ya kutunga kushtukiwa, hivi sasa mrembo huyo anatishia kujiua...
ZAIDI, INGIA HAPA: DENTI ALIYEDAI KUZAA NA DIAMOND... AUMBUKA, ATISHIA KUJIUA
9. BONGO MUVI WAMSUSIA WEMA MSIBA
Na waandishi wetu
HUKU akiwa na majonzi ya kuondo-kewa na baba yake mzazi, Balozi Isaac Abraham Sepetu aliyefariki dunia Jumapili iliyopita kwa ugonjwa wa kisukari, baadhi ya wasanii wanaounda Klabu ya Bongo Movie (muvi) Unity wanadaiwa kumsusia msiba mwingizaji mwenzao, Wema Isaac Sepetu...
ZAIDI, INGIA HAPA: BONGO MUVI WAMSUSIA WEMA MSIBA
10.  ANASWA
Stori: Richard Bukos, Issa Mnally na Imelda Mtema.
MfanyabiAshara ‘alwatani’ Bongo, mkazi wa jijini Dar, Allain Tajiri amekumbwa na skendo nzito baada ya kufumaniwa na mwanafunzi wa sekondari wa kidato cha pili mwenye umri wa miaka 16. Tukio hilo la kusikitisha lilitokea Jumatano ya Aprili 24, mwaka huu katika chumba namba 107 kwenye gesti iitwayo Jamboz iliyopo Kinondoni jijini Dar...
ZAIDI, INGIA HAPA: ANASWA!

APANDA JUU YA MNARA, ATAKA KUJIRUSHA KWA MADAI YA KUONEWA


Wanausalama wakipanda juu ya mnara kumnusuru jamaa huyo.

LEO NDIYO LEO: MKESHA WA MWAKA MPYA NDANI YA DAR LIVE

MAMLAKA YA HALI YA HEWA YATOA TATHMINI YA MUELEKEO WA MVUA KWA KIPINDI CHA JANUARI HADI MACHI, 2014

Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya hali ya hewa nchini, Dkt. Agness Kijazi (kulia) akiongea na waandishi wa habari hawapo pichani juu ya tathmini ya mvua kwa kipindi cha Januari hadi Machi 2014.
Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakimsikiliza mkurugenzi wa mamlaka ya hali ya hewa.

Monday, December 30, 2013

RAIS KIKWETE AMTEUA ERNEST MANGU KUWA MKUU WA JESHI LA POLISI NCHINI

 
Kamishna wa Polisi Ernest Mangu aliyeteuliwa na Rais Kikwete kuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete leo, Jumatatu, Desemba 30, 2013, amemteua Kamishna wa Polisi Ernest Mangu kuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini.
Taarifa iliyotolewa usiku wa leo na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue inasema kuwa Kamishna Mangu anachukua nafasi ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini anayestaafu, Saidi Mwema.
Kabla ya uteuzi wake unaoanza keshokutwa, Januari Mosi, 2014, Kamishna Mangu alikuwa Mkurugenzi wa Inteligensia ya Jinai (Director of Criminal Intelligence)katika Jeshi hilo la Polisi.
Aidha, taarifa hiyo inasema kuwa Rais Kikwete amemteua Kamishna Abdulrahman Kaniki kuwa Naibu Mkuu wa Jeshi la Polisi, ambayo ni nafasi mpya katika muundo wa sasa wa Jeshi la Polisi.
Kabla ya uteuzi wake, Kamishna Kaniki alikuwa Kamishna wa Uchunguzi wa Kijinai (Commissioner for Forensic Investigations).
Mkuu wa Jeshi la Polisi mpya ataapishwa kesho, Jumanne,  Desemba 31, 2013 katika Viwanja vya Ikulu, Dar es Salaam.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.

Imani za kishirikna zimezidi kuchukua sura mpya mkoani Mbeya baada ya mwanamke aliyefahamika kwa jina la Lucy Frank[55]mkazi wa Manyoni Singida kudai kamba iliyotumika kushushia jeneza la marehemu dada yake apewe ili aende nayo Singida

 viongozi wa Muungano wa jamii Tanzania[MUJATA]akiwemo Soja Masoko,Abdul Aziz,Diwani Kata ya Mwakibete Lucas Mwampiki na Chifu Shadrack Merere kutoka Mbarali.

MOUREEN AIBUKA SUPA STAA WA SHINDANO LA MO KIDS GOT TALENT 2013

JACK PATRICK ALIVYONASWA NA MADAWA YA KULEVYA CHINA

Jack Patrick akiwa amefunikwa uso akiwa mikononi mwa polisi nchini China baada ya kukutwa na pipi za heroin tumboni.

MADAI ya kukamatwa kwa tuhuma za kumeza madawa ya kulevya aina ya Heroin nchini China kwa msanii, Video Queen na mwanamitindo maarufu Bongo, Jacqueline Patrick, kumeibua maswali ya kila aina,  mengi yamesemwa, uvumi umeenea, lakini Ijumaa Wikienda linadondosha hatua kwa hatua.
 
Jack Patrick.
Baada ya kuinyaka taarifa hiyo ya aibu kwa staa huyo na taifa kwa jumla, kwa uchungu mkubwa timu yetu imara ilijipanga na kuingia mtaa kwa mtaa, nyumba kwa nyumba, mtu kwa mtu kuchimbua, kudadavua na kufukunyua kwa undani zaidi juu ya tuhuma hizo. Aya zinazofuata zitakupa mwanga.
ALIVYONASWA HATUA KWA HATUA
Wikienda lilichorewa mchoro kwamba, Jack alikamatwa Desemba 19, mwaka huu katika Uwanja wa Ndege wa Macau nchini humo akitokea jijini Bangkok nchini Thailand kuelekea Guangzhou, Mji Mkuu wa Jimbo la Guangdong Kusini mwa China.
Jack akiwa chini ya ulinzi.
NINI KILISABABISHA?
Inadaiwa kuwa miongoni mwa mambo yaliyochangia kunaswa kwake ni uso wa uchovu, kuanza kuwa na hali mbaya ya mwili, kushindwa kujibu maswali vizuri na hati yake ya kusafiria (passport) yake kuonesha kugongwa mihuri ya kuingia nchini humo kila mara.
Habari zinasema ndipo maafisa wa uwanja huo walipomweka pembeni na baadaye kumpeleka kwenye chombo cha kukagua kwa undani mwili wa binadamu, walipojiridhisha ana ‘mzigo’ wakampa polisi mwanamke (WP) kwa ajili ya kwenda kusimamia utoaji wa kete hizo chooni kwa njia ya haja kubwa.
Polisi wakichunguza pipi zenye dawa za kulevya alizokutwa nazo Jack Patrick.
AVALISHWA MASKI, AWEKWA MBELE YA MAPAPARAZI
Baada ya kutoka chooni, ikafuata hatua nyingine. Jack aliwekwa mbele ya mapaparazi akiwa amevalishwa maski nyeusi usoni ili asionekane sura kisha akapigwa picha za kumwaga.
Sheria za Macau, mtuhumiwa huvalishwa maski usoni ili watu wasiione sura yake. Kete alizozitoa ziliwekwa juu ya meza, pia simu zake mbili, Iphone na Samsung nyeupe zilikuwa pembeni. Baadhi ya watu Bongo walizitambua simu hizo kwamba ni zake.
AINA YA MADAWA
Jack ambaye ni Miss Ilala Namba 3, 2005, alikamatwa na madawa aina ya Heroin yenye uzito wa kilo 1.1 yakiwa na thamani ya zaidi ya shilingi milioni 223 kwa kuhifadhiwa ndani ya kete 57.
Mwanamitindo Jack Patrick.
ATANYONGWA?
Kwa sheria za Beijing, China mtu akithibitika kubeba unga hukumu yake ni kunyongwa tu lakini waandishi wetu walipozungumza na wataalam mbalimbali wa sheria za kimataifa ili kujua ni adhabu gani inaweza kutolewa kwa mrembo huyo endapo atakutwa na hatia, walisema Beijing si Macau, ni vigumu kula kitanzi lakini kwenda jela miaka mitatu, minne au nane inaweza ikamhusu. Majimbo mengi ya China yanaongozwa kwa sheria zake badala ya sheria mama moja kwa nchi nzima.
Hata hivyo, sheria za eneo alilokamatiwa zinasema kuwa uwezekano wa ndugu, jamaa na marafiki kumuona kwa sasa haupo mpaka Machi, 2014 uchunguzi utakapokuwa umekamilika.
Wanahabari nchini China wakichukua picha za dawa za kulevya anazodaiwa kukutwa nazo Jack.
WATU WA KARIBU WALIVYOPOKEA TAARIFA
Awali, baadhi ya watu wa karibu na modo huyo waligoma kuweka bayana kuhusu yaliyompata Jack huko ughaibuni wakidai si wasemaje wake na kuwataka mapaparazi kwenda kuchimba kwenye Ubalozi wa China nchini Tanzania.
Kwa sharti la kutotajwa jina mahali popote kwenye ukurasa huu, mmoja wa marafiki wa karibu wa Jack aliyeko China kwa masomo, alisema amethibitisha ukweli kupitia balozi ndogo ya Tanzania nchini humo.

MJAMZITO AJIFUNGULIA KWENYE KOKOTO


Kichanga baada ya kuzaliwa.
Stori: Gordon Kalulunga, Mbeya
MASIKINI! Mama mjamzito aliyetambulika kwa jina la Sabina Mwakyusa (28), mkazi wa Kijiji cha Iwala, Kata ya Utengule Usongwe wilayani Mbalizi mkoani hapa anadaiwa kujifungulia nje kwenye kokoto.
Mama aliyejifungua katika kokoto akiwa na mwanaye.
INASIKITISHA
Tukio hilo la kufungia mwaka lilijiri nje ya Hospitali Teule ya Ifisi-Mbalizi hivi karibuni na kusababisha masikitiko makubwa kwa mashuhuda waliodai kuwa ishu hiyo ni kali ya kufungia mwaka 2013.
Akizungumzia tukio hilo muda mfupi baada ya kujifungua, Sabina alisema alifika hospitalini hapo Desemba 18, mwaka huu na alipimwa na manesi ambapo walimwambia kuwa hawamuoni mtoto tumboni mwake.
“Baadaye alikuja daktari na kunipima, akaniambia mtoto anaonekana vizuri na ningejifungua mtoto wa kike ndipo nikaendelea kusubiri uchungu zaidi,’’ alisema kwa masikitiko.

UCHUNGU
Alisema ulipofika usiku wa Desemba 19, mwaka huu, alianza kujisikia uchungu, ndipo manesi waliompima mwanzo wakamwambia anatakiwa apimwe tena, jambo ambalo alikataa kwa madai kuwa alikuwa akiumia.
Alidai alipokataa kupimwa ndipo wakamwambia aondoke hospitalini hapo kwa sababu ana kiburi.
KUMBUKUMBU MBAYA
Mama mzazi wa mwanamke huyo, Roda Mwakyusa (50), alisema anaumia akikumbuka yaliyomkuta mwanaye ikiwa ni uzao wake wa kwanza.
Alidai walipotoka wodini huku mwanaye uchungu ukimzidi, walifika getini akazidiwa na kuanza kujifungua ndipo walinzi wa kampuni ya Mult-Lion, wakamsaidia kumpeleka katika upenu wa duka la hospitali hiyo ili kukwepa kokoto zilizopo na mvua iliyokuwa ikinyesha.
Mkurugenzi wa kampuni hiyo ya ulinzi, Kinanda Sanga, alipoulizwa kuhusu tukio hilo, alikiri kwamba lilitokea na wao wakatoa msaada.

Naye wifi wa Sabina, Prisca Nafred, alisema alimpeleka mtoto aliyezaliwa katika hospitali hiyo saa 7:00 mchana wa Desemba 20, kwa ajili ya chanjo, lakini hakupata chanjo kwa madai kuwa alikuwa amechelewa kufika.

Desemba 21, familia hiyo ilimpigia simu mwandishi wetu na kumueleza kuhusu maendeleo mabaya ya mtoto ambapo mwanahabari wetu alitoa taarifa kwa Mratibu wa Afya ya Mama na Mtoto, Mkoa wa Mbeya, Prisca Butuyuyu ambapo makubaliano yalifikiwa kuwa mtoto apelekwe Hospitali ya Rufaa, Kitengo cha Wazazi Meta.

MTOTO ANAENDELEAJE?
Mtoto huyo alipokelewa Meta na kuingizwa kwenye chumba cha joto kisha kuanza kupatiwa matibabu kwa kuwekewa dripu za maji hadi Desemba 23, mwaka huu hali yake ilipotengemaa na sasa anaendelea vizuri.
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Louis Chomboko, alipopata taarifa, alichukua hatua ya kwenda kumuona mtoto huyo Meta na kuahidi kulifuatilia suala hilo.

JAJI WARIOBA KUILIZA AU KUIPA KICHEKO CCM LEO

Jaji Joseph Warioba.
Ni rasimu ya pili mfumo wa Muungano.
Nape: Tusubiri tuone kitakachotokea.

Tume ya Mabadiliko ya Katiba leo itakabidhi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Dk. Jakaya Kikwete na Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein, rasimu ya pili na ya mwisho ya katiba mpya, huku

Watanzania wengi wakisubiri kwa hamu kubwa kuona inapendekeza muundo gani wa Muungano baada ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kukataa serikali tatu.
Kwa mujibu wa Katibu wa Tume hiyo, Assaa Rashidi, hafla ya kukabidhi rasimu ya pili itafanyika katika viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam.

Hatua hiyo inachukuliwa na Tume hiyo inayoongozwa na Waziri Mkuu mstaafu, Jaji Joseph Warioba, baada ya kupitia na kuchambua maboresho yaliyofanywa na mabaraza ya katiba ya wilaya ngazi ya kata kwenye rasimu ya kwanza ya katiba mpya miezi saba iliyopita.

Rasimu ya kwanza ya katiba mpya, ambayo ilijadiliwa na mabaraza ya katiba, kuanzia Julai 12 mpaka Septemba 2, ilizinduliwa na Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal, Juni 4, mwaka huu.

Saturday, December 28, 2013

SNURA AWASHUKURU WALIOMTOA

Snura Mushi.
Kupitia ukurasa wake wa mtandao mmoja wa kijamii mwanadada Snura mushi alimua kufunguka yafuatao kwa mdada Wema Sepetu, Tundaman, Chekibudi na Marehemu Sharo Milionea kwa jinsi walivumsaidia kufika hapo alipo leo. Snura alisema yafuatayo…
Kwa Wema Sepetu
Msema kweli mpenzi wa mungu wakati narecod wimbo wangu wa kwanza wema alihusika sana...hela yake ilihusika studio, sauti yake ilihusika kwenye wimbo huo ambao ni shogaake mama ...vazi langu la show kwa mara ya kwanza wema ndio alinibunia namm nimeliandeleza vazi hilo mpaka leo kwenye show zangu sina chakukulipa wema ila nakushukuru sana nakuombea kwa mungu akubariki zaidi na zaidi wema sepetu...

Kwa Tundaman
Sijui nianzie wapi lakini huyu ndio mtu alie tumia nguvu kuniingiza kwenye muziki baada ya kuona kama siwaelewi hivi kila waliponiambia ....wakati anazindua album yake ya starehe gharama pale maisha aliamua kutengeneza tangazo ambalo lilisema snura atatambulisha wimbo wake mpya kwa mara ya kwanza kiukweli alinivuruga kwasababu mm sikua na wimbo wowote sasa kwa kuhofia aibu nishatangazwa ndio nikalazimika kwenda kurecod shogaake mama haraka sana na nikafanya hiyo show watu wakanielewa sana huo ndio ulikua mwanzo ....leo hii nimeona faida yake asante sana kakaangu tunda man mungu akubariki sana umekua mtu muhim sana kwenye maisha yangu tuendelee kushikana hivihivi kwa shida na raha nakupenda sana kakaangu  tunda man captain ...msambinungwa..

DIAMOND, WEMA WATANGAZA NDOA

HUKU mchumba’ke, Penniel Mungilwa ‘Penny’ akifungasha virago kurejea kwao, mzee mzima Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ametangaza kumuoa Miss Tanzania 2006, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’.
Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’(kushoto) na Penniel Mungilwa ‘Penny’ wakiongea jambo enzi za mapenzi yao.
Ishu hiyo ilijiri ndani ya Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar ambapo mkali huyo wa Bongo Fleva alikuwa akikamua kwenye sherehe ya Krismasi aliyoiandaa mwenyewe. Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ baada ya kupanda jukwaani katika viwanja vya leaders.
TANGAZO LA AWALI
Awali kabla ya kufikia eneo la kutangaza kuoana, Diamond aliweka wazi jukwaani kwamba yeye na Wema wamerudiana.
Diamond Platnumz akiongea jambo baada ya Wema Isaac Sepetu ‘Madam’  kupanda jukwaani.
MTIRIRIKO ULIVYOKUWA
Diamond, akiwa ameshika kipaza sauti alikatisha kuimba na kuwauliza mashabiki wake, hasa watoto waliohudhuria kwa wingi tamasha hilo, je, wanataka kumuona shemeji yao?
“Itakuwa si vizuri mkaondoka bila kumuona shemeji yenu, nikuleteeni mumuone?” aliuliza  Diamond. Swali hilohilo akalirudia tena ambapo lilipokelewa kwa shangwe huku mashabiki wakilitaja jina la Wema.

FOLENI KUENDELEA KUTESA JIJINI DAR

Kuna kila dalili kuwa jinamizi la foleni litaendelea kuwatesa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam kwa muda mrefu zaidi kutokana na kasi ndogo ya utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa barabara za pembezoni (ring roads) na usanifu wa barabara za juu (flyig overs) ambayo kwa ujumla inahitaji walau Sh. bilioni 170.
Kero hiyo itapungua kwa kiasi kikubwa ikiwa fedha hizo zitapatikana ili kutekeleza miradi mbalimbali iliyopewa kipaumbele katika kukabili tatizo hilo.

Uchunguzi uliofanywa na NIPASHE hadi kufikia mwisho wa wiki iliyopita, umebaini kuwa ujenzi wa barabara za pembezoni unaendelea kwa kasi ya kinyonga huku ujenzi wa barabara za juu kwenye makutano ya barabara kuu ukiwa ndiyo kwanza uko katika hatua ya usanifu.

Aidha, jumla ya Sh. bilioni 171.2, ambazo ni sawa na asilimia 14 ya bajeti yote ya Wizara ya Ujenzi kwa mwaka huu wa fedha wa 2013/2014, ni sehemu tu ya mikakati iliyopewa kipaumbele katika utekelezaji ili kupunguza foleni jijini Dar es Salaam ikihusisha usanifu wa barabara za juu (Sh. bilioni 100), ujenzi barabara ya Kigogo – Jangwani (Sh. bilioni 7.6), fidia kwa majengo ya kandoni mwa barabara ya Kigogo-Jangwani (Sh. bilioni 15.8) na kipande cha kilomita tatu cha barabara ya Kimara Korogwe- Kilungule kinachogharimu Sh. bilioni 3.5.

Fedha nyingine ni Sh. bilioni 13 kwa ajili ya kilomita saba za Mbezi Mwisho-Goba, Sh. bilioni 16 za Tangi Bovu-Goba, Baruti-Msewe (Sh. bilioni 4.6) na Kigogo- Tabata Dampo (Sh. bilioni 5.7).

HALI ILIVYO
Hakika, katika jiji la Dar es Salaam kunahitaji uvumilivu wa hali ya juu, hasa kuhusiana na usafiri wa kutoka sehemu moja kwenda nyingine nyakati za asubuhi na jioni.

Kiukweli, unaweza kujikuta usingizi wako ukiathiriwa na jinamizi la foleni. Unalala ukiwaza foleni itakavyokutesa asubuhi wakati ukienda au kurejea kutoka katikati ya jiji kusaka mkate wa kila siku.

USIKU WA ZAWADI DAR LIVE DEC 3I, 2013

96% DARASA LA SABA KUJIUNGA SEKONDARI


Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Jumanne Sagini akitangaza wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza 2014 ofisini kwake Dar es Salaam jana. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Tamisemi anayeshughulikia Elimu.

ASILIMIA 96.15 ya wanafunzi wa darasa la saba waliofanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka huu na kufaulu, ndio waliochaguliwa kujiunga na sekondari za serikali.

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu –TAMISEMI, Jumanne Sagini aliwaambia waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kwamba jumla ya wanafunzi 411,127 kati ya 427,609 waliofaulu mtihani huo ndio watakaoanza kidato cha kwanza mwakani.

Alisema wasichana ni 201,021 na wavulana 210,106 na kwamba waliochaguliwa wameongezeka kwa asilimia 31.37 ikilinganishwa na asilimia 64.78 waliochaguliwa awamu ya kwanza mwaka huu.
Kwa mujibu wa matokeo ya mtihani mwaka huu, alama ya juu kabisa kwa wavulana ilikuwa 244 huku ya wasichana ikiwa ni 241 kati ya alama 250 ambapo mwaka jana alama ya juu ilikuwa 237.

“Matokeo yanaonesha kuwa jumla ya wanafunzi 427,609 (wavulana 218,093 na wasichana 209.516) walifaulu kwa kupata alama A-C kati ya 844,938 waliofanya mtihani ikiwa ni sawa na asilimia 50.61 … takwimu zinaonesha ongezeko la asilimia 19 la ufaulu ikilinganishwa na asilimia 30.6 mwaka jana,” alisema Sagini.

Friday, December 27, 2013

WATOTO WATUMIKISHWA KUJENGA UWANJA WA KUMBUKUMBU YA SOKOINE BILA MALIPO


SOLLY MAHLANGU WA AFRIKA KUSINI AKITUMBUIZA UWANJA WA TAIFA TAMASHA LA XMASS

SNURA, MAJANGA HADI MWILINI?

KWA wasiomfahamu msichana huyu, wanamuona kama chipukizi aliyeukwaa ustaa ghafla, lakini wanaofuatilia mambo ya sanaa na burudani, wanamfahamu kitambo. Ninamzungumzia Snura Mushi, ambaye anatamba sana na kibao chake cha Majanga.
 
Ni mmoja kati ya wasanii wapambanaji, wakisaka mafanikio kwa kujaribu kila aina ya njia. Amejaribu kwa muda mrefu katika filamu, lakini hakuweza kufanikiwa ‘kuchomoka’. Kama angetambua tokea mapema kuwa angeweza kuibuka mara moja katika muziki, nadhani asingepoteza muda wake mwingi kwenye filamu.

Wimbo wake wa Majanga umeiteka familia ya muziki wa mduara, huenda kwa sasa ni mmoja kati ya wasanii wachache wanaopata nafasi ya kutakiwa sana katika majukwaa na hivyo kumfanya pia awe anapata hela za kutosha.
 

JACK PATRICK ADAIWA KUNASWA NA PIPI 66 ZA DAWA ZA KULEVYA ZENYE THAMANI YA MIL 215.5 CHINA

Mrembo anayedaiwa kuwa Jack Patrick (akiwa amefunikwa uso) mikononi mwa polisi nchini China baada ya kukutwa na pipi 66 za heroin tumboni.
Mwanamitindo Jack Patrick.
Mrembo anayedaiwa kuwa Jack Patrick akipelekwa katika chumba maalum kwa ajili ya mkutano na wanahabari Jumanne Desemba 19, 2013 huko Macao China. Polisi wakichunguza pipi zenye dawa za kulevya alizokutwa nazo mrembo anayedaiwa kuwa Jack Patrick. Wanahabari nchini China wakichukua picha za dawa hizo za kulevya anazodaiwa kukutwa nazo Jack.
MODO maarufu Bongo, Jacqueline Patrick Cliff, anadaiwa kukamatwa na kilo 1.1 za dawa za kulevya aina ya heroin huko Macao nchini China. Dawa hizo zilikutwa tumboni mwake baada ya kushtukiwa na kufanyiwa X-ray ambapo alikutwa na jumla ya pipi 66 vyenye thamani ya dola za Kimarekani 137,720 sawa na shilingi milioni 215.5 za Kitanzania.
Inadaiwa kuwa Jack alikuwa akisafiri kutoka Thailand akielekea Macao Jumanne ya Desemba 19, 2013. Aliwaambia polisi kuwa alikuwa anaelekea Guangzhou ambao ni mji wa jimbo la Guangdong huko China.
Jack alipata jina aliposhika namba tatu kwenye Miss Ilala na kushiriki Miss Tanzania mwaka 2005/06. Pia uliuza nyago kwenye video ya mwanamuziki wa Bongo Fleva, Marehemu Albert Magwea ‘Ngwair’ iliyokwenda kwa jina la She Got A Gwain. Kuanzia hapo jina likawa kubwa na akawa mwanamitindo maarufu Bongo.
Ni katika kipindi hicho cha umaarufu akaolewa na mtoto wa aliyekuwa mwanasiasa mkongwe, Abdallah Fundikira, Abdulatif kabla ya jamaa huyo kutupwa nyuma ya nondo za mahabusu ya Keko, Dar akikabiliwa na msala wa kusafirisha mihadarati.

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate