EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, December 31, 2012

YANGA WAKIWASILI UTURUKI

@Antalya Airport tayari kwa safari ya kwenda hotelin
Ernest Brandts & Baraka Kizuguto

TANGAZA NASI LEO HII

Irene Mwamfupe Jamii Blog tunapenda kuwatangazia wasomaji wetu wote kuwa kuna punguzo maalum fungua Mwaka kwa kutangaza nasi ndani ya blog.Wahi sasa tangaza biashara yako.Ofa hii inaanza leo hii mpaka 2o January 2013.

Wasiliana nasi:+ 255 767 207 525.Email:rynbeny@yahoo.com
Vigezo na masharti kuzingatiwa.
Asanteni.

Je kwenye pochi yako kuna haya yote?kama hakuna bi mkubwa unahitaji na yote haya yanapatikana AK Cosmetics.

TUPO SINZA KUMEKUCHA NA KINONDONI MANYANYA-DAR

Mally Beauty Makeup Makeover Collection QVC Todays Special Value January

Breaking News:Zaidi ya kaya 30,000 Dar kukosa mawasiliano.

WAKATI zimebaki dakika chache kabla ya jijini la Dar es Salaam, kutoka katika mfumo wa analojia na kuingia katika mfumo wa dijitali, zaidi ya kaya 30,000 kukosa mawasiliano kwa njia ya luninga na redio baada ya mitambo ya kurusha mawasiliano kuzimwa rasmi kuanzia saa 6:00 usiku huu.
 
Kufuatia uchunguzi uliofanywa imebaini kwamba zaidi ya kaya 30,000 jijini Dar es Salaam,hazikufanya maandalizi ya kununua ving’amuzi kwa ajili kuuangalia matangazo ya Redio na Lninga,ambapo maeneno yatakayokumbwa na mabadiliko hayo ni pamoja Mbagala,Gongo la Mboto,Tegeta,Kigamboni pamoja Kisarawe.

HATIMAYE FILAMU YA HARAKATI YATINGA SOKONI

ILE filamu iliyotokea kuzua gumzo kabla haijatoka, inayokwenda kwa jina la ‘Harakati’, imetinga sokoni leo ambako inasambazwa na Kampuni ya Steps Entertainment.
Filamu hiyo inashirikisha nyota kadhaa wa filamu za Kibongo, akiwamo Rashid Waziri, Fikiri Salum, Jenifer Raymond na Mshindo Jumanne.
Taarifa kutoka ndani ya Kampuni ya SSG Distributors iliyotengeneza muvi hiyo, zinasema kuwa, kuanzia sasa, itapatikana nchi nzima kwenye DVD pamoja na VCD.
“Harakati ni miongoni mwa muvi kali kupita kawaida za Kampuni yetu, ambayo tunaamini itafanikiwa kuteka vilivyo nafsi za mashabiki wetu,” ilisema taarifa hiyo.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU TAREHE 31.12.2012

                                                 MAGAZETI YETU LEO-TANZANIA
.
.
.

Jinamizi la kubadili Hoteli yaikumba Yanga Uturuki.

KIKOSI  cha mabingwa wa kombe la Kagame mara mbili mfululizo timu ya Young Africans imewasili salama katika mji wa Antalya kusini mwa nchi ya Uturuki majira ya saaa 10:30 jioni kwa saa za afrika mashariki na kati na moja kwa moja kupolekewa na wenyeji wake kampuni ya Team Travel.
 
Young Africans imefikia katika hoteli ya Fame Residence Lara & Spa kilomita chahce kutoka katika uwanja wa ndege wa antalya, ambapo hoteli ya Fame Residence ipo mwambaoni mwa bahari ya mediteranian.

FERGUSON AWAKATA MAINI ASRENAL, ASEMA LUIS NANI HAUZWI

LONDON, ENGLAND
ALEX FERGUSON amefuta ndoto za Arsenal kutaka kumsajili winga wake Luis Nani, 26, wakati dirisha la usajili la mwezi Januari litakapofunguliwa.
Winga huyo wa Kireno amekuwa akihangaika kupona maumivu ya misuli ya paja yaliyomuweka nje tangu Novemba, lakini United imeeleza kuwa kuna mazungumzo ya kuongeza mkataba wake wa sasa – uvuke mwaka 2014.

Sunday, December 30, 2012

MTOTO WA ROMA MKATORIKI NI HUYU HAPA

Picha za Mtoto wa Kwanza wa Kiume wa Roma AliyeMpa Jina Ivan Yani Gift From God.

Simba yakiona kwa Tusker..Yacharazwa bakora tatu Uwanja wa Taifa.

MABINGWA wa soka wa Kenya, Tusker FC, jana walizidi kudhihirisha ubabe wao kwa miamba ya soka ya Tanzania, baada ya kuwabonyeza Simba kwa mabao 3-0 kwenye mechi ya kirafiki ya kimataifa iliyochezwa Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.

Kwa ushindi huo, Tusker ambao ni mabingwa mara 10 wa Ligi Kuu ya Kenya tangu kuanzishwa kwao mwaka 1970, wameweka rekodi ya kuvifunga vigogo vya soka nchini baada ya kuifunga pia Yanga bao 1-0 katika mechi ya kwanza katikati ya wiki.
Shujaa wa mechi ya jana alikuwa Ismail Dunga aliyeifungia timu yake mabao mawili katika kipindi cha kwanza, akifunga la kwanza dakika ya 39, baada ya kuwazidi mbinu mabeki wa Simba kabla ya kumpiga chenga kipa William Mweta na kuujaza mpira katika vyavu.

Bao hilo liliwaamsha wachezaji wa Simba ambao walizidi kulisakama lango la Tusker, lakini safu ya ulinzi ya Wakenya hao ikiongozwa na Joseph Shikokoti aliyewahi kuichezea Yanga, ilikuwa makini kuokoa hatari nyingi kumfikia kipa wao Samwel Odhiambo.
Dakika ya 45, Dunga alirejea katika lango la Simba na kumtungua Mweta kwa mara nyingine baada ya kupokea pasi murua kutoka kwa Maurice Odipo, hivyo wakali hao kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao hayo mawili.

SOKO LA SIDO,MWANJELWA JIJINI MBEYA LIMEWAKA MOTO USIKU WA KUAMKIA LEO

                Wananchi wakiwa wanashuhudia Moto huo usiku wa jana.

Unique Model 2012 ni Catherine Masumbiga.


Mwanamitindo bora wa mwaka 2012

Catherine Masumbiga (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Unique

Model Photogenic Elizabeth Pertty (kushoto) na Unique Model Talent

Vestina Charles mara baada ya kutangazwa kwa mshindi.…
Mwanamitindo bora wa mwaka 2012
Catherine Masumbiga (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na Unique
Model Photogenic Elizabeth Pertty (kushoto) na Unique Model Talent
Vestina Charles mara baada ya kutangazwa kwa mshindi.
Mwanamitindo
wa mwaka 2012 Catherine Masumbiga (katikati) amepatikana jana usiku
kwenye shindano lililofanyika kwenye Klabu ya New Maisha
jijini Dar es Salaam akiwa kwenye picha ya pamoja na washindi wa pili
Cesilia Michael (kushoto) na mshindi watatu Amina Ayubu.

MASTAA WA BONGO NA MAZITO 2012

Stori: Sifael Paul
Hakuna tamu isiyokuwa nachungu! Kwenye ulimwengu wa mastaa Bongo kulikuwa na matukio  ya mengi ya kusikitisha mwaka huu lakini Yafuatayo ndio mazito zaidi kwa mwaka 2012,Risasi jumamosi lina ripoti kamili.Matukio hayo ya huzuni yamegawanyika makundi tofauti yakiwemo yale ya vifo, kuvunjika kwa ndoa na wengine kutupwa rumande kwa misala mbalimbali.

UVCCM yapanga kufanya maandamano

JUMUIYA ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) wilayani Kahama, umedhamiria kufanya maandamano ili kushinikiza kuwang’oa watumishi wa serikalini waliopo ndani ya wilaya hiyo ambao utendaji kazi wao umekuwa kero kwa jamii.
Akizungumza na waandishi wa habari jana wilayani hapa, Mwenyekiti wa umoja huo, Solomoni Mataba, alisema wamedhamiria kuwang’oa katika nafasi zao watumishi wasio waadilifu, wanaochangia kuipaka matope serikali iliyopo madarakani.

Alisema kuwa wamejipanga kuwafichua wasiofuata maadili ya uwajibikaji kazini na kuwa kero, ikibidi kwa kufanya maandamano ili wakazi wa wilaya hiyo waweze kupata haki yao.
Mataba aliwataka watumishi waliosahau wajibu wao huku wakijifanya miungu watu, kuhakikisha wanafuata maadili na kuacha kufuata maslai binafsi ambayo imekuwa sababu kubwa ya jamii kuichukia serikali.
Mwenyekiti huyo alisema kuwa baadhi ya idara zimejisahau, huku zikiwanyanyasa wananchi hatua ambayo inazidisha chuki kwa serikali yao.

Saturday, December 29, 2012

Magari 7 yateketea kwa moto Dar

MAGARI saba yameteketea kwa moto katika nyumba ya Laurence Nchimbi (61) maeneo ya Tabata Kimanga jijini Dar es Salaam.

Kamanda wa Polisi Mkoa Kinondoni, Charles Kenyela, alisema kuwa moto huo ulitokea juzi majira ya saa 2:30 mchana katika eneo hilo ambapo ulidaiwa kuchangiwa na hitilafu ya umeme iliyoanzia kwenye gari T 312 BGJ Double Coaster.

Aliyataja magari mengine ni T 467 CFZ Scania, T 234 BSW Double Coaster, T 530 AWG Double Coaster, T 603 CAW Nissan Civilian, T 435 BFB Nissan Civilian na T 299 BWG Nissan Civilian ambayo yaliteketea kabisa.

Alisema kuwa hadi sasa thamani ya magari hayo bado haijafahamika ambapo moto huo ulizimwa na kikosi cha Zimamoto cha jiji wakishirikiana na wananchi wa eneo hilo na hakuna madhara zaidi kwa binadamu.
Kenyela alisema kuwa upelelezi wa tukio hilo unaendelea.
Katika tukio jingine, Kamanda Kenyela alisema kuwa, juzi majira ya saa 16:00 jioni katika eneo la Manzese Tip Top mtu aliyetambulika kwa jina la Ismaili Mgawo (50), dereva wa 

TANESCO alifariki baada ya kujiokoa kutokana na moto uliozuka katika hoteli ya MJ.
Kenyela alisema chanzo cha moto huo kilianzia katika chumba kilichokuwa kina kiyoyozi na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Mwananyamala.
Wakati huo huo, watu wawili wamefariki dunia jijini Dar es Salaam katika matukio tofauti likiwepo la mtoto kufa maji.

John Mnyika, Zitto, wabunge bora 2012

MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika (CHADEMA), kwa sasa ndiye anashikilia rekodi ya ukinara wa kuchangia mara nyingi bungeni kwa mwaka 2012, akifuatiwa na Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto (CHADEMA) na Godfrey Zambi wa Mbozi Mashariki (CCM).

Kwa mujibu ya rekodi zalizomo kwenye mtandao wa Bunge, Mnyika ambaye ni kipindi chake cha kwanza bungeni, ameonekana kufanya vizuri zaidi sambamba na wabunge wenzake kadhaa wa CHADEMA.
Takwimu hizo hazijawahusisha mawaziri, manaibu wao, Spika, naibu wake, wenyeviti watatu wa Bunge, Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa vile nafasi zao zinawapa uwezekano mkubwa wa kuchangia hoja wakati wowote.

Wabunge kumi ambao wameshika nafasi za juu ni Mnyika akiwa amechangia mara 184, kuuliza maswali ya nyongeza 28 na ya msingi 7, akifuatiwa na Zitto (mchango 79, maswali ya nyongeza 25 na maswali ya msingi 8) wakati Zambi anashika nafasi ya tatu kwa kuchangia mara 70, (maswali nyongeza 26) na (maswali ya msingi 9).

Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu anashika nafasi ya nne akiwa amechangia mara 93, maswali ya nyongeza 19 na yale ya msingi 7, akifuatiwa na Diana Chilolo wa Viti Maalumu (CCM) aliyechangia mara 61, maswali ya nyongeza 41 na msingi 9.

SOME TEXT MISSING-01

Mara yangu ya kwanza kuishi Ilala, Dar es Salaam kwa muda mrefu ni pale nilipokwenda kumtembelea  kaka Luka wakati anaumwa miguu kiasi cha kushindwa kutembea hata hatua moja. 
Mbaya zaidi, katika kipindi hichohicho akapata ugonjwa wa kupooza ‘stroke’, hivyo wazazi wakaniambia nifunge biashara yangu ya genge,  pale Dodoma nije kumsadia shemeji.
Nilipokelewa na mke wa kaka, mama Lilian ambaye alinishukuru sana kwa uamuzi wangu wa kuja Dar kwa kaka kwani itamsaidia yeye kufanya mambo mengine ambayo yalilala kwa sababu ya mumewe kuugua miguu na kupooza.

Kaka alikuwa hawezi kwenda chooni, kwenda bafuni bila kupelekwa na mbaya zaidi kazini kwake, walishamtosa kiaina kwani misaada ilipungua tofauti na zamani.
“Vipi nyumbani lakini, hajambo baba, mama?” kaka aliniuliza.
“Kusema ukweli kaka wote wazima, ila baba naye alikuwa akisumbuliwa na macho, lakini kwa sasa yuko sawasawa.”
“Asante sana kwa taarifa, mimi kama unavyoniona, ni muda mrefu naumwa, niko ndani tu.”
“Pole sana kaka.”
“Asante mdogo wangu.”


WEBSITE MPYA TANZANIA SALUTI 5

       Kwa Habari moto moto za Michezo,Burudani,Maisha na Jamii.TEMBELEA www.saluti5.com
                                                                          

INAKERA VIBAYA SANA SOMA HAPA

KUDAMKA KUPIGA DEKI KWENYE KORIDO WAKATI KUNA WAGENI WAMELALA
NI jambo la ajabu sana, utakuta mwanamke amepata wageni, ndugu wa mumewe wametokea kijijini. Kwa sababu sehemu ya kulala ni finyu, mume anamwambia mkewe watandikiwe kwenye korido ndani walale maana watakaa siku mbili au tatu tu.
Cha ajabu sasa, mke huyo anayeonekana ana busara zake, anadamka saa kumi na moja alfajiri na kuanza kupiga deki hivyo kuwafanya wageni waamke na kwenda kukaa nje kwa sababu ya maji, tena ya baridi maana ni asubuhi. INAKERA SANA.
 
HII NAYO INAKERA
MKE KUULIZWA CHUMBANI, KWENDA KUJIBA SEBULENI
UTAKUTA mke wa mtu yuko na mumewe chmumbani, anamuuliza ‘dear ni kwanini leo chakula kinanuka sana moshi?’ mke badala ya kujibu kulekule chumbani, anatoka kama vile hajamsikia mumewe, akifika sebuleni ndiyo anaanza:
“Si ungepika wewe kama unajua kupika. Moshi moshi, wenzako Somalia wanatafuta chakula hata kinachonuka kinyesi hawakipati, acha hizo.”
Inakera sana, ukizingatia sebuleni anakokwenda kujibia kumepakana na dirisha la nyumba nyingine ya pili!

PADRI MLA NYAMA ZA WATU-01

Mkasa huu unasimuliwa na Padri Moses au kwa kifupi Faza Moze lakini si jina lake halisi , akiweka bayana mambo aliyoyafanya mpaka kujutia. Padri Moses hakutaka kuweka wazi ni wa kanisa gani kwani Mapdri hutumiwa na makanisa ya Anglikani na Romani. Anasema:

“Ilikuwa mwaka 1999, mwezi Desemba wakati wakristo wanajiandaa kwa sherehe ya Krismasi, kanisani walikuja wazee wawili ambao ni wageni machoni pangu miongoni mwa waumini wa kanisa langu hilo .
Walikaa fomu moja na waumini wengine, lakini katika kukaa walitenganishwa na mzee mmoja. Nikiwa naendelea na ibada, kila wakati niliwaona wale wazee wageni wakiangaliana kwa kupitia mgongoni kwa yule mzee aliyewatenganisha.

Kwa sababu moyo wangu ulikosa amani na wao, nikawa nawakazia macho hatua kwa hatua ili nione kila walichokuwa wakikifanya.
Kuna wakati nilishtuka sana kuona mmoja wao akibadilika sura na kuwa kama ya bundi, lakini nilipojiweka sawa kushangaa, akarudi katika sura ya kawaida, na mwenzake akacheka kama vile alijua mwenzake amegeuka sura na mimi nimeogopa.
Ndipo nilipoanza kukumbuka ujaji wao kama ulifanana na mazingira ya kuwa waumini wangu.

Nikakumbuka kuwa, wakati wanaingia, walipitia njia zote za uumini, na pia walionekana ni wanyenyekevu kupita hata waumini wangu wa kila siku.
Wakati nikiwaza hayo, ghafla mmoja wa wale wazee alisimama mbele yangu bila kumwona akitoka kwenye fomu kuja mbele, nikashituka, lakini kumbe waumini wengine waliniona nilivyoshituka, wakakaza macho kiwangu wakishangaa.
Nilikatisha maneno ya ibada na kuinua mikono juu kisha nikafanya ishara ya msalaba, kwa jina la baba, la mwana na la roho…

UKIMWONYESHA UNAMPENDA SANA LAZIMA ATAKUTENDA.

Binadamu ndivyo walivyo, pale unaposema nampenda sana mwenzangu na ukamwonyesha mapenzi mazito mazito ndipo atakapokutenda bila kujali maumivu utakayoyapata.
Hali hii inaweza kumtokea mtu bila mwenyewe kujijua endapo atakuwa mtu wa kushindwa kutumua akili kufanya kumbukumbu za maisha.
WANAWAKE WANAONGOZA
Tabia hii ipo kwa pande zote mbili, mwanamke na mwanaume lakini kwa undani zaidi wanawake ndiyo wanaoongoza kwa kumtenda mwanaume aliyeonyesha mapenzi mazito kwake.
Wengi walioongea na safu hii kwa jinsi zote wanawake ndiyo walizidiwa na skendo hii ya kutenda wapenzi wao.
Muddy Sukari wa Dar es Salaam yeye anasema aliwahi kumpenda mwanamke kupita maelezo. Ikafika mahali akaamua kumsomesha hadi chuo kikuu kwa lengo la kumwongezea elimu ili maisha yawe bora, lakini baada ya kuyapata hayo maisha bora alimtenda.
 
MWANAMKE AKIJUA ANAPENDWA HUFANYA HAYA
Kwa mwaname, upembuzi unaonyesha kwamba akishajua mwanaume anampenda sana, huanza maringo, kutotii na kushika njia yake katika mahusiano akiamini hawezi kuachwa kwa sababu anapendwa sana.
Hili linataka kuonyeshwa kwamba, kama mwanaume atampenda sana mwanamke iwe sehemu ya siri ya moyo wake badala ya kumwambia au kumuonesha kwa vitendo.

Wahamiaja haramu 18 wafariki Misri

Balozi wa Somalia nchini Libya Bwana Abdikani Mohamed Waeys amesema ana taarifa ya vifo vya raia 18 vilivyotokea kutokana na ajali ya lori nchini Libya.Wasomali hao wanaotajwa kuwa wahamiaji haramu, 23 wameripotiwa kujeruhiwa huku wengine wakiwa katika hali mbaya.
 Wahamiaji haramu
                                          Wahamiaji haramu wakijaribu kuvuka baharini
Balozi Abdikani amesema lori hilo lililokuwa limebeba mifuko ya saruji walimokuwa wamejificha Wasomali hao, lilipinduka na kusababisha vifo, na kusema idadi yao walikuwa 120 wakiwemo wanaume na wanawake wote wakiwa ni Wasomali.Katika miaka ya hivi karibuni idadi ya wahamiaji haramu ambao wamefariki wakijaribu kuvuka baharini imeongezeka.

Friday, December 28, 2012

Hukumu kesi ya Lema yaibua mapya

MWANAZUONI aliyebobea katika sheria, Profesa Issa Shivji na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Francis Stolla wamekosoa hukumu ya Mahakama ya Rufani, iliyomrejesha bungeni, Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti juzi, wanasheria hao walisema hukumu hiyo iliyotolewa na majaji watatu wakiongozwa na Nathalia Kimaro, Salum Massati na Bernard Luanda, inapingana na sheria.

Hata hivyo, mmoja wa mawakili wa Lema, Method Kimomogoro amepinga madai hayo akisema wanaoipinga pengine hawajapata nafasi ya kuliangalia kwa undani suala la haki ya mpiga kura kupinga matokeo mahakamani.

Yaliyojiri katika muziki, burudani 2012.

MWAKA 2012 ndio uko ukingoni, ambapo Jumanne ijayo panapo majaliwa yake Mungu tutaingia katika mwaka mwingine, yaani 2013.

Leo kwa vyanzo na kumbukumbu nyingi za habari za kisanii tutakuletea baadhi ya matukio yaliyotikisa katika mwaka huu.
 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhlUJOLATpwxAiBOS2vl-D51vjuSohYxKtCD29n8pvKcrofzMOWXUiTKL5pUHRpeRsWGBGpd62Hygwtm5jqQOcQf1L3JDrGW9F12JWvCqWV8j-omrBeSmW6K4jPDSgpLEw9m_LdfV2aCojv/s1600/wema-vs-diamond.jpg
Katika mwaka wa 2012 wamiliki wengi wa bendi walionekana na kutawaliwa na mzimu wa kunyakuliana wanamuziki huku kila mmoja akiamini kwamba hiyo ndiyo ilikuwa njia ya kujipatia jina na kuzoa mashabiki.
Mwanzoni mwa kwaka huu bendi ya muziki wa dansi ya Twanga Pepeta ilipata mtikisiko mkubwa kwa kunyakuliwa aliyekuwa muimbaji kiraka wa bendi yake, Charles Gabriel ‘Chalz Baba’ aliyenyakuliwa na bendi ya Mashujaa.

Kama hiyo haitoshi, pia msanii huyo akiwa na rapa wa bendi ya FM Academia 33 waliandaliwa usiku maalumu wa utambulisho uliofanyika kwenye ukumbi wa Business Park, Dar es Salaam.
Charlz Baba alinyakuliwa mara tu baada ya bendi hiyo kutoka katika ziara yake nchini Uingereza ilikokwenda kwa mwaliko maalumu.

Sheikh Dar alaani padri kupigwa risasi.

SIKU moja baada ya padri wa kanisa Katoliki lililoko Mpendae visiwani Zanzibar, Ambrose Mkenda, kujeruhiwa kwa risasi na watu wasiojulikana nje ya nyumba yake wakati akitoka kanisani, Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Musa Salum, amelaani tukio hilo na kuwataka Watanzania kuwafichua wale wote waliohusika katika tukio hilo baya kwa mustakabali wa taifa.

Akizungumza  jana, Sheikh Salum alisema hivi sasa kumekuwa na viashiria vinavyonekana kutaka kutowesha amani, jambo linalohitaji kuwepo kwa ushirikiano wa pamoja ili kuhakikisha amani inaendelea kudumu.

Alisema ni muhimu Watanzania wakawafichua wale wote waliohusika katika tukio hilo, ili kujua ukweli na kuweza kulisaidia Jeshi la Polisi.

“Ni muhimu kujua ukweli wa tukio hili, kwani wapo wanaoweza kuamini kuwa ni viashiria vya chuki vya kidini,” alisema.

Alisema mauaji ya kimbari yaliyojitokeza katika baadhi ya nchi nyingine za Afrika yalichangiwa na vitu mbalimbali ikiwemo matatizo ya udini, ukabila vitu ambavyo vimeanza kujitokeza nchini.
Sheikh Salum alisema mfumo wa kukubali ukabila huku wengine wakinyimwa haki inaweza kuwa chanzo cha kutokea kwa vurugu, hivyo kuna haja ya kushirikiana kwa umoja, ili kukomesha viashiria hivyo.

Umeme hali tete Tanzania.

Chanzo cha habari-Tanzania Daima.
LICHA ya viongozi na watendaji wa Wizara ya Nishati na Madini pamoja na wale wa Shirika la Ugavi wa Umeme (TANESCO), kujaribu kuficha ukweli kuhusu hali ya uzalishaji na usambazaji wa umeme wa uhakika nchini, Tanzania Daima imedokezwa kuwa hali ni tete.
Kutokana na mkakati wa wizara husika ulivyo sasa, inaelezwa kuwa ili mgawo wa umeme utoweke, kiasi cha sh bilioni 42 zitapaswa kutumika kila mwezi kwa ajili ya kuyalipa makampuni yanayoiuzia TANESCO umeme.

Kwa muda mrefu sasa TANESCO imeelezwa kuwa hoi kifedha licha ya kuwa na makusanyo makubwa lakini fedha hizo zimekuwa zikiishia mikononi mwa mafisadi na hivyo shirika hilo kubakia tegemezi kwa serikali.

Kwa mujibu wa takwimu za Waziri wa Naishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo, alizozitoa bungeni wakati akihitimisha hoja ya hotuba ya bajeti yake kwa mwaka 2012/2013, TANESCO inakusanya mapato kati ya sh bilioni 60 mpaka 70 kwa mwezi.
Hata hivyo katika hali ya kushangaza, licha ya matumizi ya shirika hilo kuwa sh bilioni 11 kwa mwezi, Waziri alishindwa kufafanua ni wapi zinakwenda sh takribani bilioni 40 zinazosalia.
Waziri Muhongo alilieleza Bunge upotevu huo wa mabilioni bila kufafanua Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA), wamefanya nini kama fedha hizo zinaibiwa.

BARAZA LA WAZEE SIMBA LAPIGA MKWARA MKUTANO WA JUMAPILI

KUFUATIA mkutano ulioitishwa na baadhi wa wanachama wa Simba Jumapili hii, Baraza la Wazee wa klabu hiyo ya mtaa wa Msimbazi, limewataka wanachama hao kutoitisha mkutano huo kwa vile mkutano huo si halali.
Kaimu Katibu Mkuu wa Baraza hilo, Zuberi Mpacha, alisema jana kuwa si kweli kuwa wanachama wakifika 500 wanakuwa na uwezo wa kuitisha mkutano.
Zuberi alisema kuwa mkutano bila ya ridhaa ya uongozi si halali hivyo kufanya hivi itakuwa kinyume na katiba ya Simba.
Akinukuu baadhi ya vifungu vya katiba ya Simba, Zuberi alisema kifungu cha 22 kinakataza kuwepo kwa mkutano bila ya ridhaa ya viongozi.“Baraza la Wazee tunasema mkutano huo si halali kabisa, kama kuna matatizo ndani ya uongozi kuna sehemu ya kusuluhisha na si kutumia mikutano ambayo si halali” alisema Mpacha.
Baadhi ya wanachama wameitisha mkutano wa dharura kupinga uongozi wa klabu kufutia kufanya vibaya katika mzunguko wa kwanza wa Ligi kuu Tanzania Bara.Via saluti5.

Thursday, December 27, 2012

Mabondia wa Tanzania jana waling'ara Mada Maugo na Mbwana Matumla.

Mabondia wa Tanzania jana waling'ara katika mapambano yao yaliyofanyika katika ukumbi wa Dar Live Mbagala Zakhem.
Bondia maarufu nchini, Mada Maugo alimchapa Yiga Juma kutoka Uganda raundi ya kwanza kwa ‘Knock Out’.
Katika hali iliyoonesha kuwa siku ya vichapo kwa wageni, pambano lingine ambalo bondia Mbwana Matumla alipambana na bondia kutoka Kenya, David Charanga lililokuwa la raundi nane, Matumla aliibuka kidedea katika raundi zote nane na kumfanya aibuke na ushindi wa kishindo.


Bondia Mada Maugo (Tanzania) akitangazwa mshindi baada ya kumtwanga bondia Yiga Juma (Uganda) kwa ‘Knock Out’ raundi ya kwanza.
Bondia Mbwana Matumla (Tanzania) akitangazwa mshindi baada ya kumpa kichapo bondia David Charanga (Kenya).

VANESSA MDEE AINGIZWA MKENGE BLACKBERRY YAKE YABEBWA MAENEO YA MBAGALA.

Pamoja na kupiga show ya nguvu jana kwenye uwanja wa taifa wa burudani, Dar Live uliopo maeneo ya Mbagala, Dar es Salaam, Vanessa Mdee aliondoka na huzuni baada ya wajanja ‘kumchapa’ blackberry yake.
Kupitia Twitter, Vanessa ameandika:

ommy 2

PADRI APIGWA RISASI HUKO ZAINZIBAR.


Watu wasiojulikana jana wamempiga risasi Father, Ambros Mkenda wa Kanisa Katoliki la Mpendae Mjini Zanzibar nje ya nyumba yake majira ya saa 12 jioni wakati akitokea Kanisani.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi Aziz Juma Mohammed amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambalo alisema Father amepigwa risasi na ameumizwa sehemu ya kichwa na amekuwa akitoka damu nyingi kichwani na tayari anapatiwa matibabu katika hospitali kuu ya Mnazi Mmoja.

Alisema jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi wa tukio hilo ili kubaini wahusika walifanya uhalifu huo kwa madhumuni gani kabla ya kuchukuliwa hatua za kisheria.

“Sisi tunahesabu kuwa kitendo hiki ni kitendo cha kihalifu na tunawatafuta wahalifu waliofanya kitendo hiki kwa hivyo bado ni mapema kusema kwamba kitendo hiki kimefanywa na nani kwa kuwa bado uchunguzi wetu unaendelea na hadi sasa hakuna mtu tuliyemshika kuhusikana na tukio hili” alisema Kamanda.

VITUKO VYA KRISMASI: NGUO ZA NDAN HADHARANI, SIGARA NA MADAWA YA KULEVYA KWA SANA.

Mrembo  akiwa busy kuzikuna nyeti  zake bila kujali  watu....Kwake chupi  si kitu.Ionekane, au  isioneka  kwake ni sawa tu.....

Machangdoa nao hawakukosekana.Baadhi  yao walinaswa  wakipiga sigara na madawa  mengine ili kujipa  ganzi kwa  ajili  ya wateja  wao........

Kwa kifupi  ni kwamba, Mengi yametendeka wakati  wa sikukuu ya krismas.Kila mtu  aliamua  kutoka  kivyake  maadam  akidhi  haja zake......

 Neno  "machangu"ni la kawaida  siku hizi....Mwanamke  kuvuta  sigara  naona pia  wamelihalalisha.......

MADEMU 10 WAKALI WA MASTAA WA SOKA DUNIANI.

KUNA wake na wapenzi wengi wa wachezaji soka maarufu duniani, lakini mtandao wa SunSport umetoa picha 10 za wanaoonekana kuwa wakali zaidi ya wenzao.
Mwanamitindo wa kirusi, Irina Shayk mchuchu wa Cristiano Ronaldo
Abbey Clanx mke wa Peter Crouch wa Stoke City
Mwimbaji Shakira totoz la Gerrard Pique wa Barcelona

MANCHESTER UNITED UGONJWA WA MOYO, YAFUFUKA MARA 3 KWA NEWCASTLE, LIVERPOOL HAINA JIPYA.


KWA wapenzi wa Manchester United hali ilikuwa ni ya kihoro katika mchezo wa Ligi kuu ya Uingereza dhidi ya Newcastle uliochezwa kwenye uwanja wa Old Trafford.
Manchester United ililazimika kusawazisha mara 3 na hatimaye kupata bao la nne dakika ya tisini lililoipa ushindi wa mbinde wa 4-3.
Hernendes akipiga bao la nne na la ushindi
Imekuwa ni kama jadi sasa kwa United kutoka nyuma na kuibuka na ushindi, hali ambayo imekuwa ikiwaweka roho juu mashabiki wake katika kila mchezo.
Newcastle walianza kuongoza dakika ya 4 ya mchezo kwa goli la James Perch, John Evans akasawazisha dakika ya 25.

Wednesday, December 26, 2012

DIAMOND DAR LIVE WEE WACHA TU.

WASANII mahiri wa muziki wa kizazi kipya nchini Nasibu Abdul 'Diamond Platnumz' na Omary Nyembo 'Ommy Dimpoz' usiku wa kuamkia leo wameweka historia kwa kufanya shoo ya aina yake ndani ya ukumbi wa kisasa wa Dar Live uliopo Mbagala Zakhem jijini Dar es Salaam.
Wasanii hao walisindikizwa na mkali Juma Nature na kundi lake la Wanaume Halisi, Msanii mkongwe Ally Baucha pamoja na Bendi ya Extra Bongo.
...Chezea Diamond wewe!
..Leka dutigite: Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe na Diamond wakiwapagawisha mashabiki kwa wimbo wa Leka dutigite.
Ommy Dimpoz 'on da stage'!

Ligi ya England kuendelea leo.

Vinara wa ligi kuu ya Premier ya England kwa sasa Manchester United inajiandaa kuendelea uongozi wao wakati watakapoialika Newcastle siku ya leo.

Mabingwa watetezi Manchester City nao watakuwa nyumbani kucheza na Sunderland.
Katika mechi zingine, Reading inayoshikilia nafasi ya mkia imepangiwa kucheza na Swansea, West Brom nayo kusafiri ugenini kupepetana na QPR.

Baada ya kuandikisha matokeo yasiyoridhisha katika mechi yao ya mwishoni mwa juma lililopita, Manchester United itakuwa ikipania kujiimarisha kileleni mwa ligi hiyo kwa kuandikisha ushindi.United ilitoka sare mechi yao ya mwisho dhidi ya Swansea na kufikia wakati huu bado imo alama nne tu mbale ya mabingwa hao watetezi.

Vilabu hivyo viwili vilipoteza mechi zao za tarehe 26 Desemba msimu uliopita uliopita na makocha Alex Ferguson na Roberto Mancini tayari wametoa onyo kwa wachezaji wao kuzuia matokeo kama hayo.
Baada ya kuandikisha ushindi wa magoli manane kwa yai dhidi ya Aston Villa, Chelsea imeratibiwa kucheza na Norwich.

Liverpool kutoana jasho na Stoke city na Fulham kualika Southampton katika uwanja wao wa nyumbani wa Craven Cottage.

Mechi kati ya Arsenal na West Ham imehairishwa kutokana na uwezekano wa kuwepo kwa mgomo wa madereva wa treni.

Totten kuchuana na Aston Villa na Everton kucheza dhidi Ya Wigan.

WOLPER, BABY CANDY POZI TATA

Na Mwandishi Wetu(Habari na www.globalpublishers.info )
PICHA za mastaa wa Kibongo Jacqueline Wolper Masawe na Baby Candy zimenaswa katika mtandao wa BBM na kuzua utata kutokana na pozi lao, Risasi Mchanganyiko linakumegea.
 
Jacqueline Wolper Masawe na Baby Candy katika pozi la kimahaba.
Wawili hao ambao wote wana majina katika tasnia za filamu na muziki wamepiga picha na kukaa katika pozi tata kiasi cha kuacha maswali kwa wadau wa fani zao.
Katika picha hiyo, Wolpler anaonekana akiwa amesimama mbele ya Baby Candy na kurudisha mkono wake nyuma huku akiingiza kidole mdomoni mwa msichana mwenzake huyo (angali picha uk 16).
Mashabiki wa mastaa hao walipoiona picha hiyo iliyotupiwa kwenye mtandao huo wa BBM walisema kuwa pozi hilo ni la kimahaba na si zuri kwa watoto wa kike.

DHAMANA YA LULU MAHAKAMA KUU.


Na Mwandishi Wetu
SIKU chache baada ya kupunguziwa makali ya kesi ya kuhusishwa na kifo cha msanii mwenzake, Steven Charles Kanumba, staa aliyefanya vizuri kwenye tasnia ya filamu, Elizabeth Michael ‘Lulu’ameombewa dhamana baada ya hati maalum ya dharura kutinga Mahakama Kuu Tanzania, Jumatatu iliyopita.

Ujumbe wa Papa kwenye Twitter

Papa Benedict wa 16 ametuma ujumbe wake wa kwanza kwenye akaunti yake yaTwitter. Ujumbe huu ulikuwa umesubiriwa kwa hamu sana.

Alionekana akibonyeza kwenye tabiti yake ya iPad na kutuma ujumbe huo.

Ujumbe wake ulikuwa unasoma hivi '' Marafiki wapendwa, nimefurahi sana kuwasiliana nanyi kupitia Twitter. Asanteni sana kwa ujumbe wenu na ninawabariki nyote.''
Papa akituma ujumbe wake wa Twitter
Msemaji wake alisema kuwa ujumbe wa Papa utafikia kila mtu amjuaye kwa kutumia akaunti zake zilizo kwenye lugha saba.Akaunti ya papa iliyo kwenye lugha ya kiingereza tayari ina wafuasi zaidi ya laki sita.
Akaunti zake zote ambazo ni @pontifex zinafuatana moja baada ya nyingine.

Askofu apinga ndoa ya wapenzi wa jinsi moja.

Kiongozi wa Kanisa wa Katoliki nchini Uingereza amesema mpango wa serikali ya Uingereza kuhusu ndoa ya wapenzi wa jinsi moja ni jambo la aibu.
 Vincent Nichols
                                                                  Vincent Nichols
Askofu mkuu wa Jimbo wa Westminster Vincent Nichols ameiambia BBC kuwa serikali ya Uingereza haina wajibu wa kuhimiza ndoa ya wapenzi wa jinsia moja nchini Uingereza.

Katika hotuba yake wakati wa ibadi ya Krismasi, askofu Nichols alisema ndoa kati ya mwanamume na mwanamke inaashiria mapenzi ya Mungu.
 
Serikali ya Uinbereza inapanga kuruhusu ndoa ya wapenzi wa jinsi moja lakini imesema kuwa haitazishurutisha viongozi wa kidini kuongoza na kuidhinisha ndoa hizo.

Kwingineko, Askofu wa jimbo ya Centerbury anayeondoka, Rowan Williams amesema heshima na hadhi ya Kanisa la Kianglikana na nchini Uingereza, limeadhirika pakubwa kutokana na uamuzi wa hivi majuzi ambao ulipinga uteuzi wa kina mama kama askofu wa kanisa hilo.Dr Williams anatarajiwa kustaafu kutoka wadhifa huo mwisho wa mwezi huu.

Watu watano wauawa Nigeria.

Majeshi ya usalama kaskazini mwa Nigeria wamesema watu wenye silaha wamekishambulia kijiji kimoja chenye wakaazi wengi Wakristo na kuua watu watano na wengine wanne kujeruhiwa.
Msemaji wa jeshi ameiambia BBC kuwa washambuliaji waliwafyatulia risasi waumini wakiwa Kanisani katika ibada ya mkesha wa Krismasi.
 Watu wakisimama mbele ya Kanisa
Amesema mtuhumiwa mmoja wa mashambulio hayo amekamatwa, na ulinzi katika eneo hilo umeimarishwa ili kuwahakikishia usalama wakaazi wa eneo hilo.
Msemaji huyo amesema nyumba kadha karibu na kanisa lililoshambuliwa zilitiwa moto.
Hakuna kikundi kilichodai kuhusika na mashambulio hayo katika jimbo la Yobe, lakini katika siku za nyuma kikundi cha Kiislam cha Boko Haram kiliwashambulia Wakristo katika jimbo hilo.
                                           Chanzo cha habari BBC SWAHILI

WATOTO WAJIACHIA KWA MICHEZO MBALIMBALI SIKU YA JANA X-MAS DAR LIVE.

Pichani juu ni taswira mbalimbali za watoto wakijiachia ndani ya Dar Live siku ya jana.

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate