EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Sunday, November 30, 2014

COMMENT ZA WADAU BAADA YA DIAMOND KUIBUKA NA ZARI USIKU WA JANA SOUZ






WEMA SEPETU AZUA GUMZO BAADA YA KUMUITA DIAMOND 'KAKA'



Huku macho na masikio ya wananchi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania yakiwa kwenye bunge la katiba linalojadili lile sakata la tegeta ESCROW, mwanadada Wema sepetu ameamua naye kuzua gumzo kwenye mtandao baada ya kutoa salamu ya pongezi kwa kijana Naseeb al maarufu kama Chibu dangote ama Diamond platnumz kwa ushindi wake wa tuzo 3 kwenye tuzo za Channel O MUSIC AWARDS zilizofanyika huko Afrika ya kusini akitumia neno KAKA katika sentensi yake kitu ambacho kimezua minong’ono ya hapa na pale kwenye mtandao ule maarufu wa kijamii wa picha nchini.
Katika post yake hiyo Wema aliandika

 
 “…Hongera tele ziende kwa kaka platnumz... I must say he did Tanzania proud..”   na kufanya watu waanze kufunguka ya kwaio ya moyoni kuhusu kauli hiyo na baadhi yao walisema haya.


MELA : “Leo kawa kaka!!!!!! Aiseeee mapenz ya mastaa mafupi kama mkia wa kondoo”

MAAZIMIO MAPYA SAKATA LA ESCROW: MAMLAKA HUSIKA YASHAURIWA KUTENGUA UTEUZI WA PROF TIBAIJUKA, PROF MUHONGO, JAJI WEREMA NA MASWI



Waziri wa Madini na Nishati, Profesa Sospeter Muhongo.
WABUNGE kwa pamoja wamekubaliana kuondoa maazimio 12 yaliyoletwa bungeni na Kamati ya PAC na kuleta maazimio mapya 8 ambayo yamekubaliwa.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali,Jaji Frederick Werema.
Mojawapo ya maazimio hayo ni Mamlaka ya uteuzi kutakiwa iwawajibishe na kushauriwa kutengua uteuzi wa Waziri wa Nishati na Madini Profesa Muhongo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Frederick Werema, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof. Anna Tibaijuka na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Eliakim Maswi kwa kuhusika katika sakata la akauntii ya Tegeta Escrow.
Bunge limeanza saa 1 kamili jioni

Wakazi - Wanawake Wa Dar (WWD) (Official Video HD)

Wanawake wa Dar
Nyota wa muziki wa rap nchini, Wakazi ameachia video ya wimbo wake mpya uitwao ‘Wanawake wa Dar’ ikiwa ni siku 5 sasa tangu afanye uzinduzi wake pale O.M.G Bar & Restaurant. Itazame hapa…

Saturday, November 29, 2014

Rais Kikwete arejea nchini na kuzungumza na Wanahabari uwanja wa ndege jioni hii jijini Dar

Rais Kikwete akizungumza na Wanahabari kwenye ukumbi maalum wa mikutano,Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jiini Dar,mara tu baada ya kuwasili jiioni hii akitokea nchini Marekani kwa matibabu.

HELIKOPTA YAANGUKA UKONGA, DAR, WATU WANNE WADAIWA KUPOTEZA MAISHA


 Ajali ya Helicopter ya Maliasili na Utalii imegharimu maisha ya marubani 3 wa Jeshi la Polisi Tanzania. Sp Kidai Kaluse, Insp.Simba Must Simba, Pc. Josso Selestine, Na rubani mmoja Capt. Khalfan,Ajali  hiyo imetokea huko Kipunguni B Moshi Bar,Ukonga-Ilala jijini Dar es Salaam. Chanzo cha ajali hiyo bado hakijajulikaa mpaka sasa.
 Sehemu ya mabaki ya Helikopta baada ya kuanguka
 Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova
akifafanua jambo mbele ya Vyombo vya habari katika eneo la ajali,kufuatia kutokea kwa ajali hiyo iliyopelekea vifo vya watu wanne
 Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaa,Mh.Sadick Meck Sadick akizungumza mbele ya Vyombo vya habari katika eneo la ajali,kufuatia kutokea kwa ajali hiyo iliyopelekea vifo vya watu wanne
 Baadhi ya Wataalamu wakifanya uchunguzi wa chanzo cha ajali hiyo ya Helikopta.

BUNGE LAAHIRISHWA BAADA YA WABUNGE KUPINGA BAADHI YA MAAZIMIO YA KUWALINDA WATUHUMIWA WA SAKATA LA ESCROW

 
MAAZIMIO
Pendekezo la kwanza la kumkamata na kumfilisi bwana Seth lina marekebisho ya serikali, naibu waziri wa Sheria anasema haiwezekani
Pendekezo la pili kuhusu Rugemalira, serikali imeweka marekebisho kuhusu uhalali wa pesa za Rugemalira alizogawa
Azimio la TATU limerekebishwa kuwa waliopokea pesa wachunguzwe na kuchukuliwa hatua mahususi kwa mujibu wa sheria
Pendekezo la NNE. Kamati inazitaka mamlaka kuzitangaza benki za Mkombozi na Stanbic kama asasi za utakatishaji fedha
Azimio la 4 limepita kwamba Kamati inazitaka mamlaka husika ikiwemo benki kuu kuchukua hatua dhidi ya benki zote zilizohusika
Azimio la TANO: Serikali ipitie upya mikataba yote ya umeme na kutoa taarifa kabla ya kumalizika kwa Bunge la bajeti lijalo
Azimio la SITA: kuhusu Bodi ya TANESCO kuvunjwa kwa kusababisha pesa kuchotwa na hasara, serikali imekataa, mjadala unaendelea
Kingwangala: Kanuni zetu zinataka mtu yoyote anayetaka mabadiliko ya maazimio lazima awe amekawasilisha kabla
Kafulila: Kwa mujibu wa mkataba wa IPTL, maamuzi ya mwisho yanafanywa na mahakama ya London, bodi walikuwa na maamuzi hayo na haikuwajibika na maamuzi ya mahakama za ndani ya nchi

PICHA ZA UTUPU, VIDEO QUEENS TZ WATIA FORA


STORI: Musa Mateja
WHY? Wauza nyago wanaotumika katika video mbalimbali za wasanii wa Bongo Fleva (video queens) wametia fora kwa kurekodiwa mikanda ya utupu na kusambaa kwenye mitandao ya kijamii na simu za kupangusa, Risasi Jumamosi lina ripoti kamili.

PENNY: SIWEZI KUVUNJA USHOSTI WA WEMA, AUNT!

MTANGAZAJI  Bongo, Penniel Mungilwa ‘Penny’ amefunguka kuwa kamwe hawezi kuwagombanisha marafiki wa damu, Wema Sepetu ‘Madam’ na Aunt Ezekiel, baada ya yeye kuingilia urafiki huo. 
Mtangazaji Bongo, Penniel Mungilwa ‘Penny’ akiwa na Wema Sepetu.
Akizungumza na mwanahabari wetu, Penny alisema kuwa anaamini kabisa kuna baadhi ya watu  hawapendi kuwa na urafiki zaidi ya watu watatu kitu ambacho siyo sahihi, yeye anaamini baada ya  kupatana na Wema hivi karibuni, watakuwa marafiki watatu.

Wema Sepetu akiwa na Aunty Ezekiel.
“Nafurahi sana tunapokuwa na kampani kubwa nashangaa wengine mpaka wanafikia kupigana kisa akiona rafiki yake ana urafiki na mtu mwingine, mimi napenda tuwe wengi ili tuweze kushauriana mambo mbalimbali,” alisema Penny.

AUNTY LULU ASIMULIA ALIVYOBAKWA

My confession! (kukiri kwangu)! Mwanadada mwenye taito ya utangazaji na uigizaji wa sinema za Kibongo, Lulu Mathias Semagongo ‘Aunty Lulu’ amefungua kinywa na kutoa la moyoni akisimulia tukio baya lililowahi kumkuta la jinsi alivyobakwa, Risasi Jumamosi lina ‘exclusive story’.
Mwanadada mwenye taito ya utangazaji na uigizaji wa sinema za Kibongo, Lulu Mathias Semagongo ‘Aunty Lulu’ akipozi.
TUJIUNGE DUKANI KWAKE
Akizungumza na gazeti hili katika mahojiano maalum yaliyofanyika hivi karibuni dukani kwake Kinondoni jijini Dar, Aunty Lulu asiyeishiwa na vimbwanga alisema kwamba, kamwe hawezi kusahau tukio hilo maishani mwake.

HAMISA ABWATUKA KISA MABUZI

MWANAMITINDO kiwango Bongo, Hamisa Hassan Mobeto amepangua tuhuma ambayo amekuwa akitupiwa na  watu wanaomuona aking’aa kisha kudai anatumia mgongo wa wanaume tofautitofauti (mabuzi).
Mwanamitindo kiwango Bongo, Hamisa Hassan Mobeto
Akipiga stori na paparazi wetu hivi karibuni, Hamisa alisema amekuwa akisikitishwa na tabia hiyo ya watu kumnanga kwenye mitandao ya kijamii kuwa anatupia picha nyingi ili kujiuza kwa mabuzi kitu ambacho si cha kweli.
“Kiukweli asiyekujua hakuthamini, nasema hivi kutokana na watu wengi wamekuwa wakinisema vibaya hasa katika mitandao ya kijamii, wanikome kwani kila mtu ana maisha yake na mimi sitegemei mabuzi kuishi mjini, nina mpenzi wangu mmoja tu,” alisema Mobeto.

Friday, November 28, 2014

DIAMOND, ZARI WAUMBUKA!

Licha ya madai wanayoyatoa mastaa wawili hot kwa sasa, Nasibu Abdul ‘Diamond’ na Zarinah Hassan a.k.a Zari au The Boss Lady kuwa si wapenzi bali kuna project wanaifanya, wawili hao wameumbuka.
Kuumbuka huko kumekuja kufuatia kuvuja kwa picha inayowaonesha mastaa hao wakidendeka huku wakiwa kwenye hisia kali.



Nasibu Abdul ‘Diamond’ na Zarinah Hassan wakibusiana kimahaba.
Katika picha hizo ambazo kwa sasa zinapatikana mtandaoni, Zari anaonekana akiwa amevaa kofia ya Diamond wakionekana wenye furaha na baadaye wakahamia kwenye kupeana mahaba.
Aidha, picha ambayo inawaumbua ni ile ya kudendeka ambapo baadhi ya wadau walioiona walisema, inavyoonekana projecti wanayoifanya imevuka mipaka.

 
Nasibu Abdul ‘Diamond’ na Zarinah Hassan wakiwa kwenye pozi.
“Wasitutanie bwana, hivi kweli kwa picha hii watasema ni projekti? Hawa ni wapenzi ila hawataki tu watu wajue,” alisema mdau mmoja aliyejitambulisha kwa jina la John baada ya kuona moja ya picha hizo.

ESCROW: UTETEZI MREFU WA WATUHUMIWA UKWELI WABAKI KAMATI YA ZITTO

 
Stori: waandishi wetu
ESCROW kila kona! Wabongo wameibuka na msemo mpya kuhusu sakata la uchotwaji wa fedha za umma kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow iliyofunguliwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), wakilitolea tafsiri iliyobeba kichwa cha habari hii kwamba Escrow ni Eneza Siasa Chota Riziki Ondoa Woga.
 
Waziri mkuu Mizengi Pinda.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili, baadhi ya wananchi wamesema mtu akitaka riziki kirahisi ajiingize katika siasa na kuanza kuihubiri pia aondoe woga kama washiriki katika sakata hilo walivyofanya kwa kujipa ujasiri wa kujichotea shilingi bilioni 306 kutoka kwenye akaunti hiyo.
ISIKIE HII
“Sasa nimeamini, ukitaka kuwa tajiri mkubwa katika nchi hii, we eneza siasa, utaweza kuchota riziki (pesa) kubwa sana hususan kama utaondoa woga,” alisema Fred Jimmy ‘Fredwaa’, mkazi wa Makumbusho jijini Dar es Salaam.
Pamoja na yote hayo, wananchi hao wamesema chochote kitakachofanyika, ni lazima fedha hizo zirejeshwe kutoka kwa wahusika hao, kwani ni fedha za walipa kodi wa Tanzania ambao maisha yao ya kila siku ni ya kubangaiza.
 
Askofu Mkuu Msaidizi Jimbo la Kagera, Methodius Kilaini.
“Ripoti ya PAC tumeiona na utetezi wa Waziri Sospeter Muhongo pia tumeusikia, lakini hatuukubali. Anadai kuwa Tanesco haina fedha kwa kuwa haijaanza kutengeneza faida, kwamba kwa muda wote imekuwa ikidaiwa tu.

LUNGI: MTU AMSHOBOKEE BWANA WANGU AONE

Staa wa filamu za Kibongo, Lungi Mwaulanga amesema mwanaume aliyezaa naye (jina ni siri yake) anampenda sana na mwanamke asiyejipenda amshobokee aone kitakachompata.
 
Staa wa filamu za Kibongo, Lungi Mwaulanga.
Akipiga stori na Ijumaa Lungi amesema anajua kuwa wapo wanawake ambao wakiamua kutembea na waume za watu hawashindwi lakini akasema, kwa bwana wake aliyezaa naye akigundua kuna anayemnyemelea, atakufa naye.

JOHARI ADAIWA KUNASWA KWA MGANGA!


STAA wa filamu za Kibongo, Blandina Chagula (pichani) maarufu kama Johari, hivi karibuni alidaiwa kuonekana akiingia nyumbani kwa mganga wa kienyeji (jina linahifadhiwa) katika Kijiji cha Kibeta, mjini Bukoba mkoani Kagera.
 
Staa wa filamu za Kibongo, Blandina Chagula.
Chanzo chetu cha habari kimedai kuwa Johari akiwa katika bodaboda, aliingia kwa mganga huyo wa kike anayefahamika sana eneo hilo.
“Sijui nilikuwa namfananisha? Nimemuona msanii wenu hapa Kibeta akiingia kwa mganga ila nimeshindwa kumpiga picha maana kasimu kangu ni ka’ tochi, labda kaja kuweka mambo yake sawa,” kilidai chanzo hicho.

PICHA ZA RECHO ZAMZUIA SAGUDA MAMBO YA MAPENZI

 Stori: Gladness Mallya ALIYEKUWA mchumba wa msanii wa filamu Bongo, marehemu Sheila Haule ‘Recho’,  George Saguda amefunguka kuwa picha za mwanadada huyo zimekuwa zikimfanya asiwe na hisia za kuwa na mwanamke mwingine.
 
George Saguda akiwa na aliyekuwa mchumba wake marehemu Sheila Haule ‘Recho’.
Akipiga stori na gazeti hili hivi karibuni, Saguda alisema tangu mchumba wake huyo afariki dunia hajawahi kuwa na mwanamke na hana mpango huo kwa sasa labda hapo baadaye.
“Tangu alipofariki Recho niko peke yangu na sina mpango wa kuwa na mwanamke mwingine, kwani kila ninapozitazama picha zake naumia sana,” alisema Saguda.

CHENGE, CHENGE, CHENGE TENA?


 
Makala: Ojuku Abraham
KAMA Mwalimu Julius Kambarage Nyerere angekuwa bado anatawala nchi hii, ni watu wachache sana wangeweza kulijua jina la Andrew Chenge, yule mwanasheria mkuu wa zamani wa serikali, aliyekaa katika ofisi hiyo kubwa na yenye heshima, kuanzia mwaka 1993 hadi 2005.
Lakini katika nchi ambayo inaendeshwa kwa hila na dili, jina hili linajipatia umaarufu na kuenziwa, bila kujali ni kwa kiasi gani, Watanzania zaidi ya milioni 45 wanaishi kwa dhiki na mateso kutokana na yeye kuitumia vibaya ofisi ya umma kujinufaisha.
Ni katika kipindi chake akiwa mwanasheria mkuu wa serikali, ndipo nchi yetu imeshuhudia kashfa za mikataba mingi mibovu, isiyo na tija kwa nchi, ikisainiwa. Siyo tu mikataba bali hata sheria nyingi zisizofaa zikilazimishwa kutumika.

Thursday, November 27, 2014

MWANAMUZIKI BILEKU MPASI KUTOKA CONGO (DRC) NA MASHUJAA BAND KUFANYA ONESHO LA PAMOJA DISEMBA 12-2014 UKUMBI WA ASCAPE 1 MIKOCHENI JIJINI DAR ES SALAAM KUZITAMBULISHA NYIMBO MBILI MPYA ZA BAND HIYO‏


Rais wa Band ya Mashujaa, Chalz  Baba  
 Rais wa Band ya Mashujaa, Chalz  Baba (kushoto), akitoa burudani mbele ya wanahabari Dar es Salaam leo, kuhusu onesho hilo litakalofanyika katika ukumbi huo.. Kutoka kulia ni Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bia ya Mabibo, Joseph Emanuel na Ofisa Uhusiano wa Band ya Mashujaa, King Dodo la Buche. 
 Ofisa Uhusiano wa Band ya Mashujaa, King Dodo la Buche (katikati) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu onesho hilo. Kulia ni Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bia ya Mabibo, Joseph Emanuel na Rais wa Band ya Mashujaa, Chalz Baba

SOMA TAARIFA YA WAZIRI WA NISHANI NA MADINI PROF.MUHONGO KUHUSIANA NA SAKATA LA IPTL NA TEGETA ESCROW ALIYOIWASILISHA BUNGENI LEO




Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo.
Ameanza kwa kuomba radhi kama jana kulikuwa na usumbufu wa umeme na anawaagiza mameneja wote wa TANESCO wasikate umeme.
Anatoa pongezi juu ya mjadala wa Escrow, mengi yamesemwa na ni wakati wa kuanza mjadala kujua ukweli, Shukrani kwa CAG, TAKUKURU kwa uchunguzi. Pia nawashukuru PAC, jana tulitulia kuwasikiliza PAC na leo tutulie tusikilize utetezi wangu.


Spika wa Bunge, Anne Makinda.
Miaka ya 1990 tulikuwa tuna upungufu wa umeme kutokana na maji, 1994 serikali ilitoa kazi ya uwekezaji kwa IPTL ilikuwa inamilikiwa na VIP ya Tanzania iliyokuwa na 30% na Mechmar ya Malaysia 70%.
Kulingana na mkataba, majukumu ya IPTL yalikuwa kujenga, kumiliki na kuendesha hivyo utaifishaji utaiingiza serikali katika matatizo makubwa ikiwemo kushtakiwa kimataifa pia itafukuza wawekezaji binafsi. TANESCO na IPTL walisainiana mkataba wa miaka 20, hata hivyo uzalishaji haukuanza mara moja kutokana na mgogoro ulioibuka baina ya TANESCO na IPTL
IPTL ilianza kuzalisha umeme 2002 hivyo mkataba ukaanza kuhesabiwa hapo, kutokana na mgogoro ikafunguliwa Escrow Account na Escrow ilizungumziwa toka mkataba wa 1995.
2004 TANESCO ilifungua shauri kupinga tozo la capacity charge
Taarifa hii sio ya kweli kwani TANESCO haijawahi kufungua kesi yoyote dhidi ya Standard Charted kama ilivyosemwa na PAC. Kesi hiyo ilifunguliwa na Standard Charted na ilikuwa haihusu capacity charge. Hamna kokote mkataba kati ya Standard Charted na TANESCO.

ANDY MURRAY AMALIZIA KWA FURAHA YA USHNDI

Andy Murray poses with the Wimbledon trophy along with his fiancee Kim Sears
Andy Murray akiwa na mkewe mtarajiwa Kim Sears.

Teenage Murray, right, kisses Kim Sears after beating Australia's Lleyton Hewitt in the final match at the SAP Open in 2006
Kinda Murray, kulia, akimbusu Kim Sears baada ya michuano ya SAP Open mwaka 2006
MCHEZAJI bora nambari moja wa tenisi Uingereza na bingwa wa Wimbledon, Andy Murray amemvisha pete ya ucuhumba mpenzi wake, Kim Sears, waliyedumu naye kwa miaka zaidi ya tisa.
Wawakilishi wa Murray wamethibitisha uchumba huo wa kiajan huyo mwenye umri wa miaka 27, Murray na Sears, mwenye umri wa miaka 26, lakini hawakutoa taarifa zaidi.
Kimwana huyo, Miss Sears, ambaye Sahada, alikutana na Murray katika michuano ya US Open mwaka 2005.

KUTOKA BUNGENI DODOMA LEO: MASWALI KWA WAZIRI MKUU



Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.
KIKAO cha Bunge leo kimeanza kwa maswali kwa Waziri Mkuu ambapo aliyekuwa wa kwanza kuuliza alikuwa ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Mhe. Freeman Mbowe.

Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Mhe. Freeman Mbowe.
Alianza Mbowe: 
“…Chini ya uongozi wako kama Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ukiwa kiongozi wa shughuli za Kiserikali Bungeni, tumeiona Serikali ikikumbana na matatizo na vikwazo vingi ikiwemo ‘Operesheni Tokomeza’ ambayo ilipelekea wananchi wengi kupoteza maisha na wengine kupata vilema…“
Tumeona mauaji ya raia yakiendelea Kiteto, kashfa kubwa ambayo iko current sasa hivi ikiwa ni pamoja na kauli zako ulizowahi kuzisema kwamba fedha zilizopotea za akaunti ya Escrow hazikuwa fedha za umma bali zilikuwa fedha za watu binafsi…“– Mbowe.

ARSENAL YATINGA 16 BORA LIGI YA MABINGWA BAADA YA KUICHAPA 2-0 DORTMUND

WASHIKA Bunduki, Arsenal wamefuzu kuingia hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kufuatia ushindi wa 2-0 dhidi ya Borussia Dortmund Uwanja wa Emirates katika mchezo wa Kundi.
Yaya Sanogo aliifngia Arsenal bao lake la kwanza kwenye mechi ya mashindano dakika ya pili, ingawa kinda huyo Mfaransa alionekana kama alikuwa ameotea.
Alexis Sanchez akaifungia timu ya Arsene Wenger bao la pili dakika ya 57 na kuihakikishia kuingia hatua hiyo ya mtoano. 
Kikosi cha Arsenal kilikuwa; Martinez, Chambers, Mertesacker, Monreal, Gibbs, Arteta/Flamini dk66, Oxlade-Chamberlain/Campbell dk89, Ramsey, Cazorla, Sanchez, Sanogo/Podolski dk78.
Borussia Dortmund; Weidenfeller, Piszczek, Subotic, Ginter, Schmelzer, Gundogan, Bender, Grosskreutz, Immobile/Kagawa dk60, Mkhitaryan na Aubameyang/Ramos dk60. 
Alexis Sanchez runs towards the Arsenal fans in celebration of his second half strike against Borussia Dortmund
Alexis Sanchez akikimbia kushangilia baada ya kuifungia Arsenal bao la pili dhidi ya Borussia Dortmund
Sanogo shoots past Dortmund keeper Weidenfeller (right) to score the opening goal of the game
Sanogo akifumua shuti kumtungua kipa wa Dortmund, Weidenfeller (kulia) kuifungia Arsenal bao la kwanza

NCHI YATIKISWA NA ESCROW

 

Dodoma. 
Hatimaye mtikisiko wa tano umetimia na nchi kutikiswa; ripoti ya Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC) imependekeza kuwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Mwanasheria Mkuu, Waziri wa Nishati na Madini, naibu wake na katibu mkuu wa wizara hiyo wawajibishwe kutokana na kuhusika kwao kwenye sakata la uchotwaji wa Sh306 bilioni kutoka kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow.

Akaunti hiyo ilifunguliwa kwa ajili ya kutunza fedha za gharama za uwekezaji (capacity charge) baada ya kuibuka mzozo wa kimkataba baina ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) na kampuni binafsi ya IPTL ambayo iliingia mkataba wa kufua umeme na kuliuzia nishati hiyo shirika hilo la umma.

Ripoti hiyo ilisomwa jana bungeni kwa kupokezana kati ya Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe na Makamu mwenyekiti, Deo Filikunjombe baada ya majadiliano marefu kwenye vikao vya ndani vya CCM na Kamati ya Uongozi wa Bunge na jitihada kubwa za kutaka isisomwe na kujadiliwa.

BALOZI LIBERATA MULAMULA AMKARIBISHA BALOZI MPYA WA ZIMBABWE NCHINI MAREKANI UBALOZINI TANZANIA HOUSE

Mhe. Liberata Mulamula, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani na Mexico(Kulia) akimkaribisha Mhe. Ammon Mutembwa,(Kushoto). Balozi  Mpya wa Jamhuri ya Zimbabwe nchini Marekani Ubalozini Tanzania House Washington DC,Marekani.
Mhe.Balozi  Mulamula na Mhe. Balozi Mutembwa katika picha ya kumbukumbu baada ya kusaini kitabu cha wageni.

PUNGUZO LA ASILIMIA 40 KWA MTANZANIA ATAKAYETIBIWA HOSPITALI YA IRAN YA DUBAI


Balozo Mdogo wa Tanzania Dubai Mhe Omar Mjenga na Dkt. Asghar Farshad wa hospitali ya Iran huko Dubai wakitia saini makubaliano ambapo hospitali hiyo imetoa ofa ya punguzo la asilimia 40 ya malipo ya matibabu kwa Mtanzania yeyote atayekwenda kutibiwa hapo Iranian Hospital Dubai
Balozo Mdogo wa Tanzania Dubai Mhe Omar Mjenga na Dkt. Asghar Farshad wa hospitali ya Iran huko Dubai wakibadilishana hati za makubaliano ambapo hospitali hiyo imetoa ofa ya punguzo la asilimia 40 ya malipo ya matibabu kwa Mtanzania yeyote atayekwenda kutibiwa hapo Iranian Hospital Dubai

DIDA: EZDEN AKIOA, NITAANZA KUMCHANGIA!

MTANGAZAJI mwenye maneno lukuki kutoka Radio Times FM, Khadija Shaibu ‘Dida’ amesema kuwa endapo mtalaka wake, Ezden Jumanne akitaka kuoa yeye atakuwa wa kwanza kutoa mchango wa harusi hiyo.
Mtangazaji kutoka Radio Times FM, Khadija Shaibu ‘Dida’.
Dida ambaye kwa sasa yupo singo, alisema japokuwa wameacha na Ezden, lakini hana bifu naye kwa sababu anaamini kuwa yuko katika harakati za kutafuta mke bora hivyo haoni shida kumchangia.

GARDNER KWA HALI HII SASA IDE BASI TENA

CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS
JAHAZI linazidi kwenda mrama! Wakati shauri lao la kugawana mali likidaiwa kufikishwa mahakamani, picha mpya imenaswa ikionesha dhahiri kwamba Mtangazaji Gardner Gabriel Fikirini Habash ‘Kapteni’ ameamua kusonga mbele na maisha yake na kusahau kabisa kama alikuwa na mke aitwaye Judith Daines Wambura Mbibo ‘Jide’, Amani linakupa mchapo kamili.
Mtangazaji Gardner Gabriel Fikirini Habash ‘Kapteni’ akila ujana na binti (jina halikupatikana mara moja) mrembo bwawani (swimming pol).
PICHA IPOJE?
Picha hiyo ambayo inamuashia ‘endiketa’ Jide kuashiria kwamba, Gardner amejiweka pembeni na kuwa bize na ‘starehe’ zake, inamuonesha mtangazaji huyo akiwa ‘ziro distensi’ na kabinti kabichiii (jina halikupatikana mara moja) katika bwawa la kuogelea (swimming pol) huku wakiwa wamening’iniza miguu kwenye maji.

BABA WA MSANII ASHUSHA KICHAPO

Stori: Waandishi Wetu
Baba mmoja ambaye jina halikupatikana mara ameshusha kichapo kwa wasanii ambao ni maprodyuza waliokuwa wakimchezesha mwanaye filamu bila ridhaa yake.
Baba huyo akizuiwa ili asiendelee kushusha kichapo hicho.
Kwa mujibu wa mashuhuda wetu, tukio hilo lilijiri juzikati, maeneo  ya Mwananyamala-Komakoma jijini Dar ambapo awali binti huyo ambaye ni msanii chipukizi wa kuigiza aitwaye Jeniffer alidaiwa kupigwa mkwara na baba yake kuwa asijishughulishe na masuala ya muvi na badala yake ajikite kwenye masomo yake kufuatia tasnia hiyo kuhusishwa na skendo za ngono.
Ilidaiwa kwamba, Jeniffer alikaidi amri ya mzee wake huyo na kwenda kinyemela kurekodi vipande kadhaa vya muvi ya kikundi chao ambapo taarifa zilimfikia baba yake huyo na kuamua kutimba lokesheni.

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate