EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, April 30, 2014

BASI LA AM COACH LAPATA AJALI IPULI NA KUSABABISHA KIFO CHA MWANAFUNZI MMOJA


Umati mkubwa wa watu ambao ulifiika kushuhudia ajali hiyo.
Askari Polisi Kitengo cha usalama barabarani wakiuchukua mwili wa mtoto aliyegongwa na basi la kampuni ya A.M maeneo ya Ipuli Mnadani ambalo lilikuwa likitokea jijini Mwanza,katika ajali hiyo watu kadhaa wamejeruhiwa.
CHANZO: JAMIIFORUMS

AUNT EZEKIEL AKIJIACHIA BEACH NDANI YA DUBAI


HIVI NDIVYO ALIVYOAGWA BABA WA MWIGIZAJI FILAMU MTITU

Mtitu akiingia nyumbani baada ya kutoka hospitali kuchukua mwili wa baba yake.
Wasanii mbalimbali wa filamu wakiwa kwenye msiba.

NEW SONG : STEVE RNB - SHE DANCE

POLISI MKOANI MANYARA YAKAMATA MISOKOTO 6,000

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Manyara, (SACP) Deusdedit Nsimeki, (kulia) akiwa na polisi wengine wa mjini Babati, wakati akiwaonyesha waandishi wa habari baadhi ya misokoto 6,000 ya Bangi waliyoikamata kwenye mabasi mawili hivi karibuni ambayo ilikuwa imewekwa kwenye mikate iliyokuwa imesafirishwa na watu wawili,ambao wamewekwa ndani.

TAARIFA YA MABADILIKO YA ANUANI YA OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA

Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma inapenda kuwafahamisha wadau wake kuwa anuani yake imebadilika hivyo kuanzia sasa mawasiliano yafanyike kwa kutumia anuani ifuatayo;
OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA
UTUMISHI HOUSE
8 BARABARA YA KIVUKONI
11404 DAR ES SALAAM
au
PRESIDENT’S OFFICE, PUBLIC SERVICE MANAGEMENT
UTUMISHI HOUSE
8 KIVUKONI ROAD
11404 DAR ES SALAAM
Anuani hii inachukua nafasi ya Sanduku la Posta 2483, Dar es salaam. Hivyo, mawasiliano yote yazingatie anuani mpya.
Limetolewa na
Katibu Mkuu
Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma
Barua pepe; permsec@utumishi.go.tz

TBC NA CRI YAZINDUA TAMTHILIYA YA KICHINA ILIYOTAFSIRIWA KWA LUGHA YA KISWAHILI


 Mkurugenzi Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Clement Mshana akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kwajili ya kuzindua rasmi Tamthiliya ya Mapenzi na Furaha ya Kijana (Jin Tai Lang) uliofanyika  katika Viwanja vya TBC jijini Dar es Salaam.
 Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Elisante Ole Gabriel akitoa hotuba yake mbele ya viongozi mbalimbali wakati wa Uzinduzi wa Tamthiliya ya Mapenzi na Furaha ya Kijana (Jin Tai Lang) uliofanyika siku ya jana katika Viwanja vya TBC jijini Dar es Salaam. 
 Mtendaji Mkuu Kampuni ya Star Media (T) Ltd Bw. Jack Czhou akieleza jambo wakati wa Uzinduzi wa Tamthiliya ya Mapenzi na Furaha ya Kijana (Jin Tai Lang) uliofanyika katika Viwanja vya TBC jijini Dar es Salaam.

UTUMISHI YAIBUKA KINARA WA MPIRA WA PETE MASHINDANO YA MEI MOSI 2014


Fatuma Machenga (GS) mfungaji bora katika Mpira wa Pete wa mashindano ya Mei Mosi 2014 akiwa na kikombe baada ya kutangazwa rasmi katika hafla fupi iliyofanyika katika Uwanja wa Jamhuru mjini Morogoro.
Baadhi ya wachezaji wa Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma (jezi za kijani) wakishangilia kwa kutawazwa mabingwa wapya wa Mpira wa Pete Mei Mosi 2014 kwa kuifunga timu ya Uchukuzi. Mashindano hayo yalimalizika jana jioni katika uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro. 
Baadhi ya wachezaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi Umma, pamoja na mashabiki wao wakipongezana baada ya kuibuka mabingwa wapya wa Mpira wa Pete kwa kuifunga Uchukuzi katika mashindano ya Mei Mosi 2014 yaliyomalizika katika Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.

Tuesday, April 29, 2014

SHEREHE ZA MIAKA 50 YA MUUNGANO ZAFANYIKA PARIS UFARANSA

Watanzania waishio nchini Ufaransa walikutana Jumamosi mchana tarehe 26 Aprili nyumbani kwa Balozi wa Tanzania mjini Paris ili kusherehekea miaka 50 ya muungano kati ya Zanzibar na Tanganyika.
Balozi wa Tanzania Nchini Ufaranza,Mh. Begum Karim Taj akipokea keki maalum kwa ajili ya sherehe hizo za Muungano wa Tanzania katika hafla iliyofanyika nyumbani kwa Balozi,Mjini Paris Ufaransa.
Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa akiwa na watoto mjini Paris.

MAMA SALMA KIKWETE AZINDUA WIKI YA CHANJO DUNIANI MKOANI KILIMANJARO

Baadhi ya taasisi a NGO'S mbalimbali zilihudhuria uzinduzi huo.

Wanafunzi kutoka shule mbalimbali za msingi wakisikiliza kwa makini mambo mbalimbali yaliyokuwa yakizungumzwa.
Makundi mbalimbali ya watu yalishiriki uzinduzi wa wiki ya chanjo duniani iliyozinduliwa mjini Moshi.
Wanafunzi kutoka shule mbalimbali za msingi wakisikiliza kwa makini mambo mbalimbali yaliyokuwa yakizungumzwa.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Leonidas Gama akizungumza wakati wa uzinduzi wa wiki ya chanjo duniani.
Mwakilishi  mkazi wa shirika la Afya Duniani (WHO) Dk Rufaro Chatora akizungumza wakati wa sherehe za uzinduzi wa wiki ya chanjo duniani uliofanyika katika viwanja vya mandela mjini Moshi.
Baadhi ya washiriki katika uzinduzi huo kutoka Asasi mbalimbali mkoani Kilimanjaro.
Mwakilishi wa UNICEF,Sudha Sharma akizungumza wakati wa sherehe za uzinduzi wa wiki ya chanjo duniani uliofanyika katika viwanja vya mandela mjini Moshi.

Monday, April 28, 2014

NAY WA MITEGO ASAKWA KWA KUTISHIA KUUA

KIMENUKA! RB namba KT/RB/1178/2014-KUTISHIA KUUA KWA NJIA YA MTANDAO inamsaka staa wa Ngoma ya Nakula Ujana, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ kwa tuhuma ya kutishia kumuua mdogo wake aliyetajwa kwa jina la Amani Shija, Ijumaa Wikienda limeinyaka.
Staa wa Ngoma ya Nakula Ujana, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’.
Kwa mujibu wa chanzo makini, Nay alikuwa akiishi na Shija kwa zaidi ya miaka mitano nyumbani kwake, Manzese jijini Dar.
Habari zilitonya kuwa ugomvi wa Nay na Shija ulianza zaidi ya miezi mitatu iliyopita ambapo hivi karibuni walikuwa maeneo ya Kijitonyama, Dar, wakipata chakula cha usiku na marafiki zao wengine ndipo ghafla dogo akajichanganya na kujikuta akiropoka neno lililomuudhi Nay, akapaniki.
Ilisemekana kwamba baada ya kupaniki, Nay alianza kumfokea Shija na kutishia kumuua, ambaye alishindwa kujizuia na kujikuta akimwaga chozi.
Akaendelea kueleza kuwa hata baada ya siku hiyo, Nay aliendelea kumtumia SMS za kutishia kumuua ambazo bado anazo kama ushahidi Baada ya kudaka mchongo huo, Ijumaa Wikienda lilimtafuta Shija ambaye pia ni msanii wa Bongo Fleva na kumuuliza juu ya malalamiko hayo, akakiri kugombana na kaka yake huyo.

LIVERPOOL HOI KWA CHELSEA, YALALA 2-0

Demba Ba akiifungia Chelsea bao la kwanza dakika ya 45 ya mchezo.
Chelsea wakishangila bao lao la kwanza.

JOKATE, NATURE WATIFUANA!

Na Waandishi Wetu
PASUA jipu! Mastaa wawili wenye majina makubwa Bongo, mwanamitindo Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ na Mbongo-Fleva Juma Kasim ‘Juma Nature’ wanadaiwa kuacha mshangao kwa wasanii wenzao baada ya kutifuana, Ijumaa Wikienda limeng’atwa sikio.
Mkali wa Bongo Fleva, Juma Kasim ‘Juma Nature’.
Pamoja na kwamba Nature amekuwa akizuga kutomaindi lakini habari za kushangaza zilidai kwamba mkali huyo wa Temeke amekuwa akimtuhumu mwanadada huyo kuwa amemuibia wazo lake la biashara ya ndala au kandambili.
Kabla ya madai haya mapya, Nature aliwahi kunukuliwa redioni wakati akitambulisha wimbo wake mpya wa Chuma Ulete kuwa yupo mbioni kuingiza bidhaa hiyo sokoni.
Madai ya sasa yanaeleza kwamba Nature amekuwa akilalamika kuwa Jokate ‘amekopi’ na ‘kupesti’ wazo lake la biashara.
Mwanamitindo Jokate Mwegelo ‘Kidoti’.
Pia ilisemekana kwamba Nature amekuwa akimtafuta Jokate ili kuweka suala hilo sawa bila mafanikio.
“Nature amekuwa akimpigia simu Jokate lakini haipokelewi,” kilidai chanzo hicho kwa sharti la kutotajwa popote hata kwa mtutu wa bastola.
Kwa mujibu wa Nature bado hajabahatika kuziona kandambili za Jokate lakini amekuwa akiambiwa na watu wake kuwa mrembo huyo kamuibia.

Saturday, April 26, 2014

UUJUMBE WA KUMTISHIA MAISHA MZEE WA UPAKO

SIKU chache baada ya mwimbaji wa nyimbo za Injili, Rose Mhando kunusurika kutekwa, ujumbe wa tishio la kuuawa kwa Mchungaji wa Kanisa la Huduma ya Maombezi, Anthony Lusekelo ‘Mzee wa Upako’ umesambazwa.
Anthony Lusekelo ‘Mzee wa Upako’akisisitiza jambo
Ujumbe huo ambao ulitumwa na mtu aliyejitambulisha kama msamaria mwema, ulisambazwa kwa watu mbalimbali mpaka kuwafikia mapaparazi wetu, unaeleza kwamba mbaya wa Rose Mhando ana mpango wa kumuua Mzee wa Upako.

BABA AHUSISHWA KIFO CHA DENTI MWANZA!

Mwili wa marehemu Anastazia Lackfordukiagwa kabla ya kwenda kuzikwa.
Mwili wa marehemu Anastazia Lackford ambaye alikuwa mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Mwanza, umezikwa juzi katika makaburi ya Lunala, Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza lakini simulizi ya baba mzazi wa marehemu, Lackford Magafu kuhusishwa na kifo cha mwanaye inashangaza!
Kabla ya kifo.

UOZO MAHOSPITALINI: OFM YAIFUNGIA KAZI PALESTINA!

BADO hali ya huduma zinazotolewa na baadhi ya hospitali zetu nchini ni mbaya, utendaji mbovu na wagonjwa hawajaliwi hata pale inapotokea wamepelekwa wakiwa mahututi, Risasi Jumamosi linakufunulia.
Eneo la hospitali ya palestina.
Baada ya kuanika uozo wa hospitali kadhaa – za serikali na binafsi, sasa kikosi kazi cha Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ cha Global Publishers, kilitinga katika Hospitali ya Wilaya ya Kinondoni, Palestina na kugundua udhaifu mkubwa wa huduma mbovu zitolewazo hospitalini hapo.
OFM wakiingia hospitalini hapo.

ACHOMWA KISU KISA MUME WA MTU!

JESHIla polisi mkoani hapa linamshikilia mwanamke aliyejulikana kwa jina la Pima Mabubu kwa tuhuma za kumchoma kisu mpaka kumjeruhi vibaya mwanamke mwenzake, Amina Hussein akidai ana uhusiano wa kimapenzi na mumewe, Adam Ndekeja, Risasi Jumamosi lina mkasa wote.
Amina Hussein akipata matibabu katika hospital ya taifa Muhimbili.
Tukio hilo lililowaacha watu vinywa wazi, lilijiri Aprili 22, mwaka huu shambani katika Kijiji cha Kigwa, Kata ya Ukondamoyo wilayani Uyui, Mkoa wa Tabora.
KISU KILIVYOFANYA KAZI
Habari kutoka kwa baadhi ya mashuhuda zinasema kuwa, Amina alichomwa kisu mara mbili, kwenye paja mguu wa kushoto kisha kwenye mgongo ambapo kilizama na kutoka mpini tu!
Amina Hussein akikimbizwa hospital baada ya kupatwa na mkasa huo.
KISA KINASIMULIWA
Kwa mujibu wa taarifa za awali, siku ya tukio, Pima alitoka nyumbani kwake na kumfuatilia mumewe huyo kwenye shamba la tumbaku la kaka wa Amina (jina halikupatikana) ambako alisikia kuwa mwanamke huyo yupo na mumewe.
“Pima alisikia Amina ana uhusiano na mumewe. Siku hiyo akasikia wapo shambani. Akatoka nyumbani na kufuatilia akijua atawanasa laivu,” kilisema chanzo hicho.
Kisu kinachosadikika kilitumika kumjeruhi Amina Hussein.
MWANAMKE ALIYECHOMWA KISU
Akizungumza akiwa amelazwa akiuguza majeraha katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tabora, Kitete, Amina alisema:
“Mimi sina uhusiano na huyo mwanaume jamani. Kwanza huyo mwanamke simjui kabisa. Nimemwona kwa mara ya kwanza siku hiyo ya tukio.
“Siku hiyo mimi na mwanangu kichanga (wa miezi mitatu) tulikuwa shambani, mimi nilikuwa nikimsaidia kaka yangu kuvuna tumbaku, akaja Adam (mwenye mke) naye akawa anasaidia kuvuna. Kuna wakati nilikwenda kupumzika mahali ili nimnyonyeshe mwanangu.
“Ghafla aliibuka huyo mwanamke. Nilimwona akinifuata mimi moja kwa moja. Aliponifikia alinirukia na kuanza kunichoma kisu mgongoni na kwenye paja la kushoto.
“Ilikuwa ni hatua chache tu tokea mahali ambako mume wake alikuwa akivuna. Nilipiga kelele za kuomba msaada, mume wake akaja mbio kusaidia kwa kumdhibiti mke wake asiendelee kunichoma kisu zaidi,” alisema Amina.
Akaendelea: “Nilianguka chini na kuanza kugalagala huku damu nyingi zikinitoka. Ndipo wasamaria wema nao walifika na kumkamata Pima, wakamfunga kamba na kumpeleka ofisi ya kata ambako alipelekwa Kituo Kikuu cha Polisi Tabora.”
BODABODA YAMKIMBIZA HOSPITALI
Habari zaidi zinasema kuwa, Amina akiwa hoi na damu chapachapa, alipandishwa kwenye bodaboda na kukimbizwa kweynye hospitali ya rufaa ya mkoa kwa ajili ya matibabu huku hali yake ikionekana si ya kuridhisha.

Friday, April 25, 2014

Hii hapa top 20 ya 'Mama Shujaa wa Chakula' watakaoingia kijiji cha Maisha Plus wikiendi hii

Shindano la Mama Shujaa wa Chakula linaloendeshwa na kusimamiwa na Oxfam limefikia tamati ya hatua ya awali ya kutafuta washindi kwa kutangaza wanawake 20 kuingia katika top 20 ya shindano hilo la aina yake.

Wanawake hao wenye wasifu tofauti tofauti sasa wataingia katika kijiji cha maisha plus kwa muda wa wiki tatu ikiwa ni katika hatua ya kutafuta mshindi wa shindano hilo ambalo linalenga kuhamasisha jamii juu ya kilimo, hifadhi ya chakula na namna ya kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na njaa. Mbali na wanawake hao 20 pia kuna mshiriki mmoja ambaye yeye amepatikana kwa shindano la mtandaoni.

Hapa nakuletea orodha ya akina mama hao mmoja baada ya mwingine. 

GRACE G.D MAHUMBUKA (46) mkazi wa Karagwe Kagera nambari yake ya ushiriki ni MS 08, ni mkulima wa shamba la ekari 18 na na mfugaji wa ng’ombe, kondoo na mbuzi.


ANADHANI YEYE NI MFANO WA KUIGWA: Kwa sababu anawahamasisha wana kijiji kutumia vyema mvua za kwanza na kupanda miti kwa ajili ya utunzaji wa vyanzo vya maji na kutunza mazingira."Nina shamba lenye ukubwa wa ekari 18. Kwa mwaka ninavuna mazao gunia 35"


NEEMA URASSA KIVUGO (48) (Mshindi: Mama Shujaa wa Chakula Mtandaoni) ni mkazi wa Kiteto Manyara, namba yake ya ushiriki ni MS 12, na mkulima wa shamba la ukubwa wa ekari 10. 

ANADHANI YEYE NI MFANO WA KUIGWA: Yeye ni mchapakazi na anachukulia kilimo kama njia ya kumkwamua dhidi ya umasikini. Yeye ni mbunifu na hujifunza kwa haraka. Anavuna mazao gunia 78 kwa mwaka.


MARY JOHN MWANGA (52) ni mkazi wa Mkalama Singida, ni mkulima na mfugaji anashamba la ekari 5 na analima mahindi na anafuga ng’ombe watano

ANADHANI YEYE NI MFANO WA KUIGWA: Kwa sababu anashiriki katika shughuli za maaendeleo ya kijiji, michango na mikutano. "Kwa mwaka ninavuna mazao gunia 22" anasema.

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate