EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, October 21, 2015

Mwalimu mkuu, mzazi wanaswa

FUMANIZI (3)Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Umoja wa Mataifa iliyopo Upanga jijini Dar na mwanamke huyo.
Mwandishi Wetu 
DUNIANI kuna mambo! Katika hali ambayo haikutarajiwa, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Umoja wa Mataifa iliyopo Upanga jijini Dar, mwishoni mwa wiki iliyopita alinaswa live ofisini kwake akiwa na mwanamke anayedaiwa kuwa ni mzazi wa mmoja wa wanafunzi wa shule hiyo, kisa kikitajwa ni maandalizi ya kuivunja amri ya sita ya Mungu, Risasi Mchanganyiko lina mkanda kamili.
Tukio hilo la kufedhehesha, lilishuhudiwa na makamanda wa Global Publishers Kitengo Maalum cha Operasheni Fichua Maovu (OFM) ambapo pia watu wengine kadhaa walijionea kioja hicho cha mwaka.
FUMANIZI (2)HIVI NDIVYO ILIVYOANZA
Awali, Kamanda wa OFM akiwa kazini, alipokea simu kutoka kwa mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo, akimfahamisha juu ya hali isiyo ya kawaida kwenye ofisi za mwalimu huyo zilizopo ndani ya geti la shule, kwani aliwaona askari polisi wakihaha kama wanaotaka kuzuia uhalifu.
“Jamani OFM, njooni hapa Shule ya Msingi Umoja wa Mataifa. Kama kuna ishu, naona askari wapo na pia ndani kwa mwalimu mkuu kama kuna ishu. Sijui ni nini!” kilisema chanzo hicho.Mara moja, kamanda huyo alifanya mawasiliano na wenzake waliokuwa ‘fildi’ na kuwafahamisha kuhusu ishu hiyo. Wakitumia pikipiki zao ‘zinazopaa’, makamanda hao walifika eneo la tukio dakika chache baadaye na kukuta mambo ndiyo kwanza yanaanza.

Shilole atoboa siri tattoo ya Nuh

shilole (1)Gladness Mallya
STAA wa muziki na filamu Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ ametoboa siri ya kujichora tattoo yenye jina la mpenzi wake Naftari Mlawa ‘Nuh’ akisema alifanya hivyo ili kumpa imani mwanaume huyo kuwa anampenda sana.
shiloleNUH
Akizungumza na gazeti hili juzikati, Shilole alisema siku zote mpenzi wake hakuwa akiamini kama anampenda, licha ya ukweli kwamba naye alikuwa amechora tattoo yenye jina lake.
“Nuh alikuwa haamini kama kweli nina mapenzi ya dhati kwake, niliamua kuchora tattoo ya jina lake na sasa ameamini nampenda, mapenzi yetu yameimarika kuliko mwanzoni, amejiona ni mtu muhimu sana kwangu, kwani hata mwanaume yeyote akiona nimejichora jina hili, lazima ashtuke na aone kwamba nina mtu tunayependana,” alisema.

Monalisa: Mwaka huu lazima nipige kura

Cdrisa4-1
Msanii wa filamu Bongo , Ivon Cherry Ngatikwa ‘Monalisa’.
Mayasa Mariwata
ZIKIWA zimebaki siku tatu kuelekea uchaguzi mkuu, msanii mkongwe wa filamu Bongo , Ivon Cherry Ngatikwa ‘Monalisa’ amesema safari hii lazima apige kura, hata kama kutakuwa na foleni ya aina gani.
Akichezesha taya na paparazi wetu, Monalisa alisema bila kujali ustaa wake, siku ya uchaguzi atapanga foleni hata kama ni kubwa ili kutimiza azma yake ya kumpigia kura kiongozi anayefaa kuiongoza nchi.
“Japokuwa nina hofu, lakini lazima nikapige kura hivyo nawaomba Watanzania wawe watulivu na kudumisha amani, wakubaliane na matokeo ili kuepusha machafuko yasiyokuwa na maana ambayo yanaweza kuyagharimu maisha yetu,” alisema Monalisa.

Wednesday, October 14, 2015

ROSE NDAUKA: SITAKI KUWACHANGANYA MASHABIKI

MWANADADA staa wa filamu Bongo, Rose Ndauka amesema hataki kujihusisha na harakati za siasa kwa sasa kwa vile anaogopa kuwachanganya mashabiki wake.
Mwanadada staa wa filamu Bongo, Rose Ndauka.
Akipiga stori na gazeti hili, Rose alisema kwa kuwa yeye ni kioo cha jamii anayeelimisha kupitia kazi yake, alisema kujiweka wazi upande ulipo ni kuwagawa watu wake kitu ambacho asingependa kitokee.
“Wasanii wanaozunguka kwenye kampeni hawafanyi vibaya, lakini mimi siwezi na sikutaka kufanya hivyo ila kura nitapiga na kuhusu ni nani nitakayemchagua kuwa rais ni siri yangu,” alisema nyota huyo ambaye anakiri kuwa soko lao limeyumba.

Kampeni zambadilisha akili Johari


johari (1)
Sta wa sinema za kibongo, Blandina Chagula maarufu kama Johari.
CHANZO: GPL
BLANDINA Chagula maarufu kama Johari, ambaye ni mmoja wa wasanii wanaozunguka nchi nzima kuipigia kampeni CCM katika uchaguzi mkuu, amesema baada ya kutembea na kufanya kazi, amejikuta akiihamishia akili yake katika siasa.
johari (3)

Jokate, Kiba picha sasa zinaiva

Mwanamitindo Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ na mwandani wake Ally Salehe Kiba wakikumbatiana.
MAYASA MARIWATA NA BONIPHACE NGUMIJE
MWANAMITINDO Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ na mwandani wake Ally Salehe Kiba, wamethibitisha kuwa wana maelewano mazuri (picha zinaiva) baada ya mwishoni mwa wiki kuonekana pamoja katika bonanza maalum la wanafunzi, lililofanyika katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Jangwani, jijini Dar es Salaam.
Tukio hilo lililojulikana kama Kidoti Bonanza liliandaliwa maalum kwa ajili ya kuthamini vipaji vya wanafunzi na ambalo lilihudhuriwa na madenti wa shule mbalimbali ambao pia walipata burudani kutoka kwa wasanii na makundi tofauti.
Jokate alikuwa jukwaani pamoja na msanii anayetamba na kibao cha Ni Yule, Hellen George ‘Ruby’ ambaye alishika kipaza sauti na kuwauliza madenti hao kama wanafahamu mtu aliyeimbwa na Kidoti katika kibao chake cha Leoleo ambao wote kwa pamoja walijibu kuwa mtu huyo ni Ali Kiba.

MECHI ZA LIGI KUU BARA WIKIENDI HIZI HAPA MWANAWONE


Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania (VPL) inatarajiwa kuendelea wikiendi hii kwa michezo sita kuchezwa katika viwanja mbalimbali nchini, ikiwa katika mzunguko wa saba timu 14 zitapambana kusaka pointi 3 muhimu.

Young Africans watawakaribisha Azam FC katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam siku ya Jumamosi, huku timu zote zikiwa na pointi 15 kileleni zikitofautiana kwa magoli ya kufunga na kufungwa.
Kabla ya mchezo wa Yanga dhidi ya Azam, kutakua na mchezo wa utangulizi wa kuombea amani kuelekea kwenye uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika Oktoba 25, 2015.
Mchezo huo utawakutanisha viongozi wa dini watakocheza dhidi ya mabalozi wanaofanya kazi nchini, mechi hiyo itaanza saa 8:25 mchana na kumalizika saa 9:15 alasiri.
Majimaji FC ya mkoani Ruvuma watakua wenyeji wa African Sports kwenye uwanja wa Majimaji mjini Songea, huku Ndanda FC wakiwakaribisha Toto African kutoka jijini Mwanza katika uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.
Jijini Mbeya, watoza ushuru wa jijini hilo Mbeya City FC watawakaribisha Simba SC katika uwanja wa Sokoine, Chama la wana Stand United watakuwa wenyeji wa Tanzania Prisons uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga, huku Coastal Union wagosi wa kaya wakiwakaribisha wakata miwa wa Mtibwa Sugar katika uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.
Ligi hiyo itaendelea Jumapili kwa michezo miwili kuchezwa, Mgambo Shooting watakua wenyeji wa Kagera Sugar katika uwanja wa Mkwakwani, huku Mwadui FC wakicheza na maafande wa JKT Ruvu katika uwanja wa Mwadui Complex.

RAYUU: WANAUME WANNE WAMEINGIA MITINI


Msanii wa filamu Bongo, Alice Bagenzi ‘Rayuu’.
MAYASA MARIWATA
NYOTA wa filamu Alice Bagenzi ‘Rayuu’ amesema anajihisi kama mwanamke mwenye mkosi baada ya wanaume wanne alioshiriki nao mapenzi kuonesha nia ya kumuoa, lakini ghafla waliingia mitini na kupeperusha ndoto yake ya kuwa mke wa mtu.
Akipiga stori na gazeti hili, muigizaji huyo alisema umri wake unamruhusu kuolewa na anafanya kila njia ikiwa ni pamoja na kutii maelekezo yote ya mwanaume ili kumvutia aingie naye katika ndoa, lakini kinachomshangaza hubadilika ghafla na kumpotezea kabisa.
“Siyo siri naumia sana, huenda nimerogwa nisiolewe, mwanaume anajitambulisha hadi kwa wazazi na kuanza mchakato wa ndoa lakini baadaye anaingia mitini,” alisema Rayu

FLORA MBASHA AKIRI: MWANANGU SI WA MBASHA!

Mwimbaji wa nyimbo za Injili, Flora Mbasha na aliyekuwa mumewe, Emmanuel Mbasha.
CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS
OHOOO! Kimenuka tena. Mwimbaji wa nyimbo za Injili, Flora Mbasha amesema mwanaye mdogo (jina linahifadhiwa) hahusiani hata kidogo na aliyekuwa mumewe, Emmanuel Mbasha huku akidai kuwa anamtambua mwanaume huyo kama mzazi mwenzake kwa mtoto mmoja tu (Liz), Risasi Jumatano linakupa zaidi.
Mtoto anayedaiwa kuibuwa mazito.
Akizungumza na waandishi wetu kwa njia ya simu mwishoni mwa wiki, Flora alisema amechoshwa na manenomaneno yanayosemwa juu yake na Emmanuel na kwamba kama mumewe huyo ameamua kumwaga ugali, yeye yupo tayari kumwaga mboga.
Mwimbaji huyo alisema kwamba kauli aliyoitoa hivi karibuni kuwa anampenda mumewe na kwamba yupo tayari kuishi naye haikutoka moyoni, isipokuwa alifanya hivyo kwa huruma tu, kwa sababu mwanaume huyo ni mtu katili, mwenye roho mbaya na asiyemuogopa Mungu.
“Mtu mwenyewe alimtelekeza mtoto (Liz) kwa zaidi ya mwaka mmoja, ni mtu mbaya sana, sina mapenzi na Mbasha hata kidogo, ni afadhali niolewe na chizi anayeokota makopo kuliko kurudiana na mtu katili na mnyama kama huyo, namheshimu kama mzazi mwenzangu kwa Liz,” alisema.

Saturday, October 3, 2015

Wolper kufunga ndoa ya siri

Imelda Mtema
BAADA ya kuvishwa pete na mwanaume aliyedaiwa kuwa na mume wa mtu, raia wa Kongo, mwigizaji Jacqueline Walper ‘Wolper’ amesema kamwe watu hawatajua siku atakayofunga ndoa kwani amegundua watu wengi wana husda.
Wolper alisema anaamini kuwa siyo kila mtu ana mapenzi ya dhati kwake hivyo atafunga ndoa ya kimyakimya ndipo baadaye atafanya sherehe.“Siku hizi wanga wengi watu watashtukia nimeshafunga ndoa sherehe baadaye kwa wale ndugu na marafiki maana najua siyo wote wanaopenda jambo hili litimie,” alisema Wolper.

JB: Bora uigizaji kuliko ubunge

JB (2)Erick Evarist
MKURUGENZI wa Jerusalem Film Company, Jacob Stephen ‘JB’ ameweka wazi kuwa kamwe hafikirii kuwa mwanasiasa kwani sanaa inamlipa zaidi.
Akizungumza na mwanahabari wetu katika mahojiano mafupi, JB alisema kipindi cha nyuma ziliibuka tetesi kuwa huenda anaweza kuwa mwanasiasa lakini ukweli kutoka moyoni, sanaa inamlipa.
“Sanaa inanilipa, sifikirii kama ubunge au siasa kwa ujumla inaweza kunilipa kama sanaa ambayo naipenda kutoka moyoni. Labda nikupe mfano, kupitia kampuni yangu, nikizalisha filamu moja inatoa ajira kwa wafanyakazi wasiopungua 30, itatoa ajira katika maduka, machinga na sehemu mbalimbali zinazouzwa filamu.
“Sanaa imetoa ajira kwa wasanii Mil 10. Unafikiri hao watu wangefanya nini kama si sanaa?,” alisema JB.
JB aliongeza kuwa, kwa sasa anamuunga mkono mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), John Magufuli kwani mwenyekiti wa chama hicho, Jakaya Kikwete ameweka misingi mizuri katika sanaa.
“Kikwete ametusaidia kwa kiasi kikubwa kuitangaza sanaa yetu, amekuwa akishiriki katika shughuli zetu kitu ambacho kwetu sisi kina maana kubwa sana katika suala zima la kututangaza na ndiyo maana tunaunga mkono CCM na ukizingatia Ilani ya CCM ya uchaguzi huu, imetugusa moja kwa moja,” alimalizia JB.

Hatari kubwa! Mafuta ya Transfoma kukaangia Chips, Wabongo wengi kufariki!

Mayasa mariwata na Shani ramadhani
HATARI! Kufuatia kuwepo kwa madai kwamba, baadhi ya wakaanga chipsi mijini, hususan jijini Dar, wamekuwa wakitumia mafuta ya transifoma kukaangia chakula hicho, timu ya Oparesheni Fichua Maovu ‘OFM’ ya Global Publishers iliingia mtaani kwa lengo la kujiridhisha.
OFM iliingia kwenye viunga mbalimbali vya jiji hasa sehemu ambazo zina vibanda vya wauza chipsi na kuzungumza nao.
Muuza chipsi maeneo ya Mwananyamala aliyejitambulisha kwa jina moja la Ushie, alipoulizwa kuhusu kuwepo kwa madai hayo, alisema amesikia wapo wanaotumia lakini yeye hatumii.
Mwingine alikutwa na OFM maeneo ya Kinondoni akajitambulisha kwa jina la Idi Juma. Yeye alisema: “Kuna mtu aliwahi kuniletea mafuta ya transifoma akidhani nitanunua ili niwe natumia kukaangia chipsi nikagoma. Lakini wapo wauza chipsi wengi ambao si waaminifu wanatumia.”
Karibu wauza chipsi wote walioulizwa na OFM hawakukiri kuhusu kutumia mafuta hayo. Lakini walisema wenzao wanatumia.Inadaiwa kuwa, wauzaji wanapenda mafuta ya transifoma kwa sababu yanaweza kutumika kwa muda mrefu, hata mwezi mmoja bila kukauka kwenye karai na hayafanyi chipsi kuwa nyeusi kama mafuta halali. Inadaiwa pia, chipsi zilizokaangwa na mafuta hayo ni tamu sana.
TANESCO YATOA TAMKO
Jumatano iliyopita, OFM ilizungumza na Afisa Habari wa Shirika la Ugavi Tanzania (Tanesco), Adrian Severin na kumuuliza kama shirika linajua kutumika kwa mafuta hayo kukaangia chipsi ambapo alisema:
“Tunajua japokuwa hatujawahi kuthibitisha kwa kumwona mtu akiyatumia. Wengine wanayatumia kwenye vipodozi, wengine wanachanganya na oil ya magari. Lakini Tanesco tunatoa wito kwa Watanzania, hususan wanaoishi jirani na transifoma kutoa taarifa mara wanapomwona mtu anapanda kwenye transifoma huku si mfanyakazi wa Tanesco.
“Wizi wa mafuta haya unasababisha transfoma kushindwa kufanya kazi na hivyo maeneo husika kukosa umeme.”
DAKTARI AFAFANUA
OFM lilimtafuta daktari mmoja wa jijini Dar es Salaam, dokta Chale kwa lengo la kumuuliza kama mafuta ya transifoma yakitumika kwenye chakula yana madhara, akajibu:
“Makubwa tu. Kwanza, mtumiaji anaweza kupata ugonjwa wa kansa ya tumbo. Pili, hayo mafuta yanaweza kusababisha maini na figo kushindwa kufanya kazi. Na tabia hii ikiendelea, Wabongo wengi watakufa.”

CHANZO: Global Publishers

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate