EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Friday, November 30, 2012

Poleni tasnia ya sanaa kwa kupoteza wasanii.

Awali ya yote naanza kwa kutoa mkono wa pole kwa wapenda burudani kote nchini kutokana na misiba ya wasanii iliyofuatana, jambo lililoipelekea kuwa na majonzi yasiyokoma.
Awali alianza Maria Khamis ‘Paka Mapepe’ aliyekuwa muimbaji wa muziki wa taarab wa kundi la Tanzania One Theatre (TOT) aliyefariki kutokana kifafa cha uzazi.
 
Wakati watu wakiwa hawajakaa sawa wala machozi kufutika vema usoni au kwa msemo mwingine naweza kusema ikiwa bado tanga halijaanuliwa sawasawa tasnia ya filamu ikaondokewa na Khalid Mohamed a.k.a Mlopelo (41) aliyeng’ara na kikundi cha Kaole kilichokuwa kikirushwa na kituo cha televisheni cha ITV ambako ndiko alikopata umaarufu wake na hatimaye kushirikishwa katika filamu kadhaa.

Wakati msiba wa Mlopelo haujaisha msanii mwingine wa Bongo Movie John Maganga akafariki Jumamosi iliyopita na kuzikwa Jumanne wiki hii.
Wakati kukiwa kuna msiba wa Maganga Jumatatu usiku msanii Ramadhan Mkiteti alipata ajali maeneo ya Maguzoni Muheza mkoani Tanga.
Hakika wasanii na tasnia wamekumbwa na misiba yote ya uchungu; nachukua fursa hii kuwapa pole.
Ni kweli hakuna msiba unaozoeleka hata siku moja kama babu au bibi yako amefariki miaka kadhaa iliyopita, inauma sana.

‘Dada’ aiba mtoto mwenyeji wa mkoa wa Kigoma.

MSAIDIZI wa ndani, Doyi Yusuph (13), mwenyeji wa mkoa wa Kigoma, anasadikiwa kuiba mtoto wa kike, Yasinta Joel (5), katika nyumba aliyokuwa akifanya kazi wilayani Bukombe, Geita, na kisha kutoweka naye kusikojulikana.
Akizungumza  juzi, bibi wa mtoto huyo, Perepatua Alphonce, alisema dada huyo amefanya wizi huo huku akiacha sanduku lake la nguo, jambo ambalo liliwahadaa kwa kutogundua haraka kitendo hicho.

Perepetua maarufu kwa jina na Bibi Mgaya, alisema mjukuu wake huyo alikuwa akisoma chekechea kwa Mwalimu Kapesa na alikuwa akiishi na babu yake, Edward Mgasa.
Alisema dada huyo ambaye alikuwa na wiki moja tangu aanze kazi katika familia ya Mzee Mgasa, alimuiba mtoto huyo Novemba 23, mwaka huu, majira ya saa tatu asubuhi. Wakati akiondoka naye mtoto huyo alikuwa amevaa blauzi ya maua yenye mchanganyiko wa rangi nyekundu na zambarau na sketi ya Jeans rangi ya bluu.

“Niliishaachana na Mzee Mgasa ambaye alioa mke mwingine na walikuwa wakishirikiana kumlea mjukuu wetu. Siku ya tukio mzazi mwenzangu alikuwa kwenye machimbo madogo ya Ng’anzo kwenda kutafuta riziki,” alisema Perepetua.
Alisema amesharipoti suala hilo katika kituo cha polisi cha wilayani Bukombe na kufunguliwa jalada namba USH/IR/177/2012 na kuwaomba raia wema wanaomuona mtoto huyo kutoa taarifa katika kituo chochote cha polisi au kuwasiliana naye kwa simu namba 0755 910 377.

CHAMA cha Washereheshaji Nchini (Sherehe Arts Association –SAA) yatoa rambi rambi kwa Sharomilionea

CHAMA cha Washereheshaji Nchini (Sherehe Arts Association –SAA), kinatoa pole za rambirambi kwa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, familia ya Marehemu Hussein Ramadhan 

‘Sharomilionea’ kutokana na kifo cha msanii huyo.
Rambirambi hizo zimetolewa na Katibu Mkuu wa chama hicho, MC Bryceson Makena, alipokuwa akizungumza na mwanadishi wa habari hizi.

Alisema SAA inawatakia wanafamilia wote ujasiri wa kulipokea jambo hilo na kuvuta subira kwani wote njia ni moja ila wakati ndio tofauti.Pia ametoa wito kwa wasanii wote nchini kuwa na umoja na mshikamano endelevu katika kipindi hiki kigumu.

VURUGU ZA JANA JIJINI DAR ES SALAAM RIPOTI KAMILI,

Mabomu Dar
Na: Joseph Zablon Dar  
POLISI wamewajeruhi watu watatu kwa mabomu, mmoja kati yao akiwa katika hali mbaya katika matukio mawili tofauti ya kusambaratisha mikusanyiko iliyotokea Tegeta, Dar es Salaam na Rufiji mkoani Pwani.

Aliyejeruhiwa vibaya ametambuliwa kuwa mkazi wa Tegeta, John Paul ambaye baada ya tukio hilo alipelekwa katika Hospitali ya Mwananyamala na baadaye Muhimbili.Tukio la Tegeta lilitokea wakati polisi walipokuwa wakiwatawanya wananchi waliokuwa wakipinga operesheni ya kuwaondoa katika hifadhi ya barabara katika eneo hilo saa nne asubuhi baada ya wafanyakazi wa Kampuni ya Udalali ya Mwankinga wakiwa na polisi waliyolikamata gari la mkazi mmoja wa eneo hilo.Hali hiyo ilizua ubishi na baadaye vurugu baada ya wakazi hao kutaka gari hilo lisichukuliwe na polisi.

Bakwata yamkana Sheikh Ponda mahakamani.

BARAZA Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata), limemkana Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda na wenzake, baada ya kudai mahakamani kuwa eneo walilovamia wakidai ni mali ya Waislamu linamilikiwa kihalali na kampuni ya Agritanza.
 
Katibu Mkuu wa Bakwata, Sheikh Suleiman Lolila alisema hayo jana wakati akitoa ushahidi katika kesi ya jinai inayomkabili Ponda na wenzake 49 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakidaiwa pamoja na mambo mengine kuvamia na kupora ardhi na wizi wa vifaa vya ujenzi.Akitoa ushahidi wake jana huku akiongozwa na Wakili Mwandamizi wa Serikali, Tumaini Kweka, Lolila ambaye ni shahidi wa kwanza wa upande wa mashtaka alidai kuwa eneo hilo awali lilikuwa likimilikiwa kihalali na Bakwata.

Katiba iwazuie viongozi kupendelea ndugu zao.

WANANCHI wa Kata ya Ketumbeine, wilaya ya Longido mkoani Arusha wametaka Katiba Mpya itakayoandikwa kuwadhibiti viongozi na wenye madaraka kutumia nyadhifa zao kujijengea wigo kwa kuwajaza ndugu,jamaa na marafiki zao kwenye ofisi za umma.

Wakitoa maoni mbele ya Ujumbe wa Tume ya Katiba inayokusanya maonimkoani Arusha, wananchi hao walisema kuna hatari ya ofisi zote za ummakushikiliwa na watoto, ndugu, jamaa na marafiki wa viongozi kutokanana mwanya uliopo kwenye Katiba na sheria zisizowabana viongozi kuhusuajira na uteuzi.
Lemomo Alambala (44), Richard Mollel (28) na Michael Laizer wote,licha ya kutaka viongozi wadhibitiwe ndugu zao kwenye medani yauongozi wa ofisi za umma, pia walitaka watakaotuhumiwa kwa rushwa naufisadi wa mali na fedha za umma kuondolewe madarakani, kushtakiwa nakufilisiwa wakitiwa hatiani.

Magazeti ya Kampuni Mwananchi yaongoza kwa wasomaji nchini.

TAASISI ya Utafiti ya Synovet imeweka hadharani matokeo ya utafiti wao kuhusu vyombo vya habari nchini kwa mwaka 2012, unaoonyesha kwamba magazeti yote matatu ya Kampuni ya Mwananchi Communication Ltd, MCL, yanaongoza kwa kuwa na wasomaji wengi.

MCL ndiyo wachapishaji wa magazeti ya Mwananchi, The Citizen na Mwanaspoti.
Kwa mujibu wa utafiti huo, kwa magazeti ya Kiswahili ya kila siku, Mwananchi limeyaacha mbali magazeti mengine ikiwa ni zaidi ya nusu ya wasomaji wanaofikia asilimia 59.

AMANDA POSHY NA MPENZI WAKE MPYA BWANA MISOSI.

AMANDA POSHY na EMMANUEL LUSHAHU a.k.a BWANA MISOSI ni wapenzi wenye malengo ya kuja kuwa mume na mke.Amanda ambaye ni muigizaji wa movie za kibongo wa siku nyingi na Bwana misosi ni mwanamziki wa Bongo Fleva.Wote wanapendana sana IRENE MWAMFUPE JAMII BLOG inawatakia maandalizi mema ya ndoa yao siku zijazo.

VIDEO YA " NATAKA KULEWA" YA DIAMOND ITAKUWA HEWANI JUMAPILI HII.

Ile music video ya msanii Diamond Platnumz, ambao wimbo wake ulileta utata baina ya wasanii watatu, namaanisha H-Baba, Pasha na yeye Diamond, “Nataka kulewa” imekamilika na kilichobaki ni kuachiwa siku ya Jumapili ya wikiendi hii.
Kwa mujibu msanii Diamond na wa meneja wa msanii huyo Raqey ambaye ndiye alikuwa muongozaji mkuu wa utayarishaji wa video hiyo, kila kitu kimeshakamilika ikiwemo post production editing na sasa kilichobaki ni kuachiwa rasmi siku ya Jumapili katika Street Bash Party iliyoandaliwa na Clouds media kusherehekea kutimiza miaka 13 kwa kituo cha Radio ya Clouds FM.

Thursday, November 29, 2012

Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodom yaanza kuwasaka wanafunzi wa chuo hicho wanaojihusisha na biashara ya kujiuza kimwili.

RAIS wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOSO), Paul Yunge, amesema kuwa wanafanya uchunguzi wa kina ili kuwanasa wanafunzi wa chuo hicho wanaojihusisha na biashara ya kujiuza kimwili ili
wawachukulie hatua.

Yunge alifafanua kuwa, wanafunzi watakaobainika kujihusisha na vitendo hivyo watachukuliwa hatua kali za kinidhamu ili iwe fundisho kwa wengine.

Polisi afukuzwa kazi kwa kumbaka mtuhumiwa.

JESHI la Polisi mkoani Mbeya limemfukuza kazi askari wake Enock Daffa (22) kwa tuhuma za kufanya  mapenzi na mtuhumiwa wa kike mwenye umri wa miaka 25 katika Kituo cha Polisi cha Mji mdogo wa Tunduma, Wilaya ya Momba, mkoani hapa.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Athuman Diwani, askari huyo alitenda kosa hilo Novemba 21,2012 na kwamba mtuhumiwa aliyefanya naye mapenzi alikuwa akikabiliwa na kosa la wizi.

Kamanda Athumani alisema kuwa mbali ya kufukuzwa kazi askari huyo tayari amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Mbozi ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.
Aidha alisema kuwa hali kama hiyo haitaweza kuvumiliwa na Jeshi la Polisi na kwamba atakayebainika kufanya tukio kama hilo adhabu yake itakuwa ni kufukuzwa kazi.

Jaji chande aikwepa kesi ya Lema.

JAJI Mkuu wa Tanzania, Mohamed Othman Chande amejitoa kusikiliza rufaa ya kesi ya aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, badala yake nafasi yake imechukuliwa na Jaji Bernard Luanda.

Kujitoa kwa jaji mkuu kumekuja ikiwa zimebaki siku tano kusikilizwa upya kwa rufaa hiyo Desemba 4, mwaka huu, baada ya awali Mahakama ya Rufani, kuona rufaa hiyo ilikuwa na dosari.
Mahakama hiyo ilikubali hoja ya wajiburufaa kuwa rufaa hiyo ilikuwa na dosari kutokana na tofauti ya vifungu vya sheria vilivyotumika katika hukumu iliyomvua ubunge Lema na vilivyotumika katika hati ya kukaza hukumu, iliyowasilishwa mahakamani sambamba na rufaa hiyo.
Jaji Mkuu Othman Chande ambaye ameonyesha nia yake ya kujitoka katika kesi ya Lema  Mwananchi

VIONGOZI WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI WAZINDUA BARABARA YA ARUSHA-NAMANGA-ATHI RIVER.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi Kenya Jumatano Novemba 28, 2012 tayari kuhudhuria sherehe za ufunguzi wa barabara ya Arusha-Namanga-Athi River pamoja na Mkutano wa Wakuu wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki utaozungumzia maendeleo ya miundombinu. Kiongozi wa Jumuiya ya Waislamu wa Ismailia Mtukufu Aga Khan naye alikuwepo hapo uwanjani.
 
PICHA NA IKULU

MUDDY Suma ndiye mmliki wa gari aina ya Toyota Harrier namba T 478 BVR asema mi namwachia Mungu.

 
Hussein Ramadhan Mkieti ‘Sharo Milionea’.
Na Musa Mateja
MUDDY Suma ndiye mmliki wa gari aina ya Toyota Harrier namba T 478 BVR ambalo lilipinduka na kusababisha kifo cha staa wa vichekesho Bongo, Hussein Ramadhan Mkieti ‘Sharo Milionea’ ameibuka na kusema machache ambayo Watanzania wengi wangependa kujua kutoka kwake.
Akizungumza jana na paparazi wetu msibani Kijiji cha Lusanga, Muheza, Tanga, mmiliki huyo alisema haikuwa mara ya kwanza kwa Sharo Milionea kuazima gari kwake na kwenda nalo Muheza kisha kurudi salama Dar es Salaam.

ZAMARADI AFIWA NA MAMA MZAZI.

Na Imelda Mtema
MTANGAZAJI wa Runinga ya Clouds, Zamaradi Mketema (pichani) amepata pigo baada ya mama yake mzazi kufariki dunia Novemba 28, mwaka huu.
 
Kwa mujibu wa mtu wa karibu na familia, mama huyo alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa kansa ambapo hivi karibuni alifikishwa katika Hospitali ya Ocean Road jijini Dar, akaruhusiwa na ndipo mauti yalipomkuta nyumbani kwake Kinondoni Studio, Jijini Dar.
“Ni pigo kubwa kwa Zamaradi kwani kuondokewa na mama yake si kitu cha mchezo, inauma sana,” alisema mtu huyo aliye karibu na familia.
Hadi gazeti hili lilipokuwa linakwenda mitamboni, taratibu za mazishi zilikuwa zikiendelea ambapo ilielezwa kuwa mazishi yatafanyika leo.
                                       Chanzo cha habari www.globalpublishers.info

VIONGOZI WAKUU WA NCHI WANACHAMA WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI WAZINDUA JENGO LA MAKAO MAKUU YA JUMUIYA JIJINI ARUSHA.


Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakiangalia mfano wa jengo jipya la makao makuu ya Jumuiya hiyo pamoja na maelezo yake baada ya kulifungua rasmi  Novemba 28, 2012 jijini Arusha
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi wenzie wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wakikata utepe kufungua rasmi jengo jipya la makao makuu ya Jumuiya  Novemba 28, 2012 jijini Arusha

WOLPER: NIKIACHIKA TENA, NATIMKA BONGO NA KWENDA UGHAIBUNI KUOLEWA HUKO.

PAMOJA na kukataa kumwanika hadharani mpenzi wake mpya, staa wa filamu za Kibongo, Jacqueline Wolper Massawe amesema kuwa akipigwa chini na jamaa yake huyo, atatimka nchi na kwenda kuolewa ughaibuni.Akiteta na Tollywood Newz hivi karibuni jijini Dar, Wolper alisema anajitahidi kulilinda penzi lake jipya ili lisiweze kuvunjika na ikitokea hivyo, hatataka  tena kuwa na mpenzi wa  Kibongo.
 
“Kwa kweli siwezi kuachika tena sasa hivi.Ikitokea sitakuwa na amani moyoni mwangu na sitataka kuwa na mpenzi mwingine hapa nchini, nitaenda kuolewa nje ya nchi,” alisema Wolper ambaye hivi karibuni alimwagana na aliyekuwa mpenzi wake, Abubakar Mtoro ‘Dalas’.Chazo cha hii habari ni Gazeti pendwa la Risasi Mchanyiko uk wa 3.

AMANDA POSHY HUMWAMBII KITU KWA MPENZI WAKE BWANA MISOSI.

Wanaonekana wapenzi wenye malengo ya baadae.Amanda msanii wa movie amekufa ameoza kwa Emmanuel Lushahu 'Bwana misosi' msanii wa Bongo Fleva na kwamba ana wivu kwake kama vile tayari wameoana.

Amanda amekuwa akimtaja mara kwa mara mwanaume huyo huku akionekana amempenda kuliko wanaume wote waliompitia.Ameweka penzi lake wazi na kutumia picha ya mpenzi wake kwa profile yake facebook
Picha hii ni kuonyesha kafa kaoza akiwa na mpenzi wake Bwana misosi wakiwa kimahaba .
                        Hapa chini ni baadhi ya comment za picha hii facebook.

Majaji wasusia kazi kumpinga rais Mursi.

Majaji wa mahaka ya rufaa nchini Misri wanajiandaa kususia kazi na kuunga mkono waandamanaji dhidi ya rais wa misri Mohammed Morsi kujipa mamlaka zaidi.
Sheria ya kumapaka mamlaka zaidi rais Mursi ilipitishwa siku ya Alhamisi wiki jana. Sheria hiyo inampa mamlaka rais kuchukua hatua zozote kulinda mapinduzi na kusema kuwa hakuna mahakama yoyote inaweza kuamua vinginevyo.

MATOKEO ZA LIKI KUU YA ENGLAND USIKU WA JANA

Dembele Gerrard 
Rodgers fuming at referee decisions.
Brendan Rodgers has criticised the performance of referee Phil Dowd during Liverpool's 2-1 loss to Tottenham at White Hart Lane on Wednesday.

BOSI WA ZAMANI WA SHARO MILIONEA LAWAMANI …HAKUKANYAGA MSIBANI.

MMILIKI wa kampuni ya Al Ryami Production, Khalfan Abdallah, ameingia kwenye lawama nzito kwa kushindwa kwake kuhudhuria mazishi ya msanii Sharo Milionea yaliyofanyika jana Lusanga wilayani Muheza, Tanga.
Khalfan ni Bosi wa zamani wa Sharo Milionea, kutokuhudhiria kwake mazishi hayo kumezua maswali mengi hasa kutokana na ukweli kuwa hakuvutiwa na namna wasanii wake wa zamani akiwemo Sharo walivyomkiambia.
Wasanii wengine nyota waliotimka kwa Khalfani ni pamoja na Mzee Majuto na Kitale.
Kitale aliiambia Saluti5 kuwa siku ya tukio Khalfan alipigiwa simu na akasema apigiwe baadae ili asikilize kwanza vyombo vya habari kujua kama habari hizo zina ukweli wowote.
Mtu mwingine wa karibu sana na Khalfan ambaye hakutaka jina lake litajwe, aliiambia Saluti5 kuwa siku nzima ya juzi (Jumanne) simu zote za Khalfan zilikuwa zimezimwa, hivyo akaamua kwenda ofisini kwake ambapo huko akaambiwa Bosi tayari ameenda Tanga msibani.
Mtu huyo anasema alipofika msibani hakumkuta Khalfan na hata alipowauliza wasanii wa Bosi huyo wa zamani wa Sharo waliokuwa kambini Tanga mjini wakawa na majibu tofauti kwamba wanachojua wao ni kwamba Bosi ameenda Dodoma.
Wasanii wengi wa vichekesho wameelekeza shutuma nyingi kwa Khalfan na kusema kwamba hawawezi kumwelewa kwa kitendo hicho cha kutohudhuria mazishi ya msanii mwenzao.
Saluti5 ilijaribu kumpigia simu Khalfan ili kujua nini kilichomsibu lakini bado simu zake zilikuwa hazipatani.Chanzo cha habari na www.saluti5.com

NDEGE YA FAST JET:BEI NAFUU ,DAR to MWANZA or KILIMANJARO Tsh.32,000 TU HII HAPA.

ZINANZA SAFARI SIKU YA LEO ALHAMISI NA ZITAKUWA NA SAFARI MARA MBILI KWA SIKU,KUTOKA DAR HADI KILIMANJARO HADI MWANZA NA KURUDI DAR TENA.NAURI KWA SAFARI MOJA NI $ 20 sawa na Tsh. 32000.

WANYANGE WANAOWANIA TAJI LA MISS EAST AFRICA 2012 NDANI YA DAR ES SALAAM.

Miss East Africa 2012-Tanzania. Grand Finale to be held on 07th December at Mlimani City, Dar es Salaam.

Miss East Africa 2012-Eritrea. Grand Finale to be held on 07th December at Mlimani City, Dar es salaam
Miss East Africa 2012-Rwanda. Grand Finale to be held on 07th December at Mlimani City, Dar es salaam

Miss East Africa 2012-Burundi. Grand Finale to be held on 07th December at Mlimani City, Dar es salaam Warembo wa Miss East Africa 2012 wakiwa katika vazi la ufukweni, jijini Dar es salaam.Picha zaidi Click read more hapa chini

MASELE CHA POMBE NAE ‘AMKACHA’ SHARO MILIONEA …ZE COMEDY, ORIJINO KOMEDI NAO HAWAJAONEKANA MAZISHINI.

MCHEKESHAJI Chrispin Masele “Masele cha pombe”, jana alikuwa ni miongoni mwa sura chache zilizokosekana kwenye mazishi ya Sharo Milionea.
Masele ambaye ni msanii wa Al Riyami Production (mabosi wa zamani wa Sharo), ni mmoja kati ya wasanii waliofanya kazi nyingi na kwa ukaribu sana na Sharo Milionea.
Wasanii wa Al Riyami waliiambia Saluti5 kuwa Masele yuko safarini Dodoma pamoja na Mkurugenzi wao Khalfan Abdallah.
Wasanii wengine wa vichekesho walioshindwa kuhudhuria mazishi ya Sharo, hususan wale ambao vituo vyao vya kazi ni Dar se Salaam ni pamoja na Ze Comedy (EATV) na Orijino Komedi (TBC1).
Ukiondoa wasanii hao, karibu wasanii wote wa sanaa za maigizo sambamba na wale Bongo Fleva, walihudhuria mazishi ya kihistoia ya Sharo Milionea.Via saluti5

MAMIA WAPOTEZA FAHAMU,WASANII WAANGUA VILIO NI BAADA YA MWILI WA MAREHEMU KUWASILI NYUMBANI KWAO SIKU YA JANA.

Rafiki mkubwa wa marehemu Sharo Milionea, Mzee Majuto akielezea machache kuhusu marehemu.
                                                 (Picha hii chanzo ni Global Publishers.info)
 Mwili wa Marehemu Sharo Milionea ukiswaliwa mapema mchana huu kabla ya kupelekwa kwenye nyumba yake ya milele 
 Rafiki mkubwa wa marehemu Sharo Milionea,Mzee Majuto akiwa ameshikwa mkono wakielekea kwenye mazishi mapema mchana huu,Muheza mkoani Tanga.
Angalia picha zaidi >>> read more hapa chini....

HUYU NDO MAMA YAKE MZAZI SHAROMILIONEA AKILIA KWA UCHUNGU.

MAMA YAKE MZAZI MAREHEMU  HUSSEIN R MKIETI a.k.a SHAROMILIONEA

Wednesday, November 28, 2012

KABURI LA KANUMBA LAGEUKA KIMBILIO LA WASANII.

JANA mara baada ya kumalizika kwa mazishi ya John Stephano Maganga, baadhi ya wasanii wa filamu walikwenda ng’ambo ya pili ya makaburi kulifuata kaburi la The Great Steven Kanumba.
Katika hali iliyovuta macho ya wengi, kaburi la Kanumba ambalo liko umbali wa kama mita 100 kutoka kaburi la John Maganga, lilikuwa kimbilio la wasanii wengi huku wengine wakisema wanakwenda ‘kuhiji’ kwenye kaburi la The Great.
Miongoni mwa wasanii waliobahatika kupita kwenye kamera ya saluti5 ni pamoja na Mainda, Mzee Chilo, Pendo na Top Model wa Miss Tanzania miaka kadhaa iliyopita, Rashida Wanjara.Chanzo cha habari na Saluti5

Sumatra kusitisha huduma za daladala Jiji la Dar es Salaam.

MAMLAKA ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), itasitisha utoaji wa leseni mpya za usafirishaji wa abiria katika Jiji la Dar es Salaam kwa mmiliki mmoja mmoja kuanzia Desemba Mosi mwaka huu.
Taarifa iliyotolewa jana na Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra, Ahmad Kilima, ilisema hatua hiyo inatokana na kushauriana kati ya Sumatra, wamiliki wa Daladala, Mradi wa Mabasi yaendayo Kasi (Dart) na wadau wengine.
 
Wakati wa mkutano wa kukusanya maoni uliofanyika mwanzoni mwa mwaka 2010 ,baadhi ya wamiliki wa daladala walipinga utaratibu huo kutokana na uwezo wao kifedha kuwa mdogo wakihofia kuwa kuwaathiri.Walisema huduma ya usafirishaji kupitia kampuni, inalenga katika kuwaondoa kabisa katika biashara hiyo.

King Majuto amlilia Sharo Milionea.

KIFO cha msanii Hussein Ramadhan ‘Sharo Milionea’ kimemshutua msanii mwenzake King Majuto hadi akaanguka na kupata shinikizo la damu.

Majuto alipatwa na hali hiyo baada ya kupata taarifa za msiba huo na hadi anazungumza na gazeti hili, ingawa alikuwa na nafuu, mwili wake ulikuwa umevimba.
Akizungumza na Mwananchi Majuto alisema: “Kimeniuma sana kifo cha mwanangu Sharo.
“Nimeshirikiana naye kwa mambo mengi, nilifahamiana naye tangu mwaka 2009 tulikutana pale Vijana Production, na tangu nimefahamiana naye, kuna mambo mengi sana tumefanya,” alisema Majuto ambaye mara baada ya kupata taarifa ya kifo cha msanii huyo alipata na shinikizo la damu.

Waziri azindua ndege ya Fastjet.

NAIBU Waziri wa Uchukuzi, Charles Tizeba ameagiza Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), kuandaa mazingira mazuri na miundombinu katika Viwanja vya Mwanza na Kilimanjaro kukabiliana na ongezeko la abiria wanaotarajia kuvitumia.

Akizindua safari za ndege za Kampuni ya Fastjet Dar es Salaam jana, Tizeba alisema kuanzishwa kwa safari za ndege za bei rahisi kwa mikoa mitatu ya Dar es Salaam, Kilimanjaro na Mwanza kunatoa changamoto kwa Serikali kuboresha miundombinu kukidhi mahitaji ya ongezeko la wasafiri.

“Kuanzishwa kwa safari za ndege za bei rahisi ya Sh32,000 na Kampuni ya Fastjet kunatarajiwa kuvutia abiria wengi zaidi, hali ambayo viwanja vingi nchini vikiwamo vya Mwanza na Kilimanjaro haviwezi kutimiza mahitaji,” alisema Tizeba.

Tizeba alisema hadi sasa Serikali inaendelea kurekebisha baadhi ya viwanja vya ndege nchini, vikiwamo vya Kigoma, Tabora na Mafia huku Kiwanja cha Mwanza kikiendelea kurekebishwa sehemu ya abiria na barabara za ndege.

“TAA ihakikishe hakuna abiria atakayeshindwa kusafiri kwa sababu ya wingi wa watu na ukosefu wa miundombinu kwa kiwanja chochote cha ndege nchini,” aliagiza Tizeba.

Washukiwa wa ICC Kenya kuunda Muungano.

Washukiwa wawili wakuu wa ghasia za baada ya uchaguzi nchini Kenya, Uhuru Kenyatta na William Ruto wanajadiliana kwa lengo la kuunda muungano wa kisiasa watakaotumia kugombea uongozi wa nchi.Taarifa za awali zilisema kuwa wawili hao tayari wameunda muungano huo ingawa baadaye afisa wa mawasiliano wa vigogo hao alikana kuwepo makubaliano yoyote.

MAREHEMU SHARO MILIONEA KUZIKWA LEO JUMATANO KIJIJINI KWAO LUSANGA, LUSHOTO TANGA .

MSIBA wa msanii nyota wa uchekeshaji hapa nchini, Hussein Mkiety, maarufu kama 'Sharomilionea' umegusa hisia za wengi, huku King Majuto akikimbizwa Hospitali baada ya kushikwa na presha, hivyo kutishia usalama wake.

Mtoto wa King Majuto, Hamza Majuto, aliimbia HANDENI KWETU kuwa hali ya baba yake inaendelea vizuri kutokana na kuumizwa zaidi na msiba wa Sharomlionea anayetamba katika ulingo wa filamu na muziki hapa nchini.

Msanii huyo alikufa jana saa mbili za usiku Maguzoni, kilimita chache na kijijini kwao Lusanga, wilayani Muheza mkoani Tanga, baada ya gari lake alilokuwa akisafiria lenye namba za usajili T478 BVR Toyota Harrier kupinduka na kusababisha kifo chake.  
Kamanda wa Polisi mkoani Tanga, Constantine Masawe, alikiri kutokea kwa msiba huo na kusema kuwa mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Teule, Muheza, mkoani Tanga kwa taratibu za mazishi zinazopangwa na familia yake.

“Marehemu alikufa majira ya saa mbili za usiku kwenye barabara ya Segera alipokuwa anatoka Dar es Salaam kwenda Muheza, hivyo mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Teule, huku gari lake likihifadhiwa pia kwasababu haliwezi kutembea,” alisema Masawe.

Taarifa za kifo cha msanii huyo aliyeibukia hivi karibuni na kufanya vema katika ulingo huo zilianza kuzagaa saa tatu za usiku, ikiwa ni dakika chache baada ya kufariki katika ajali hiyo ya kusikitisha kwa nyota huyo.

PICHA 5 ZA GARI ALILO PATA NALO AJALI MAREHEMU SHARO MILIONEA

Hili ndilo gari aina ya Toyota Harrier lenye namba T278 BVR ilipinduka na kusababisha ajali iliyopelekea kifo cha msanii Sharo milionea USIKU WA JANA MIDA YA SAA MBILI USIKU.

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate