EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, August 31, 2015

UKAWA YAMTANGAZA RASMI JULIUS MTATIRO KUGOMBEA UBUNGE JIMBO LA SEGEREA

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Segerea kupitia CUF, Julius Mtatiro.
Ndugu zangu, hivi punde nimepokea simu za Hongera kutoka kwa waandishi kadhaa wa habari waliotoka kwenye mkutano wa UKAWA wa kutangaza majimbo ambayo yalikuwa hayajagawanywa. Wamenijulisha kuwa jimbo la Segerea limewekwa chini ya CUF katika nafasi ya ubunge ikiwa na maana kuwa nakuwa mwakilishi rasmi wa UKAWA katika jimbo hili.
Nimeongea na viongozi wakuu wa vyama ambao wamenithinitishia taarifa hizi na kwa hivyo naziweka hapa kama taarifa rasmi.
Nitumie fursa hii kuwashukuru wana Segerea wote ambao kwa wiki kadhaa simu zao hazikuisha kuja kwangu, wote niliwataka tusubiri maamuzi yafanywe na sasa yameshatangazwa rasmi na tutaendelea na kazi iliyobakia, kuliletea taifa mbunge wa UKAWA kutoka hapa Segerea.
Jambo moja ambalo nataka niwaahidi wanachama wa CUF na CHADEMA ni kwamba natambua mgawanyo wa kata zote 13 ulishafanywa na viongozi wa wilaya na majimbo wa vyama vyetu.
Nitasimamia utekelezaji huo na nitawanadi na kuwapigania madiwani wote wa UKAWA. Chama changu kimepewa kata 5 na CHADEMA ina kata 8, kama kuna kata yoyote imeingiliwa na diwani asiyehusika tutahakikisha anajitoa kabla ya kuisha wiki hii ili 25 Oktoba niwakabidhi madiwani 13 waliochaguliwa na wananchi.
Namshukuru sana dada Anatropia Theonest kwa kusubiri maamuzi haya kama mimi. Natambua mchango wake katika kuimarisha upinzani Segerea na namuomba aungane nami tusimamie mabadiliko haya muhimu.

SITTA AMJIBU SUMAYE KUHUSU MABEHEWA MABOVU

Waziri wa Uchukuzi, Samwel Sitta, akizungumza na wanahabari (hawapo pichani).
Sitta akisisitiza jambo.
Wanahabari wakichukua matukio katika hafla hiyo.
Wanahabari wakifuatilia tukio.
WAZIRI wa Uchukuzi, Samwel Sitta, amemjibu Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye, baada ya kuituhumu serikali ya Rais Kikwete kuwa imewafumbia macho watendaji walioisababishia hasara nchi zaidi shilingi bilioni 220 kwenye ununuzi wa mabehewa yanayotajwa kuwa ni feki.
Akizungumza na wanahabari kwenye ofisi za wizara yake, Sitta amesema watendaji wote waliohusika na kashfa hizo watafikishwa mahakamani muda wowote kutoka sasa baada uchunguzi kukamilika.

WATUMIAJI WA MITANDAO VIBAYA SHERIA KUWADHIBITI KUANZA LEO SAA 6:00 USIKU


 Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dares Salaam leo.
Baadhi ya waandishi wa habari wakiwa kazini jijini Dar es Salaam leo.

Na Magreth Kinabo 
SHERIA mpya   ya Makosa ya Mtandao ya mwaka   2015 na Sheria ya Miamala ya Kielektroniki ya mwaka 2015 zitaanza kutumika rasmi kesho Septemba Mosi mwaka huu, hivyo watumiaji   na watoa huduma waaswa kuzingatia sheria hizi ili kuepuka mkondo wa sheria.

 Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Profesa Makame Mbarawa wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dares Salaam kwenye ukumbi wa mikutano wa wizara hiyo.

“Sheria hizi ni nzuri zitaanza kutumika Septemba Mosi mwaka huu,kuanzia saa 6.00 usiku . zina maslahi katika nchi yetu. Ninatoa wito kwa wananchi kuzingatia matumizi salama ya mtandao kwa manufaa yako na maendeleo ya Taifa letu,” alisema Profesa Mbarawa.

 Aliongeza kuwa sheria hiyo ya makosa ya mtandao ya mwaka 2015 hazihitaji utungaji wa kanuni kwa kuwa iko wazi.

 Alisema tayari wizara imeanza kuelimisha watu kuhusu sheria hiyo na itendelea kuwajengea uwezo wadau mbalimbali.

Profesa Mbarawa alisema sheria ya makosa ya mtando ya mwaka 2015 na Tanzania sio nchi ya kwanza kuwa nayo, bali nchi mbalimbali zina sheria kama hiyo ,ambapo alitolea mfano Uingereza,India,Malaysia, Uganda na Korea ya Kusini.

 Akizungumzia kuhusu  madai sheria hiyo kuhusika na suala la Uchaguzi Mkuu, alisema si kweli, bali imekamilika katika kipindi hicho ndio maana baadhi ya watu wanadai hivyo.Aliongeza kwamba sheria hiyo imetunga ili kudhibiti matumizi ambayo  si mazuri. 

“ Mtu akitumiwa ujumbe akiupokea hapaswi kuisambaza  kwani atakapousambaza atakuwa na amefanya kosa,”alisisitiza.

Aliyataja baadhi ya makosa kuwa ni usiri, usalama wa upatikanaji wa taarifa za kompyuta na mifumo  kama vilekuingilia mawasiliano ya kompyuta au mifumo ya kompyuta kinyume cha sheria na wizi wa taarifa kimtandao.

Makosa  dhidi ya kompyuta ikiwa ni pamoja na,udanganyifu kwa kutumia kompyuta,kugushi kwa kutumia kompyuta wizi wa utambulisho wa mtu binafsi  mtandaoni, matumizi ya vifaa kinyume cha sheria.

Makosa yanayohusiana kimaudhui kama vile usambazaji wa ponografia, ponografia za watoto makosa dhidi ya ubaguzi wa rangi na chuki, michezo ya kmari mtanadaoni kiunyume cha sheria, kashfa na habari za uongo na makosa dhidi ya haki na hati miliki.

Pia inatambua muungano wa makosa inajumuisha kama vile utakatishaji wa fedha haramu na ugaidi kwa kutumia mtandao.

Kwa upande wa sheria ya miamala ya kieletroniki ya mwaka 2015, baadhi ya makosa likiwemo la wajibu wa watoa huduma kwa walaji, bidhaa ,huduma au mawasiliano ambayo hayajaombwa na uhalali wa Muamala wa elektroniki.

Aliongeza kuwa kanuni za sheria hiyo zinatayarishwa zikiwa tayari zitangazwa  na zitaanza kutumika wakati wowote.

DK AZIDI KUWACHANGANYA WAPINZANI KAMPENI ZA URAIS NJOMBE

 Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk John Magufuli akihutubia katika mkutano wa hadhara wa kampeni kwenye Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe
Makamu Mwenyekiti wa CCM, Tanzania Bara, Philip Mangula akihutubia kwa kumnadi Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk John Magufuli  katika mkutano wa hadhara wa kampeni kwenye Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe

 Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk John Magufuli akimtambulisha Naibu Waziri wa Ujenzi, ambaye anagombea ubunge Jimbo la Njombe Kaskazini, Gerson Lwenge katika mkutano wa hadhara wa kampeni wilayani Wanging'ombe, mkoani Njombe
 Msanii wa muziki wa kizazi kipya  Shilole akitumbuiza leo kwenye mkutano wa kumnadi Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM kwenye Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe.
Dk Magufuli akitoa shukrani kwa viongozi wa CCM Mkoa wa Mbeya baada ya kumaliza ziara mkoani humo  na kuanza kampeni katika Mkoa wa Njombe
  Dk.Magufuli akijinadi kwa wananchi na kutoa ahadi  katika nKijiji cha Igoma, Mbeya Vijijini aliposimama kwa muda akielekea Makete mkoani Njombe kuendelea na kampeni.  Akichaguliwa ameahidi kujenga barabara  ya lami ya Njombe hadi Mbeya kuptia Makete na kijijini hapo. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Wananchi wakishangilia baada ya kuelezwa na Dk Magufuli kuhusu ijenzi wa barabara ya lami itakayopita kijijini hapo
 Wananchi wakimshangilia Dk Magufuli kijijini hapo
 Dk Magufuli akijinadi katika Kijiji cha Ilungu Mbeya Vijijini mpakani na Mkoa wa Njombe
 Wananchi wakishangilia huku wakiwa na vipeperushi vyenye picha za Dk Magufuli
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), ambaye pia alikuwa Mbunge wa Jimbo la Makete,  Binilith Mahenge akimpigia debe Dk Magufuli pamoja na Mgombea ubunge wa Jimbo la Makete, Norman Sigalla.
 Dk. Magufuli akijinadi kwa wananchi katika mkutano uliofanyika Iwawa wilayani Makete
 Dk Magufuli akimtambulisha mgombea ubunge jimbo la Makete, Dk Norman Sigalla katika mkutano wa kampeni uliofanyika Iwawa Makete
 Mwenyekiti wa Shirikisho la Vyama vya Wenye Ulemavu nchini, Amon Mpanju akimpigia debe Dk Magufuli eneo la Iwawa wilayani Makete
 Wananchi wakimsikiliza kwa makini Dk Magufuli mjini Makete
 Dk Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafuasi wa vyama vya upinzania waliovihama vyama vyao na kujiunga na CCM katika mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika  Iwawa, Makete leo.PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG

 Mmoja wa wafuasi wa Chadema akiwa amesamama karibu na pikipiki yenye bendera ya chama hicho huku akimsikiliza kwa makini Dk Magufuli akijinadi katika Kijiji cha Kenja, wilayani Makete leo.
 Mfuasi wa Chadema (kulia) akishangilia baada ya kumsikia Dk Magufuli akitangaza kwamba akichaguliwa kuwa urais watoto watakuwa nasoma bure kuanzia darasa  la kwanza hadi kidato cha nne. Kutano huo ulifanyika katika Kijiji cha Kenja wilayani Makete baada ya msafara kuzuiwa wananchi katika eneo hilo wakiwa na hamu ya kusikiliza sera zake.
 Baadhi ya wananchi katika Kijiji cha Kenja wakimsikiliza Dk Magufuli huku wakiwa na mabango yenye picha za mgombea huyo wa urais wa CCM
 Dk Magufuli akisisitiza jambo katika mkutano uliofanyika katika Kijiji cha Kenja wilayani Makete
 Mjumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya CCM,  William Lukuvi akizungumza na Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Philip Mangula katika mkutano wa kampeni wilayani Wangi ng'ombe, Mkoa wa Njombe leo
 Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Pindi Chana akihutubia katika kutano wa kampeni wa kumnadi Dk Magufuli wilayani Wanging'ombe mkoani Njombe leo

 Makamu Mwenyekiti wa CCM, Tanzania Bara, Philip Mangula akisalimiana na Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk John Magufuli katika mkutano wa hadhara wa kampeni wilayani Wanging'ombe, mkoani Njombe
 Wananchi wa Kijiji cha Igagala wakiwa na mabango yenye ujumbe mbalimbali walipokuwa wakimlaki Dk Magufuli, wilayani Wanging'ombe, Njombe
 Dk Magufuli akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Igagala, wilayani Wanging'ombe
 Wananchi wakiwa katika mkutano wa kampeni wa CCM mjini Njombe
Msanii Cgegge akitumbuiza katika mkutano wa kampeni za CCM kwenye Uwanja wa Sabasaba mjini Njombe leo

Saturday, August 29, 2015

Mkopo noma! Mfanyabiashara atupiwa vitu nje, Nyumba yauzwa!

DSC_0594
Mfanyabiashara maarufu, Mohamed Majid Seif akitaharuki.
Boniphace ngumije
Mkopo noma! Mfanyabiashara maarufu, Mohamed Majid Seif, mkazi wa Mikocheni A, Kinondoni jijini Dar, ametolewa vitu ndani ya nyumba yake namba A35/210 baada ya kushindwa kulipa mkopo wa Sh. Milioni 210 aliouchukua kwenye Benki ya Boa (Bank Of Africa) mwaka 2011.
Kwa mujibu wa shuhuda wetu, katika tukio hilo lililojiri nyumbani hapo, Seif alikopa kiasi hicho cha fedha akiwa na wenzake, lakini baada ya kushindwa kulipa kwa muda wa miaka miwili kama makubaliano yalivyoonesha, wenzake waliingia mitini na kumuachia msala.
DSC_0486
Vyombo vikipakizwa kwenye gari.
Ilidaiwa kwamba, baada ya Seif kuachiwa msala huo, aliiomba Boa kumuongezea muda ili aweze ‘kuklia’ deni hilo lakini benki haikuwa tayari kutokana na makubaliano waliyoweka Aprili 18, 2011 kuwa zikizidi siku sitini (60) kwenye muda wa makubaliano ya mkopo, bila kulipwa kwa fedha hizo pamoja na riba nyumba iuzwe.
“Baada ya makubaliano kushindikana, benki hiyo ilitangaza kuipiga mnada nyumba hiyo kupitia magazeti ya kila siku ambapo siku ya mnada, ilinunuliwa na Mwanaiba Mohamed Mzee, mkazi wa hapohapo Mikocheni kwa Sh. Milioni 56,” kilisema chanzo hicho.
DSC_0499‘Ubuyu’ uliendelea kudondoshwa kuwa, Seif hakuridhishwa na uamuzi huo uliochukuliwa na benki hiyo, jambo lililomfanya kukimbilia kwenye Mahakama ya Ardhi na Makazi, Kinondoni kuomba kutenguliwa kwa mnada huo.

Friday, August 28, 2015

LIONEL MESSI MCHEZAJI ULAYA

2BB6AC0D00000578-3213173-image-a-3_1440697335072

Mchezaji Bora wa Ligi ya Mabingwa Ulaya,  Lionel Messi.

MONACO, Ufaransa LIONEL Messi ametangazwa kuwa Mchezaji Bora wa Ligi ya Mabingwa Ulaya na kumpiku Cristiano Ronaldo katika tuzo zilizotolewa jana ambazo pia dunia ilishuhudia Manchester United ikirejea kwenye michuano hiyo hatua ya makundi. Messi, staa wa Barcelona, aliingia hatua ya fainali ya tuzo hizo pamoja na straika wa timu yake, Luis Suarez pamoja na Ronaldo wa Real Madrid, ambapo waandishi wa habari wa michezo ndiyo waliompigia kura.

Upande wa Man United ambao ni mabingwa wa michuano hiyo mwaka 2008, wamepangwa katika kundi ambalo linaonekana kuwa jepesi kwao ambapo wapo Kundi B wakiwa pamoja na PSV Eindhoven ya Uholanzi, CSKA Moscow (Urusi) na Wolfsburg (Ujerumani).

2BB6988800000578-3213173-image-a-31_1440696152306

Lionel Messi (kushoto)akipokea tuzo ya mchezaji Bora wa Ligi ya Mabingwa Ulaya kutoka kwa Michel Platini (kulia) na Cristiano Ronaldo akiwa kwa nyuma.

Vijana wa Kocha Arsene Wenger, Arsenal, wamepangwa Kundi F wakiwa pamoja na vigogo wenzao, Bayern Munich ya Ujerumani pamoja na Olympiacos (Ugiriki) na Dinamo Zagreb (Croatia). Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho atakutana na timu yake ya zamani ya FC Porto katika Kundi G, ambapo wapo pamoja na timu za Dynamo Kyiv na Maccabi Tel Aviv. Ratiba kamili na jinsi makundi yalivyopangwa soma ukurasa wa 24.

Thursday, August 27, 2015

MSHINDI WA TMT 2015 MPAKAKIELEWEKE APOKELEWA KWA NDEREMO MJINI MOSHI‏

Baadhi ya ndugu, jamaa na marafiki wa Mshindi wa Shindano la TMT 2015 #mpakakieleweke Dennis Lwasai wakiwa na bango linalomwelezea mahindi huyo wakati walipojitokeza kumpokea wakati akirejea nyumbani kwao Mambogini Moshi
 
Mshindi wa TMT 2015 #mpakakieleweke Dennis Lwasai akiwasalimia wakazi wa mji wa Moshi waliokuwa wakimpongeza wakati akirejea kwao Mambo
 Wakiendelea kumpongeza

Lulu amhenyesha Mboto ukumbini

IMG_1826
Haji Salum ‘Mboto akisaidia kulibeba gauni la Lulu.
DIVA wa filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’ hivi karibuni amemhenyesha staa mwenzake wa filamu, Haji Salum ‘Mboto’ baada ya kumpa kibarua cha kulishika gauni lake lisiguse chini.
Tukio hilo lilitokea kwenye fainali ya shindano la kusaka vipaji vya kuigiza lijulikanalo kama Tanzania Movie Talents (TMT 2015) iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa, Posta jijini Dar ambapo Lulu na Mboto walikuwa washehereshaji.
IMG_1779Katika hali iliyoonesha Lulu alikuwa ‘siriaz’ stejini alimsisitizia Mboto kila mara ahakikishe amelishika gauni lake vizuri na asiliachie.
“Mboto hapa kazi yako ni kulishika gauni langu kwa nyuma kila nitakapokuwa nawe na ole wako uliachie,” alisikika Lulu ambapo Mboto alitekeleza ombi la Lulu.

Waandishi 2 wauawa wakiwa hewani Marekani

 
Waandishi wawili wa habari wamepigwa risasi katika jimbo la Marekani la Virginia wakati wakifanya mahojiano ya moja kwa moja ya runinga.
Kanda ya video inaonyesha mwandishi wa habari wa kike akimtania mgeni aliyekua akimuhoji kabla ya risasi kufyatuliwa mara nane.
Mwandishi huyo anaonekana akiruka na kamera kuanguka sakafuni huku mwanamume aliyevalia nguo nyeusi na kubeba bunduki akipita karibu.
Kituo kilichoajiri waandishi hao cha WDBJ kinasema mwandishi huyo wa habari Alison Parker na mpiga picha Adam Ward walikufa katika tukio hilo .
Polisi wanasema mshukiwa hajulikani aliko.

Siri 4 matusi ya Diamond kwa Diva


diva
Loveness Malinzi ‘Diva’
NI mtifuano! Agosti 24, mwaka huu ilikuwa siku mbaya kwa nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ au baba Tiffah na mtangazaji anayekimbiza kwa sauti tamu hewani, Loveness Malinzi ‘Diva’ kufuatia kupishana lugha ndani ya studio za redio na hivyo, Diamond kumvurumishia matusi mwenzake.
Kupishana kauli huko kuliashiria kuwepo kwa uhasama wa siku nyingi kwa wawili hao huku kila mmoja akiwa anaamini mwenzake ana makosa na ndipo siri tano za Diamond kumtusi Diva zikajulikana.
MCHEZO ULIVYOANZA
Siku hiyo majira ya saa 9:00 alasiri, Diamond alitia timu kwenye studio za redio hiyo zilizopo Mikocheni, Dar kwa lengo la kumtambulisha msanii wake mpya kutoka studio yake ya Wasafi Records iliyopo Sinza-Mapambano, Dar.Mwanyeji wa Diamond alikuwa mtangazaji Hamis Mandi ‘B12’. Lakini ndani ya studio hiyo alikuwepo Diva.
platnumz
Nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ au baba Tiffah.
ALIANZA DIAMOND
Kabla Diamond hajaanza kumtambulisha msanii wake, alianza na Diva kwa kumsema kwamba amekuwa akimchoresha mitandaoni kwa kumchafua.
DIVA AKAJIBU
Diva alijibu kuwa, kisa cha yeye kumchoresha, aliwahi kumuita Diamond kwenye Kipindi cha Ala za Roho lakini staa huyo hakutokea wakati meneja wake, Salam alimpa taarifa, akakubali na yeye Diva akaanza kutangaza mitandaoni kuwa, siku moja atakuwa na Diamond hewani jambo lilimfanya wasikilizaji wake kusema aliwaongopea na wengine kuanza kumtusi mitandaoni.
DIAMOND ACHAFUA HALI YA HEWA
Baada ya maneno hayo ya Diva, ndipo Diamond apoonesha dalili ya kukasirika na kutoa lugha ya matusi ambayo haiandikiki gazetini lakini akimaanisha kuwa, kama Diva angewahi kuwa mpenzi wake, angemheshimu.
MANENO BILA MPANGILIO
Diva naye alijimjia juu Diamond kwa kumwambia kuwa, hana hadhi ya yeye kuwa mpenzi wake, maneno ambayo yalimchefua baba Tiffah na kuanza kutupiana maneno bila utaratibu hali iliyomlazimisha B12 kuingiza matangazo ili kuwatoa hewani wawili hao.
Baada ya sitofahamu hiyo, Amani lilichimba na kubahatika kuibuka na siri nne (4) zilizomfanya Diamond kumtukana Diva.
SIRI YA KWANZA
Kwanza inadaiwa kuwa, meseji za Diva kwenye mitandao kumsema Diamond kwa kitendo chake cha kutotokea kwenye Kipindi cha Ala za Roho zilimfanya mzazi mwezake, Diamond, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kumbana baba wa mtoto wake huyo akimtaka aseme ukweli kama kuna siri iliyofichika kati yao
“Diamond amekuwa akimkatalia Zari kuwa, hakuna siri wala uhusiano wake na Diva. Kwenye kipindi hicho kama Diamond angekwenda, ilikuwa aongozane na Zari maana alikuwa hajajifungua. Diamond akawa anamwona Diva kama ana lengo la kuvuruga mapenzi yao.
SIRI YA PILI
“Kitendo cha Diva kutumia mitandao kumshambulia, Diamond alikiweka moyoni na kuahidi siku wakikutana laivu atampasulia ya moyoni mwake liwalo na liwe. Hata alipokwenda studio jana (Jumatatu), hakujua kama angekutana na Diva.”
SIRI YA TATU
“Diamond aliamini kuwa, Diva kumshambulia mitandaoni alilenga kumshushia heshima mbele ya jamii ili kumuua kisanii. Maana yeye mwenyewe alisema anaamini maneno ya Diva kwenye mitandao kuna zaidi ya kitendo chake cha kutotokea studio,” kilidai chanzo chetu.
SIRI YA NNE
Kwa upande wake, Diamond alipozungumza na Amani alianika siri ya nne akisema:
“Yule Diva dizaini f’lani kama ananitaka vile lakini mimi simpi nafasi ndiyo maana anatengeneza bifu na mimi.”
DIAMOND ANAENDELEA
“Diva amekuwa akinisema mara kwa mara. Mimi nilikwenda pale kwa lengo lingine, yeye akaanza kuleta zake za kuleta. Kila nikiitafuta sababu siioni. Sijawahi kumkosea popote pale.”
DIVA TAYARI KWA MWANASHERIA WAKE
Amani lilimtafuta Diva juzi kwa lengo la kumsikia anasemaje kuhusiana na sakata hilo ambapo alisema:
“Hii ishu iko kwa wanasheria wangu (tayari kwa kumpeleka Diamond mahakamani). Amenidhalilisha sana kama mwanamke nisiyefaa katika jamii. Ushahidi upo kila kona kwenye mitandao.”
ATISHIWA KUPIGWA, MAISHA
“Akaenda mbali zaidi na kutaka kunipiga maana lugha ya matusi haikutosha. Amenitishia maisha jambo ambalo halitakiwi kisheria. Hakuna aliye juu ya sheria. Sitazungumza zaidi.”
Imeandaliwa na Musa Mateja na Nyemo Chilongani.

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate