EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Saturday, February 28, 2015

UNDANI WA KIFO CHA KEPTENI JOHN KOMBA!

Marehemu Kapteni Komba.
Picha ya kwanza ya Marehemu komba mara baada ya kufariki dunia.
...Komba enzi za uhai wake.
MBUNGE wa Mbinga Magharibi, Kapten John Komba amefariki dunia jioni hii jijini Dar es Salaam.
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye amethibitisha kutokea kwa kifo hicho, hata hivyo hakuwa tayari kuelezea kwa undani kwa madai kuwa taarifa hizo zimemfikia sasa hivi.
Mmoja wa watoto wa Komba ambaye aliyejitambulisha kwa jina la Herman amethibitisha kutokea kwa msiba huo na akasema, huku akilia, msiba wa baba yake upo nyumbani kwake Mbezi Tangi Bovu, Dar.
Habari zinasema asubuhi ya leo Komba alikwenda kwenye shughuli zake za kikazi kama kawaida lakini baadaye akajisikia vibaya, hivyo akaamua kurudi nyumbani ambako alizidiwa ndipo familia yake ilipoamua kumkimbiza Hospitali ya TMJ lakini alipopimwa na madaktari ikathibitika kuwa alikuwa tayari ameaga dunia. habari zaidi zinasema kuwa hivi sasa mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Jeshi ya Lugalo.
Kapteni Komba ambaye pia ni Mkurugugenzi wa Kikundi cha Maigizo cha Tanzania One Theatre (TOT),  ambacho kina kikundi cha taarabu na bendi  inayokwenda na mtindo wa Achimenengule, amekuwa akikisaidia sana chama chake, Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika kampeni zake wakati wa uchaguzi kwa kutunga nyimbo za kuhamasisha wapiga kura na kushiriki kupiga live kwenye majukwaa ya kisiasa.

Friday, February 27, 2015

SKENDO! LULU, WOLPER WAONESHANA JEURI YA MABWANA!


Stori Musa Mateja/Ijumaa
Sakata la kupangishiwa nyumba za kifahari na wanaume linazidi kuchukua sura mpya kwa mastaa wa kike ndani ya tasnia ya sinema za Kibongo ambapo safari hii mastaa wawili, Elizabeth Michael ‘Lulu’ na Jacqueline Walper ‘ Wolper’ Massawe wanadaiwa kuoneshana jeuri ya mabwana wakipima ni yupi mwenye mshiko zaidi huku akina Wema Isaac Sepetu na Kajala Masanja ambao awali walikuwa juu wakipotezwa.
Staa katika tasnia ya filamu Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’.
TAMBO ZA NANI ZAIDI?
Uchunguzi wa Ijumaa umebaini kwamba, kumekuwa na kasumba ya baadhi ya mastaa hao kutambiana kuwa ni nani zaidi anayemiliki bwana mwenye mawe au mshiko kuliko wengine.
Ilidaiwa kwamba, baada ya Lulu kuripotiwa kupangishiwa bonge la jumba la kifahari na milionea maarufu wa jijini Arusha lililopo maeneo ya Mbezi-Beach jijini Dar, Wolper naye anadaiwa kujibu mapigo kwa kupangishiwa mjengo wa maana na bwana’ke uliopo maeneo hayohayo.
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu ambavyo ni watu wa karibu wa mastaa hao, kwa sasa wawili hao ni moto wa kuotea mbali kwani kila mmoja amepata bwana mwenye ‘mpunga’ mrefu.
WOTE WANALIPA SH. MIL. 30
Ilidaiwa kwamba, kama ilivyokuwa kwa Lulu, Wolper naye analipiwa nyumba hiyo kiasi cha dola za Kimarekani 1,500 kwa mwezi (zaidi ya Sh. milioni 2.4) karibia Sh. milioni 30 kwa mwaka.
Staa katika tasnia ya filamu Bongo, Jacqueline Walper.
CHUMBA KAMA BOUTIQUE
Habari zilidai kwamba, kama ilivyo ya Lulu, nyumba hiyo aliyopangishiwa Wolper ina vyumba kibao vya kulala, ukumbi wa wageni, sehemu ya kulia chakula, mabafu, majiko n.k.
Pia nje ya nyumba hiyo kuna eneo kubwa la bustani iliyopambwa kwa maua mazuri na eneo la kutosha la maegesho ya magari.

UCHAGUZI MKUU 2015 WASANII BONGO WANAUZUNGUMZIAJE?

Laurent Samatta
Habari ya mjini kwa sasa ni Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani unaotarajiwa kufanyika Oktoba, 2015 ambapo Watanzania wote watatumia haki yao ya msingi ya kupiga kura, kuwachagua viongozi wanaowataka.
Showbiz Plus imewatafuta wasanii wa tasnia tofauti Bongo na kuwauliza mtazamo wao juu ya uchaguzi huo na hali ya upepo wa kisiasa Bongo ambapo wamefunguka kama ifuatavyo:
MRISHO MPOTO ‘MJOMBA’
 Mkali huyu wa kughani na tungo za Kiswahili, yeye amefunguka:
“Kwanza kabisa uchaguzi umegawanyika sehemu mbili, kuna viongozi ambao wanahitaji madaraka na kuna wengine wanahitaji kufanya biashara.
“Vilevile hata wapiga kura nao wapo wanaojiandaa kufanya biashara kwa kujua kwamba wakimpigia kura kiongozi fulani, watanufaika na kitu fulani, tofauti na zamani ambapo utii na nidhamu kwa viongozi na wapiga kura ulikuwa mkubwa.“Sasa hivi hata wasanii nao wanafanya biashara kwa kutazama mgombea gani ana fedha ndiyo wanaenda kumfanyia kampeni, kwa hali hii tutegemee kuwa uchaguzi utakuwa wa kibiashara na si kutafuta kiongozi bora kwa taifa.”
EMMANUEL ELIBARIKI ‘NAY WA MITEGO’
Msanii huyu wa Bongo Fleva ameeleza mtazamo wake kuelekea uchaguzi mkuu:
“Uchaguzi wa mwaka huu unaweza kuwa mgumu sana kwa sababu watu wameelimika tofauti na zamani ambapo watu walikuwa wanafanya mambo bila kujielewa. Vijana na watu wengine wameelimika na kujua kiongozi gani anafaa na nani hafai.“Ule ujanja wa kusema baadhi ya vyama vitaiba kura nadhani hilo litakuwa gumu sana mwaka huu kwani kila mtu anapiga kura akiwa anajua haki zake za msingi.”
KHADIJA KOPA ‘MALKIA’
Malkia huyu wa mipasho, ambaye pia ana uelewa mkubwa kwenye mambo yanayohusu siasa alisema: “Kwa kweli mi naona mwaka huu utakuwa mzuri kwa upande wa wanawake kwa sababu katiba inayopendekezwa ikipitishwa kutakuwa na usawa katika kila nafasi ya uongozi kati ya wanaume na wanawake.
BABY MADAHA.
“Nawasihi wanawake kama wapo wanaoweza kuongoza nafasi mbalimbali wajitokeze kupigania nafasi hizo kuanzia urais, ubunge mpaka udiwani. Naamini tutaweza kufika mahali ambapo na sisi tutajivunia kuwa na viongozi wengi wanawake.”

MKE WA MTU ANASWA AKIZINI KWENYE GARI

Waandishi wetu, Mwanza/Ijumaa
BIASHARA ya kuuza miili imezidi kushamiri katika viunga vya Jiji la Mwanza na mwanzoni mwa wiki hii Kitengo Maalum cha Oparesheni Fichua Maovu (OFM) cha Global Publishers, kilifanya zoezi lingine kubwa baada ya kumnasa mwanamke mmoja akifanya mapenzi ndani ya gari katika eneo la Kirumba, Ijumaa lina data kamili.

Mwanamke huyo anayedaiwa kuwa ni mke wa mtu.
Baada ya kutajiwa maeneo yanayosifika kwa biashara hiyo maarufu kama uchangudoa, OFM ambao juzikati walilifumua danguro lililopo maeneo ya Liberty jijini hapa, Jumanne wiki hii lilifanya matembezi katika eneo hilo ili kubaini jinsi biashara hiyo haramu inavyofanyika.

TOP TEN YA MASTAA KUVAA NUSU UTUPU SIYO ISHU KWAO!

MAKALA: AMRAN KAIMA/Ijumaa
Ukifuatilia sana kwenye nchi za wenzetu kama vile Marekani na kwingineko, mastaa hawako makini na suala la uvaaji. Yaani si ajabu kuona staa mkubwa akikatiza mtaani akiwa amevaa nguo ya ndani na ukishangaa utaonekana mshamba.
Jokate Mwegelo.
Wanaovaa hivyo hawajakosa nguo za heshima za kuvaa bali ni ule ulimbukeni wa kutaka wawe gumzo na kuendelea kuwa maarufu.Kutokana na athari ya utandawazi, hapa Bongo wapo mastaa ambao nao wameiga kiasi cha kutoona aibu kuvaa nguo zinazoacha wazi maungo yao.Najua wapo wengi lakini leo nimeona nikupe kumi bora ya mastaa hao.

TIKO: NATAKA MTOTO WA PILI, WA KUNIPA MIMBA SINA

Na Hamida Hassan/Ijumaa
Staa wa filamu za Kibongo, Tiko Hassan amesema kuwa anatamani kupata mtoto wa pili kwa sababu mtoto wake wa kwanza amefikisha miaka 10, tatizo hana wa kuzaa naye.
Staa wa filamu za Kibongo, Tiko Hassan.
Akipiga stori na Ijumaa Tiko alisema yeye ni ‘mgonjwa’ wa watoto wachanga na anahisi sasa ni muda muafaka ila tatizo mwanaume aliyenaye hana mpango wa kupata mtoto.
“Yaani acha tu, mpenzi niliyenaye naona kama hajajiandaa maana hata nikiongelea ishu ya kubeba mimba, naona ananipotezea lakini kiukweli nahitaji mtoto wa pili,” alisema Tiko.

NISAMEHE: HAKYANANI, NENO HILI LITAMWINGIZA LOWASSA IKULU


CHANZO: UWAZI MIZENGWE
KIPYENGA! Mpambano wa kuteuliwa na hatimaye kupeperusha bendera ya Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Uchaguzi Mkuu Oktoba, mwaka huu kuwania urais unazidi kushamiri huku jina la waziri mkuu wa zamani, Edward Lowassa ‘EL’ likiongoza kutajwa midomoni mwa Watanzania.
Imebainika kuwa pamoja na  kelele nyingi zinazosikika mitaani za “Lowassa! Lowassa!” bado hazitoshi kumwingiza madarakani, kama Rais Kikwete hatamwona anafaa kuwa mrithi wake.
Lowassa alikuwa mmoja wa wanamtandao waliofanikisha kuingia ikulu kwa Rais Jakaya Kikwete ‘JK’ katika uchaguzi wa mwaka 2005. Baada ya JK kuingia ikulu,  Lowassa aliteuliwa kuwa waziri mkuu wa serikali ya awamu ya nne hadi alipojiuzulu, Februari 2008 kufuatia tuhuma za kashfa ya mkataba tata wa Kampuni ya Kufua Umeme ya Richmond.
Rais Jakaya Kikwete ‘JK’.
WANAMTANDAO WENGINE
Mbali na Lowassa, wanamtandao wengine waliofanikisha JK kuingia ‘magogoni’ ni Bernard Membe, Emmanuel Nchimbi, Abdulahman Kinana na Rostam Aziz.
Kwa utaratibu usio rasmi wa mitandao ya kisiasa duniani, Rais Kikwete baada ya kumaliza muhula wake wa miaka kumi anatakiwa kumrithisha kiti mmoja kati ya wanamtandao waliopigana kufa na kupona kumwingiza madarakani.

MAIMARTHA AFUNGUKIA MAMBO YA CHUMBANI ZAIDI


Wiki hii kupitia safu hii tunaye Maimartha Jesse ‘Mai’ ambaye ni mtangazaji na mjasiriamali. Mwandishi wetu Hamida Hassan alimbana kwa maswali 10 mengi yakiwa yanahusu mambo ya chumbani zaidi, ungana naye…
Mtangazaji na mjasiriamali Maimartha Jesse ‘Mai’.
TQ: Ni chakula gani kizuri ambacho ukimpikia mumeo anasikia raha?
Mai: Mume wangu ni mpenzi sana wa wali samaki au ugali samaki, sambamba na vikorombwezo vingine.
TQ: Ukiwa sebuleni na mumeo mkiangalia vipindi mbalimbali vya televisheni ni mavazi gani unavaa na mapozi gani mnakaa?

Wednesday, February 25, 2015

STRESS HAZIPUNGUZWI KWA KUCHEPUKA!

LABDA haijawahi kukukuta, lakini maisha tunayoishi katika wakati wa sasa yanasababisha watu wengi wanapatwa na msongo wa mawazo, maarufu kama stress. Hali ni mbaya kwa wafanyakazi wenye mabosi wakorofi na hata wafanyabiashara wanaoyumba kiuchumi.
Lakini inakuwa mbaya zaidi mambo yanapoharibika ndani ya familia, kwa maana ya wanandoa au walio katika uhusiano wa kimapenzi. Ingawa sina takwimu kamili, lakini uzoefu unaonyesha tafrani katika ndoa zinasababisha watu wengi sana kuchanganyikiwa na hata kusababisha kukosa amani ndani ya mioyo yao.
Na siyo kukosa amani na kuchanganyikiwa tu, wengi pia wamepoteza maisha baada ya kushindwa kuhimili mikanganyiko iliyotokea. Mtu anaona mwenzake anakwenda ndivyo sivyo katika uhusiano wake anaamua kujimaliza mwenyewe, achilia mbali wanaoamua kujimaliza wote ili kila mmoja akose.

MONALISA, BANANA WAPATA AJALI KAZINI

MASTAA wa filamu ya Daddy’s Wedding, Yvone Sheryl ‘Monalisa’, Banana Zoro, Sandra, Mama Abdul na wenzao hivi karibuni walipata ajali walipokuwa kwenye maandalizi ya filamu hiyo kwenye mbuga ya Saadani.
Staa wa filamu ya Daddy’s Wedding, Yvone Sheryl ‘Monalisa’.
Ajali hiyo ilitokea katika daraja moja dogo mbugani hapo ambapo walikusanyika kwa ajili ya kushuti mojawapo ya vipande vya filamu hiyo mpya, lakini likaporomoka na kuwafanya baadhi yao kuumia na wengine kupata mshtuko mkubwa.

THEA: NIMEEPUKA MAJUNGU!

MSANII mkongwe katika filamu Bongo, Salome Urassa ‘Thea’ amefunguka na kusema kwamba kwa sasa amebadili aina ya maisha yake kwa kuwaepuka marafiki wanafiki aliokuwa akikutana nao kwenye makundi ya majungu.
Msanii mkongwe katika filamu Bongo, Salome Urassa ‘Thea’.
Akipiga stori mbili tatu na gazeti hili hivi karibuni, Thea alisema siku hizi hata akienda location anafanya kile kilichompeleka  na baada ya hapo anarudi nyumbani mapema ili kumuwahi mumewe.
“Siku hizi nikienda location nafanya kilichonipeleka, nabadilisha nguo narudi nyumbani kwangu maana sipendi sana kukaa kwenye vikao yaani makundi maana ndiyo mwanzo wa manenomaneno na majungu hivyo nayaepuka, kwani hayanisaidii pia nimepunguza marafiki maana mimi ni mke wa mtu,” alisema Thea.

NDOA YA SLIM YAVUNJWA MAHAKAMANI

IMELDA MTEMA/Mchanganyiko
NDOA ya staa wa filamu nchini, Salim Mbegu ‘Slim’ na mkewe Asia Morgan imevunjwa rasmi na Mahakama ya Mwanzo ya Magomeni jijini Dar kufuatia mgogoro wa muda mrefu.
Aliyekuwa mke wa staa wa filamu nchini, Salim Mbegu ‘Slim’, Asia Morgan akiwa katika pozi.
“Mahakama hii imevunja baada ya mdai (mke) kusema hata iweje hawezi kurudi tena kwa mumewe huyo kutokana na kuwa na wivu wa kupindukia na kingine kibaya walivyokuwa kwenye mgogoro kuna

WASTARA AZIMIA KISA MAPENZI

Waandishi wetu/Mchanganyiko
DIVA wa filamu nchini, Wastara Juma ambaye kwa sasa anaripotiwa kuwa katika mapenzi na mwigizaji mwenzake, Bond Bin Suleiman anadaiwa kupoteza fahamu mara tu baada ya kupewa taarifa kuwa mpenziwe huyo amepata mtoto wa nne kwa mwanamke mwingine, Risasi Mchanganyiko linakupa stori kamili.
DIVA wa filamu nchini, Wastara Juma akiwa hospitali baada ya kuzimia.
TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo makini, Wastara alipenyezewa ubuyu na mpenzi wa zamani wa Bond, Lulu Semagongo ‘Aunty Lulu’ na kuambiwa kwamba asijishebedue kwani Bond ana mwanamke mwingine ambaye amejifungua mtoto wa nne hivi karibuni.
“Tunakushangaa unavyojinadi kuwa Bond ni wako na kumpa zawadi ya keki ya bethidei wakati mwenzako amezaa na mwanamke mmoja baamedi hivi karibuni. Tena si kwamba mtoto huyo ni wa kwanza, ni wa nne,” kilisema chanzo hicho kikimnukuu Aunty.

Tuesday, February 24, 2015

PSPTB YAFANYA SEMINA YA UTAFITI KWA WANAFUNZI WA BODI YA WATAALAMU WA UNUNUZI NA UGAVI‏

Bodi ya Wataalam wa Ununuzi na Ugavi PSPTB imeendesha mafunzo kwa wanafunzi wa fani ya ununuzi na ugavi wanaofanya tafiti kama sehemu ya mafunzo yao ya shahada ya
Ununuzi na ugavi.
Mafunzo hayo yalifunguliwa tarehe 16 Februari 2015 na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi Dr. Clemence Tesha, ambaye aliwaasa wanafunzi hao wazingatie mafunzo hayo ili kuongeza ubora wa kazi za utafiti watakazofanya kwa ajili ya kupata shahada ya juu ya ununuzi na ugavi. Aidha, alisisitiza kuwa wanapaswa kuzingatia maadili katika kufanya utafiti, jambo ambalo ndio msingi na matakwa ya Bodi. wanafunzi wanatakiwa kufanya utafiti wao wenyewe na sio kuchukua kazi zilizofanywa na wanafunzi/watafiti wengine au kufanyiwa na watu wengine maana kufanya hivyo ni kuvunja sheria.
Pamoja na kuwajengea uwezo wa kufanya utafiti, pia wanafunzi wanajengewa uwezo wa kujiamini, kuandika ripoti na kujieleza na hata kuwasilisha ripoti katika sehemu zao za kazi. Hivyo lengo kuu la semina hii ni kuwajengea uwezo wa kuandika, kujieleza na kutoa huduma bora kwa taifa, kwani ufaulu wa mwanafunzi, unategemea sana uwezo wake wa kuitetea kazi yake, ambapo katika mtihani huo mwanafunzi atawasilisha kazi yake mbele ya wataalam, ili kupima uwezo wake.
New Picture (88) 
Mr. Godfred Mbanyi, Mkurugenzi wa Mafunzo PSPTB akitoa neno katika ufunguzi wa semina ya utafiti iliyofanyika kwenye ukumbi wa TEC Kurasini Dar es Salaam tarehe 16/2/2015
New Picture (89)
Mkurugenzi wa mafunzo Mr. Godfred Mbanyi akimkaribisha Mkurugenzi mtendaji wa PSPTB Dr. Clemence TEsha kufungua semina ya utafiti katika ukumbi wa TEC Kurasini Dar es Salaam. Tarehe 16/02/2015

KAKA ADAIWA KUMTOROSHA DADA YAKE KWA MUME

ALLY Issa anayeishi Mombasa nchini Kenya, anadaiwa kumtorosha dada yake Hasina Issa (22)  aliyekuwa akiishi na mumewe, Baraka Ally (32), Mbezi Mwisho jijini Dar es Salaam.Tukio hilo lilitokea siku ya mkesha wa Siku ya Wapendanao ‘Valentine’s Day’.
Hasina Issa siku ya harusi yake.
Akizungumza na gazeti hili mwishoni mwa wiki iliyopita, Ally alisema alitoa taarifa polisi na kufunguliwa jalada namba KMR/RB/1996/15 Kimara, akiamini mke wake ametoroshwa.
Alisema mkewe huyo, aliyemuoa Julai 6, mwaka 2013 Tandale, alitoweka baada ya kaka yake huyo akiwa na mkewe Mzungu, kuwatembelea nyumbani kwao.

MAITI YA MCHUNGAJI YAZUA TAFRANI

MAITI ya Mchungaji James Regnald Mhando  aliyefariki  Februari 18, mwaka huu imezua tafrani nzito kwa ndugu na jamaa baada ya kujulikana kuwa alikuwa na wake wawili ambapo mke mmoja alitaka mwili uagwe hospitali na upande wa pili ukitaka ukaagwe kwa mama yake marehemu.
Mchungaji James Regnald Mhando enzi za uhai wake.
Katika msiba huo ilibainika kuwa, mchungaji huyo (kanisa lake tunalihifadhi kwa sababu maalum), alikuwa na watoto sita kwa mama tofauti na wote walijitokeza katika mazishi ya baba yao.
Inadaiwa  kuwa Mchungaji Mhando alianza kuumwa Jumamosi ya Februari 14, mwaka huu lakini inadaiwa baadhi ya watoto na ndugu wengine hawakujulishwa hadi Jumanne ambapo inadaiwa alibebwa na gari la wagonjwa kutokea Morogoro hadi Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Jeneza la mchungaji James Regnald Mhando.
Habari zinasema ilipofika Jumatano saa tano usiku, mchungaji huyo aliaga dunia na mbali ya kuaga dunia, bado tukio hilo lilikuwa ni siri na ilidaiwa ilikuwa afanyiwe shughuli za mazishi kwa siri bila ya baadhi ya watoto wake wakubwa kujua.

AMANDA AZIDIWA, ASHINDWA KUMZIKA MEZ B

MREMBO kunako tasnia ya filamu Bongo, Tamrina Mohamed Poshi ‘Amanda’ ameshindwa kuhudhuria mazishi ya aliyekuwa mwanamuziki wa Bongo Fleva, Moses Bushagama aliyefariki mwishoni mwa wiki iliyopita mkoani Dodoma kutokana na kuugua ghafla.
Mrembo kunako tasnia ya filamu Bongo, Tamrina Mohamed Poshi ‘Amanda’.
Akizungumza na Uwazi kwa masikitiko, Amanda ambaye pia ni mtu wa karibu na marehemu, alisema kuwa alishapanga kusafiri kwenda Dodoma kwa ajili ya maziko lakini kitendo cha kuugua ghafla kimeharibu kila kitu.
“Imeniuma sana kwa sababu ya ugonjwa wa taifodi kuniandama ambapo nilikuwa nikitapika mfululizo,” alisema Amanda.Mez B alikuwa akiumwa ugonjwa wa homa ya mapafu, alikuwa amelazwa katika Hospitali ya Mwananchi kabla ya umauti kumkuta. Amezikwa Jumatatu katika makaburi ya Wahanga mkoani Dodoma.

JOYCE KIRIA ADAIWA MILLION 500

MTANGAZAJI wa Kipindi cha Wanawake Live, Joyce Kiria amepokea samansi ya mashtaka kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Dimani, Zanzibar, Abdallah Sharia Ameir (CCM) ambaye amedai amlipe fidia ya kumdhalilisha sh. Milioni 500 au amuombe radhi kupitia  kipindi chake.
Mtangazaji wa Kipindi cha Wanawake Live, Joyce Kiria.
Akiongea na Uwazi, Joyce Kiria alisema kuwa amepokea barua hiyo kwa mikono miwili na anawasubiri wanasheria wake ili waijadili.“Nilimpokea mke wa Mbunge aitwaye Hawa kama mwanamke mwenye matatizo ambaye alifika kutoa sauti yake ili watu wamsaidie mtoto wake mwenye ulemavu.
Baada ya kuongea naye nilimtafuta mheshimiwa ili kumpa nafasi naye aongee ya kwake kama wajibu wangu, lakini cha kushangaza yeye alinikamata na kunipeleka polisi, leo anasema nimemdhalilisha,” alisema Joyce .
Joyce anadaiwa fidia na Mbunge huyo kwa kuitangaza habari ya kumtelekeza mtoto mlemavu ambaye alilepelekwa kwenye kipindi chake na mkewe, Hawa Deusi.   

MAPIGANO TANGA, NGOMA BADO NZITO WALE MAGAIDI WATAJWA KUWA NI MAKOMANDO


Na Waandishi Wetu/Uwazi
YALE mapigano yaliyotikisa Mapango ya Amboni jijini Tanga kwa saa 48 kati ya watu wanaodaiwa na wananchi kuwa ni magaidi na majeshi ya ulinzi ya Tanzania bado ngoma nzito kufuatia baadhi ya wananchi kusema mengine mapya wanayoyajua kuhusu magaidi hao, Uwazi limechimba na kuchimbua.

Polisi wakipambana na magaidi hao.
Kwa mujibu wa baadhi ya wakazi wa Vijiji vya Mafuriko, Mikocheni, Majimoto, Kilomoni na Amboni yenyewe, wanaamini wahalifu hao ni makomandoo wazuri na waliishi kwenye mapango hayo wakijua siku wakivamiwa watapambana vikali.
KWA NINI MAKOMANDOO?
Mkazi mmoja wa Kijiji cha Majimoto alisema kwa jinsi watu hao walivyofanikiwa kutoweka katika mazingira tata huku wakiwa salama haingii akilini kwamba ni wapiganaji wenye mafunzo ya kawaida.
“Wakati risasi zinapigwa na serikali inatuambia tuchukue tahadhari kwa mtu tusiyemjua tumtolee taarifa tuliamini lazima watakamatwa hata kama si wote. Lakini tulipoambia hali imetulia lakini hajakamatwa hata mmoja tulishangaa sana,” alisema mkazi huyo akiomba asitaje jina lake.

Monday, February 23, 2015

DIAMOND ATUPIWA JINI, LAMPATA MAMA'KE


Musa mateja/Ijumaa wikienda
Imevuja! Kuna madai kwamba staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ ametupiwa jini lakini likamkosa na kumpata mama yake mzazi, Sanura Kassim ‘Sandra’ kisha kumsababishia ‘gonjwa’ la ajabu, Ijumaa Wikienda linakupa mchapo kamili.


Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa na mama yake mzazi, Sanura Kassim ‘Sandra’.
TUJIUNGE NA CHANZO
Kwa mujibu wa chanzo makini, watu wanaodaiwa kuwa ni wabaya wa Diamond (Anti-Diamond) walimtupia jini staa huyo lakini bahati nzuri likamkosa na kwa bahati mbaya likampata mama yake ambaye alipata ugonjwa wa kupooza ghafla.

“Ujue kumekuwa na sintofahamu kwa muda mrefu juu ya ugonjwa wa mama Diamond lakini habari za uhakika ni kwamba, mama Diamond yupo hoi baada ya kutupiwa jini ambalo mlengwa wake alikuwa Diamond.

SNURA: NILIPOTELEA SAUZ NA MOMBASA

Alikuwa wapi? Baada ya kupotea kwa muda mrefu, staa wa sinema na muziki wa Bongo Fleva, Snura Mushi hatimaye ameibuka na kueleza sababu za ukimya wake.
Staa wa sinema na muziki wa Bongo Fleva, Snura Mushi.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda katika mahojiano maalum, Snura amefunguka kwamba ukimya wake ulitokana na kwenda Afrika Kusini ‘Sauz’ kushuti video ya wimbo wake wa Najidabua na siyo kweli kwamba alikuwa mkoani Mbeya kwa mwanaume.

Katika intavyu hiyo, Snura alikanusha tetesi za kuzaa mtoto wa pili na kusisitiza ana mtoto mmoja na wanaosema maneno hayo wamekosa la kusema.Ijumaa Wikienda: Huoni kukaa kwako kimya mashabiki wamekusahau?Snura: Hawajanisahau kabisa na hilo nililithibitisha hivi karibuni kwenye shoo niliyofanya Msasani Club (Dar), ambapo walijaa tofauti na mwanzo japokuwa mwanzoni kabla ya shoo nilikuwa nawaza wamenisahau.

CHAMA CHA NCCR-MAGEUZI CHATOA TAMKO KUHUSU SERA YA ELIMU NA MAFUNZO YA MWAKA 2014 ILIYOZINDULIWA NA RAIS JAKAYA KIKWETE FEBRUARI 13, 2015‏


 Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha NCCR-Mageuzi, Zanzibar, Musa Kombo Musa (kulia), akimkaribisha Mwenyekiti wa chama hicho Taifa, James Mbatia (katikati), ili azungumze na wanahabari Dar es Salaam jana asubuhi wakati akitoa tamko hilo. Kushoto ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Mosene Nyambabe.
 Mwenyekiti  wa Chama cha NCCR-Mageuzi, Taifa, James Mbatia (kulia), akionesha kitabu cha Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 wakati akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Dar es Salaam jana asubuhi, wakati akitoa tamko la chama hicho juu sera hiyo. Kushoto ni Katibu Mkuu wa chama hicho, Mosene Nyambabe na kulia ni Naibu Katibu Mkuu, Zanzibar, Musa Kombo Musa.
 Hapa mkutano na waandishi wa habari ukiendelea.
 Wanahabari wakichukua taarifa hiyo.

Saturday, February 21, 2015

PENZI LAKE NA WEMA ,KUMBE DIMPOZ BOYA TU

HABARI ya mjini ni kwamba, lile penzi linalonadiwa la Mbongo-Fleva, Omary Faraji Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ na mwigizaji Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ limejaa magumashi, ikidaiwa kuwa jamaa huyo kawekwa kama boya tu, nyuma yake kuna kigogo mzito serikalini ndiye anayekula vinono, Risasi Jumamosi limetonywa.
Mbongo-Fleva, Omary Faraji Nyembo ‘Ommy Dimpoz’ akiwa na mwigizaji Wema Isaac Sepetu ‘Madam’.
Kwa mujibu wa chanzo cha kuaminika, Dimpoz ameagizwa na kigogo huyo awe mpenzi kivuli wa Wema ili kuzuga watu wasishtukie mchezo kama yeye ndiye anayesukuma gududumu la malovee kwa Madam.

ODAMA AFUNGUKA KUCHANGIA WANAUME!

Laurent Samatta
MAMBO yanazidi kunoga ndani ya safu hii ya Sindano 5 za moto, kutokana na maombi yenu, leo tumemleta kwenu mwigizaji Jeniffer Kyaka ‘Odama’, tiririka naye:
Staa katika tasnia ya filamu Bongo, Jeniffer Kyaka ‘Odama’.
Paparazi: Mambo vipi Odama! Tuanze moja kwa moja na swali la kwanza, hivi kwa sasa una mpenzi? Mbona hatumjui?Odama: Mambo poa! Mpenzi ninaye, nampenda muda bado wa kumuanika.Paparazi: Ulishawahi kuchangia bwana na mwanamke mwingine katika maisha yako?
Odama: Hapana, sina kumbukumbu hiyo.

MRITHI WA MAMA SALMA KIKWETE VITA NZITO!

Mwandishi wetu
TAYARI imebainika kwamba, baadhi ya viongozi walioonesha nia ya kugombea urais mwaka huu wameanza kupigiwa debe na wake zao ndani ya mitandao ya kijamii ili waume hao watakapoibuka na ushindi wapate nafasi ya ‘u–First Lady’, Risasi Jumamosi linakupa zaidi!
Mama Salma Kikwete.
Taarifa zilizotua juu ya dawati la gazeti hili juzi zilisema kuwa, vita ni nzito kwani baadhi ya wake wa wagombea nao wapo ndani ya mkakati wa kukusanya watu wa kuwaunga mkono waume zao katika kinyang’anyiro hicho kitakachochukua nafasi Oktoba, mwaka huu.
Wakati vita hiyo ikiwa imepamba moto, mnajimu maarufu nchini, Maalim Hassan Hussein naye ameibuka kwenye Risasi Jumamosi na kuanika utabiri mzito juu ya wasifu wa mtu atakayeshinda urais huo.
HALI ILIVYO SASA
Habari zinadai kuwa, baadhi ya wake wa viongozi hao nao wamekuwa wakipita chini kwa chini kukusanya na kuweka sawa makundi ya kisiasa tayari kwa kampeni za kuwaingiza ikulu waume zao.
ISHU NI KUMRITHI MAMA SALAMA KIKWETE
“Kila mke wa mgombea anafanya kampeni za chini kwa chini. Unajua wenyewe kila mmoja anafahamu kwamba ‘mzee’ akiingia ikulu yeye atakuwa First Lady kumrithi wa sasa (mama Salma Kikwete), ndiyo maana siku hizi karibu wake wa wagombea wote wana safari za mikoani kupanga timu ushindi,” kilisema chanzo kimoja.

Mke wa waziri mkuu mstaafu Edward Lowassa.
FARAJA KOTA YUKO WAZI ZAIDI
Miss Tanzania 2004, Faraja Kota ambaye ni mke wa Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu aliyetangaza nia, amekuwa akitupia maneno yenye kumpigia kampeni mumewe huyo kwenye Instagram na mitandao mingine ya kijamii.

AIBU! TICHA MBARONI KWA KUMUUZISHA MTOTO MAYAI MUDA WA SHULE

CHANZO: GLOBAL PUBLISHERS
MATUKIO ya mateso, unyanyasaji na utumwa kwa watoto yanashika kasi nchini! Safari hii mwalimu wa shule moja ya msingi iliyopo Mburahati jijini Dar aliyetajwa kwa jina moja la Lucy ametia aibu baada ya kutiwa mbaroni katika Kituo cha Polisi cha Magomeni, Dar akituhumiwa kumtumikisha mtoto mwenye umri wa miaka 12 aitwaye Sakina kwa kumuuzisha mayai ya kuchemsha na soseji.

Mwalimu huyo akijitetea juu ya sakata hilo.
Kwa mujibu wa mashuhuda wetu, tukio hilo lilichukua nafasi maeneo ya Kashuda Bar, Magomeni hivi karibuni baada ya wakazi wa eneo hilo kuhamaki kumuona binti huyo akitembeza mayai na soseji mtaani wakati umri wake ni mdogo kinyume na sheria za ajira.
RAIA WAMZUNGUKA
Ilisemekana kwamba, baada ya kukerwa na kitendo hicho huku Sakina akionekana hana furaha, raia hao wenye hasira kali walimhoji ambapo alimtaja mwalimu huyo kuwa ndiye bosi wake aliyemchukua kutoka Tanga kwa ajili ya kufanya kazi za ndani (hausigeli).

Friday, February 20, 2015

PUSH OBSERVER YAZINDUA TEKNOLOJIA YA KISASA YA UKUSANYAJI WA TAARIFA IJULIKANAYO KWA JINA LA NEWSRADAR

 Mshauri mkuu wa mradi wa NewsRadar, Romana Gersuni kutoka Ujerumani akielezea jinsi teknolojia hiyo mpya na ya kisasa ya ukusanyaji taarifa mbalimbali ya Push Observer inavyofanyakazi zake.
 mkuu wa mikakati wa kampuni ya Six Telecoms ambayo ni kampuni mama ya Push Observer, Rashid Shamte akielezea faida ambazo watazipata kampuni mbalimbali nchini, husasani za kibiashara kwa kujiunga na huduma ya NewsRadar waliyoianzisha nchii.

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate