EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Makala

Muendelezo wa Makala 02,03 Soma chini yake Muda wote hapa

PADRI MLA NYAMA ZA WATU-01
Mkasa huu unasimuliwa na Padri Moses au kwa kifupi Faza Moze lakini si jina lake halisi , akiweka bayana mambo aliyoyafanya mpaka kujutia. Padri Moses hakutaka kuweka wazi ni wa kanisa gani kwani Mapdri hutumiwa na makanisa ya Anglikani na Romani. Anasema:

“Ilikuwa mwaka 1999, mwezi Desemba wakati wakristo wanajiandaa kwa sherehe ya Krismasi, kanisani walikuja wazee wawili ambao ni wageni machoni pangu miongoni mwa waumini wa kanisa langu hilo .
Walikaa fomu moja na waumini wengine, lakini katika kukaa walitenganishwa na mzee mmoja. Nikiwa naendelea na ibada, kila wakati niliwaona wale wazee wageni wakiangaliana kwa kupitia mgongoni kwa yule mzee aliyewatenganisha.

Kwa sababu moyo wangu ulikosa amani na wao, nikawa nawakazia macho hatua kwa hatua ili nione kila walichokuwa wakikifanya.
Kuna wakati nilishtuka sana kuona mmoja wao akibadilika sura na kuwa kama ya bundi, lakini nilipojiweka sawa kushangaa, akarudi katika sura ya kawaida, na mwenzake akacheka kama vile alijua mwenzake amegeuka sura na mimi nimeogopa.
Ndipo nilipoanza kukumbuka ujaji wao kama ulifanana na mazingira ya kuwa waumini wangu.

Nikakumbuka kuwa, wakati wanaingia, walipitia njia zote za uumini, na pia walionekana ni wanyenyekevu kupita hata waumini wangu wa kila siku.
Wakati nikiwaza hayo, ghafla mmoja wa wale wazee alisimama mbele yangu bila kumwona akitoka kwenye fomu kuja mbele, nikashituka, lakini kumbe waumini wengine waliniona nilivyoshituka, wakakaza macho kiwangu wakishangaa.
Nilikatisha maneno ya ibada na kuinua mikono juu kisha nikafanya ishara ya msalaba, kwa jina la baba, la mwana na la roho…

Akapotea mbele ya macho yangu na kuonekana amekaa na mwezake kama mwanzoni, wakacheka sana lakini si kwa kutoa sauti.
 “Nilishtuka sana , nikafikicha macho kuyaweka sawasawa kwani yalionekana kama yana ukungu wa moshi.
Yalipokaa sawasawa, nikaendelea na ibada lakini mwili wangu ukiwa umechoka sana, hauna nguvu tena mwilini kama kuna vitu vunatembeatembea.
Baadhi ya waumini walipata picha hiyo, kwamba sikuwa sawasawa, lakini walikuwa hawajui kama nilikuwa naona watu wa ajabu.

Nilipofika eneo la kuongea maneno ambayo ikawalazimu waumini wasimame, wale wazee wawili wakawa wa kwanza kusimama kabla sijamaliza maneno na  wakawa warefu kuliko waumini wangine.
Kurefuka kwao kama kuliambatana na moshi mkubwa wa moto wa kuni.

Nilipowaangalia waumini wengine walionekana hakuna wanalolijua kuhusu maono yangu kwani walisimama, wakafunga mikono kwa unyenyekevu mkubwa wakinisikiliza.
Kama wangekuwa wamegundua kitu, basi hata wale waumini waliokaa jirani wangejua, kwani wao walikuwa wakinitazama tu wakati jirani yao kuna mambo ya ajabu!

Nilikata maneno ya ibada na kuwaamuru waumini wakae, wakatii lakini mshangao:
“Humu ndani kuna watu wawili naona kama si wa imani yetu,” nilisema.
Waumini wote wakawa wanageukageuka na kutazamana wakiwatafuta wao watu wawili.
Walichokifanya wale wazee sasa, muumini aliyekaa katikati yao alipogeuka kumwangalia mmoja wao, wakaonekana wote wamekaa pamoja na yule muumini akawa amekaa pembeni yao, kwa hiyo alipogeuka akawa anamwangalia muumini ambaye anamfahamu.

“Naamini hakuna atakayeweza kuwaona, maana wanatumika sana na ibilisi,” nilisema.
Ninawapa muda wa wao kujisema ni akina nani?” Nilisema huku nikiwaangalia kwa kuwakazia macho huku waumini nao wakinikazia macho mimi na kuyafuatilia ninakoangalia.  
Walichokifanya wale wazee sasa, muumini aliyekaa katikati yao alipogeuka kumwangalia mmoja wao, wakaonekana wote wamekaa pamoja na yule muumini akawa amekaa pembeni yao , kwa hiyo alipogeuka akawa anamwangalia muumini ambaye anamfahamu.

“Naamini hakuna atakayeweza kuwaona, maana wanatumika sana na ibilisi,” nilisema.
Ninawapa muda wa wao kujisema ni akina nani?” Nilisema huku nikiwaangalia kwa kuwakazia macho huku waumini nao wakinikazia macho mimi na kuyafuatilia ninakoangalia.  
Mara walipotea machoni pangu. Niliwaambia waumini kuwa, wametoweka na nikaonesha mahali walipokuwa wamekaa.

Yule mzee aliyewekwa kati akasema, anachojua yeye ni kwamba, waumini waliokwenda kukaa kulia na kushoto kwake ni wanawake na alitaka kuwauliza kisa cha kukaa upande ule wa wanaume.
Basi, niliendelea na ibada huku kila muumini akionekana hana amani moyoni. Hata pale alipoingia mtu na kuliza mlio wa viatu sakafuni, waumini wote waligeuka kuangalia mpaka ikabidi mimi nisitishe kuendelea na ibada ili waumini wamalize  kuangalia.
Ibada ilipokwisha, niliingia kwenye chumba nikavua mavazi ya utumishi, nikabaki na mavazi yangu ya kawaida. Nikiwa natoka nje ya chumba, ghafla nikaona giza nene mbele.

Nikawahi kushika flemu ya mlango huku nikiwa nahakikisha sianguki au kukanyaga sehemu ambayo siyo ardhi. Mpaka hapo nilikuwa siunganishi tatizo la kuona giza na uwepo wa wale waumini wawili wa ajabu ajabu.
“Mtumishi wa Mungu kwema?” Nilisikia sauti ikiniuliza.
“Siyo kwema kabisa.”
“Unaona nini mbele?”
“Naona giza .”
“Fumba macho.”
Nilifumba.
“Haya fumbua sasa.”
Nilifumbua.

Nikaendelea kuona kama kawaida, lakini hakukuwepo na mtu yeyote aliyesimama mbele, nyuma, kulia wala kushoto kwangu.
Lakini pamoja na hali hiyo, niliisaka ile sauti akilini mwangu na kuigundua kuwa, ilikuwa ya yule mzee aliyekaa jirani na wale watu wa ajabu.
“Khaa!” Nilijikuta nikishangaa sasa.

Nilitembea kwa mwendo wa haraka hadi kwa waumini waliokuwa wamesimama nje ya kanisa wakiongea, wengine wakisalimiana na kuulizana maisha, kwani waumini wengi huitumia Jumapili kuonana na kuongea mambo yao mbalimbali ya maisha.
Nilizungusha macho kumwangalia yule mzee, nikamwona katikati ya watu akicheka na kupiga soga na wazee wenzake, nikamfuata, lakini huku waumini ninaowapita wakinisalimia, wengine wakionekana kutaka kujua kile kisa cha ndani ya kanisa.

Wakati nakaribia kumfikia, nilijiuliza mwenyew, je, kweli kwa sauti ile kama angekuwa ni yeye angeshafika katikati ya watu?
“ Kama ni hivyo, mbona sasa wakati nafumbua macho sikumwona mbele yangu?”
“Faza pole na majukumu bwana,” yule mzee niliyekuwa namfuata alinisalimia na kuwawahi wenzake wote aliyosimama nao. Sauti yake niliikumbuka vizuri sana, ndiyo ile iliyonielekeza mpaka nikafumbua macho.

“Nimeshapoa mzee wangu.”
Wazee wengine nao pia wakanisalimia huku wakinipa mikono.
“Eti mzee ulikuwa unasemaje?” Nilimuuliza yule mzee.
“Wapi?” Na yeye aliniuliza.
“Hukusimama na mimi pale mlangoni?”
“Mlangoni! Wapi?”
“Kule kwenye chumba?”
“Hata, hapana.”

Wazee wengine nao wakaonesha kunishangaa mimi, nikajisikia soni kwa nafasi yangu ya u-Padri.
“Oke, sawa basi.”
Nilitembea kwenda kwenye ofisi yangu, lakini nyuma nikamsikia mzee mmoja akisema.
“Kwani mzee Makwaya imekuwaje?”
“Sijui chochote,” mzee Makwaya alijibu, hali ya mshangao na minong’ono ya chini kwa chini iliendelea hadi ilipofika mahali nikawa siwasikii.
Kule ofisini nilikuwa peke yangu, nikainamia mezani na kuwaza ile hali mwanzo hadi pale ilipofikia nikaona giza nene mbele yangu.
“Hivi, wale ni akina nani?”
“Ni kwanini walinijia kanisani?”
“Wametumwa au?”
Nikiwa naendelea kuwaza hivyo, mara nikasikia sauti ndani ya ofisi.
“Unaendeleaje mtumishi wa Mungu?”
Ilikuwa ni sauti ya yule yule mzee Makwaya.
Nilishtuka sana , nikaangalia kila kona ya ofisi.
“Hakuwepo popote pale jambo lililonifanya nizidi kuogopa.
Nikiwa natafakari huku kijasho chembamba kikinichuruzika, mara nikasikia kishindo kikuu kwa nje kama vile kuna kitu kizito kinatua toka juu kwenda ardhini.

“Wewe ni nani?” Niliuliza lakini sauti yangu ikitoka kwa woga.
Sikusikia jibu wala sauti yoyote, ulipita ukimya, nikaendelea kutafakari huku kama nashikwa na usingizi mzito na macho yangu hayaoni.
Ghafla nilihisi kiumbe kusimama mbele yangu, nikajitahidi kufumbua macho.
Niliona binadamu mwenye mguu mmoja, sikio moja, mkono mmoja, tundu moja la pua, jicho moja amesimama mbele yangu akiachia tabasamu la kutisha.
“Kwa jina la baba na la mwana na la…”
Kabla sijamaliza kusema, alipotea mbele yangu, lakini bado macho yangu yakawa yana kivuli chake kwani alikuwa wa kutisha sana sijapata kuona mfanowe.

Nilitamani waumini wangu, hata mmoja tu aje, lakini ajabu ni kwamba hakukuwa na dalili na si haikuwa kawaida yao, kwani mara zote, kila baada ya ibada waumini walikuja ofisini kwangu na kueleza matatizo yao.
Ilifika mahali nikahisi labda siko mahali salama, labda mimi niliona nipo ofisini lakini kumbe sikuwa ofisini, ingawa nilipojaribu kutupa macho huku na kule, akili yangu iliamini niko ofisini kwangu.
“Ngo ngo ngo.”
Mlango uligongwa.

“Karibu, ingia,” niliitikia haraka.
Waliingia wanawake wawili, wakiwa wamejitanda vitenge hadi kichwani na kubakiza uso tu. Walikuwa wageni machoni pangu, nikiwa na maana sijawahi kuwaona hata siku moja katika maisha yangu ya utumishi.
“Karibuni sana akina mama.”
Hakuna aliyejibu hata kwa kutingisha kichwa.
Waliangalia wenyewe sehemu ya kuketi, wakaketi na kunikazia macho mimi.
Na mimi niliwaangalia kwa uso wa kuwauliza shida yao . Lakini hakuna aliyesema mpaka mimi nilipotoa sauti yangu.
“Niwasaidieni nini akina mama zangu?”
Ajabu iliyotokea hapo sijapata kuona wala kuisikia siku yoyote ile.
“Tuna shida na wewe Padri,” alisema mmoja, lakini kwa sauti nene na nzito,  ya kiume.
Kwanza nilishtuka sana kusikia sauti ya kiume ikitoka kwenye mwili ule mwembamba.
“Shida gani mama zanguni?” Niliwauliza kwa sauti yenye woga woga kwani sasa nilianza kuyaona maisha yangu kama yanajaribiwa.

“Tunataka kuwa na wewe kazini kwetu,” alisema yule wa pili ambaye naye sauti yake ilikuwa nene zaidi kupita ya wa kwanza hadi nikajikuta nikitetemeka.
“Mna…mnanitaka kwe…kwenye kazi gani?” Niliuliza huku sauti yangu ikitetemeka kwa wasiwasi mkubwa moyoni, jasho jembamba lilizidi kuchuruzika licha ya kwamba nilipoingia niliwasha pangaboi.
“Ina maana hutujui?” Wote walisema kwa wakati mmoja huku wakisimama na kujivua vitenge. Nilishangaa sana kuwaona wamebaki na suruali  na mashati, ina maana kumbe  ni wanaume kama mimi na walivaa vile kike ili kinipoteza mawazo ya awali, niliwaza kwa wasiwasi huku nikiwakodolea macho pima.

“Mtumishi wa Mungu aliye hai, tunakutaka kwenye kazi yetu bwana, eee?”
Mmoja wao alisema akinisogelea nilipokuwa nimekaa mimi. Sasa niliibaini sauti yake, ndiyo ile ya yule mzee muumini wangu.
“Nyinyi si mliingia kanisani kwangu loe mkawa mnafanya maajabu?”
“Eee, ni sisi,” walinijibu huku yule wa pili naye akisimama, akanisogelea na kusimama sambamba na mwenzake.
“Sasa mnataka nikafanye kazi gani na nyinyi, ya maajabu kama nyinyi?”
“Eee, ndiyo,” walijibu wote.
“Mnatoka wapi?”
Mmoja wao akajibu:
“Tunatoka kwa Mungu.”

“Yupi?” Niliwauliza huku nikiwa nataka kusema ‘kwa jina la baba na la mwana…lakini wakaniwahi wao kwa kusema:
“Mungu kama wako, ametutuma kwako, amesema unatakiwa kupata nguvu ambayo na sisi tunayo, kwa hiyo na sisi tunakupa nguvu hii, POKEA!”
Waliposema ‘pokea’ walinigusa kwa pamoja kwenye paji la uso, nikaanguka chini na kupoteza fahamu.
Nilipokuja kuzinduka, nilikuwa katikati ya pori lenye miti minene, mirefu na matawi yakiwa juu sana .

Nililala kwenye nyasi, pembeni yangu nilizungukwa na watu wengi ambao niliwaona miguu tu. Kwa haraka haraka nilihesabu miguu ile na kupata idadi ya ishirini na sita, ina maana watu waliosimama walikuwa kumi na watatu.
Niliinuka ili kukaa, lakini mmoja wa wale watu alinizuia nisikae, niendelee kulala, nikatii kwa vitendo na kurudi kujilaza majanini.
Ghafla nikasikia sauti nzito, yenye tetemeko.

“Umetakiwa kupokea nguvu ya kwetu,” ilisema ile sauti.
Yakapigwa makofi pale, halafu ukafuatia ukimya wa muda mrefu kama vile nililala peke yangu bila kuwepo mtu mwingine.
“Simama,” ile sauti ilisema kwa haraka na kwa amri.
Nilijikuta nasimama lakini nikiwa ndani ya ofisi yangu. Nilijiangalia na kujiona niko kama nilivyovaa awali, kila kitu ndani ya ofisi kilikuwa sawasawa, hakuna hata kitu kimoja kilichoharibika au kutokuwepo.
Hofu ikaniingia kuhusu waumini wangu nje, kwamba kama walikuja wakakuta mazingira yenye utata wataelewaje?
Niliusogelea mlango na kushika kitasa, nikaufungua polepole na kuangalia nje. Hakukuwa na muumini hata mmoja, hata mtoto.

“Khaaa!” Nilishangaa.
“Ina maana nimetumia muda mwingi sana ?” Nilijiuliza.
Niliangalia saa ya ukutani na kugundua kuwa, wakati namaliza ibada ilikuwa saa nne na nusu, muda ule naangalia saa ilikuwa saa saba mchana, ina maana kuingia kwa wale watu, kupoteza fahamu hadi kuzinduka ilipita saa tatu?!

Mlango uligongwa, akaingia mtu mmoja, simfahamu. Nilimkaribisha, akakaa kwenye fomu.
“Nikusaidie?”
“Ee baba, mimi nimekuja uniombee,” alisema akijiweka sawasawa.
“Nikuombee nini?”
“Uniombee naumwa.”
“Unaumwa nini?”
“Huwa nikilala usiku naona watu wanakuja kunikaba.”
“Unaona au unaota?”
“Naona, wakati mwingine huwa napiga kelele kwa kuwaogopa.”
“Wewe ni muumini wangu?”
“Hapana, nasali mjini.”
“Sasa kwanini usiende kwa mtumishi wa Mungu wa kanisa lako?”
“Ameshaniombea sana lakini hakuna mafanikio.”
“Sasa unaamini nini kuja kwangu, kuna mafanikio?”
“Naamini yapo mtumishi.”
Nilihisi ni miongoni mwa wale watu walionijia na kunifanyia maajabu yao, lakini sijui ni nini, kwani ghafla nilijawa na ujasiri wa kutoogopa lolote na kuamua kumwombea kweli.
Nilisimama, nikamtaka yeye apige magoti kisha nikamwekea mkono wangu wa kulia kichwani kwake na kuomba sana mpaka akaanguka chini.
Alipokuja kusimama, akasema anajisikia mwepesi, ana imani amepona kabisa.
“Usijali, nenda kwa amani lakini jilinde na dhambi.”
“Sawa Padri.”

Alipoondoka tu, mzee mmoja, aliyevaa shuka jeusi kuzunguka kiuno, chini akiwa hana kiatu wala sendoz, pekupeku, ju mabega wazi, mkononi alishika mkia wa mnyama, alisimama mbele yangu bila kujua aliingiaje?
“Karibu mzee wangu,” nilimkaribisha kwa ujasiri mkubwa sana, moyoni sikuwa na hofu wala wasiwasi. Pamoja na kuvaa kiajabu kama vile, lakini nilimwona kama mtu wa kawaida sana kwangu.
“Fumba kiganja cha mkononi,” aliniambia kwa amri.
Nikajikuta nafumba bila kuhoji yeye ni nani na ametoka wapi na kaja kwangu kufanya nini.
“Fumbua.”
Nilipofumbua, unga mweusi ulikijaza kiganja changu.
“Jipake kidogo usoni.”

Nilijipaka kidogo huku nikiwa nimeinama kuangalia chini.
“Unaona nini?”
“Sioni kitu.”
“Haya, hiyo dawa ndiyo tunayotumia kufanyia kazi, tunapotoka usiku kwenda kazini kila mmoja anakuwa na dawa hiyo, ndiyo inayosaidia watu wasituone…
“Fumba kiganja.”
Nikafumba.
“Fumbua.”

Nilipofumbua, sikuona ile dawa, kiganja kilikuwa cheupe kama mwanzo.
“Fumba tena kiganja.”
Nikafumba…
 “Fumbua.”
Nilipofumbua mkononi, nusu kulikuwa na unga unga wa kijani nusu unga unga mweusi.
“Chota huo unga kisha changanya.”

Nilitii, kisha akaniambia nijipake kidogo usoni, nikafanya hivyo na kujikuta nakuwa mwepesi kuliko kawaida ya siku zote.
“Unaona nini?”
“Najiona mwepesi sana .”
“Unaweza kujaribu kupaa?”
“Nijaribu?”
“Jaribu basi.”

Niliinua mikono kama vile ndege anavyoinua mabawa, taratibu nilijiona napaa juu huku miguu ikiiacha ardhi taratibu bila ridhaa yangu.
“Unaonaje?”
“Napaa sasa.”
“Shusha mikono.”
Niliishusha, taratibu miguu ikakanyaga ardhi na kusimama kama mwanzo.
Baada ya hapo yule mtu akapotea machoni pangu na kuniacha nikiwa na maswali kibao.
Nilijiweka sawa, nikafunga madirisha ili kutoka, nikafunga mlango na kuondoka kabisa katika eneo la ofisi.
Nilikwenda kwenye makazi yangu, lakini kwa wakati huo nilijihisi mnyonge sana, mwili ulikuwa hauna nguvu, macho hayaoni vizuri mbele na miguu mizito.

* * *
Saa saba za usiku, nilishtuka kutoka usingizini baada ya kushikwa na kuvutwa kidole cha mguu wa kulia na mtu. Kulikuwa na giza kwa hiyo sikujua nani alifanya zoezi lile.
Swichi ya kuwashia taa haikuwa mbali na nilipolala, nikaiwasha chapchap, chumba kilipojaa mwanga sikuona kitu, nikaendelea kulala.
Baada ya muda nikawa katika ndoto.

“Wewe Padri, unadhani utafanya kazi mpaka lini?”
“Mungu apende,” nilijibu.
“Je, asipopenda?”
“Atapenda tu.”
“Kwanini unafanya kazi lakini huna nguvu.”
“Nguvu gani?”
“Ya kiroho.”
“Kwa sababu bado.”
“Bado nini?”
“Wakati wa kuwa na nguvu.”
“Ni sasa.”
“Kwa maana ipi?”
“Njoo.”

Nilimfuata huyo mtu, akanishika na kunivuta hadi mahali, akasimama na kuniambia.
“Nenda kaingie kwenye kanisa lile.”
Mbele yangu kulikuwa na kanisa, nikaenda kuingia.
Lilikuwa kanisa langu, waumini wangu, wake kwa waume wengine wamekaa wengine wamesimama. Walikuwa wengi sana.
Mimi nikapita hadi mbele kwenye madhabahu na kusimama pale.
“Wale wenye matatizo waje niwaombee.”
Karibu kanisa zima walipita mbele kuombewa.
Ule wingi wao, nikaanza kuogopa kwamba nitaweza kweli?
Wa kwanza nikamwekea mikono juu kichwani na kumwombea, pale pale aliposimama akaanza kupiga kelele na kuanguka chini kisha akasimama akiwa amepona na kurukaruka huku akimtukuza Mungu wake.
“Hee, hee nimekuwa mzima sasa.”
“Nenda usitende dhambi tena, sawa?”
“Sawa.”
Niliombea karibu kanisa zima, nilipomaliza nikawa natoka huku napigiwa makofi na waumini waliokuwa wamesimama kulia na kushoto kwangu.
“Padiri Padiri Padiri,” walisema wakipiga makofi, pwa pwa pwa.
Kufika nje, nikakutana na yule mtu aliyenichukua nyumbani.
“Umefanikiwa?”
“ Sana ,” nilimjibu.
“Umekubali?”
“Nini?”
“Kwamba wakati wa kuwa na nguvu ya kiroho ni sasa?”
“Nimekubali.”
“Haya, sasa twende kwa aliyekupa nguvu.”
“Kwa Mungu?”
“Wetu sisi.”

Tuliongozana hadi kwenye mti mmoja mkubwa, mrefu sana kwenda juu.
Chini walikaa watu wengi wakiwa kama wapo kwenye maongezi.
Kilichonishangaza miongoni mwa hao watu walikuwepo waumini wangu wa kanisani.
“Afadhali umekuja faza.”
“Faza nimefurahi sana kukuona.”
“Faza karibu sana .”
Wale waumini wangu wote walinikaribisha kwa furaha, amani na upendo wa hali ya juu.
Nilikaa sehemu ambayo kulikuwa na nafasi ya mtu mmoja, yule mtu niliyekwenda naye sikumwona tena alikopotelea.

“Bwaba umekuja huku, uko tayari kwa lolote?” Aliniuliza mzee wa kanisani ambaye sikuwa na mazoea naye.
“Kwani hapa ni wapi?” Nilihoji.
“Hapa ni kwa wachawi.”
“Wachawi!”
“Eee, umekuja kwa wachawi, kazini kwetu, karibu.”
Alipomaliza kusema, alikaa chini, akasimama sasa yule mzee ambaye siku ile kanisani walipoingia wale watu wawili wa ajabu, yeye alikaa katikati yao.
 “Eee, nina kila sababu ya kujisifu kwa kupewa heshima hii ya kumkuza kazini mtu mkubwa kama huyu,” alisema yule mzee.

Yakapigwa makofi kwa muda wa dakika tano nzima huku yule mzee akiwa amesimama tu akisubiri yaishe ili aendelee kuongea.
Lakini kwa jinsi nilivyokuwa namwangalia mimi, alikuwa anaongea kwa kujiamini sana na hakuonekana kujali kama mimi ni kiongozi wake wa kiroho.
“Kwa hiyo kuanzia leo mtumishi utakuwa chini yangu ukizitii na kuzifuata amri zangu, sawa bwana mdogo?”
Nilimjibu kwa sauti ya unyonge sana :
“Sawa.”
Pale pale alitembea kuelekea nilikokuwa mimi, akaniwekea mkono kichwani.

***
Wiki moja ilikatika toka hayo yatokee, lakini hakukuwa na jipya jingine, sikuwahi kumwona mtu mwingine akinijia nyumbani wala kanisani ninapokuwa nafanya kazi za Mungu.
Lakini siku hiyo, nikiwa nimelala majira ya saa saba usiku, nilishtuka ghafla. Nikatupa macho mlangoni. Kwa sababu ya giza sikuona vizuri, ila dalili ya kama kitasa cha mlango kikifunguliwa.
Nilinyoosha mkono hadi kwenye taa ya kitandani (bed switch) nikawasha kwa umakini sana ili mlio wa swichi usisikike.

Kitasa kikawa kinakaribia chini, lakini kikanata kwa muda. Nadhaani ni baada ya mimi kuwasha taa.
Hali hiyo ilinifanya nitoke kitandani na kusimama katikati ya chumba huku macho yote yakiwa kwenye kile kitasa mlangoni.
Huku taa ikiwa bado inawaka, kitasa kiliendelea kwenda chini, yaani kufunguka, lakini ilionekana aliyekuwa anakifungua yupo makini sana kwani kwa kukitazama haraka tu ilikuwa vigumu kujua kitasa kinafunguka kwa kwenda chini.

Mara mlango ukaanza kusukumwa polepole  na mimi nilisimama nikaza macho kujua nani aliyekuwa akifanya kazi ile. Wazo kwamba ni mwizi sikuwa nalo kwani nawajua wezi, wao ni papara au kushtukiza.
Mlango uliendelea kusukumwa mpaka ukawa wazi wote, yaani kama kuna mtu alisimama kwenye korido angeona chumbani, lakini cha kushangaza hakukuwa na binadamu wala kiumbe chochote nyuma ya mlango.
Nilipotaka kuuliza nani mwenzangu, nikasikia sauti ya mtu kukohoa kwa kujibana. Halafu nikasikia mlio wa viatu, ko! Ko! Ko! Ko! Ukisikika kuingia ndani ya chumba, nikarukia kusimama pembeni kwani niliamini aliyekuwa akiingia angeweza kunikumba.

Mlio wa viatu kutembea uliposimama ukafuata mlio wa kufunguliwa kwa dirisha la chumba, na kweli likawa linafunguka hadi mwisho, halafu pazia ikawa inakunjwa na kufungwa katikati kama vile mkunjaji alitaka upepo uingie kwa vizuri.
Baada ya hapo, nikiwa nimesimama pembeni, mlio wa viatu ukatembea kwa mwendo ule ule wa ko! Ko! Ko hadi ukutani kwenye swichi, ghafla nikasikia tap na giza likatanda. Ina maana huyo mtu alizima taa.
Halafu mlio wa viatu ukaendelea tena hadi usawa wa kitanda, ukakwamba pale. Giza likiwa limetanda, nikasikia hali ya mtu anayepanda kitandani kwani kitanda kilitoa mlio Fulani na baadaye, kama baada ya dakika moja ikasikika sauti ya mtu kukoroma.
“Khooooo! Khoooo!”

Niliamini ni uonevu usiokuwa na maana kwangu kwani sikuwa na kosa la kunifanya nishindwe kulala  na kulala mtu mwingine, nilikasirika sana . Nikatembea kijeuri hadi ukutani na kuwasha taa.
Ile inawaka tu, ile swichi ya kitandani ikasikika ikizimika, tap! Kukawa giza tena.
Niliifuata kwa fujo ile swichi ya kitandani, nikaiwasha na macho yangu yakakimbilia moja kwa moja kitandani. Mtu mnene, mrefu alikuwa amejifunika shuka huku akiwa amenyoosha miguu na anaangalia juu, yaani amelala chali.
“Wewe ni nani?” Nilimuuliza bila woga.
“Msafiri,” sauti nzito ilijibu kwa mkato.
“Ndiyo jina lako au msafiri unakwenda mahali?”
“Siendi popote.”
“Khaa! Sasa hapa kwako?”
“Hapana.”

“Sasa kwanini umefungua mlango bila hodi na umepanda kitandani kulala bila ridhaa yangu?”
“Nisamehe sana .”
“Basi ondoka.”
Kauli yangu hiyo haikupata jibu zaidi ya mlio wa kukoroma kusikika kama mwanzo.
Nilimsogelea yule mtu pale kitandani kwa lengo la kumfunua shuka na kumwona vizuri. Niliishika shuka kwenye ncha moja, nikaifunua kwa nguvu…     
“Ha ha ha ha ha ha!” Alicheka sana yule mtu huku akitoka kitandani na kuficha uso kwa mkono mmoja.
Nilijitahidi sana kuhakikisha namwona uso yule mtu, lakini na yeye alikuwa akawa anaangalia ukutani huku akiendeelea na kicheko chake.
“Wewe ni nani?” Nilimuuliza kwa ukali kidogo.
“Ha ha ha ha! Msafiri bwana, si nilikwambia!”
“Umetumwa?”
“Hapana.”
“Umekuja tu mwenyewe?”
“Ha ha ha ha! Eee!”

Kusema ule ukweli nilichanganyikiwa, kwani sasa nikawa sijui ukweli upo wapi, kila ninachomuuliza ananijibu kinyume na matarajio yangu.
“Basi mimi naomba uondoke humu chumbani kwangu,” nilimwamuru.
“Ha ha ha ha ha! Sawa,” alisema akielekea mlangoni na kutoka kweli lakini nikiwa sijafanikiwa kuona sura. 

Kwa hiyo mpaka hapo nikawa sijui ni nani yule.
Alipovuka tu ukuta wa chumba changu, nikajikuta napata wasiwasi na woga tofauti na mwanzo alipoingia.
Nilifunga mlango ili nipande kitandani kulala, lakini kabla sijapanda, nikasikia vishindo ti ti titi! Watu kama sita walisimama katikati ya chumba changu.
“Mtumishi wa Mungu vipi? Habari za kulala?”
“Salama.”

“Aaa, tumetumwa kwako.”
“Na nani?”
“Aaa, vaa miwani yako kwanza kisha utuangalie vizuri.”
Nilipeleka mkono kwenye stuli ndogo iliyokuwa pembeni ya kitanda na kuchukua miwani, nikaivaa na kuwaangalia.
Walikuwa tofauti na nilivyowaona wakati wanatua. Walikuwa wamevaa viguo vyeusi (kaniki) kukatisha kiunoni kwenda chini ya mapaja, kila mmoja alionekana amekasirika na hana utani na usoni walipaka vitu vyeupe, kama si unga, basi chokaa.
“Unatuona vizuri sasa?”
“Ndiyo.”
“Basi ndivyo tulivyo, toa miwani.”
Nilipotoa tu, walirejea na kuwa kama walivyotua, wamevaa kawaida.
“Unatakiwa kuhudhuria mateso ya waumini wako usiku wa sasa,” mmoja wao aliniambia, wengine wakatingisha vichwa kama ishara ya kukubaliana na maneno ya mwenzao.
“Wapi?”
“Katika kila nyumba yenye muumini au waumini wako.”
“Ni mateso ya aina gani?”
“Utajua huko huko na huna hiyari katika hili, kwani ulishapata baraka zote za uchawi.”

Nilijikuta nasimama, naanza kutembea kuwafuata kutoka nje mpaka uwanjani mbele ya nyumba, wakaanza kutengeneza duara na mimi nikawa mmoja wa wanaduara.
Mmoja akapeleka mikono na kuwashika wa kulia na kushoto kwake, wengine wakafanya hivyo mpaka mimi. Tukawa tumekamatana mikono. Yule aliyeanza kushika, akainama kama dalili ya kusujudia, wengine wakafuatia na mimi pia, kufumba na kufumbua, tukajikuta tukipaa juu na kutua chini ya mti mkubwa wa Mvule. Sikumbuki tulitumia dakika ngapi kuwa angani na kushuka.

Milio ya ngoma iliyotawala pale ilinifanya niamini kuwa, kweli nilikuwa katikati ya maskani ya kichawi.
“Bila kupoteza muda sasa tunaingia mitaani, hasa kwenye nyumba za waumini wa kanisa ambalo padri wao tunaye kwenye kundi letu na kufanya kazi ya kuwatesa, sawa?” Sauti nzito, iliyokuwa ikisikika na kitetemeshi ilisema.

Nilipomwangalia msemaji huyo, ni mzee mmoja aliyekuwa amevaa kanzu ndefu nyeusi, juu, yaani kichwani alivaa pembe za mnyama, mkononi alishika mkia, pia wa mnyama.
“Sawa,” wenzangu waliitikia kwa sauti ya juu.
Kifupi mimi nilikuwa sijui kitu chochote. Nilikuwa sijui watafanyaje huko kwenye kutesa watu, sijui nani atakayeteswa, kama ni waumini wote pia sikujua. Ila, mzee mmoja alinifuata na kuniambia:

“Tuondoke mimi na wewe.”
Nikawa namfuata hadi kando kando ya ule mti mkubwa, akasimama ghafla hadi nikamkumba.
Kufumba na kufumbua, tulitua nje ya nyumba ya muumini wangu mmoja ambaye anamiliki mashine ya kusaga na trekta moja.
“Haa! Hapa si kwa..?”
Kabla sijamaliza kusema, yule mzee akaniambia kwa kunikatisha:
“Ulisikia tulivyoambiwa kule?”
“Kwamba?”

“Tunawatesa akina nani?”
“Waumini wangu.”
“Sasa unauliza nini?” Alinijibu huku akitembea kwa kurukaruka kwa mguu mmoja.
Alipoona mimi nimezubaa akanifuata:
“Jipige kifuani kwa mkono.”
Nikafanye hivyo.
“Hapo sawa sasa, nifuate mimi kwa kila hatua mpaka ndani na kuanza kazi, sawa?” Aliniuliza.
 Inaendelea!!!!!!!!!!!!!!!! Usikae mbali na Irene Mwamfupe Ndauka pande hizi.

          PADRI MLA NYAMA ZA WATU-2
Tulikwenda hadi kwenye mlango mkubwa, nikadhani atagonga ili tufunguliwe, kumbe sivyo bwana.
“Kila ninachofanya mimi na wewe unaniiga, sawa?” Aliniambia akinigeukia, kwani nilikuwa nimesimama nyuma yake.
“Sawa.”
“Haya tunaanza sasa.”
Alijipiga tena kifua na mimi nikajipiga. Kufumba na kufumbua tukawa ndani, sebuleni.
“Sasa niigize kwa kila kitu.”
“Sawa,” nilimjibu kwa sauti ya chini kama ile aliyoitumia yeye kuniambia.
Alitembea kwa kurukaruka kwa mguu mmoja, huku mguu wa pili ukiwa unaning’inia tu. Kwa mimi nilivyoona, hakukuwa na sababu yoyote ya kutembea vile, ila kwa kichawi nadhani ni sawa na ni kawaida kwao.
Na mimi niliruka ruka kwa mguu mmoja huku mwingine ukining’inia hadi kwenye mlango wa kuingia kwenye vyumba, yule mzee akasimama, lakini kwa mguu mmoja.
Tulisimama vile mpaka mimi nikabadili msimamo, nikatumia mguu mwingine maana nilichoka sana .
Ghafla akaweka mguu mwingine chini huku akigeukageuka kuniangalia.
“Sasa tunaingia chumbani kwa baba mwenye nyumba, sawa?”
“Sawa.”
“Una swali lolote kabla hatujaingia?” Aliniuliza.
“Ndiyo.”
“Enhe, lipi hilo ?”
“Haaa…”
“Uliza haraka.”
“Sawa, hatutaonekana?”
“Wapi?”
“Tunakokwenda.”
“Kwani si nimekwambia kila kitu unaigiza kwangu?”
“Kabla sijaigiza je?”
“Hatutaonekana.”
“Basi, swali langu ni hilo tu.”
“Kwa hiyo huna swali jingine?”
“Sina na wala sitakuwa nalo.”
“Oke  nifuate.”
“Niko nyuma yako.”
Aliinua mikono juu, akapiga makofi na mimi nikafanya hivyo hivyo. Kufumba na kufumbua tukawa tumesimama katikati ya chumba.
Yule mzee akanigeukia, akaniangalia lakini hakusema kitu. Mdomo akauangalizia juu na kufanya tendo kama anapuliza moto, na mimi nikafanya hivyo hivyo. Akamsogelea mzee mwenye nyumba aliyekuwa amelala usingizi mzito wa chali, akamkalia tumboni huku akijisotesha kuanzia kiunoni kwenda kifuani na kurudi.
Mimi nikawa mtazamaji tu, lakini yule mzee akaniangalia na kunipa ishara kwamba na mimi nimpandie mke wa yule mwenye nyumba ambaye alikuwa amelala kitanda kingine na mtoto mdogo kama wa mwaka mmoja.
Nilipanda bila kujiuliza maswali kwanini napanda, nikajisotesha kama alivyokuwa akifanya yule mzee, lakini nilipotua macho usoni kwa yule mama ambaye naye alilala chali, nikamjua kuwa ni muumini wangu mzuri pale kanisani.
Kusema ule ukweli niliumia sana moyoni, nikajihisi ni mtenda dhambi nisiyestahili msamaha wa aina yoyote ile.
Lakini ilinibidi niendelee tu na kazi niliyokuwa naifanya kwani ni jukumu ambalo nilishalivalia njuga sikuwa na budi kulimaliza sawasawa na safari yetu ya kuingia ndani ya nyumba ile.
Mara yule mzee alishuka kutoka kwenye tumbo la yule mzee mwenye nyumba huku akinifanyia ishara ya mimi pia kushuka.
Tulishuka wote, tukasimama tukiangaliana. Mara mwenzangu akaufuata ukuta sehemu ya kichwani ya yule mzee, akasimama na kumwinamia kisha akapeleka mkono hadi jirani na shingo yake na kuukunja kama vile ameshika shingo na kumkaba.
Yule mwenye nyumba akawa anarusharusha miguu kama anayeitafuta pumzi baada ya kuziba kwa pua na kinywa, huku akisema maneno yasiyojulikana:
“Mmmh! Mmmmmm! Mmm!”
Alivyokuwa akiendelea kubana mkono ndivyo na yule mtu alivyokuwa akizidi kulalamika, sasa akapeleka mikono kwenye koo lake na kujishika huku akizidi kulalamika.
Alichofanya yule mchawi, akawa anambana huku mkono mmoja anafanya kama anamtisha kwa ngumi ya uso yule mzee. Alipokuja kumwachia, akasimama pembeni yake kisha yule mtu mwenye nyumba akashituka kutoka usingizini na kukaa huku akikohoa sana.
“Mungu wangu, Mungu weee! Ooo! Mama,” alisema akiendelea kushika koo lake.
Akamwita mkewe kwa sauti ya juu, naye akashituka na kumuuliza kulikoni:
“Kuna nini mume wangu?”
“Nimekabwa vibaya sana .”
“Na nani?”
“Najua ni wachawi tu hao.”
“Umejuaje?”
“Wamenishika koo kwa kunikaba kisha wakanipiga ngumi za uso. Kwani huoni kama umevimba?”
“Nini?”
“Uso wangu?”
“Hata, ila macho kama mekundu.”
“Ni hao hao lakini mmoja kama nimemwona.”
“Unamjua?”
“ Kama namjua.”
“Ni nani?” 
“ Kama ..!”
“Vipi tena mume wangu?”
“Tumbo nalo kama limejaa, ooo linauma sasa, wachawi hao mke wangu.”
Mara mkewe naye akaanza kulia huku akishika tumbo lake na kulalamikia.


Moyoni nilitamani sana yule mzee atokee ili akabiliane na zile tuhuma zile ambazo mimi zilinifika shingoni na niliingiwa na kinyongo na kazi ile ya kichawi ambapo awali niliambiwa hakuna ambaye angeweza kutuona wakati tukiwa kwenye matukio yetu.
“Eee Bwana niepushe na aibu hii, sirudii tena mimi, nimeshajirekebisha,” nilisali kimoyomoyo peke yangu pale mbele ya madhabahu. Nikajikuta nakohoa pia bila sababu.
Ghafla mzee mwingine akanyoosha kidole, wakawa wawili sasa. Lakini pia wakati yule akiendelea kuongea na vile vidole viwili vikiwa juu, mke wa yule mzee aliyekuwa akiongea naye akanyoosha kidole.

 “Mbaya zaidi, watu waliotuingilia kutufanyia hivyo huwezi kuamini ukiambiwa, hii ni aibu kwa kanisa na pia ni kufa kiroho. Mungu hawezi kuuvumilia ubaya huu.”
Wakati anazidi kubomoa, mimi haja ndogo ilinibana, nikawa navumilia tu.
Nilitamani ardhi ipasuke, mimi niingie ndani mwake na nisionekane tena maishani mwangu. Mwili ulinitetemeka, akili ikanipotea, nikawa sijui niamue nini.
“Hali ikiwa hivi kuna siku humu huku kanisani watu watashikania mapanga kutoana damu, hakiyanani vile.”
Yule mzee alipomaliza kusema hayo, akaa ghafla kama vile alishikwa na kukalishwa kwa nguvu.
Nikataka kusema muda umekwisha, lakini mzee mmoja kati ya wale walionyoosha vidole alisimama hata bila kuruhisiwa, alipoona mwenzake amekaa tu.
“Nashukuru sana na mimi kwa kupata muda huu. Zamani uchawi hapa kanisani ulikuwa ni msemo tu, si kitu ambacho kinatingisha, lakini mimi nina habari kwamba, sasa uchawi umo ndani kabisa ya hili kanisa, tena washiriki ukitajiwa majina unaweza kubisha hadi unaanguka chini.
“Mimi kama nitapata baraka za waumini wenzangu niko tayari nitaje majina, lakini nilindwe.”
Nilimwangalia vizuri yule mzee nikamwona kama ametumwa, kwani wakati anaongea, hakuwa ananiangalia mimi, wala mtu mwingine, alaiinama tu huku akibwabwaja.
“Sema.”
“Wataje.”
“Waweke wazi bwana.”
“Tutajie.”
“Tuambie.”
Hayo yalikuwa maneno ya waumini wa kanisa lile ambayo yalinichanganya kabisa. Baadhi ya waumini wakawa wanainama kunong’onezana huku wakiniangalia kwa kuniibiaibia.
“Niwataje?” Yule mzee aliuliza tena kwa sauti ya juu.
“Watajeeee.”
Wakati huo, yule mzee mwingie na yule mke wa yule wa kwanza, vidole vyao vilikuwa bado juu wakiomba nafasi ya wao kuongea.
“Eti niwataje?”
Inaonekana aliniuliza mimi kwani aliniangalia. Na hapo ndipo nilipojua kuwa, hata mimi niko ndani ya tuhuma za kutajwa kwani kama nisingekuwemo, yule muumini angeniuliza hivi, ‘eti mtumishi wa Mungu niwataje?’ sasa hakusema mtumishi kwa sababu alishajua sina cha utumishi wala uchungaji.
“Nalinda heshima ya kanisa, siwataji, ila nawataka waache mara moja tabia hiyo,” alimaliza yule mzee na kukaa.
Ghafla tena akasimama mzee mwingine hiku akiendelea kunyoosha kile kidole chake.
Jamani muda naona umetuishia, siwezi kuruhusu mambo hayo, ila nitaunda kamati ya kushughulikia, matokeo yatatangazwa humu humu kanisani.
“Lini?” Waumini walihoji kwa pamoja.
“Eee, Jumapili ijayo.”
“Tuhakikishie.”
“Ha! Niwahakikishie kwani mimi ndiye mchawi?” Nilijibu kwa jabza sasa.
“Mh!”
“Mh!”
“Mh!”
Waumini waligunia chini kwa chini. Sasa sikujua waliguna kwa sababu ya majibu yangu au kwa sababu walishajua mimi ni mchawi. Hiyo iliniuma sana , lakini sikuwa na jinsi zaidi ya kusema hivyo.
Kilichonishangaza zaidi hata wale wazee wenye hekima zao katika kanisa hakuna aliyetoa sauti kuongea kitu kwa kunitetea wala kutengeneza amani.
Nilimaliza ibada, watu wakatoka nje mmoja baada ya mwingine. Lakini kule nje wakasimama katika makundi makundi isivyo kawaida.
Halafu wakawa wanaonekana wakiongea kwa tahadhari sana, kwani kila mara walionekana kuangalia mlango wa kuingilia kanisani na wa ofisini kwangu.
Na mimi nilitoka nje na kuiacha ofisi tupu, nikasimama ili kuangalia nini kinaendelea kwa waumini wangu, lakini nao wakaanza kutimka mmoja mmoja.
Hoja kwamba walinigundua mimi ilipata nguvu baada ya baadhi ya waumini kunipita tu wakati wanaondoka wakati su jambo la kawaida kwao.
“Mama,” nilimwita muumini mmoja, akasimama. Mimi ndiyo nikamfuata aliposimamia.
“Mama kwani kuna nini leo?” Nilimuuliza.
“Hujui?”
“Sijui kitu.”
“He he! Uchawi kanisani,” alisema.
“Sasa mbona watu wananitenga?” Nilimuuliza, lakini badala ya kunijibu akaondoka zake haraka.
Ghafla nikasikia mlango wa ofisini kwangu ukigongwa kwa nguvu kama kuna mtu ndani, nikaenda haraka.
Kufika nikamkuta yule mzee tuliyekwenda kuwanga naye usiku nyumbani kwa wale waumini.
“Umefanya nini sasa? Ona yaliyokupata.” Aliniuliza kwa hasira sana .
 “Kwani kosa langu ni nini?” Nilimuuliza na mimi nikiamini sikuwa na hatia, bali yeye ndiye aliniingiza mkenge.
“Wewe umekwensa kanisani bila kumwomba mkuu kwa sala.”
“Mkuu gani?”
“Kwani mkuu wako kwa sasa ni nani?”
“SI Mungu!”
“Ha ha ha ha! Siyo Mungu, Mungu yupi kwanza, yule wako wa zamani?”
“Hata sasa.”
“Amekwambia nani, hujui kama umeshasajiliwa kwa mkuu wa giza ? Kuanzia siku ile pale wewe ni wa mkuu wa giza kama sisi.”
“Oke, turudi kwenye msingi wa maongezi, kosa langu ni lipi?”
“Kosa nimeshakwambia, leo kanisani kila mtu amekushangaa wewe kwa jinsi ulivyokuwa umevaa nguo za kulalia madhabahuni, lakini wewe mwenyewe ulidhani uemvaa joho.”
Moyo ulinilipuka lip. Nikashangaa sana huku nikijiuliza maswali mengi na kuvuta picha ya jinsi nilivyoonekana.
Lakini mpaka hapo, nilipojiangalia mwenyewe nilikuwa nimevaa joho la utumishi, sasa hizo nguo za kulalia ni zipi!
“Mbona nimevaa inavyotakiwa?” Nilimuuliza.
“Ndivyo unavyojidanganya?”
“Kh! Si hivi, kwani we hunioni?”
Yule mzee alicheka, akaangalia chini kisha akatembeza mkono wake chini kama anafuta, ukawa na vumbi kisha akanipaka lile vumbi usoni kwangu.
Pale pale nilipojiangalia, kweli nilionekana nimevaa pajama ya kulalia, ya chini na ya juu.
Nilishtuka zaidi, mwili ukaingiwa na ganzi na kuanza kuhisi mshangao niliousababisha kwa waumini wangu, nikaanza kupitia maongezi ya wale waumini waliosimama kuongea wakisema hivi:
“Mbaya zaidi, watu waliotuingilia kutufanyia hivyo huwezi kuamini ukiambiwa, hii ni aibu kwa kanisa na pia ni kufa kiroho. Mungu hawezi kuuvumilia ubaya huu.”
 “Hali ikiwa hivi kuna siku humu humu kanisani watu watashika mapanga kutoana damu, hakiyanani vile.”
(Mzee mwingiune anasimama).
 “Nashukuru sana na mimi kwa kupata muda huu. Zamani uchawi hapa kanisani ulikuwa ni msemo tu, si kitu ambacho kinatingisha, lakini mimi nina habari kwamba, sasa uchawi umo ndani kabisa ya hili kanisa, tena washiriki ukitajiwa majina unaweza kubisha hadi unaanguka chini.
“Mimi kama nitapata baraka za waumini wenzangu niko tayari nitaje majina, lakini nilindwe.”
 “Sema.”
“Wataje.”
“Waweke wazi bwana.”
“Tutajie.”
“Tuambie.”
 “Niwataje?”
“Watajeeee.”
 “Eti niwataje?”
 “Nalinda heshima ya kanisa, siwataji, ila nawataka waache mara moja tabia hiyo.”
“Niachieni mimi, nitalifanyia kazi na matokeo yatatangazwa humu kanisani.”
“Lini?”
“Eee, Jumapili ijayo.”
“Tuhakikishie.”
“Ha! Niwahakikishie kwani mimi ndiye mchawi?” (Waumini wanaguna).
“Mh!”
“Mh!”
“Mh!”
(Anamwita muumini mmoja nje).
 “Mama kwani kuna nini leo?”
“Hujui?”
“Sijui kitu.”
“He he! Uchawi kanisani.”
“Sasa mbona watu wananitenga?”
(Yule mama anaondoka haraka).
“Oooph! Kweli nitakuwa nimeumbuka sana , sasa?” Nilimuuliza yule mzee baada ya kuwaza hayo yote yalivyokuwa kwenye ibada.
“Hakuna cha sasa, hapa kampeni moja tu, kuhakikisha wale wote waliosimama kuuliza maswali wanakufa.”
“Mh! Kwa njia gani. Halafu na wewe una makosa, kwanini usije kunishtua pale madhabahuni kuwa nimevaa pajama?” Nilimwambia na kumuuliza yule mzee.
“Nilijitahidi lakini kukufikia pale mbele ikawa kazi. Unajua makanisa karibu yote yana nguvu ya Mungu mbele, huwezi kufika kirahisi. Mimi nilisimama kushoto kwako nikawa nakuangalia.”
 Tukiwa tunaongea hayo, mara mama mmoja akasimama mbele yetu, ni muumini wa kanisani lakini sikujua kama ni mchawi.
“Leo padri umechemsha sana.”

Mwili wote ulikufa ganzi tena, nikahisi roho inataka kumrudia aliyeiumba, mwili kwenda mavumbini.
“Kwani unadhani mimi sijui kitu kuhusu wewe kujiunga na Mungu wa giza , najua.”
Niliendelea kumkodolea macho ya mshangao.
Yule mzee alimwangalia sana , akamuuliza.
“Wewe upo kwenye kambi ya mzee Masomo?”
“Ndiyo,” alijibu yule mwanamke lakini akionekana kama hana habari sana na yule mzee kuliko mimi. Akaniuliza.
“Ni kwanini umeamua kumtumikia Mungu wa upepo?”
“Sijamtumikia mimi,” nilimjibu kwa hasira.
Wote, yaani yule mwanamke na yule mzee wakacheka.
“Umechelewa sana, kama unataka kufa endeelea kusema hivyo,” yule mzee aliniambia kwa sauti ya kukazia, nikaogopa mwenyewe.
Yule mwanamke akasimama sawasawa kisha akainama kidogo aliponyanyua shingo, akasema:
“Padri mimi nimekuja na ujumbe wako, naamini utaupokea na utaufanyia kazi haraka sana, naomba uupokee.”
“Ujumbe gani na umetoka kwa nani?” Nilimuuliza nikimwangalia kuuona huo ujumbe wenyewe, kama ni barua au maneno tu.
 “Ni maneno tu Padri,” alisema huku yule mzee akimkazia macho.
“Una maanisha nini?”
“Kwani hujui?”
“Ningejua nisingekuuliza.”
“Ulikujaje kanisani vile?”
“ Hilo ndilo tunalolizungumza hapa.”
“Hapa hatuzungumzi, ni kuachana na huyu, sisi tukutane usiku kwa ajili ya kupanga mikakati mizito mizito ya kuua wale wote walijidai ni vinara kwa kusimama na kusema sema ovyo,” alisema yule mzee.
Tulikubaliana kuwa hivyo, wote tukatoweka, kwa ahadi ya kukutana usiku ili kupanga hiyo mikakati mizito ya kuua.

***
Ilikuwa ni usiku wa saa sita, nikiwa nimemaliza kusali kwa Mungu wangu, sasa nausaka usingizi mwingine wa awamu ya pili.
Nilipokuwa naanza kusinziasinzia tu, nikasikia kishindo tii!
Nikashtuka na kuangalia mle chumbani, nikaona miguu ya watu karibia kumi, lakini  niliona kuanzia miguuni hadi kwenye magoti, lakini kwa upande wa nyuma.
Hii miguu ilikuwa minene, na ilitembea kwa mwendo wa pole kutoka pale iliposimama kuelekea ukutani.
Halafu ghafla nikawa naona ile miguu inaongezeka katika kuonekana kwake, yaani inaonekana zaidi ya magotini na kuelekea juu hadi kwenye mapaja.
Nikasikia sauti nzito:

“Sisi ni wenzako, tumekuja, amka.”
Niliamka polepole kitandani mpaka nikakaa, nikaangalia kulia na kushoto, wote wakajionesha moja kwa moja. Wengine niliwafahamu, wengine sikuwafahamu.
“Simama,” yule mzee wangu alisema akiniangalia na tena akawa ananyoosha mkono kuelekea kwangu kama vile alikuwa akitaka na mimi nimpe mkono wangu ili anishike.
Nilinyoosha mkono, nikamshika, naye akanishika, nikasimama lakini mwili ukiwa mzito sana.
Nilipoweza kusimama vizuri mwenyewe, mwanamke mmoja akanirushia nguo nyeusi, ikanivaa mwilini, watu wakapiga makofi chumbani kwangu, nikashangaa sana kwani sikuona ni jambo la kawaida watu wengi kuwemo ndani ya chumba changu na kupiga makofi na kelele za vifijo kwa wingi.
Yule mzee akasema wote tushikane, yaani kila mmoja aliposimama amshike mwenzake mkono, wote tukafanya hivyo, tukashikana mikono.

Kufumba na kufumbua tukawa kwenye mti mmoja mkubwa sana , chini palikuwa na moto mkubwa uliokuwa unawaka kwa kasi huku waliouzunguka moto ule wakiwa wanacheza ngoma ya kienyeji.
Kufika kwetu kukasababisha wasitishe ngoma na kuungana na sisi, wote tukasimama mstari mmoja.
Tukiwa mstarini, mzee mmoja akasimama mbele na kusema kuwa, mkutano ule ulikuwa ni maalum kwa ajili ya kunisimika mimi kuwa kiongozi wa kundi mojawapo la wachawi akidai naweza.
Nilinyoosha mkono ili kupinga, lakini wachawi wote walikataa wakisema aliyoyaongea bosi wao ni ya kweli kabisa.
Basi, nilipitishwa mbele huku nikiwa sijui itakuwaje na wachawi wengine walinisindikiza huku wakipiga makofi kwa furaha ya mimi kusimikwa.

“Haya, piga magoti hapa,” yule mzee aliniamuru.
Nilipiga magoti kwa unyenyekevu wa hali ya juu huku nikishikanisha mikono kama ninavyokuwaga mbele za Mungu wangu.
Yule mzee alinishika kichwa, pale pale mwili wote ukabadilika, nikajiona shujaa, jasiri, sina woga na wala siogopi kitu cha kufikiria au kuonekana.
Kisha akaanza kusema maneno ya kilugha na sijui alikuwa akitumia lugha gani.
Alitumia muda wa kama dakika tano kusema kilugha alipokuja kubadilisha, akasema Kiswahili na pale pale nikahisi nipo usingizini, nikaota ndoto.
Nilikuwa nikipita kwenye kundi la watu nikiwa uchi wa mnyama, lakini watu walikuwa hawanioni kama napita na nikaelekea kwenye ukingo wa barabara huku nikiwa nawashika vichwa watu niliokuwa nawapita.
Hakuna aliyejua hata kwa dalili kama kuna mchawi anapita katikati yao, hivyo nikajiona ni jasiri na mjanja kuliko wajanja wengine wote wa dunia hii ya mambo na vituko.

Niliposhtuka kutoka katika ndoto hii, nilijiona nipo bado chini na wachawi wenzangu wakiniangalia kwa macho ya ushindi.
Nilisimama haraka, nikasema:
“Si muda wa kupoteza huu, wako wanaojifanya wanajua, lazima wakatoke uhai.”
“Ndiyo,” wachawi wakaitikia.
“Na sasa kila wote mjipange vikundi vitano, vya watu wanne wanne na kwenda kukabiliana na uovu huu, mume makini sana,” nilisema.

“Sawa, tutakuwa makini,” walisema kwa pamoja.
Nilipomaliza kusema, niliwachagua wachawi watatu na mimi wa nne, wengine wakachaguana hivyo hivyo, safari ya kwenda kuvamia nyumba za wale watu waliojifanya wana maswali mengi kanisani ilianza pale pale huku mimi nikiwa jasiri kabisa, siogopi mtu wala sihofii maisha yangu ya baadaye.
“Mtakuwa mnanifuata mimi ninavyofanya, sawa jamani?” Niliwaambia watu wangu huku tukisonga mbele.
“Sawa mkuu.”
 “Nilitembea kukanyaga ardhi huku wachawi wakinifuata kwa nyuma, kila nilipotoa mguu, nyuma yangu alikanyaga mtu.
Tuliingia kwenye nyumba moja ya miongoni mwa wale watu waliosimama kuuliza kule kanisani.
Wote tulifikia sebuleni, nikasimama na kuinua mikono huku nikisema kila jicho la mtu aliye ndani ya nyumba hii lisituone, hata kama lina nguvu.

Nilipomaliza, nilitangulia mbele, nikasimama kwenye mlango wa chumba, lakini hatukujua ni cha nani.
Nilichofanya, niliufanya mkono kwa ishara kama nafungua pazia la dirisha ili mwange upite, pale pale  tukaona ndani ya chumba, walilala watu watatu kwenye kitanda kimoja kidogo, lakini tukajua ni watoto.
Mimi nikageukia mlango mwingine ambao nao ulikuwa umefungwa, nikafanya vile vile kama mwanzo, mlango na ukuta vikayeyuka, chumba kikawa wazi.
Kitandani walilala watu wawili, tukajua ni mke na mume. Nikiwa kama kiongozi wa msafara, sikutaka tuingie ndani, nilinyoosha mkono, nikafanya ishara kama ya kuwaita waje pale mlangoni tuliposimama sisi wachawi.
Nilikuwa nachezesha kiganja kwa staili ya kuita, nachezesha, nachezesha, mpaka wakainuka kitandani na kukakaa. Walifanya hivyo kwa pamoja, yaani mke na mume.

Walitutumbulia macho, nikajua wanatuangalia sisi, wakakaza macho sana kwetu, lakini hakuna aliyeonekana kututambua. Nikazidi kuwaita kwa kutumia ile ishara ya mikono.
Taratibu walianza kutoka pale kitandani huku wakiziacha shuka zao mpaka waliposimama wima wakasita kutembea. Ilibidi nitumie tena njia ile ile ya kuwaita kwa ishara ya kiganja cha mkono, wakaanza kutembea kuja mpaka mlangoni.
Mambo hayo yalikuwa yakifanyika kwa mwendo wa pole pole sana mpaka wakatufikia, na mimi nikagueka, wachawi wenzangu nao waligeuka, wote tukaanza kutembea kwenda nje ya nyumba hiyo.
Ulikuwa uwazi mkubwa nje, ni eneo ambalo unaweza kujenga nyumba hata mbili. Nilisimama na kuwaambia wenzangu watengeneze mduara, wakatii.

Mduara ule uliwaweka kati wale watu wa familia tuliowatia ndani kwao. Wakiwa kati, niliinama na kuchota mchanga, nikawarushia, ukawamwagikia, wale watu wakawa wadogo kama mpira, nilikuwa wa kwanza kuwafuata na kuwapiga teke kama mpira, wachawi nao wakaja na kuanza kuwacheza kama mpira. Ikawa vurugu ndogo pale nje, huyu anapiga, yule anadaka, yule anaurusha.
Tulifanya hivyo mpaka kunakaribia kucha, kama kwenye saa tisa na nusu usiku, nikasitisha. Nilichota mchanga na kuwamwagia tena, wakarudi katika hali zao za kawaida.
Nilitangulia ndani, wakafuata wale wana familia, baadaye wakaja na wachawi wenzangu.
Tuliwaingiza hadi chumbani kwao, sisi tukasimama pale mlangoni, wao wakaenda mpaka kitandani, wakapanda na kulala tena kwa kujifunika gubi gubi.

***
Asubuhi, kwenye saa tatu nilitoka kwenda mjini, njiani nilisimamishwa na mwanamke mmoja, akanisalimia vizuri sana.
“Padri, umesikia uchawi unavyoshika kasi kwenye eneo lako?” Yule mwanamke aliniambia, nikajifanya kushangaa, lakini nilishangaa kweli, maana sikujua alikuwa na maana gani.
“Imekuwaje tena?” Nilimuuliza nikimkazia macho.
Aliniuliza kama namfahamu mzee…(jina).
“Ndiyo namfahamu, kafanyaje?”

“Basi, wachawi wamewaingilia usiku wamewachukua na kwenda kuwalimisha usiku kucha, wameamka asubuhi wakiwa wamechoka sana, wamechafuka pia.”
Nilijifanya kushtuka na kwamba siyajui hayo huku ukweli ni kwamba, kila kitu alichokiaongea mimi ndiye nilikuwa kinara ingawa si kweli kwamba tuliwalimisha.
“Sasa waliwatambua?”
“Hapana, mchawi unaweza kumtambua?”
“Kweli huwezi.”

“Eee, mchawi hata akiwa baba yako au mama yako, anaweza kukuingilia na usimjue, labda kama una malaika wakali,” alisema.
Tuliagana, akaendelea na safari yake na mimi na safari yangu. Mbele nikasimamishwa na mzee mmoja, huyu mzee tunaelewana sana kupita wote wanaoabudu katika kanisa lile.
“Bwana nilikuwa nataka kuja kwako,” alisema.
“Sasa?”
“Sasa basi, labda niongee hapa hapa.”
“Ongea mzee wangu.”

Alianza kwa kuniambia kuwa, kuna watu wanajiandaa kwenda kwa Askofu kutoa malalamiko kuhusu siku ambayo mimi nilipanda madhabahuni na pajama badala ya mavazi ya kitumishi.
Nilishtuka sana kusikia hivyo, nikamuuliza majina ya hao wazee, miongoni mwao ni wale wote waliosimama siku hiyo na kujifanya wanajua zaidi, akiwemo yule tuliyemcheza mpira yeye na mkewe usiku.
“Aaa, sasa kwani kuvaa pajama jamani si bahati mbaya tu, wao walichukuliaje?”
“Wao walichukulia ulikuwa unatuwangia. Na hivi sasa kanisa limegawanyika, wengine wanasema wewe ni mwanga, wengine wanakataa, Padri hawezi kuwa mwanga.”
“Wewe unanichukulia mimi ni nani?” Nilimuuliza yule mzee.
“Ni mtumishi wa Mungu aliye hai.”

“Sawa, usimwambie mtu maneno hayo, waache wafikirie hivyo hivyo.”
Tuliagana, akaondoka zake lakini mbele kidogo, nikasimamishwa na mwanamke mmoja, mzee sana, yaani bibi kizee, sijawahi kumwona hata siku moja. Lakini kwa rika langu angeweza kuwa mama yangu mzazi.
“Shikamoo mama.”
“Marhaba, hujambo mwanangu?”
“Sijambo mama, haya unasemaje?”
“Ah! Nina usemi basi, njaa tu.”
“Hujala mama?”
“Nimekula, tena nimeshiba sana ,” alinijibu.
“Sasa njaa ya nini?”
“Nyama.”
“Nyama! Nyama gani mama, ya ng’ombe?”
Badala ya kunijibu, alinisogelea hadi mlangoni kabisa kwenye gari, akanyoosha shingo ili kunifikia sikioni.
“Nyama nzito.”
“Mh! Mama, mbona sijakuelewa, nyama nzito ni ipi?”
 Inaendelea!!!!!!!!!!!!!!!! Usikae mbali na Irene Mwamfupe Ndauka pande hizi.
 --------------------------------------------------------------
           PADRI MLA NYAMA ZA WATU-03
“Ile yenye minofu minene.”
“Mbona siijui, ya nguruwe?”
“Hapana, ya mtu! Najua unaweza kufanya nikapata.”
Damu zilinisisimka mwili mzima, nikahisi kupoteza fahamu huku nikiwa nawaza yule mama alinifikiriaje au alisikia nini kuhusu mimi mpaka kusema maneno yale.
“Sasa mama, mimi nyama ya mtu nitaipata wapi?”
“Popote pale.”
“ Kama wapi?” Nilimuuliza.
“Utanipa hunipi?” Aliuliza kwa sauti ya juu sasa.
Nilitaka kufunga kioo cha gari niondoke, lakini kwa vile sikuwa nimemjua kiundani sana, niliamua kuacha.
“Nataka uniletee nyumbani kwangu usiku wa leo.”
“Wapi?”

“N’takuonesha,” alisema huku akianza kutembea kwenda upande mwingine.
Sikujua atanionesha kwa mimi kumnyima nyama ya mtu au wapi atapatikana ili nimpe hiyo nyama. Niliamua kumpuuza na kuendelea na safari yangu.
Nilifika njia panda moja ambapo nilitakiwa kwenda kulia, lakini nikaona kuna mlima upande huo ambapo kawaida huwa hakuna mlima kama nilivyoona pale.
Nilisimama kwa muda wa kama nusu dakika nikiuangalia ule mlima. Ulianza kurefuka, ukaendelea kidogo kidogo huku ukiota majani ya kijani pembeni. Urefu wake ulizidi hata mlima Kilimanjaro, lakini kufumba na kufumbua ukafutika na kusindikizwa na sauti nzito.
“Huo urefu wa mlima ndiyo utakuwa wako katika ulimwengu wa kichawi.”
Ile sauti ikakata, barabara ikaonekana kama kawaida, nikaelekea upande huo.

***

Usiku wa siku hiyo, nikiwa nyumbani, nilianza kumfikiria yule mama aliyesema anataka nyama ya mtu na alivyoondoka. Pia nilifikiria ni kwanini baada ya kuondoka tu, mbele ya safari yangu ndiyo mlima  mkubwa ukachipuka kimaajabu?
Nikiwa bado nawaza, nikachukuliwa na usingizi mzito sana, kuja kushtuka nikasikia filimbi ya kuitwa kwenye makutano yetu wachawi.
Nilisimama, nikageuka kuangalia kitandani, nikanyoosha mkono pembeni na kuchukua shuka jeupe, nikalivaa kama taulo, kufumba na kufumbua nilikuwa kwenye makutano yetu. Waliokwishafika walikuwa wakipiga ngoma na kucheza huku wote waliokuwa wakicheza wakitumia mguu mmoja kutembelea eneo lile lote.
Baada ya wachawi wengi kufika, nilisimama katikati yao na kunyoosha mikono yangu juu, wakatulia, nikapiga makofi, wote wakaunga kwa makofi.
“Pa pa pa pa pa!”

Kabla sijasema, mwanamke mmoja wa kanisani ambaye pia ni mchawi alipita mbele akasimama jirani yangu, huku akiinamisha kichwa akasema:
“Unanikumbuka mkuu?”
Nilimwangalia kwa umakini sana, nikawaza kwanini anasema vile wakati wachawi wote wa kanisani tunajuana na ni siri yetu.
“Nakufahamu vizuri sana ,” nilimjibu nikimkazia macho.
“Uliniona wapi?”
“Khaa! Wewe si tuko pamoja hapa na pia kule kanisani?” Nilimhoji.
“Ndiyo najua, lakini je hukumbuki leo tumeonana mahali?”
“Sikumbuki, labda unikumbushe wewe.”
Alinikazia macho huku taratibu akianza kuzeeka na nguo alizovaa zikianza kubadilika. Ilifika mahali akawa ni yule bibi kizee aliyeniomba nimpatie nyama ya mtu na akasema atanionesha.
     Mpaka hapo nilikuwa siunganishi tatizo la kuona giza na uwepo wa wale waumini wawili wa ajabu ajabu.
“Mtumishi wa Mungu kwema?” Nilisikia sauti ikiniuliza.
“Siyo kwema kabisa.”
“Unaona nini mbele?”
“Naona giza .”
“Fumba macho.”
Nilifumba.
“Haya fumbua sasa.”
Nilifumbua.

Nikaendelea kuona kama kawaida, lakini hakukuwepo na mtu yeyote aliyesimama mbele, nyuma, kulia wala kushoto kwangu.
Lakini pamoja na hali hiyo, niliisaka ile sauti akilini mwangu na kuigundua kuwa, ilikuwa ya yule mzee aliyekaa jirani na wale watu wa ajabu.
“Khaa!” Nilijikuta nikishangaa sasa.
Nilitembea kwa mwendo wa haraka hadi kwa waumini waliokuwa wamesimama nje ya kanisa wakiongea, wengine wakisalimiana na kuulizana maisha, kwani waumini wengi huitumia Jumapili kuonana na kuongea mambo yao mbalimbali ya maisha.

Nilizungusha macho kumwangalia yule mzee, nikamwona katikati ya watu akicheka na kupiga soga na wazee wenzake, nikamfuata, lakini huku waumini ninaowapita wakinisalimia, wengine wakionekana kutaka kujua kile kisa cha ndani ya kanisa.
Wakati nakaribia kumfikia, nilijiuliza mwenyew, je, kweli kwa sauti ile kama angekuwa ni yeye angeshafika katikati ya watu?
“ Kama ni hivyo, mbona sasa wakati nafumbua macho sikumwona mbele yangu?”
“Faza pole na majukumu bwana,” yule mzee niliyekuwa namfuata alinisalimia na kuwawahi wenzake wote aliyosimama nao. Sauti yake niliikumbuka vizuri sana , ndiyo ile iliyonielekeza mpaka nikafumbua macho.
“Nimeshapoa mzee wangu.”
Wazee wengine nao pia wakanisalimia huku wakinipa mikono.
“Eti mzee ulikuwa unasemaje?” Nilimuuliza yule mzee.
“Wapi?” Na yeye aliniuliza.
“Hukusimama na mimi pale mlangoni?”
“Mlangoni! Wapi?”
“Kule kwenye chumba?”
“Hata, hapana.”
Wazee wengine nao wakaonesha kunishangaa mimi, nikajisikia soni kwa nafasi yangu ya u-Padri.
“Oke, sawa basi.”
Nilitembea kwenda kwenye ofisi yangu, lakini nyuma nikamsikia mzee mmoja akisema.
“Kwani mzee Makwaya imekuwaje?”
“Sijui chochote,” mzee Makwaya alijibu, hali ya mshangao na minong’ono ya chini kwa chini iliendelea hadi ilipofika mahali nikawa siwasikii.
Kule ofisini nilikuwa peke yangu, nikainamia mezani na kuwaza ile hali mwanzo hadi pale ilipofikia nikaona giza nene mbele yangu.
“Hivi, wale ni akina nani?”
“Ni kwanini walinijia kanisani?”
“Wametumwa au?”
Nikiwa naendelea kuwaza hivyo, mara nikasikia sauti ndani ya ofisi.
“Unaendeleaje mtumishi wa Mungu?”
Ilikuwa ni sauti ya yule yule mzee Makwaya.
Nilishtuka sana , nikaangalia kila kona ya ofisi.
“Hakuwepo popote pale jambo lililonifanya nizidi kuogopa.
Nikiwa natafakari huku kijasho chembamba kikinichuruzika, mara nikasikia kishindo kikuu kwa nje kama vile kuna kitu kizito kinatua toka juu kwenda ardhini.

“Wewe ni nani?” Niliuliza lakini sauti yangu ikitoka kwa woga.
Sikusikia jibu wala sauti yoyote, ulipita ukimya, nikaendelea kutafakari huku kama nashikwa na usingizi mzito na macho yangu hayaoni.
Ghafla nilihisi kiumbe kusimama mbele yangu, nikajitahidi kufumbua macho.
Niliona binadamu mwenye mguu mmoja, sikio moja, mkono mmoja, tundu moja la pua, jicho moja amesimama mbele yangu akiachia tabasamu la kutisha.
“Kwa jina la baba na la mwana na la…”
Kabla sijamaliza kusema, alipotea mbele yangu, lakini bado macho yangu yakawa yana kivuli chake kwani alikuwa wa kutisha sana sijapata kuona mfanowe.
Nilitamani waumini wangu, hata mmoja tu aje, lakini ajabu ni kwamba hakukuwa na dalili na si haikuwa kawaida yao, kwani mara zote, kila baada ya ibada waumini walikuja ofisini kwangu na kueleza matatizo yao.
Ilifika mahali nikahisi labda siko mahali salama, labda mimi niliona nipo ofisini lakini kumbe sikuwa ofisini, ingawa nilipojaribu kutupa macho huku na kule, akili yangu iliamini niko ofisini kwangu.
“Ngo ngo ngo.”
Mlango uligongwa.

“Karibu, ingia,” niliitikia haraka.
Waliingia wanawake wawili, wakiwa wamejitanda vitenge hadi kichwani na kubakiza uso tu. Walikuwa wageni machoni pangu, nikiwa na maana sijawahi kuwaona hata siku moja katika maisha yangu ya utumishi.
“Karibuni sana akina mama.”
Hakuna aliyejibu hata kwa kutingisha kichwa.
Waliangalia wenyewe sehemu ya kuketi, wakaketi na kunikazia macho mimi.
Na mimi niliwaangalia kwa uso wa kuwauliza shida yao . Lakini hakuna aliyesema mpaka mimi nilipotoa sauti yangu.

“Niwasaidieni nini akina mama zangu?”
Ajabu iliyotokea hapo sijapata kuona wala kuisikia siku yoyote ile.
“Tuna shida na wewe Padri,” alisema mmoja, lakini kwa sauti nene na nzito,  ya kiume.
Kwanza nilishtuka sana kusikia sauti ya kiume ikitoka kwenye mwili ule mwembamba.
“Shida gani mama zanguni?” Niliwauliza kwa sauti yenye woga woga kwani sasa nilianza kuyaona maisha yangu kama yanajaribiwa.
“Tunataka kuwa na wewe kazini kwetu,” alisema yule wa pili ambaye naye sauti yake ilikuwa nene zaidi kupita ya wa kwanza hadi nikajikuta nikitetemeka.

“Mna…mnanitaka kwe…kwenye kazi gani?” Niliuliza huku sauti yangu ikitetemeka kwa wasiwasi mkubwa moyoni, jasho jembamba lilizidi kuchuruzika licha ya kwamba nilipoingia niliwasha pangaboi.
“Ina maana hutujui?” Wote walisema kwa wakati mmoja huku wakisimama na kujivua vitenge. Nilishangaa sana kuwaona wamebaki na suruali  na mashati, ina maana kumbe  ni wanaume kama mimi na walivaa vile kike ili kinipoteza mawazo ya awali, niliwaza kwa wasiwasi huku nikiwakodolea macho pima.
“Mtumishi wa Mungu aliye hai, tunakutaka kwenye kazi yetu bwana, eee?”
Mmoja wao alisema akinisogelea nilipokuwa nimekaa mimi. Sasa niliibaini sauti yake, ndiyo ile ya yule mzee muumini wangu.

“Nyinyi si mliingia kanisani kwangu loe mkawa mnafanya maajabu?”
“Eee, ni sisi,” walinijibu huku yule wa pili naye akisimama, akanisogelea na kusimama sambamba na mwenzake.
“Sasa mnataka nikafanye kazi gani na nyinyi, ya maajabu kama nyinyi?”
“Eee, ndiyo,” walijibu wote.
“Mnatoka wapi?”
Mmoja wao akajibu:
“Tunatoka kwa Mungu.”
“Yupi?” Niliwauliza huku nikiwa nataka kusema ‘kwa jina la baba na la mwana…lakini wakaniwahi wao kwa kusema:

“Mungu kama wako, ametutuma kwako, amesema unatakiwa kupata nguvu ambayo na sisi tunayo, kwa hiyo na sisi tunakupa nguvu hii, POKEA!”
Waliposema ‘pokea’ walinigusa kwa pamoja kwenye paji la uso, nikaanguka chini na kupoteza fahamu.
Nilipokuja kuzinduka, nilikuwa katikati ya pori lenye miti minene, mirefu na matawi yakiwa juu sana .
Nililala kwenye nyasi, pembeni yangu nilizungukwa na watu wengi ambao niliwaona miguu tu. Kwa haraka haraka nilihesabu miguu ile na kupata idadi ya ishirini na sita, ina maana watu waliosimama walikuwa kumi na watatu.

Niliinuka ili kukaa, lakini mmoja wa wale watu alinizuia nisikae, niendelee kulala, nikatii kwa vitendo na kurudi kujilaza majanini.
Ghafla nikasikia sauti nzito, yenye tetemeko.
“Umetakiwa kupokea nguvu ya kwetu,” ilisema ile sauti.
Yakapigwa makofi pale, halafu ukafuatia ukimya wa muda mrefu kama vile nililala peke yangu bila kuwepo mtu mwingine.

“Simama,” ile sauti ilisema kwa haraka na kwa amri.
Nilijikuta nasimama lakini nikiwa ndani ya ofisi yangu. Nilijiangalia na kujiona niko kama nilivyovaa awali, kila kitu ndani ya ofisi kilikuwa sawasawa, hakuna hata kitu kimoja kilichoharibika au kutokuwepo.
Hofu ikaniingia kuhusu waumini wangu nje, kwamba kama walikuja wakakuta mazingira yenye utata wataelewaje?
Niliusogelea mlango na kushika kitasa, nikaufungua polepole na kuangalia nje. Hakukuwa na muumini hata mmoja, hata mtoto.
“Khaaa!” Nilishangaa.
“Ina maana nimetumia muda mwingi sana ?” Nilijiuliza.

Niliangalia saa ya ukutani na kugundua kuwa, wakati namaliza ibada ilikuwa saa nne na nusu, muda ule naangalia saa ilikuwa saa saba mchana, ina maana kuingia kwa wale watu, kupoteza fahamu hadi kuzinduka ilipita saa tatu?!
Mlango uligongwa, akaingia mtu mmoja, simfahamu. Nilimkaribisha, akakaa kwenye fomu.
“Nikusaidie?”
“Ee baba, mimi nimekuja uniombee,” alisema akijiweka sawasawa.
“Nikuombee nini?”
“Uniombee naumwa.”

“Unaumwa nini?”
“Huwa nikilala usiku naona watu wanakuja kunikaba.”
“Unaona au unaota?”
“Naona, wakati mwingine huwa napiga kelele kwa kuwaogopa.”
“Wewe ni muumini wangu?”
“Hapana, nasali mjini.”
“Sasa kwanini usiende kwa mtumishi wa Mungu wa kanisa lako?”
“Ameshaniombea sana lakini hakuna mafanikio.”
“Sasa unaamini nini kuja kwangu, kuna mafanikio?”
“Naamini yapo mtumishi.”

Nilihisi ni miongoni mwa wale watu walionijia na kunifanyia maajabu yao , lakini sijui ni nini, kwani ghafla nilijawa na ujasiri wa kutoogopa lolote na kuamua kumwombea kweli.
Nilisimama, nikamtaka yeye apige magoti kisha nikamwekea mkono wangu wa kulia kichwani kwake na kuomba sana mpaka akaanguka chini.
Alipokuja kusimama, akasema anajisikia mwepesi, ana imani amepona kabisa.
“Usijali, nenda kwa amani lakini jilinde na dhambi.”
“Sawa Padri.”
Alipoondoka tu, mzee mmoja, aliyevaa shuka jeusi kuzunguka kiuno, chini akiwa hana kiatu wala sendoz, pekupeku, ju mabega wazi, mkononi alishika mkia wa mnyama, alisimama mbele yangu bila kujua aliingiaje?

“Karibu mzee wangu,” nilimkaribisha kwa ujasiri mkubwa sana , moyoni sikuwa na hofu wala wasiwasi. 
Pamoja na kuvaa kiajabu kama vile, lakini nilimwona kama mtu wa kawaida sana kwangu.
“Fumba kiganja cha mkononi,” aliniambia kwa amri.
Nikajikuta nafumba bila kuhoji yeye ni nani na ametoka wapi na kaja kwangu kufanya nini.
“Fumbua.”
Nilipofumbua, unga mweusi ulikijaza kiganja changu.
“Jipake kidogo usoni.”
Nilijipaka kidogo huku nikiwa nimeinama kuangalia chini.
“Unaona nini?”
“Sioni kitu.”

“Haya, hiyo dawa ndiyo tunayotumia kufanyia kazi, tunapotoka usiku kwenda kazini kila mmoja anakuwa na dawa hiyo, ndiyo inayosaidia watu wasituone…
“Fumba kiganja.”
Nikafumba.
“Fumbua.”
Nilipofumbua, sikuona ile dawa, kiganja kilikuwa cheupe kama mwanzo.
“Fumba tena kiganja.”
Nikafumba…
 “Fumbua.”

Nilipofumbua mkononi, nusu kulikuwa na unga unga wa kijani nusu unga unga mweusi.
“Chota huo unga kisha changanya.”
Nilitii, kisha akaniambia nijipake kidogo usoni, nikafanya hivyo na kujikuta nakuwa mwepesi kuliko kawaida ya siku zote.
“Unaona nini?”
“Najiona mwepesi sana .”
“Unaweza kujaribu kupaa?”
“Nijaribu?”
“Jaribu basi.”

Niliinua mikono kama vile ndege anavyoinua mabawa, taratibu nilijiona napaa juu huku miguu ikiiacha ardhi taratibu bila ridhaa yangu.
“Unaonaje?”
“Napaa sasa.”
“Shusha mikono.”
Niliishusha, taratibu miguu ikakanyaga ardhi na kusimama kama mwanzo.
Baada ya hapo yule mtu akapotea machoni pangu na kuniacha nikiwa na maswali kibao.
Nilijiweka sawa, nikafunga madirisha ili kutoka, nikafunga mlango na kuondoka kabisa katika eneo la ofisi.
Nilikwenda kwenye makazi yangu, lakini kwa wakati huo nilijihisi mnyonge sana , mwili ulikuwa hauna nguvu, macho hayaoni vizuri mbele na miguu mizito.

* * *
Saa saba za usiku, nilishtuka kutoka usingizini baada ya kushikwa na kuvutwa kidole cha mguu wa kulia na mtu. Kulikuwa na giza kwa hiyo sikujua nani alifanya zoezi lile.
Swichi ya kuwashia taa haikuwa mbali na nilipolala, nikaiwasha chapchap, chumba kilipojaa mwanga sikuona kitu, nikaendelea kulala.

Baada ya muda nikawa katika ndoto.
“Wewe Padri, unadhani utafanya kazi mpaka lini?”
“Mungu apende,” nilijibu.
“Je, asipopenda?”
“Atapenda tu.”
“Kwanini unafanya kazi lakini huna nguvu.”
“Nguvu gani?”
“Ya kiroho.”
“Kwa sababu bado.”

“Bado nini?”
“Wakati wa kuwa na nguvu.”
“Ni sasa.”
“Kwa maana ipi?”
“Njoo.”
Nilimfuata huyo mtu, akanishika na kunivuta hadi mahali, akasimama na kuniambia.
“Nenda kaingie kwenye kanisa lile.”
Mbele yangu kulikuwa na kanisa, nikaenda kuingia.
Lilikuwa kanisa langu, waumini wangu, wake kwa waume wengine wamekaa wengine wamesimama. Walikuwa wengi sana.

Mimi nikapita hadi mbele kwenye madhabahu na kusimama pale.
“Wale wenye matatizo waje niwaombee.”
Karibu kanisa zima walipita mbele kuombewa.
Ule wingi wao, nikaanza kuogopa kwamba nitaweza kweli?
Wa kwanza nikamwekea mikono juu kichwani na kumwombea, pale pale aliposimama akaanza kupiga kelele na kuanguka chini kisha akasimama akiwa amepona na kurukaruka huku akimtukuza Mungu wake.
  Inaendelea!!!!!!!!!!!!!!!! Usikae mbali na Irene Mwamfupe Ndauka pande hizi.
----------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
        
           PADRI MLA NYAMA ZA WATU-04

“Hee, hee nimekuwa mzima sasa.”
“Nenda usitende dhambi tena, sawa?”
“Sawa.”
Niliombea karibu kanisa zima, nilipomaliza nikawa natoka huku napigiwa makofi na waumini waliokuwa wamesimama kulia na kushoto kwangu.

“Padiri Padiri Padiri,” walisema wakipiga makofi, pwa pwa pwa.
Kufika nje, nikakutana na yule mtu aliyenichukua nyumbani.
“Umefanikiwa?”
“ Sana ,” nilimjibu.
“Umekubali?”
“Nini?”
“Kwamba wakati wa kuwa na nguvu ya kiroho ni sasa?”
“Nimekubali.”
“Haya, sasa twende kwa aliyekupa nguvu.”
“Kwa Mungu?”
“Wetu sisi.”
Tuliongozana hadi kwenye mti mmoja mkubwa, mrefu sana kwenda juu.
Chini walikaa watu wengi wakiwa kama wapo kwenye maongezi.
Kilichonishangaza miongoni mwa hao watu walikuwepo waumini wangu wa kanisani.
“Afadhali umekuja faza.”
“Faza nimefurahi sana kukuona.”
“Faza karibu sana .”

Wale waumini wangu wote walinikaribisha kwa furaha, amani na upendo wa hali ya juu.
Nilikaa sehemu ambayo kulikuwa na nafasi ya mtu mmoja, yule mtu niliyekwenda naye sikumwona tena alikopotelea.
“Bwaba umekuja huku, uko tayari kwa lolote?” Aliniuliza mzee wa kanisani ambaye sikuwa na mazoea naye.
“Kwani hapa ni wapi?” Nilihoji.
“Hapa ni kwa wachawi.”
“Wachawi!”

“Eee, umekuja kwa wachawi, kazini kwetu, karibu.”
Alipomaliza kusema, alikaa chini, akasimama sasa yule mzee ambaye siku ile kanisani walipoingia wale watu wawili wa ajabu, yeye alikaa katikati yao .
“Eee, nina kila sababu ya kujisifu kwa kupewa heshima hii ya kumkuza kazini mtu mkubwa kama huyu,” alisema yule mzee.

Yakapigwa makofi kwa muda wa dakika tano nzima huku yule mzee akiwa amesimama tu akisubiri yaishe ili aendelee kuongea.
Lakini kwa jinsi nilivyokuwa namwangalia mimi, alikuwa anaongea kwa kujiamini sana na hakuonekana kujali kama mimi ni kiongozi wake wa kiroho.
“Kwa hiyo kuanzia leo mtumishi utakuwa chini yangu ukizitii na kuzifuata amri zangu, sawa bwana mdogo?”
Nilimjibu kwa sauti ya unyonge sana :
“Sawa.”
Pale pale alitembea kuelekea nilikokuwa mimi, akaniwekea mkono kichwani.
***
Wiki moja ilikatika toka hayo yatokee, lakini hakukuwa na jipya jingine, sikuwahi kumwona mtu mwingine akinijia nyumbani wala kanisani ninapokuwa nafanya kazi za Mungu.
Lakini siku hiyo, nikiwa nimelala majira ya saa saba usiku, nilishtuka ghafla. Nikatupa macho mlangoni. Kwa sababu ya giza sikuona vizuri, ila dalili ya kama kitasa cha mlango kikifunguliwa.Nilinyoosha mkono hadi kwenye taa ya kitandani (bed switch) nikawasha kwa umakini sana ili mlio wa swichi usisikike.
Kitasa kikawa kinakaribia chini, lakini kikanata kwa muda. Nadhaani ni baada ya mimi kuwasha taa.

Hali hiyo ilinifanya nitoke kitandani na kusimama katikati ya chumba huku macho yote yakiwa kwenye kile kitasa mlangoni.
Huku taa ikiwa bado inawaka, kitasa kiliendelea kwenda chini, yaani kufunguka, lakini ilionekana aliyekuwa anakifungua yupo makini sana kwani kwa kukitazama haraka tu ilikuwa vigumu kujua kitasa kinafunguka kwa kwenda chini.Mara mlango ukaanza kusukumwa polepole na mimi nilisimama nikaza macho kujua nani aliyekuwa akifanya kazi ile. Wazo kwamba ni mwizi sikuwa nalo kwani nawajua wezi, wao ni papara au kushtukiza.

Mlango uliendelea kusukumwa mpaka ukawa wazi wote, yaani kama kuna mtu alisimama 
kwenye korido angeona chumbani, lakini cha kushangaza hakukuwa na binadamu wala kiumbe chochote nyuma ya mlango.
Nilipotaka kuuliza nani mwenzangu, nikasikia sauti ya mtu kukohoa kwa kujibana. Halafu nikasikia mlio wa viatu, ko! Ko! Ko! Ko! Ukisikika kuingia ndani ya chumba, nikarukia kusimama pembeni kwani niliamini aliyekuwa akiingia angeweza kunikumba.

Mlio wa viatu kutembea uliposimama ukafuata mlio wa kufunguliwa kwa dirisha la chumba, na kweli likawa linafunguka hadi mwisho, halafu pazia ikawa inakunjwa na kufungwa katikati kama vile mkunjaji alitaka upepo uingie kwa vizuri.

Baada ya hapo, nikiwa nimesimama pembeni, mlio wa viatu ukatembea kwa mwendo ule ule wa ko! Ko! Ko hadi ukutani kwenye swichi, ghafla nikasikia tap na giza likatanda. Ina maana huyo mtu alizima taa.
Halafu mlio wa viatu ukaendelea tena hadi usawa wa kitanda, ukakwamba pale. Giza likiwa limetanda, nikasikia hali ya mtu anayepanda kitandani kwani kitanda kilitoa mlio Fulani na baadaye, kama baada ya dakika moja ikasikika sauti ya mtu kukoroma.

“Khooooo! Khoooo!”
Niliamini ni uonevu usiokuwa na maana kwangu kwani sikuwa na kosa la kunifanya nishindwe kulala na kulala mtu mwingine, nilikasirika sana . Nikatembea kijeuri hadi ukutani na kuwasha taa.
Ile inawaka tu, ile swichi ya kitandani ikasikika ikizimika, tap! Kukawa giza tena.

Niliifuata kwa fujo ile swichi ya kitandani, nikaiwasha na macho yangu yakakimbilia moja kwa moja kitandani. Mtu mnene, mrefu alikuwa amejifunika shuka huku akiwa amenyoosha miguu na anaangalia juu, yaani amelala chali.
“Wewe ni nani?” Nilimuuliza bila woga.

“Msafiri,” sauti nzito ilijibu kwa mkato.

“Ndiyo jina lako au msafiri unakwenda mahali?”

“Siendi popote.”

“Khaa! Sasa hapa kwako?”
“Hapana.”
“Sasa kwanini umefungua mlango bila hodi na umepanda kitandani kulala bila ridhaa yangu?”
“Nisamehe sana .”
“Basi ondoka.”----------------------------------------------------

    
            PADRI MLA NYAMA ZA WATU-05
 Kauli yangu hiyo haikupata jibu zaidi ya mlio wa kukoroma kusikika kama mwanzo.
Nilimsogelea yule mtu pale kitandani kwa lengo la kumfunua shuka na kumwona vizuri. Niliishika shuka kwenye ncha moja, nikaifunua kwa nguvu…   
“Ha ha ha ha ha ha!” Alicheka sana yule mtu huku akitoka kitandani na kuficha uso kwa mkono mmoja.
Nilijitahidi sana kuhakikisha namwona uso yule mtu, lakini na yeye alikuwa akawa anaangalia ukutani huku akiendeelea na kicheko chake.
“Wewe ni nani?” Nilimuuliza kwa ukali kidogo.
“Ha ha ha ha! Msafiri bwana, si nilikwambia!”
“Umetumwa?”
“Hapana.”
“Umekuja tu mwenyewe?”
“Ha ha ha ha! Eee!”
Kusema ule ukweli nilichanganyikiwa, kwani sasa nikawa sijui ukweli upo wapi, kila ninachomuuliza ananijibu kinyume na matarajio yangu.
“Basi mimi naomba uondoke humu chumbani kwangu,” nilimwamuru.
“Ha ha ha ha ha! Sawa,” alisema akielekea mlangoni na kutoka kweli lakini nikiwa sijafanikiwa kuona sura. Kwa hiyo mpaka hapo nikawa sijui ni nani yule.
Alipovuka tu ukuta wa chumba changu, nikajikuta napata wasiwasi na woga tofauti na mwanzo alipoingia.
Nilifunga mlango ili nipande kitandani kulala, lakini kabla sijapanda, nikasikia vishindo ti ti titi! Watu kama sita walisimama katikati ya chumba changu.
“Mtumishi wa Mungu vipi? Habari za kulala?”
“Salama.”
“Aaa, tumetumwa kwako.”
“Na nani?”
“Aaa, vaa miwani yako kwanza kisha utuangalie vizuri.”
Nilipeleka mkono kwenye stuli ndogo iliyokuwa pembeni ya kitanda na kuchukua miwani, nikaivaa na kuwaangalia.
Walikuwa tofauti na nilivyowaona wakati wanatua. Walikuwa wamevaa viguo vyeusi (kaniki) kukatisha kiunoni kwenda chini ya mapaja, kila mmoja alionekana amekasirika na hana utani na usoni walipaka vitu vyeupe, kama si unga, basi chokaa.
“Unatuona vizuri sasa?”
“Ndiyo.”
“Basi ndivyo tulivyo, toa miwani.”
Nilipotoa tu, walirejea na kuwa kama walivyotua, wamevaa kawaida.
“Unatakiwa kuhudhuria mateso ya waumini wako usiku wa sasa,” mmoja wao aliniambia, wengine wakatingisha vichwa kama ishara ya kukubaliana na maneno ya mwenzao.
“Wapi?”
“Katika kila nyumba yenye muumini au waumini wako.”
“Ni mateso ya aina gani?”
“Utajua huko huko na huna hiyari katika hili, kwani ulishapata baraka zote za uchawi.”
Nilijikuta nasimama, naanza kutembea kuwafuata kutoka nje mpaka uwanjani mbele ya nyumba, wakaanza kutengeneza duara na mimi nikawa mmoja wa wanaduara.
Mmoja akapeleka mikono na kuwashika wa kulia na kushoto kwake, wengine wakafanya hivyo mpaka mimi. Tukawa tumekamatana mikono. Yule aliyeanza kushika, akainama kama dalili ya kusujudia, wengine wakafuatia na mimi pia, kufumba na kufumbua, tukajikuta tukipaa juu na kutua chini ya mti mkubwa wa Mvule. Sikumbuki tulitumia dakika ngapi kuwa angani na kushuka.
Milio ya ngoma iliyotawala pale ilinifanya niamini kuwa, kweli nilikuwa katikati ya maskani ya kichawi.
“Bila kupoteza muda sasa tunaingia mitaani, hasa kwenye nyumba za waumini wa kanisa ambalo padri wao tunaye kwenye kundi letu na kufanya kazi ya kuwatesa, sawa?” Sauti nzito, iliyokuwa ikisikika na kitetemeshi ilisema.
Nilipomwangalia msemaji huyo, ni mzee mmoja aliyekuwa amevaa kanzu ndefu nyeusi, juu, yaani kichwani alivaa pembe za mnyama, mkononi alishika mkia, pia wa mnyama.
“Sawa,” wenzangu waliitikia kwa sauti ya juu.
Kifupi mimi nilikuwa sijui kitu chochote. Nilikuwa sijui watafanyaje huko kwenye kutesa watu, sijui nani atakayeteswa, kama ni waumini wote pia sikujua. Ila, mzee mmoja alinifuata na kuniambia:
“Tuondoke mimi na wewe.”
Nikawa namfuata hadi kando kando ya ule mti mkubwa, akasimama ghafla hadi nikamkumba.
Kufumba na kufumbua, tulitua nje ya nyumba ya muumini wangu mmoja ambaye anamiliki mashine ya kusaga na trekta moja.
“Haa! Hapa si kwa..?”
Kabla sijamaliza kusema, yule mzee akaniambia kwa kunikatisha:
“Ulisikia tulivyoambiwa kule?”
“Kwamba?”
“Tunawatesa akina nani?”
“Waumini wangu.”
“Sasa unauliza nini?” Alinijibu huku akitembea kwa kurukaruka kwa mguu mmoja.
Alipoona mimi nimezubaa akanifuata:
“Jipige kifuani kwa mkono.”
Nikafanye hivyo.
“Hapo sawa sasa, nifuate mimi kwa kila hatua mpaka ndani na kuanza kazi, sawa?” Aliniuliza.
Tulikwenda hadi kwenye mlango mkubwa, nikadhani atagonga ili tufunguliwe, kumbe sivyo bwana.
“Kila ninachofanya mimi na wewe unaniiga, sawa?” Aliniambia akinigeukia, kwani nilikuwa nimesimama nyuma yake.
“Sawa.”
“Haya tunaanza sasa.”
Alijipiga tena kifua na mimi nikajipiga. Kufumba na kufumbua tukawa ndani, sebuleni.
“Sasa niigize kwa kila kitu.”
“Sawa,” nilimjibu kwa sauti ya chini kama ile aliyoitumia yeye kuniambia.
Alitembea kwa kurukaruka kwa mguu mmoja, huku mguu wa pili ukiwa unaning’inia tu. Kwa mimi nilivyoona, hakukuwa na sababu yoyote ya kutembea vile, ila kwa kichawi nadhani ni sawa na ni kawaida kwao.
Na mimi niliruka ruka kwa mguu mmoja huku mwingine ukining’inia hadi kwenye mlango wa kuingia kwenye vyumba, yule mzee akasimama, lakini kwa mguu mmoja.
Tulisimama vile mpaka mimi nikabadili msimamo, nikatumia mguu mwingine maana nilichoka sana .
Ghafla akaweka mguu mwingine chini huku akigeukageuka kuniangalia.
“Sasa tunaingia chumbani kwa baba mwenye nyumba, sawa?”
“Sawa.”
“Una swali lolote kabla hatujaingia?” Aliniuliza.
“Ndiyo.”
“Enhe, lipi hilo ?”
“Haaa…”
“Uliza haraka.”
“Sawa, hatutaonekana?”
“Wapi?”
“Tunakokwenda.”
“Kwani si nimekwambia kila kitu unaigiza kwangu?”
“Kabla sijaigiza je?”
“Hatutaonekana.”
“Basi, swali langu ni hilo tu.”
“Kwa hiyo huna swali jingine?”
“Sina na wala sitakuwa nalo.”
“Oke  nifuate.”
“Niko nyuma yako.”
Aliinua mikono juu, akapiga makofi na mimi nikafanya hivyo hivyo. Kufumba na kufumbua tukawa tumesimama katikati ya chumba.
Yule mzee akanigeukia, akaniangalia lakini hakusema kitu. Mdomo akauangalizia juu na kufanya tendo kama anapuliza moto, na mimi nikafanya hivyo hivyo. Akamsogelea mzee mwenye nyumba aliyekuwa amelala usingizi mzito wa chali, akamkalia tumboni huku akijisotesha kuanzia kiunoni kwenda kifuani na kurudi.
Mimi nikawa mtazamaji tu, lakini yule mzee akaniangalia na kunipa ishara kwamba na mimi nimpandie mke wa yule mwenye nyumba ambaye alikuwa amelala kitanda kingine na mtoto mdogo kama wa mwaka mmoja.
Nilipanda bila kujiuliza maswali kwanini napanda, nikajisotesha kama alivyokuwa akifanya yule mzee, lakini nilipotua macho usoni kwa yule mama ambaye naye alilala chali, nikamjua kuwa ni muumini wangu mzuri pale kanisani.
Kusema ule ukweli niliumia sana moyoni, nikajihisi ni mtenda dhambi nisiyestahili msamaha wa aina yoyote ile.
Lakini ilinibidi niendelee tu na kazi niliyokuwa naifanya kwani ni jukumu ambalo nilishalivalia njuga sikuwa na budi kulimaliza sawasawa na safari yetu ya kuingia ndani ya nyumba ile.
Mara yule mzee alishuka kutoka kwenye tumbo la yule mzee mwenye nyumba huku akinifanyia ishara ya mimi pia kushuka.
Tulishuka wote, tukasimama tukiangaliana. Mara mwenzangu akaufuata ukuta sehemu ya kichwani ya yule mzee, akasimama na kumwinamia kisha akapeleka mkono hadi jirani na shingo yake na kuukunja kama vile ameshika shingo na kumkaba.
Yule mwenye nyumba akawa anarusharusha miguu kama anayeitafuta pumzi baada ya kuziba kwa pua na kinywa, huku akisema maneno yasiyojulikana:
“Mmmh! Mmmmmm! Mmm!”
Alivyokuwa akiendelea kubana mkono ndivyo na yule mtu alivyokuwa akizidi kulalamika, sasa akapeleka mikono kwenye koo lake na kujishika huku akizidi kulalamika.
Alichofanya yule mchawi, akawa anambana huku mkono mmoja anafanya kama anamtisha kwa ngumi ya uso yule mzee. Alipokuja kumwachia, akasimama pembeni yake kisha yule mtu mwenye nyumba akashituka kutoka usingizini na kukaa huku akikohoa sana .
“Mungu wangu, Mungu weee! Ooo! Mama,” alisema akiendelea kushika koo lake.
Akamwita mkewe kwa sauti ya juu, naye akashituka na kumuuliza kulikoni:
“Kuna nini mume wangu?”
“Nimekabwa vibaya sana .”
“Na nani?”
“Najua ni wachawi tu hao.”
“Umejuaje?”
“Wamenishika koo kwa kunikaba kisha wakanigiga ngumi za uso. Kwani huoni kama umevimba?”
“Nini?”
“Uso wangu?”
“Hata, ila macho kama mekundu.”
“Ni hao hao lakini mmoja kama nimemwona.”
“Unamjua?”
“ Kama namjua.”
“Ni nani?”
“ Kama ..!”
“Vipi tena mume wangu?”
“Tumbo nalo kama limejaa, ooo linauma sasa, wachawi hao mke wangu.”
Mara mkewe naye akaanza kulia huku akishika tumbo lake na kulalamikia.



Moyoni nilitamani sana yule mzee atokee ili akabiliane na zile tuhuma zile ambazo mimi zilinifika shingoni na niliingiwa na kinyongo na kazi ile ya kichawi ambapo awali niliambiwa hakuna ambaye angeweza kutuona wakati tukiwa kwenye matukio yetu.
“Eee Bwana niepushe na aibu hii, sirudii tena mimi, nimeshajirekebisha,” nilisali kimoyomoyo peke yangu pale mbele ya madhabahu. Nikajikuta nakohoa pia bila sababu.
Ghafla mzee mwingine akanyoosha kidole, wakawa wawili sasa. Lakini pia wakati yule akiendelea kuongea na vile vidole viwili vikiwa juu, mke wa yule mzee aliyekuwa akiongea naye akanyoosha kidole.
“Mbaya zaidi, watu waliotuingilia kutufanyia hivyo huwezi kuamini ukiambiwa, hii ni aibu kwa kanisa na pia ni kufa kiroho. Mungu hawezi kuuvumilia ubaya huu.”
Wakati anazidi kubomoa, mimi haja ndogo ilinibana, nikawa navumilia tu.
Nilitamani ardhi ipasuke, mimi niingie ndani mwake na nisionekane tena maishani mwangu. Mwili ulinitetemeka, akili ikanipotea, nikawa sijui niamue nini.
“Hali ikiwa hivi kuna siku humu huku kanisani watu watashikania mapanga kutoana damu, hakiyanani vile.”
Yule mzee alipomaliza kusema hayo, akaa ghafla kama vile alishikwa na kukalishwa kwa nguvu.
Nikataka kusema muda umekwisha, lakini mzee mmoja kati ya wale walionyoosha vidole alisimama hata bila kuruhisiwa, alipoona mwenzake amekaa tu.
“Nashukuru sana na mimi kwa kupata muda huu. Zamani uchawi hapa kanisani ulikuwa ni msemo tu, si kitu ambacho kinatingisha, lakini mimi nina habari kwamba, sasa uchawi umo ndani kabisa ya hili kanisa, tena washiriki ukitajiwa majina unaweza kubisha hadi unaanguka chini.
“Mimi kama nitapata baraka za waumini wenzangu niko tayari nitaje majina, lakini nilindwe.”
Nilimwangalia vizuri yule mzee nikamwona kama ametumwa, kwani wakati anaongea, hakuwa ananiangalia mimi, wala mtu mwingine, alaiinama tu huku akibwabwaja.
“Sema.”
“Wataje.”
“Waweke wazi bwana.”
“Tutajie.”
“Tuambie.”
Hayo yalikuwa maneno ya waumini wa kanisa lile ambayo yalinichanganya kabisa. Baadhi ya waumini wakawa wanainama kunong’onezana huku wakiniangalia kwa kuniibiaibia.
“Niwataje?” Yule mzee aliuliza tena kwa sauti ya juu.
“Watajeeee.”
Wakati huo, yule mzee mwingie na yule mke wa yule wa kwanza, vidole vyao vilikuwa bado juu wakiomba nafasi ya wao kuongea.
“Eti niwataje?” 
Inaendelea!!!!!!!!!!!!!!!! Usikae mbali na Irene Mwamfupe Ndauka pande hizi.

4 comments:

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate