EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, July 16, 2012

Kamati ya Zitto yaingilia kati kusimamishwa bosi Tanesco

SIKU moja baada ya Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kumsimamisha  kazi  Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Shirika  hilo, Mhandisi William Mhando, Kamati  ya Bunge ya Mashirika ya Umma (POAC), imeitisha kikao cha dharura kujadili uamuzi huo.
Juzi, Bodi hiyo chini ya Uenyekiti wa Mkuu wa Majeshi Mstaafu Jenerali Robert Mboma, iliwasimamisha kazi, Mhando na viongozi wengine wa Tanesco ambao ni Naibu Mkurugenzi Mtendaji Huduma za Shirika, Robert Shemhilu, Ofisa Mkuu wa Fedha, Lusekelo Kassanga na Meneja Mwandamizi, Ununuzi Harun Mattambo. 

Akizungumza na gazeti hili jana, Mwenyekiti wa Kamati Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), Zitto Kabwe alisema kufuatia uamuzi huo wa Bodi ya Tanesco, ameomba ruhusa kwa Spika wa Bunge, Anne Mkinda kuitisha kikao cha dharura na bodi hiyo ijieleze.  Zitto alisema kuwa, mbali na bodi hiyo wamemwita Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA). 
“Siku ya Jumatano (kesho kutwa) kamati imemwomba Spika ruhusa ya kuitisha kikao ili bodi nzima ya 

Tenesco kuja kutupa maelezo ya nini kimetokea, maana taarifa ya CAG na PPRA haina hizo tuhuma wanazosema watu wa Serikali,” alisema Zitto na kuongeza:
“POAC tunahusika na usimamizi wa fedha za shirika, tunataka kujua ubadhirifu na masuala ya kisheria na  itahakikisha uwajibikaji na tutasimamia hilo kwa nguvu zote kwani  hatutaki uonevu na tutalinda wanaoonewa.  Hata hivyo, kauli hiyo ya Zitto inakuja wakati baadhi ya wabunge akiwamo yeye mwenyewe hivi karibuni walishinikiza mawaziri ambao wizara zao zilitajwa kuhusika na tuhuma za ufisadi katika ripoti ya CAG wajiuzulu.

Zitto pia ndiye aliyeongoza zoezi la kukusanya saini za wabunge kwa ajili ya kupiga kura za kutokuwa na imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda baada ya ripoti ya CAG kuonyesha ufisadi mkubwa serikalini.  Akisoma ripoti ya POAC baada ya kutolewa ripoti na CAG, Zitto alisema kuwa, Tanesco kulikuwa na ongezeko la gharama za ununuzi kutoka Sh300 bilioni za mwaka juzi hadi Sh600 bilioni katika ripoti ya mwaka huu na kuhoji, chanzo cha ongezeko la gharama hizo kwa asilimia 100.
Hata hivyo, taarifa za ndani kutoka Wizara ya Nishati na Madini zinaeleza kuwa uamuzi wa bodi hiyo kumng'oa Mhando na wenzake unatokana na kushindwa kuwajibika kwa Mkurugenzi huyo kumaliza mgawo wa umeme na kuendelea kuwapo kwa vitendo vya hujuma katika uzalishaji wa umeme.

Kauli ya Utouh
Hata hivyo, akizungumzia suala hilo Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh alisema hana taarifa zozote za kuitwa na Kamati ya POAC kuhusiana na sakata la kusimamishwa viongozi wa Tanesco.
“Sijapata taarifa za kuitwa na Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma, wewe ndiyo unanijulisha kuhusu hilo.”

Utouh alisema kwa sasa hawezi kuzungumza kuhusu ripoti ya hesabu za Tanesco kama walipata hati safi au hati chafu hadi aipitie upya ripoti hiyo.
“Kwa harakaharaka siwezi kufahamu kama Tanesco walipata ripoti ya aina gani inayohusu matumizi ya fedha hadi niisome upya ndipo ninaweza kulizungumzia,” alisema Utouh.
CAG alisema taarifa za kusimamishwa viongozi wa Tanesco ameziona na kuzisoma katika vyombo vya habari.
 
Mwambalaswa Mmoja wa Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi, Victor Mwambalaswa alitaja baadhi ya tuhuma zilizosababisha bodi hiyo kumsimamisha Mhando pamoja na maofisa wenzake kuwa ni kuhusika katika matumizi mabaya ya fedha za umma.
Mwambalaswa ambaye pia ni Mbunge wa Lupa (CCM), alizitaja tuhuma nyingine  kuwa, ni matumizi mabaya ya madaraka likiwamo la kuongoza kwa upendeleo.
Alidai upandishwaji vyeo unafanywa kwa misingi ya ukabila.
“Msingi wa tuhumu hizo ni ziara aliyofanya Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Sospter 

Muhungo  hivi karibu ambapo aliwataka wafanyakazi wenye kero kuwasilisha malalamiko yake wizarani ili yafanyiwa kazi,” alibainisha Mwambalaswa.
Pia, uamuzi wa kutaka watendaji nao wawajibike ulitangazwa na Rais Jakaya Kikwete Ikulu Mei 4, wakati akitangaza baraza jipya la mawaziri ambapo alisema kuwa, mbali ya uwajibikaji kisiasa, bodi za wakurugenzi na watendaji ambao taasisi zao zimetajwa katika ripoti ya CAG kuhusika na matumizi mabaya ya fedha za umma, watapaswa kuwajibishwa.    
Ilivyokuwa  Hatua hiyo ilitangazwa juzi jijini Dar es Salaam kufuatia  kikao cha dharura cha Bodi ya 

Wakurugenzi ya Tanesco kilichofanyika  Julai 13 mwaka huu, ambacho kilijadili tuhuma mbalimbali dhidi ya menejimenti ya Tanesco.  Kikao hicho kiliongozwa na Mwenyekiti wake, Jenerali Mstaafu Robert Mboma  na kuchukua uamuzi wa kumsimamisha kazi Mhando ili kupisha uchunguzi wa tuhuma za ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka.  
“Hivyo, bodi iliazimia pamoja na mambo mengine kama ifuatavyo: Uchunguzi wa tuhuma hizo uanze mara moja kwa kutumia uchunguzi huru na kumsimamisha kazi Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco, Mhandisi William Mhando ili kupisha uchunguzi huo na kwa kuzingatia matakwa ya sheria za kazi nchini,” ilieleza sehemu ya taarifa aliyoitoa  Mboma kwa vyombo vya habari.  Mhando aliteuliwa kuwa Mkurugenzi wa 

Tanesco kuanzia Juni Mosi Mwaka 2010.  
Baada ya uteuzi huo, Mhando alisema atahakikisha wateja wote wa Tanesco wanakuwa na mita za Luku.  Kabla ya uteuzi huo, Mhando alikuwa ni Meneja Mkuu Usambazaji Umeme na Masoko katika shirika hilo.  Mhando alichukua nafasi ya aliyekuwa Mkurugenzi wa shirika hilo, Dk Idris Rashid ambaye alimaliza muda wake wa uongozi. 

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate