EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, June 5, 2013

Rasimu ya Katiba Mpya yapendekeza rais apunguziwe uwezo

Dar/Dodoma. 
Rasimu ya Katiba Mpya iliyozinduliwa jana, imependekeza kupunguzwa kwa madaraka ya Rais wa Tanzania maeneo tofauti ya utendaji wake, ukiwamo uteuzi wa viongozi na watendaji wakuu wa Serikali.

Tume hiyo inapendekeza kwamba Rais ashirikiane na mihimili mingine ya dola katika uteuzi huo, huku ikiwataja Mawaziri na Naibu Mawaziri, Jaji Mkuu, Naibu Jaji Mkuu na Katibu Mkuu Kiongozi kuwa uteuzi wao utakapofanywa na Rais lazima uthibitishwe na Bunge.


Mapendekezo hayo ni tofauti na hali ilivyo sasa wakati uteuzi unaofanywa na Rais hauthibitishwi na Bunge, isipokuwa nafasi ya Waziri Mkuu na Makamu wa Rais itapotokea ikawa wazi kwa sababu zozote zile.


Pia, tume inapendekeza Rais ashauriane na chombo kipya kitakachoundwa cha Baraza la Ulinzi la Taifa kuwateua viongozi wote wa taasisi za ulinzi nchini.


Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba alisema mfumo wa utawala utaendelea kuwa kama ulivyo hivi sasa na kwamba, Rais ndiye mtendaji wa Jamhuri ya Muungano na atachaguliwa moja kwa moja na wananchi.


Jaji Warioba alisema Tume imependekeza mgombea urais lazima apate zaidi ya asilimia 50 ya kura zilizopigwa na kwamba, kinga ya kutokuhoji matokeo ya uchaguzi mahakamani iondolewe.

“Mgombea urais anaweza kupendekezwa na chama cha siasa au kuwa mgombea huru, mgombea wa nafasi hiyo atatangazwa kuwa mshindi iwapo atakuwa amepata zaidi ya asilimia 50 ya kura zote zilizopigwa,” alisema Jaji Warioba na kuongeza: “Hata hivyo, matokeo ya uchaguzi wa Rais yanaweza kulalamikiwa mahakamani, lakini siyo kila mtu anaweza kufungua kesi, wanaoweza kufungua kesi ni wagombea urais na Mahakama ya Juu pekee ndiyo itakuwa na mamlaka na uwezo wa kusikiliza malalamiko kuhusu matokeo ya uchaguzi wa Rais na shauri lazima liamuliwe ndani ya mwezi mmoja, yaani siku 30.”


Alisema Tume inapendekeza Rais achaguliwe moja kwa moja na wananchi na kwamba, suala la umri pia lilijadiliwa kwa upana.


“Wengine walisema umri wa mtu kuruhusiwa kugombea urais uwe miaka 35 au 50 na kuendelea, Tume imeyachambua maoni yote na ikafanya utafiti kwa kupitia Katiba za nchi zingine ,” alisema Jaji Warioba na kuongeza:




“Wengi walioomba kugombea nafasi hiyo walikuwa na umri wa miaka 40 au zaidi, kwa kuzingatia maoni ya wananchi, utafiti na hali halisi, Tume imependekeza Rais aendelee kuchaguliwa na wananchi pamoja na sifa nyingine mtu atakayegombea Urais asiwe chini ya miaka 40.”


Kutokupunguzwa kwa umri wa urais kutakuwa ni pigo kwa wansiasa vijana nchini waliopendekeza ushushwe na kuwa miaka 35, akiwamo Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Januari Makamba.

Zitto, Makamba watoa kauli

Akizungumzia suala hilo jana, Zitto alisema uamuzi huo wa umri hana la kusema, kwa sababu yaliyotolewa ni mapendekezo ya Tume na kwamba, Chadema watatoa kauli baada ya viongozi kuwasiliana.
Kwa upande wake, Makamba iwapo amebadili msimamo wake, alisema: “Suala la umri siyo kigezo pekee cha kupata uongozi mzuri.”
Makamba alisema ujana wala uzee siyo kigezo cha kumnyima mtu uongozi.
Siku za nyuma Makamba, ambaye ni Mbunge wa Bumbuli, aliwahi kunukuliwa akitaka umri wa kugombea urais uwe miaka 35 badala ya 40 ya sasa.
Alisema suala la umri lisingemwathiri binafsi, kwani mwaka 2015 atakuwa na umri wa miaka 41.
“Ninapongeza Watanzania kwa kutoa maoni yao na kutaka vijana kupewa nafasi za uongozi,” aliongeza Makamba.    

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate