EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Monday, November 18, 2013

MKUU WA MKOA WA RUKWA AMTEMBELEA MAMA MARIANNE MJERUMANI ALIYEHAMIA TANZANIA NA KUJITOLEA KULEA WATOTO YATIMA 12

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akiteta jambo na Mama Marianne Lwanetzki  raia wa Ujerumani alipomtembelea nyumbani kwake jana kujionea maisha ya mama huyo ambae kwa sasa anaishi Mkoani Rukwa katika nyumba yake inayoitwa 'Kinder House" na watoto yatima 12 ambao aliamua kuwachukua kutoka katika mazingira magumu na kuishi nao kama watoto wake huku akiwapatia huduma mbalimbali za chakula, malazi, elimu na tiba. Watoto hao yatima wapo wanaume sita na wanawake ni sita.
Katika historia yake fupi Mama huyo alifika Mkoani Rukwa kwa shughuli za kitalii na ndipo alipomuona mtoto mmoja katika moja ya kituo cha kulelea mayatima akiwa na hali mbaya ya kiafya huku akiwa mgojwa sana, Aliamua kumchukua mtoto huyo na kuishi nae hadi akapona ndipo aliposhawishika na kuamua kuhamia Tanzania na kuchukua watoto wengine yatima hadi kufikia 12 ambao kwasasa amesema wanatosha kulingana na uwezo alionao.
 Aliongeza kuwa katika kuwalea watoto hao anatumia uwezo wake yeye binafsi pamoja na misaada  mbalimbali kutoa kwa ndugu, jamaa na marafiki wa nchini kwake Ujerumani.
Mtoto Kastory Mabruki ambaye ametajwa kuwa na sifa mbalimbali ikiwemo Uongozaji wa kwaya kama inavyoonekana pichani na hata uongozaji wa midahalo"debate" mbalimbali shuleni kwao zikiwemo za wanafunzi wa madarasa ya juu zaidi ya lile analosoma na kuzimudu vizuri. Katika watoto hao 12 kila mmoja anaonekana kuwa na kipaji cha aina yake ambapo Mama yao Mlezi anajitahidi kuviendeleza na kuvipa nafasi.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akiongea kumpongeza Mama Marianne kwa juhudi alizozichukua ambapo ameguswa sana na mpango huo wa mtu binafsi kulea watoto kama familia moja tofauti na sehemu nyingine nyingi ambazo taasisi ndizo zinazojishughulisha na vituo vya kulelea mayatima. Mkuu huyo wa Mkoa amewaasa watanzania wenye uwezo kuiga mfano huo kusaidia jamii kuondokana na kero za watoto wa mitaani.
Picha Ndani: Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya (katikati mbele waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na Mama Marianne Lwanetzki (wapili kushoto mbele waliokaa) raia wa Ujerumani na watoto yatima 12 alioamua kuwachukua na kuwalea kama watoto wake wakitokea katika mazingira magumu na ambao anaishi nao katika nyumba yake anayoiita "Kinder House" iliyopo katika Manispaa ya Sumbawanga Mkoani Rukwa. Mama huyo anawapatia watoto hao mahitaji yao yote ikiwemo chakula, malazi na elimu. Kulia ni Katibu wa Mhe. Manyanya Frank Mateni. 
 Picha Nje: Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya (watatu kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na Mama Marianne Lwanetzki (watatu kulia) raia wa Ujerumani na watoto yatima 12 alioamua kuwachukua na kuwalea kama watoto wake wakitokea katika mazingira magumu na ambao anaishi nao katika nyumba yake anayoiita "Kinder House" iliyopo katika Manispaa ya Sumbawanga Mkoani Rukwa. Mama huyo anawapatia watoto hao mahitaji yao yote ikiwemo chakula, malazi na elimu. Wapili kulia ni Hamza Temba - Afisa Habari Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa.
Handshaking.
Nyumba hii inajulikana kama "KINDER HOUSE" ambapo kwa mujibu wa Mama mwenye nyumba hii Marianne Lwanetzki ambae ni raia wa Ujerumani alisema neno "kinder" kijerumani lina maana ya watoto. Mama Marianne amesema nyumba hiyo ambayo ni kubwa ikiwa na eneo la kutosha ameshaiandikia kisheria na kwamba ni urithi kwa watoto hao 12 anaowalea hata kama hatokuwepo tena duniani basi hapo ndipo nyumbani kwao.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa akiagana na familia ya Mama Marianne Lwanetzki yenye watoto yatima 12 pamoja na wafanyakazi wake wanaomsaidia kwenye shughuli za malezi. (Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa @Rukwareview.blogspot.com)

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate