EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, June 25, 2014

MKASA MZIMA WA WEMA AZIMIA UPO HAPA

CHUKI tu! Katika jambo ambalo limeuumiza moyo wa Miss Tanzania 2006/07, Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ tangu awe staa, ni ishu iliyotokea wikiendi iliyopita baada ya mtu asiyejulikana kutengeneza picha chafu ya mama mzazi wa mrembo huyo, Mariam Sepetu na kisha kuisambaza kwenye mitandao ya kijamii kitu ambacho kilimshtusha na kujikuta akipoteza fahamu (kuzimiainatoka uk.1
Diva katika tasnia ya filamu Bongo Wema Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’.

Akizungumza na Risasi Mchanganyiko, mmoja wa marafiki zake wa karibu ambaye aliomba chondechonde asitajwe gazetini alisema kwamba, mara ya mwisho kuona chozi la Wema ni siku ya msiba wa marehemu baba yake, mzee Isaac Sepetu lakini hili lilizidi kilio kile kwani ni tukio la udhalilishaji kwa mzazi wake huyo hivyo kuzimia ilikuwa ni lazima kwani yaliyomkuta yanasikitisha.
Chanzo hicho kilidai kwamba, Wema hakutegemea kama ipo siku mama yake atadhalilishwa kiasi hicho hadi kufikia yeye kupoteza fahamu.
“Kiukweli ile picha ilichafua sana hali ya hewa hasa kwa wanaompenda Wema na hata kwa wanaomchukia Wema kwani kila mmoja alikuwa analaani kitendo kile ambacho si cha kiungwana.
“Unajua inafika hatua unatakiwa ufahamu mama wa mwenzio ni mama yako pia halafu usifurahie ubaya anaofanyiwa mama wa mwenzio tutukanane sisi wenyewe na si kuwaingiza wazazi kwenye mambo wasiyojua mbele wala nyuma,” kilidai chanzo hicho.
“Hebu fikiria mama yako mzazi atengenezewe picha ya utupu na jamii iaminishwe kuwa ni yeye wakati si kweli, inauma sana jamani. Utadhani huyo mtu hajazaliwa na mama.”
TIMU DENGUE NA MKAKATI MZITO
Katika kipindi cha vuguvugu la kuchafuana kilichoanza mwanzoni mwa wiki iliyopita, kuna wachangiaji katika mitandao ya kijamii waliojiita kwa jina la Timu Dengue, walionekana kumkandia Wema.
Staa katika tasnia ya filamu Bongo Aunt Ezekiel.
Chanzo chetu kinadai kuwa, timu hiyo ina mkakati mzito wa kumchafua Wema kwa kila namna.
“Wamepanga mkakati mzito, wanadai eti Wema anajisikia. Lakini watu wanasema haiwezekani watu wafanye mambo bila sababu. Sasa hapo wanamhusisha Kajala (Masanja) kwa kuwa ndiye mtu aliye na bifu naye kwa sasa,” kilipasha chanzo hicho na kuongeza:
“Lakini kuna wengine wanabishana, wanadai kuwa inawezekana watu wasio na kazi za kufanya au wenye chuki binafsi na Wema wameamua kutumia mwanya huo kumchafua Wema na familia yake wakiamini lazima Kajala atahusishwa kwa kuwa ana ugomvi naye.”
BOFYA HAPA KUMSIKIA WEMA
Risasi Mchanganyiko iliposhuhudia picha hiyo ya utupu na kujiridhisha kuwa siyo ya mama Wema, lilimtafuta Wema kuzungumzia ni kwa jinsi gani alivyoumia baada ya kuona picha ile ambapo majibu yake alionekana bado ana maumivu makali ambayo yalidhihirisha wazi yalikuwa  hayajamuisha moyoni.
“Nimeumia sana mama yangu kudhalilishwa na si mimi tu familia yangu yote kwa jumla, tumeumizwa sana kwa tukio lile lakini mimi nasema namuachia Mungu kwani yeye ndiye anajua ila siyo siri ni tukio ambalo lilinifanya niugue ghafla,” alisema Wema na kuongeza:
“Yaani nilikuwa napewa pole nyingi sana utadhani mimi mgonjwa. Hata wale ambao hawanipendi nao walikuwa wakinipa pole. Naomba serikali itazame upya hili suala hili la watu kuchafuana kwenye mitandao ya kijamii.”
AUNT EZEKIEL AFANYA KAZI YA ZIADA
Katika ishu hiyo, staa mwenzake wa sinema za Kibongo ambaye kwa sasa ni mashosti, Aunt Ezekiel Grayson alifanya kazi ya ziada kumuokoa Wema na kumfariji asichukue uamuzi mgumu.
Inaelezwa kuwa, Aunt alitumia dakika 29 kumpepea shosti wake huyo ili aweze kurejewa na fahamu, jambo zoezi ambalo lilizaa matunda.
Akizungumza na Risasi Mchanganyiko, Aunt alisema tukio hilo limemuumiza kila mtu hata wale ambao wanaonekana wako tofauti na Wema lakini kwa hili nao wameumia na kuungana naye kumtetea na kuwakemea waliyofanya kitendo kile.
Mama Wema.
“Nimeumia kwa tukio ambalo limefanywa na kusababisha Wema wangu kulia sana hadi kufikia kuumwa ghafla na kupoteza fahamu. Dah! Binadamu wengine sijui tukoje, lakini hamtaweza kufanikisha kwa sababu Wema ana watu wengi wanaompenda kuliko wanaomchukia,” alisema Aunt.
KAJALA SASA
Gazeti hili lilifanya jitihada za kumtafuta Kajala kupitia simu yake ya mkononi ili kujibu tuhuma za  kuhusishwa na picha hiyo lakini simu yake ilikuwa ikikatika kila ilipopigwa.
Baadaye ilijulikana kuwa, aliamua kuifunga kwa muda (inawezekana alikuwa sehemu inayohitaji utulivu).
Baadaye akatumiwa ujumbe uliosomeka: “Habari. Una taarifa ya picha chafu ya kutengenezwa ya mama Wema iliyosambazwa mitandaoni? Lakini unatajwa kuhusika kwa sababu una bifu na Wema, unasemaje?”
Hata hivyo, tunakwenda mitamboni, Kajala hakujibu meseji hiyo wala kupiga simu chumba cha habari kufafanua kuhusiana na madai hayo ambayo bado hayajathibitishwa.
MAMA WEMA ANASEMAJE?
Jitihada za kuzungumza na mama Wema juu ya sakata hilo ziligonga mwamba kwani simu yake iliita bila kupokelewa.
Msanii Kajala Masanja aliyetajwa katika sakata hilo.
SERIKALI NAYO
Timu yetu ilijaribu kufanya mawasiliano na Waziri wa Sayansi na Teknolojia, Mhe. January Makamba bila mafanikio, kwani simu yake haikupatikana.
Hata hivyo, wananchi wametoa kilio chao kwa Wizara ya Sayansi na Teknolojia kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kudhibiti usambazwaji wa picha chafu mitandaoni.
TUJIKUMBUSHE
Hivi karibuni, kuliibuka picha chafu katika mitandao ya kijamii za waheshimiwa wabunge, kabla ya baadaye wabunge kulaan ambazo mpaka sasa hazijulikana kuwa zilikuwa halisi au za kutengen
TAHADHARI
Kumekuwa na wingu la kuchafuana kwenye mitandao ya kijamii ambapo ukiacha watu maarufu kutengenezewa picha chafu pia wanafunzi wa vyuo wamekuwa waathirika wakubwa hivyo ni vyema kila mtu akachukua taadhari na mamlaka husika ilishughulikie.

CHANZO NI GPL

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate