EFM RADIO

EFM RADIO

HERICONY

Tangaza hapa

Tangaza hapa

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

TANGAZA NA BLOG YAKO HAPA

Wednesday, January 28, 2015

DIAMOND, KIBA UCHAWI MTUPU!

Na Waandishi Wetu/RISASI MCHANGANYIKO
HALI inazidi kuwa mbaya kwa mastaa wawili wa muziki wa Bongo Fleva wanaogombea unyota kimuziki, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Ali Saleh Kiba, safari hii yameibuka mapya kwa kila msanii kuogopa kumshika mkono mwenzake kutokana na imani za kishirikina.
Mashabiki wa Mbongofleva Ali kiba waliionyesha kumkubali zaidi kuliko, 'Daimond Platnumz' katika viwanja vya Leaders Club.
TUJIUNGE LEADERS
Matukio hayo ya kusisimua yaliwatia hofu kubwa mashabiki na wadau wa muziki Bongo muda mfupi kabla ya nyota hao kukaribishwa stejini kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar, mwishoni mwa wiki iliyopita.

HIRIZI ZAKUTWA UWANJANI
Kwa mujibu wa wanahabari wetu, katika Viwanja vya Leaders, Kinondoni, kulikutwa hirizi zilizozagaa, zilizodaiwa kudondoshwa  na vijana waliokamatwa wakiwa wamevalia sare zenye majina ya mastaa hao wawili.
Moja ya Hirizi iliyotupwa katika viwanja hivyo.
Katika hali ya kushangaza, mmoja wa mashabiki waliohudhuria onyesho hilo ambaye aliziona hirizi hizo, aliwashangaza mashabiki wenzake alipodai kuwa anaiona mojawapo ikitweta mithili ya inayopumua!
“Oneni wadau, hii hirizi si inapumua, iangalieni vizuri,” alisikika shabiki huyo na kuwaacha watu wakiwa wamepigwa na butwaa kuona vitendo hivyo vya kishirikina katika eneo la burudani.
Wakati matukio hayo ya kukutwa kwa hirizi hizo yakiendelea, Diamond, baada ya kupanda jukwaani kabla ya kuanza kuimba, akajikuta akiteleza na kuanguka jukwaani na kusimama mwenyewe huku vijana wanaodaiwa kuwa ni wa Timu Kiba wakipiga kelele kwa nguvu kuashiria kuwa walipendezewa na kitendo hicho kutokea.
Mashabiki waliotinga katika shoo hiyo wakishuhudia hirizi zilizo zagaa katika viwanja hivyo vya Leaders.
Pamoja na Diamond kula mwereka hadi chini, hali ilizidi kuwa mbaya kwake baada ya muziki kuanza kusikika vibaya huku ukiwa unakatakata, kitendo kilichoamsha hisia kuwa kulikuwa na ushirikina unaoendelea ili kumshusha kisanii kwa kuonekana amefanya vibaya katika shoo hiyo.
CHUPA ZARUSHWA
Baada ya kuona hali inazidi kuwa mbaya huku chupa za maji zikirushwa jukwaani hapo na baadhi zikimpiga na nyingine akizikwepa wakati akiendelea kupiga shoo, Diamond aliamua kutumia akili ili kuzima kelele hizo kwa kuanza kumwaga noti.
Kikosi cha ulinzi kikiwajibika kudhibiti vijana walioonyesha tabia korofi.
Ishu hiyo iliwafanya mashabiki na Timu Kiba kuachana na zoezi hilo na kuanza kusukumana kugombea noti hizo za elfu mbilimbili ambapo alimwaga kwa awamu tatu.
SADAKA?
Wakati akizidi kuwatupia noti mashabiki, Diamond alisikika akisema kuwa pesa hizo ni maalum kwa mashabiki kwani ni sadaka kwao kutokana na sapoti kubwa wanayompa ingawa hataweza kumpa kila mmoja.
Makamanda wa Polisi na kikosi cha Ulinzi wakihakikisha usalama unakuwepo kwa mastaa waliopangwa kutoa shoo.
DIAMOND KAMA MICHAEL JACKSON
Hata hivyo, baadhi ya mashabiki waliokuwa wakisukumana na kuokota noti hizo walisikika wakisema:
“Huu mchezo alikuwa akiufanya Michael Jackson (Mwanamuziki marehemu wa Marekani) tena alikuwa akitumia ushirikina na Freemasons.
“Michael alikuwa anadaiwa kumwaga fedha hizo zilizokuwa na nguvu ili kuwafanya wale waliokuwa wakimzomea kukaa kimya,” alisikika shabiki mmoja akisema.
MSHANGAO
Katika hali ya kushangaza zaidi,  Diamond alivua tisheti na vesti ya ndani na kujifuta jasho kisha kuwarushia mashabiki huku akijua wazi kuwa amefutia jasho lililokuwa likimiminika mwilini mwake kama maji.
Mbongofleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’
KIBA HAKUTAKIWA KUZUNGUMZA?
Wakati matukio ya kushangaza aliyokuwa akiyafanya Diamond na yale ya kurushiwa chupa za maji machafu na yenye mikojo yakiendelea, ilidaiwa kuwa Kiba alipoingia kwenye chumba cha wasanii hakutaka kuzungumza na mtu yeyote huku ikidaiwa kuwa hiyo ni ishara kubwa kuwa hakutakiwa kuzungumza na mtu kwani angeweza kupoteza nguvu za kufanya shoo.
POLISI MZIGONI
Wakati mashabiki wakizidi kuwa na wasiwasi juu ya wasanii hao, jeshi la polisi lililokuwa na zana zote za kukamatia wahalifu, walianza doria ya kukamata vijana ambao wanadaiwa kuwa ni Timu Kiba waliokuwa wakibishana na kutupa chupa zenye mikojo na maji  huku wakipokea kipigo kama cha mbwa mwizi.
Mbongofleva, Ali Saleh Kiba.
KIBA ARUKA UKUTA
Awali kabla ya shoo hizo kuanza matukio ya kishirikina yalijidhihirisha zaidi baada ya Ali Kiba kuingia uwanjani hapo kwa njia ya kuruka ukuta na hata alipozama kwenye chumba maalum walichokuwa wametengewa wasanii hakuweza kushikana mikono na wenzake.Wasanii ambao Ali Kiba aliwachunia ni AY, MwanaFA, Shaa, Shilole, Vanessa Mdee na Jux, ambao wote aliwakuta ndani ya chumba hicho.
Imeandaliwa na Gladness Mallya, Musa Mateja, Chande Abdallah, Mayasa Mariwata, Shani Ramadhani, Denis Mtima na Laurent Samatta

No comments:

Post a Comment

HABARI MBALIMBALI

‘Dk. Cheni’ ‘Sharo Milionea ‘Thea’ African Women AGNESS MASOGANGE AK CLASSIC COSMETICS ALI KIBA Amanda Poshy Ant ANT LULU Ashley Toto Aunt Ezekiel Aunty Ezekiel AUNTY LULU Azam Fc Baby Madaha BAHATI BUKUKU Barnaba BATULI BBA Beauty of the day Belle 9 BI KIDUDE BIBI BOMBA Big Brother Big Brother Africa Bill Gates BINTI KIZIWI BOB JUNIOR Bodi ya Filamu Bongo Movie Bongo Movies CCM CHADEMA Chombezo Christina Shusho Chuchu hans. Clouds Media Group Club Bilicanas DAR LIVE DAVINA Dayna Nyange Diamond Dida Diva Loveness Love Dj Ommy Crazy wa Maisha Club DOGO JANJA DOKI DR.CHENI DSTV Dude Dully Sykes EBSS 2013 Elizabeth Michael Epiq Bongo Star Search (EBSS) ESHA BUHETI Ester Bulaya Feza Kessy FIESTA 2014 Flaviana Matata FLORA MBASHA FLORA MVUNGI Francis Cheka GARDNER GLOAL PUBLISHERS GLOBAL TV ONLINE H. BABA Halima Mdee HAMISA Happy birthday Hemedi Hemedy Suleiman HOTUBA YA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE Hoyce Temu Huddah Monroe HUSINA IRENE PAUL Irene Uyoya ISABELLA J film 4 life Jack Chuz JACK PATRICK Jacob Steven ‘JB’ Jacqueline Dustan JACQUELINE WOLPER Jaji Khamis 'Kashi' Jay Dee JENNIFER KYAKA (ODAMA) JIDE JINI KABULA JK JO Johari Jokate Mwigelo ‘Kidot’. JOTI Joyce Kiria Joyce Kiwia JUX K-LYNN KADINDA kaja Kajala Masanja Kapotive Star Singers KATUNI Kemmy Kero Zetu KHADIJA OMAR KOPA KIKWETUKWETU KILI MUSIC AWARDS KOLETA Lady Jay Dee Lady Jaydee Lake Oil LAVEDA Linah Sanga Linex Lisa Jensen Loveness Diva Lucy Francis Komba Lulu M2 The P MABILIONEA Madam Rita MADELA Magazeti Mahusiano Maimartha Jesse MAINDA MAISHA Makala Malkia Elizabeth MAMTEI MANDELA MARIAM ISMAIL Masanja Mkandamizaji Mashindano ya Miss Tanzania Matangazo Matonya MaxMalipo MAYA MELLIS EDWARD MENINAH MGOSI MKOLONI Mh Halima Mdee mic Michezo MILLEN HAPPINESS MAGESE MISS CHANG'OMBE MISS DAR CITY CENTER Miss East Africa MISS REDD'S IRINGA 2013 MISS TANGA 2013. MISS TANZANIA 2014 Miss Tanzania mwaka 2011 MISS TEMEKE 2014 MISS USTAWI MISS UTALII TANZANIA 2012/13 Miss vyuo vikuu 2013 MKALA MREMBO HUDDAH Mrisho Mpoto Mrisho Ngassa MSHINDI WA REDD'S MISS LAKE ZONE 2013 NI LUCY CHARLES. MSHINDI WA TAJI LA REDDS MISS KANDA YA KATI 2013 Mtitu muziki Mwana FA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Mzee Majuto Nancy Sumari Nani Mtani Jembe? NAPE Nassoro ‘Nora’ Natasha Nay wa Mitego Necta Nelly Kamwelu NEY WA MITEGO Nisha NSSF;Zantel Nyamwela NYimbo Nyota yako OBAMA TANZANIA OMMY DIMPOZ P FUNK PAM D Peniel Mgilwa ‘Penny’ PETIT MAN Profesa Jay Q - CHILA Q Boy Q Chilla QUEEN DARLEEN RACHEL NDAUKA RAIS KIKWETE Rais Kikwete. Rasimu Ya Katiba TZ Ray Ray C Redd’s Miss IFM REDD'S MISS KAGERA 2013 REDD'S MISS TZ REDDS MISS TANZANIA 2014 Redds Miss wa Mikoa REHEMA FABIAN RICHIE RICHIE Rihanna ROSE MUHANDO Rose Ndauka Ruge Mutahaba. SABASABA 2013 Saida Karoli Saikolojia Sajeti SAJUKI Sandra SHAA Shamsa Ford Sheikh Ponda Shilole Sintah Siwema Skin Tricks Snura Mushi Spika Makinda staa Staa Wetu Stella Mwangi STYLE ZA NYWELE Taifa Stars Tamasha la matumaini TAMASHA LA SERENGETI FIESTA 2013 Tangazo TANZANIA TEGO TENGENEZA WEBSITE NA BLOG TID Tundaman Tupo wangapi? TUZO ZA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2013/14 Twanga Pepeta USA PAGEANT 2014‏ VAI Wastara WEMA WEMA SEPETU Yanga Yanga Bingwa 2013 YOUNG D Yvonne Cherry ‘Monalisa’ Z Anton. Zari Zito kabwe

Translate